The Chant of Savant

Tuesday 24 November 2009

Southern Sudan: The Birth of a New Era?






Sudan will soon cease to be the largest country on the continent. It won’t even be the second or third biggest. Soon, the language of Junubi, kaffirs and slaves in Sudan will die. Soon the newly born baby will be seen. The much ignored, exploited and despised will take their future in their own hands. It’s just soon and very soon.

Salva Kiir Mayardit, president of South Sudan (and vice president of Sudan) has said that Southern Sudanese have two choices come next elections-cum- referendums about the future of this biggest country in Africa: to vote for toto freedom or to vote for being second class citizens in their own motherland. This can not be something to pooh pooh.

"When you reach your ballot boxes, the choice is yours: you want to vote for unity so that you become a second class in your own country, that is your choice," Kiir said addressing worshipers at a Juba cathedral. "If you want to vote for independence so that you are a free person in your independent state, that will be your own choice and we will respect the choice of the people," he continued.

Logically, all sane people will vote for freedom. Apart from being their leader’s vision, they are tired of the thuggish and exploitative North. The South has no reason to solemnize any marriage with the North.

Khartoum’s skeptics wrongly think that if the South goes solo, she will be orphaned. On the contrary, the South has a good partner in Kenya even Uganda. Presently, the South gets almost all of its supplies from and through Kenya. Kenya has hosted Southerners since the inception of the concept of emancipation. Nairobi was a hub and bastion for leaders of Southern Sudan's freedom fighters. So, warm and strong was the relationship between Kenya and the late John Garang. Southern Sudan will thus be more at home doing business with a reliable and supportive partner than the suspicious and bully one.

Being a baby in the making, Southern Sudan has a brighter future in the East African Community than in Khartoum. After all, Khartoum needs the South more than the South needs it thanks to how it underdeveloped, degraded, neglected and exploited it for long. There is nothing that gears the North to support the re-unification of Sudan but resources in the South, especially oil. Will the South allow itself to be bitten twice?

Racism and ideological differences

North Africans regard themselves as Arabs. Northerners discriminate against Southerners for two reasons: One, Southerners are either Christians or traditionalists and two, they’re blacker than they. With time, the perception of colour-though artificially conceived (for even northerners are Africans)-and hate influence from the Arab world is likely to go even deeper. Northerners do not like Southerners. But given that the South is awash with oil, they’ve no alternative.

Incorporating South Sudan in the East African Community should be done with all assurance and urgency as it has more to offer than Burundi and Rwanda put together.

Another thing that is likely to force Khartoum regime to its knees is the whole burden of Darfur. There are fears that Darfur may team up with the oil-rich South so as to take and Square circle on the north and assume power of the whole Sudan thereby making the dominant northerners to become subjects of their former subjects. This shocks President Omar Bashir to the bone.

Though separation defeats the spirit of African unity, it is better than wasting time wrangling and scheming against one another. Hither we can borrow a leaf from Eritrea. Its secession from Ethiopia enhanced peace and tranquility in the region.

On the one hand, some people are blaming Mayardit as being myopic and a separatist different from his predecessor, the late John Garang de Mabior Atem who wanted to take Khartoum through the ballot box. It must be appreciated that things have changed since the untimely demise of Garang. By then it was easy to take Khartoum by the way of referendum. But currently, it is easy to take Khartoum and re-unify Sudan by going solo so as to team up with Darfur and reclaim it.

Khartoum, without oil, will be nothing but a sitting duck. Though many fear that marriage of convenience with China can hamper its reclamation, this is hogwash. China, just like any other moneymaker, will bet on the winning horse. This being the situation, it remains to be seen if going solo for South Sudan means gain or peril.

Source: The African Executive Magazine Nov. 25, 2009.

Namna hii Kikwete hawezi kuikwepa Richmond

MANENO ya Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM), mbele ya mkutano wa kamati ya wazee wa chama hicho, iliyoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, mjini Dodoma hivi karibuni, kama yatafanyiwa kazi ilivyo, hakuna jinsi ya kumnusuru Rais Jakaya Kikwete na kashfa inayozidi kutokota ya Richmond.

“Ni huyu Rostam aliyekodisha jopo la waandishi wa habari watatu mashuhuri nchini kwa ajili ya kupoza makali. Tumezungumza na waandishi wa habari hawa mmoja baada mwingine na wote wametuthibitishia hili.” Alibainisha Seleii.

Alitaja hata majina ya waandishi hao kuwa ni Gideon Shoo, Jimmy Mdoe na Salva Rweyemamu, ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya rais. Hii ni kwa mujibu wa gazeti la kila wiki la Mwanahalisi.

Ukizingatia maneno ya mbunge na jinsi serikali yake inavyoitumia Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), kutaka kuiua kashfa ya Richmond, unaaza kupata ni kwa jinsi gani rais alishiriki mchakato mzima.

Isitoshe katika kipindi cha siku 100 za kuwa ofisini, rais aliuambia umma kuwa mgawo wa umeme ungegeuka historia kutokana na serikali yake kuwa kwenye majadiliano na kampuni ya kufua umeme kutoka Marekani. Ukizingatia kuwa hapakua na kampuni nyingine kutoka Marekani zaidi ya Richmond, unapata picha kamili.

Cha ajabu, badala ya kushughulikia hili na kulimaliza. Watawala wameamua kuanza kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani japo haipo wazi sana. Watanzania tuzidi kumbana na kumkumbusha rais kwamba, hajatimiza ahadi hata moja, ukiachilia mbali serikali yake kuwa chaka la mafisadi.

Isitoshe, tamko la hivi karibuni la Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kuwa Ikulu ndiyo iliiamuru TAKUKURU kuwahoji wabunge, ndiyo kabisa unapata ushiriki wa moja kwa moja wa rais, ukiachia mbali kukwepa kuliongelea au kuchukua hatua kwa rais.

Rais anatoa amri ya kuwabana wabunge kwa masilahi ya nani kama si mshiriki nyuma ya pazia? Asingekuwa mshiriki asingehatarisha ofisi yake na kukiuka viapo vya ofisi.

Hizi ni harakati za kutaka kujinusuru. Kuna haja ya Watanzania kutoa shinikizo kuwa kama Kikwete atamaliza muda wake bila kutatua kashfa hii, asigombee hata CCM wapige debe usiku na mchana.

Maana akirejea ataharibu kama alivyofanya mtangulizi wake, Benjamin Mkapa, aliyesifika kufanya vizuri kwenye miaka yake mitano ya kwanza. Alipopata lala salama akaingiwa na tamaa ya utajiri. Historia ndiyo hiyo.

Wakati rais akijiaminisha kuwa atachaguliwa, mawaziri wake wameghubikwa na kashfa mbalimbali hasa za matumizi mabaya ya fedha za umma, imebainika kuwa wanaagiza mashangingi yawafuate kila waendapo ili kujishaua na asichukue hatua! Kwanini awavumilie mawaziri limbukeni wasiojali kuwa nchi hii ni maskini?

Kitu kingine, rais kuendelea kumbakiza Salva Rweyemamu ambaye amewahi kufanya kazi ya kuisafisha Richmond ni kielelezo kingine cha kuridhika na kuhusika kwake.

Je, haiwezekani kuwa ukaribu wa wenye Richmond (yaani Rostam Aziz kwa mujibu wa maneno ya Selelii) na Kikwete ndiyo ulimshawishi kumteua mhusika? Hivyo, uteuzi wake una mazingira ya ufisadi.

Maana, anaonyeshwa (kwa mujibu wa maneno ya mbunge) kama mwandishi kidhabu, anayewaza kusaliti taaluma yake kwa kujiachia kukodishwa na kila fisadi amsafishe. Huyu hafai kuwa mkuu wa kurugenzi ya habari Ikulu hata kidogo.

Maana, Ikulu ni mahali patakatifu, tena pa patakatifu, kama alivyowahi kuhusia mwanzilishi wa taifa hili, Mwalimu Julius Nyerere.

Kwa nini rais anaendelea kumbakiza kwenye ofisi yake mtu ambaye ameishachafuka, ili iweje? Kama haoni uchafu wake, tulio nje tunauona na ofisi wanayotumia kishikaji ni yetu si yao.

Kwa mtu anayejua ukali wa Rweyemamu kabla ya kuingia kwenye utetezi wa mafisadi, anapata sababu ni kwanini aligeuka ghafla wakati wa kampeni na kuanza kulamba matapishi yake.

Je, haiwezi kuwa Rostam aliwatafuta mapema ili kuandaa mazingira ya ushindi na kupata tenda ya kufanya yanayoendelea kulisumbua taifa? Na ukichukulia kuwa huyu mtuhumiwa ndiye yule yule aliyenunua vyombo vya habari kwa pesa ambayo Dk. Harrison Mwakyembe, aliwahi kusema ni ya EPA akimtumia mtu wake huyu huyu.

Je, hii si ushahidi kuwa kumbe Ikulu yetu ni ya ubia ingawa rais aliwaahidi wananchi kuwa asingekuwa na ubia na mtu? Kama ilivyo kuwa kwa maisha bora, si ajabu rais alimaanisha kinyume aliposema hatakuwa na ubia na mtu wala kikundi cha watu.

Rweyemamu ni mwajiriwa mwingine wa rais, mbali na waziri mkuu na mawaziri waliojiuzulu au kuwajibishwa, kuguswa na Richmond moja kwa moja na rais hataki kuchukua hatua! Je, hapa kuna njia rais anapoweza kukwepa kuhusika moja kwa moja?

Kuna uwezekano mkubwa kashfa ya Richmond kama haitashughulikiwa ikafumua mengi. Kwa mfano, mtuhumiwa mkuu Rostam Aziz amebainika kuwa ndiye mwenye Dowans. Je, huyu hatimaye hawezi kuwa Kagoda?

Na je, hii ndiyo sababu Kagoda na Richmond yamegeuka mazimwi yanayoyumbisha utawala wa Kikwete kuliko hata majanga? Selelii alinakiriwa akisema: “Kwa maana nyingine, Dowans, Richmond na Caspian ni baba mmoja, mama mmoja.”

Kama Kikwete hatatoa sababu za kuwagwaya wezi hawa, atajikuta akihusishwa na kashfa zote kuanzia Richmond, EPA, Meremeta na mwingine utakaofichuka baadaye.

Haiwezekani mtu ambaye hakushiriki akaacha mambo yajiendee na kuendelea kumuweka pabaya bila kushiriki. Na hapa ndipo viburi vya watu kama Rostam, Makongoro Mahanga kusema eti ripoti ya kamati ya Bunge ni feki au kina Edward Hosea kusema wazi hawatawajibika. Wanajua wana mwenzao aliyeshika rungu.

Tukimalizia na Rostam anayeshutumiwa kuwa nyuma ya CIS, Dowans, EPA na Richmond, hata utetezi wake unatia shaka. Hauwezi kuishawishi akili yoyote timamu. Alikaririwa hivi karibuni kwenye gazeti hili, ukurasa wa kwanza, akiliita “Kujibu Mapigo. Alikaririwa akisema: ‘‘Hawa ni wapuuzi, wanasukumwa na chuki.”

Rostam hakueleza chuki hii inasababishwa na nini! Kwa wenye kujua historia nzima ya kashfa na mhusika wanaona kama ni kutapatapa. Ipo siku atamrukia hata anayemkingia kifua.

Umefika wakati wa kuliita koleo, koleo badala ya kijiwe kikubwa. Binafsi, naamini huko tuendako, ataunganika moja kwa moja na kashfa hizi zote hasa ikizingatiwa kwamba hajajibu shutuma za ushindi wake kutokana na pesa chafu, mikakati na watu wachafu ambao bado amejizungushia akizidi kuwakingia kifua.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 25, 2009.

Ukishangaa ya Madevu na Karumekenge...

BAADA ya kushuhudia ngunguri na ngangari wakingungulana, sasa tunaambiwa pepo limefukuzwa na ubani. Sasa umefukizwa kiasi cha uzuri wa harufu ya marashi ya Pemba kurejea!

Upande wa pili tumefunguliwa macho na Mbunge Lucas Selelii kuwa kumbe kuna wenzetu pamoja na majina yao makubwa ni hovyo!

Hawa ni wale wanaojiita waandishi wa habari waandamizi waliogeuka waandishi wa habari wadandindizi na wapuuzi. Inakuwakuwaje mwandishi mzima, tena mwandamizi, unanunuliwa na mafisadi kufanya chafu yao?

Alisema Luca kuwa jamaa zangu wa kujishoo-shoo na kudoea bila kumsahau kasuku shangingi la kihaya, walinunuliwa na Richamondu kuitakasa wasifanikiwe.

Hapa ndipo kitendawili cha Njaa Kaya kutokuwa kwenye uchafu huu kinapofunguka. Kama hakushiriki amewezaje kumwajiri nyemelezi huyu kuwa msemaji wake in the first place?

Kweli wanasiasa na wasanii ni watu wa kuangaliwa kwa makini. Tapeli mmoja anaweza kuja akakuaminisha atakupeleka peponi kumbe anakupeleka motoni kama ilivyotokea walevi na jamaa yangu Njaa kaya na sasa shangingi Sylvia anayejifanya spika wa Njaa Kaya.

Nani alijua yule jamaa wa madevu na mwana wa mteule wangekaa jukwaa moja kwa bashasha na mashamsham bila kujali gemu lao liliumiza wengi?

Hayawi hayawi yamekuwa! Ule mzuka wa kipopobawa uliokuwa umevivamia vile visiwa viwili sasa umetulia na watu wanaweza kufanya madili yao bila bughudha.

Ila wakati usanii ukifanyika twapaswa kuzingatia. Waliofikia makubaliano si wanuka jasho bali walaji wachache wanaoendekeza libeneke ya usaliti na ufisi ndani ya ufisadi.

Nani alijua Rweyependekeza angelamba matapishi yake kwa kumuangukia Njaa Kaya na kujikabidhi atumiwe? Hili tumbo! Njaa nyingine bwana. Yaani jamaa kauza hata News Corp kwa tamaa za kijinga kiasi cha kujibinafsisha kwa mafisadi wanaomtumia kama nepi!

Ukishangaa ya Richamondu utaona ya mwafaka-siri. Ukishangaa ya Kagoda utaona ya Dowans. Na ukishangaa ya Rostitamu utaona ya Ewassa kama siyo Sofii!

Na yote kati ya yote ukishangaa ya Tunituni utaona ya Chekacheka. Ukishangaa ya Anae Tamaa Tunituni utaona ya Salama Shari Kikwekwe! Ni maajabu jabu jaabu jaabu tupu kwenye anga hili la Danganyika ya Tanzia.

Hata hivyo ieleweke wazi. Mzee mzima sina ugomvi na ndoa hii mpya iitwayo matambuano ingawa wenye chao wanaitilia shaka tena kubwa. Hayo ni mambo yao binafsi ingawa kuna masilahi ya umma.

Sitaki nionekane mnoko ingawa jamaa zangu hawa hawaaminiki. Hujamsikia Prof akisema wamecheza karata tatu na kujitia kitanzi kisiasa. Wazungu husema political risk.

Kwanini kujiingiza kwenye hatari hii ya kisiasa kama kweli hakuna ulaji binafsi nyuma yake? Mnakimbizwa na nini zaidi ya salata na njaa? Kwani hii ni mara ya tatu wakionyesha sanaa zao za kufunga ndoa na kuachana kila mtu akisema lake.

Tungoje tuone nani atamliza nani au kumtwisha mkenge ingawa ni wazi mwenye rungu atammaliza mwenye matumaini yasiyokuwepo.

Wakati tukiangalia upande wa wanandoa mashaka hawa, wapambe nao, hasa huyu mwingine, sijui kama watakubali kuingizwa kwenye mkenge huu.

Ingawa ndoa ni jambo la heri, nyingine ndoana. Unaweza kumkimbia mjusi ukajikuta kitanda kimoja na mamba si kenge. Tuyaache.

Kwanini sasa baada ya miaka tisa ya Karumekenge kuwa kwenye maulaji? Hapa kinachokera ni kupoteza muda hata maisha ya watu. Sasa jamaa alikuwa anadengua nini au kalishwa limbwata?

Yako wapi? Tulisikia viapo kibao kuwa jamaa alikuwa amekwapuliwa ulaji. Sasa umerudishwa na kama umerudishwa mbona haki za waathirika wa mchezo huu wa karata tatu hazikuzingatiwa?

Kweli tukiamua kuchunguzana kuna watu wengi wameghushi vyeti vyao. Hivi jitu lenye PhD kutumiwa na wezi uchwara (tena wasio na elimu kama yake), kufilisi taifa lake kweli hili halikughushi?

Je, huu nao si uchangudoa wa aina yake kujiruhusu kutumika kinyume? Baalalii angekuwapo angekwambia alivyodanganywa na majuha na vimada wake naye akaishia kuwa juha na mhanga bila kusahau Tunituni bishororo aliyejitia usomi wakati mweupe kama Njaa kaya.

Hamkusikia ya jamaa yangu wa rada ambaye sasa ni mzito wa shirika la moto na kashfa ya kununua maua na samani kwa milioni 50 za madafu? Hivi ni kufuru kiasi gani kuchezea pesa hivi wakati walalanjaa wakizidi kuteketezwa na umaskini?

Hivi huyu jamaa na Kagoda kweli hawana shea kwenye lisirikali la Njaa Kaya kweli? Angalia kila kashfa wamo wao. Richamondu, rada, CIS, Meremeta, EPA, kujiuzia nyumba za umma, wamo wao! Je, hawa si mamlaka ndani ya mengine jamani?

Inaonekana kuna viumbe wanatisha kiasi cha kumfanya hata mkuu kuwagwaya kama ukoma! Je, ni kwanini? Ni kwa sababu wanajua uchafu wake na ushiriki wake katika kuunda ujambazi mbuzi kuanzia EPA hadi mwingine utakaoundwa kuokoa jahazi mwakani?

Je, lisirikali la jamaa halimo mfukoni mwa Rostitamu anayarostisha taifa na Njaa Kaya mwenyewe? Hawa jamaa hawajui kuwa liponjoro hili na wenzake kaya ikiwaka moto watatimkia makwao wakituacha sisi tunamalizana kama pale kwa kaya ya nyayo?

Siwezi kuamini nyuzi nilizozinyaka juzi kuwa nambari wahedi imeunda jopo la kuchangisha pesa kwa ajili ya Njaa Kaya kwenye kipute kijacho.

Huwezi kuamini jopo hili linaundwa na wezi watupu wakiongozwa na Rostitamu, Kadamage Ni-ziro, Tamil Msumaiya na majambazi wengine.

Je, hapa hawajatufungua macho kuwa jamaa yetu kumbe ni mtoto wa mafisadi wanaomuweka ndani ya mifuko yao kumuwezesha kuhonga na kupeta? Je, huyu anafaa kukaa patakatifu pa patakatifu?

Nirejee kwa jamaa yangu wa kujishoo-shoo. Upo? Jim wa Kudoea bila kumsahau shangingi wa kihaya mnanipata hapa? Nyinyi ni vyangu tu hata kama mtajiona wajanja.

Huwezi kwa kutumiwa na walafi kula makombo kama jibwa ukawa mjanja bado. Mbwa ni mbwa hata alale kwenye busati. Mbwa ni mbwa hata alale ikulu bado ni mbwa tu.

Yaani tunafanya upuuzi wa wanakijiwe wenzetu bila kujua adha itokanayo na umaskini na vipigo kwa kutumikia matumbo yetu yasiyo na dirisha wala mlango!

Huwa siachi kujiuliza. Hivi uchafu kama huu unapofichuka huwa anajisikiaje mbele ya mkewe na watoto? Hebu piga picha.

Anakuja mtu anakupa laivu kuwa dingi au mume wako unayemheshimu kuliko yeyote anatumiwa na mafisadi kinyume na taaluma na umjuavyo. Kwa ndugu zangu toka Iringa usishangae mtu akachukua kamba na kusema swela-lazima nijinyotoe roho.

Ujumbe wa leo kwa kina Mdoezi, Bishoo na Shangingi wa kihaya, tafuta kazi ya kuuza nyanya badala ya kujiita waadamizi wakati ni wadandizi na wafua nepi za mafisadi.

Hakuna jambo baya kama mtu mzima na akili yake kutumia tumbo kufikiri badala ya ubongo kiasi cha kujigeuza changu hata kama ni la kisiasa.

Kwa Madevu, kaka umeula wa chuya na hili lazima likung’oe taka usitake. Kabla hata wino haujakauka, Karumekenge ameishaanza kuichokonoa ndoa hii hatari kwa kuanza kuonyesha kuwa kina Madevu walijileta akawapokea lakini wasitegemee kitu! Ngoja nikawasake hawa gendaeka niwatie adabu na mapema.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 25, 2009.

Sunday 22 November 2009

Hongera Sophia Simba kwa kutufumbua macho


UKIMUWEKA mwanaharamu kwenye chupa, atatoa kidole. Hii imejidhihirisha juzi kwenye mkutano wa kamati ya mipasuko ya ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), iliyoongozwa na rais mstaafu mzee Ali Hassan Mwinyi mjini Dodoma.

Wapo wanaohoji mantiki ya kamati ya Mwinyi kukutana na wabunge Dodoma, sambamba na kikao cha Bunge kujadili ripoti ya serikali juu ya utekelezaji maagizo ya kamati teule ya Bunge, iliyochunguza Richmond Development LLC.

Japo yaliyopita ni historia yenye kutia simanzi, kuua matumaini na kuiacha uchi CCM, serikali na rais Jakaya Kikwete, kuna mengi ya kujifunza kama tutaamua kuyadurusu vilivyo.

Hapa ndipo pongezi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utawala Bora na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), Sophia Simba zinachimbukako.

Tukubaliane. Japo Simba alitoka nje ya mstari kiasi cha kuitwa mjinga, mgonjwa wa akili na mpayukaji, kuna kila sababu za kumpongeza kuonyesha na kuutanua ufa ndani ya chama kilichotuhadaa kuwa ki makini na thabiti wakati sivyo.

Sina sababu za kuunga mkono madai ya Simba. Nakubaliana naye. CCM imejaa mafisadi kiasi cha kuamini kila kigogo wa CCM ni fisadi. Ndiyo. Alisema Mwalimu Nyerere ukiona chama kinaanza kutekwa na matajiri wenye kutia shaka ujue mambo yameharibika.

Zamani hatukuwa na wafanyabiashara kwenye safu za juu za chama kama ilivyo sasa. Majina ya matajiri yanatajika kwa kicho na wapenda dezo waliojazana chamani.

Kwanini nampongeza waziri Simba? Mosi, amemkumbusha bosi wake rais Kikwete kuwa ukimya wake si dhahabu bali adhabu. Maana si chama wala serikali yake, kila mtu anajipayukia atakavyo kana kwamba maneno ya hayati Horace Kolimba yanatimia, aliposema CCM imepoteza mwelekeo na dira.

Pili, Simba ameonyesha ujeuri wa ajabu, hata kusimamia vitu visivyoingia akilini, hasa aliposema kuwa waziri mkuu aliyezamishwa na kashfa ya Richmond, ambayo imegeuka muuaji wa CCM, Edward Lowassa, anaonewa wivu kwa sababu alichuma mali zamani.

Kitu kimoja tumsaidie na kumsahihisha Simba. Hivi kweli Lowassa anaonewa wivu? Tujalie ni hivyo. Je, watu, majina na udhu wao kama hayati Mwalimu Nyerere, aliyemtolea uvivu na kumtimua kwenye kugombea urais mwaka 1995, naye alikuwa akimuonea wivu kwa lipi?

Tatu, Simba si mnafiki wala hafichi msimamo wake. Japo ametuhumiwa kuwa na matatizo ya akili, anajua analofanya. Ingawa utetezi wake wa wazi wa mafisadi ni kinyume na kiapo chake, na maneno ya bosi wake (Kikwete), ameudhihirishia umma kuwa anaunga mkono mafisadi. Anapata faida gani? Jibu analo.

Ukiachia mbali kutoona aibu na kuchagua maneno yanayolingana na wadhifa wa uwaziri, nampongeza Simba kwa kufichua ubovu, upogo na ombwe la uongozi-niseme utawala. Maana siku hizi hatuna viongozi, bali watawala.

Inapofikia waziri na mwimbaji taarabu wakakosa mpaka, jua kuna tatizo, tena kubwa. Lakini kwanini tulilaumu panga ilhali mwenye kulitumia kakaa kimya? Kuna haja gani ya kumlaumu waziri Simba kusema hafai wakati Kikwete anamuona ni kifaa? Tuzidi kudodosa. Ina maana waziri Simba alikurupuka bila ya kuwapo mikakati nyuma ya pazia?

Haiwezekani. Ukitaka kujua namaanisha nini, jiulize kwanini Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilitaka kuwahoji wabunge kabla ya wao kumaliza mfupa unaoonekana kumshinda fisi (serikali)?

Tusiishie hapa. Tuzidi kudurusu. Ni kwanini kamati ya Mwinyi, ikijua wazi ufinyu wa muda wa bunge na unyeti wa suala la Richmond, kwa makusudi mazima, ikaamua kuzidi kuupunguza muda kwa ku-bize wabunge, kama hakuna mikakati nyuma ya pazia?

Nikope maneno ya Arthur Koestler, "Bravo, the Wolves Devour each other- Hongera, mbwa mwitu wakitafunana wao kwa wao.”

Ingawa taifa limegeuka la wasahaulifu, la waziri Simba si rahisi kulisahau. Na kama tutafanya kosa hili, tujue tunajitia kitanzi wenyewe. Sitaki nionekane nawazushia Watanzania. Iko wapi kashfa ya akaunti ya madeni ya nje (EPA) na harakati chafu za TAKUKURU, kutaka kuzamisha hoja ya Richmond? Wako wapi watuhumiwa wa wazi wa Richmond na walioghushi, zaidi ya kuendelea kutugonganisha vichwa kama mataahira?

Kwa vile sera ya serikali ya Kikwete si kuwalinda mafisadi, basi mawaziri au watendaji wa serikali wenye uchungu nao au walioajiriwa nao wapaswa kuachia nyadhifa zao ili wawatetee mabwana zao vizuri.

Hapa ndipo nazidi kumpongeza Simba kwa kumtoa paka kwenye kofia. Kama Kikwete hana faida na machukizo tunayoona yakitendwa na kutamkwa na wateule wake, ana nini nao hadi asiwapumzishe?

Hivi hili linahitaji uwe mshauri wa rais kuliona na kulifanyia kazi? Je, kama Kikwete ni mkimya hivi, ana nini cha kutufanyia kiasi cha kutaka tumchague kwa ngwe ya pili iwapo ya kwanza inaonyesha kuwa hasara na ajali?

Tusiogopane. Ingawa tunaweza kuwalaumu akina Simba, tuna haja ya kuwapongeza kwa kuonyesha ubovu na uoza wa chama na serikali yao. Kwa wapenda maendeleo hili ni jambo la kupongezwa. Wezi wakianza kutoana makoo jua mwenye mali anasalimika.

Simba nampongeza pamoja na wenzake wanaotuhumiwa ufisadi kuzidi kuizika CCM, kwa kutaka kuokoa nafsi zao kosefu.

Nikope maneno ya spika wa Bunge. Huwezi kuwa na siasa za majitaka ukaleta maendeleo.Wala huwezi kutumia majitaka kumsafisha nguruwe.

Nimalizie na kumpongeza mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, aliyetaka achunguzwe na majaji ndipo aridhike ni mshirika na mwezeshaji wa Richmond na EPA. Msimamo wake ni mzuri japo unatia shaka.

Kama ameshindwa kuwaamini wabunge wenzake na kamati aliyoshiriki kuridhia iundwe, atawaamini majaji? Je, kama ameshindwa kuwaamini wawakilishi wa umma atawaamini wateule wa rais?

Msimamo wake ungekuwa mzuri zaidi kama asingekuwa na uswahiba na mamlaka. Pia ningemshauri aende mahakamani, kwa vile kuna majaji atatendewa haki na atawaamini. Hata hivyo, alikuwa wapi muda wote? Watamaliza waganga na ndwele haiondoki.

Chanzo: Mwanahalisi Nov. 19, 2009.

Wednesday 18 November 2009

Reparations: Which Way for Africa?


BBC recently published an article demanding African traditional rulers to make an apology for collaborating in vending their subjects during the notorious and heinous slave trade. According to Civil Rights Congress, a Nigerian rights group’s letter to traditional chiefs: "We cannot continue to blame the white men, as Africans, particularly the traditional rulers, are not blameless." In addition, proponents of the slave trade, such as Archibald Dalzel, argue that African societies were not affected much by slave trade.

Let us face it. Who were the true harbingers and beneficiaries of this sacrilegious trade that saw an estimated 9.4 and 12 million Africans shipped to the new world? The answer is crystal clear. The West and Arab countries.

In the 19th century, European abolitionists, most prominently Dr. David Livingstone, argued that Africa’s fragile local economy and societies were severely harmed by the trade. Scholars such as Basil Davidson later conceded it might have had some benefits while still acknowledging its largely negative impact on Africa.

We’re talking about 10 to 12 million people. Who bothered to document those that died on the way and struggles to catch them? Why doesn’t the UN want to recognize this? Isn’t this deliberate racism and complicity-cum-duplicity?

I once read a certain infamous and fictitious literature blaming Africans for their miseries thanks to their leniency and sheepish behaviour towards slavery, colonialism and imperialism. But if we face it, there’s another missing link that has never been observed and appreciated.

Why was it possible for gluttonous colonialists, traders, missionaries, merchants and what not to take North even South America and Australia but not Africa with all her abundant natural resources? The reason is clear: there was fierce resistance. Some give far-fetched reasons such as mosquitoes, diseases and so on. But is this true? True history of African resistance has nary been written. In its place there is a bogus and dubious one that incriminates and misleads.

Back to this thing-apology, what must be done is not to make an apology but to redress the victims. If someone asked me who must make an apology between the descendants of the chiefs and the current slave masters in state houses in Africa, I’d prefer the latter. The miseries they are causing are graver than those caused by traditional rulers. If apology is such an in-thing, well, our slave masters that have hijacked us must do it. They’re the ones representing their masters. Who would think a sane person would foolishly name any of his street or anything after Queen Victoria or Elizabeth, king leopard, Bismark, etc whose rule robbed our continents?

Africa is weak economically and democratically partly because it was fractured to make it succumb to exploitation. Were it not for the current slave masters, Africans are able to prescribe their future. Who hampers them? The same-western countries that support their lapdogs in power in Africa. Today Africa has notorious and thuggish regimes in Congo, DRC, Ethiopia, Equatorial Guinea, Gabon, Rwanda, Tanzania, Uganda and elsewhere. In principle, these autocratic regimes are weak and 'toppleable'. But thanks to the backing by Western countries, they’re still in power terrorizing innocent citizenry.

Almost all promising African post independent leaders either were manipulated or felled by imperialists. Refer to Kwame Nkrumah and Patrice Lumumba; genocide in Rwanda and Burundi not to mention crimes against humanity in Angola, South Africa, DRC and elsewhere. Who provided the arms and military trainings to those behind those crimes? A cudgel breeds the peace of him that bears it.

We can castigate our traditional rulers. But what of churches and mosques whose roles in slavery and colonialism are clear? Who is ready to confront the Vatican, for example, to spend its tax-free riches solicited from poor countries to redress affected countries? Do all those seeking apology from Africa remember the infamous Berlin conference 1884? Have they confronted European countries to make an apology-cum-redress?

How many tonnes of minerals, timber not to mention labour and taxes were stolen by colonial masters? This is the secret behind the riches of Belgium, Britain, France, Germany, Spain, Portugal and others. The Jewish nation of Israel is not rich because it is made of geniuses or hard workers. But because of the redress and special treatments it has always lapped up from rich countries thanks to their conspiracy about Jewish persecution.

Switzerland, island of Man and other tax heavens are not swimming in lucre simply because they are smarter. They’re enhanced by our moneys hidden there by our rat-like thugs in power and slave masters.

Apology is not a big deal. Redress is. But importantly, it must be clear. Those trying to mislead by inculpating us and demanding apology instead redress must be taken as agents of the same evil. Indeed slavery is but holocaust II.

Source: The African Executive Magazine Nov. 18, 2009.

Tuesday 17 November 2009

Sakata la Richmond: Madai dhidi ya Sitta ni upuuzi


MADAI yanayozushwa juu ya mawasiliano ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta na kinara wa Richmond, Mohamed Gire, ni upuuzi unaopaswa kutiliwa shaka na kupuuzwa.

Kwa nini sasa baada ya Bunge kuibua, kuchunguza na kuianika kashfa hii? Hata ukiyaangalia, hakuna mwenye akili awezaye kuyaamini.

Kusema Sitta alikuwa na mawasiliano na Gire, kitu ambacho Sitta hakanushi, hakumfanyi spika huyo kuwa fisadi wala mshirika kwenye ujambazi huu wa mchana.

Kwa cheo chake (wakati ule) cha Ukurungenzi wa Taasisi ya Uwekezaji (TIC), Sitta bila kupinga au kuvunja sheria, alikuwa na uwezo na uhuru wa kuwasiliana na yeyote aliyeonyesha nia ya kuwekeza nchini.

Na hii ndiyo kazi iliyokuwa inafanya alipwe mshahara na marupurupu yote yatokanayo.

Wale wanaojaribu kutushawishi na kutuaminisha kuwa Sitta ni fisadi, wangetueleza ni lini na pesa kiasi gani Sitta alipokea kutoka kwa Gire na akawezesha nini? Hata wangeonyesha sheria au taratibu alizovunja katika kuwasiliana na Gire.

Kama Sitta alidhamiria kupata pesa yoyote kutoka kwa Gire, basi onyesheni japo ushahidi badala ya uzushi. Ingawa Sitta si malaika, ukimlinganisha na wanaomshutumu japo yu mtakatifu.

Nadhani, watu wazima na wenye akili timamu wangejinasua kwenye uchafu huu kwa kueleza ukweli waujuao na si kulalama na kutafuta kuwachafua wenzao.

Hii haitaondoa nongwa yao. Na ukitaka kujua nani mwizi, tazama yule anayesema: “Na fulani alifanya hivi.” Jitetee mwenyewe.

Kwa nini mawasiliano ya Gire na Sitta yawe habari ilhali ile hali ya serikali kuruhusu Richmond ‘kuuza’ sijui kukabidhi au kushirikiana na Dowans mitambo inayojulikana kuingia nchini kinyume cha sheria?

Kama hawa wanaotaka kutuaminisha ni wasafi, ingawa ni wachafu, ili tuwaamini watwambie miujiza iliyotumika Richmond kuuza mitambo yake wakati iliishabainika ni utapeli mtupu na wizi wa pesa za umma.

Hivi kuna ufisadi wenye ukubwa na kuchukiza kama huu unaoihusisha serikali hii? Je, ‘uchafu’ huu wa kutengeneza wa Sitta unaletwa kwa makusudi ili kuepusha udadisi wa umma juu ya kashfa yenyewe? Ni upuuzi na harakati gani za kipuuzi hizi!

Hata kama kuna namna yoyote yenye kutia shaka Sitta alishiriki wahusika walichelewa. Kwa nini wamuone fisadi baada ya kuwafichua na wasimfichue kabla?

Au ni yale ya Waziri wa Nchi (Utawala Bora) Sophia Simba, kujua maovu ya wenzake akayaficha, asichukue hatua, aje kuyamwaga hadharani baada ya kushikwa pabaya?

Ikichukuliwa kuwa ‘majizi’ ya Richmond yapo kwenye saa yao ya mwisho kuumbuliwa, uongo mwingi dhidi ya Sitta na wanaopinga ufisadi utatungwa na kusambazwa kwenye vyombo vyao vya habari vya kifisadi.

Je, watu wetu watakuwa mataahira kiasi hiki kubugizwa uchafu na uongo huu unaoenezwa na wafa maji hawa?

Ni hivi, tulishuhudia kinara wa Richmond na EPA akipayuka kuwa angetaka achunguzwe kama kweli alishiriki uchafu wa Richmond! Haya hayamwingii hata kuku, achilia mbali wanadamu.

Kama huyu anashindwa kuwaamini wabunge wenzake ambao alishirikiana nao kuunda kamati teule ya Bunge, atawaaminije majaji?

Je, anataka achunguzwe kwa vile anajua atatumia ukaribu wake na mamlaka zinazowateua alioamini wanaweza kumchunguza na wamsafishe kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilivyofanya?

Huyu aliomba kuchunguzwa na majaji. Nani anataka kurudia upuuzi wa kuteua majaji hata mahakimu kama kwenye kesi ya shutuma za rushwa ya sh 500,000,000 alizotoa Augustine Mrema, dhidi ya mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wakati ule?

Ijulikane. Bunge lilipoamua kuunda kamati teule, jamaa huyu alikuwa bungeni na hakupinga wala kutoa wazo hili! Wabunge ni wawakilishi wa moja kwa moja wa umma kuliko hata majaji wa huyu jamaa.

Ambaye hawaamini wabunge tena naye akiwa mbunge, aache ubunge na akubali kufikishwa mbele ya mahakama ili akutane na majaji wake vizuri huko.

Kwa kutoliamini Bunge ni kashfa tosha, hasa ikizingatiwa mhusika ni mbunge na alikuwapo wakati haya yakiidhinishwa na ndani ya Bunge.

Je, mtapatapa huyu hakusema haya kwa vile aliamini angeihonga kamati teule na kujinasua ingawa hakufanikiwa? Acheni utoto na kutapatapa.

Nchi hii haiwezi kuenea mifukoni mwenu. Mnatakiwa kufahamu kwamba, pesa yenu itokanayo na ufisadi, haiwezi kumnunua kila mtu.

Turejee kwa Samuel Sitta. Yeye si mpumbavu kujipalia mkaa akijua utamchoma mwenyewe. Hapa ndipo unapata ushahidi tosha kuwa Sitta hakushiriki kwenye upuuzi huu.

Maana, angekuwa ameshiriki kama Spika, alikuwa na mamalaka ya kuweza kuizima kashfa ya Richmond bungeni. Na hii ndiyo dhambi aliyoitendea CCM kiasi cha mafisadi kukamia damu yake.

Tukirejea maneno ya mwenyekiti wa kamati teule, Dk. Harrison Mwakyembe, kuwa kuna mambo yaliachwa ili kutowaaibisha wakubwa na wengine, kama ukweli ukirejewa, mafisadi hawana haja ya kumlaumu Sitta.

Tujalie, Mwakyembe na wenzake wakiamua kusema kila kitu, kweli kutakuwa na serikali au chama hapa? Je, ni vigogo wangapi walinusuriwa katika kile alichosema Mwakyembe, kuwa kuna mengine waliyaacha ingawa si vizuri kupindisha mambo?

Hapa ndipo serikali inapaswa kuchukua hatua kujinasua kwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa, vinginevyo inaweza kujikuta msambweni.

Hii njama ya kujaribu kuwapatiliza wabunge haisaidii bali kuchochea hasira na kujenga ithibati ya kuweza kuzobokwa yote bila kujali cheo cha mtu wala chama.

Kwanini hatupendi kuukubali ukweli hata kama ni mchungu kuwa kulikuwa na rushwa kwenye Richmond? Hapa lazima tukubali.

Bila kuwa na rushwa, aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa asingekubali kirahisi kuachia ngazi. Alifanya hivyo kwa kujua dhahiri hatari iliyokuwa ikinyemelea serikali, chama na yeye binafsi bila kusahau bosi wake - Rais Jakaya Kikwete, ambaye ametajwa mara nyingi kuwamo kwenye mchakato wa kuileta Richmond, ukiachia mbali kufanya kazi kwa niaba ya bosi wake.

Hata hivyo, hawa wanaojilizaliza sasa wakumbuke: walipewa mwanya wa kujitetea. Lakini, hawakuwa tayari kufika mbele ya kamati kufanya hivyo!

Je, walijua kwenda kwao kungekuwa ni kujipaka mafuta na kuingia kwenye moto? Bila shaka. Wale wanaodhania kuwa maamuzi ya Bunge yanaweza kubatilishwa licha ya kuwa wajinga, wanapoteza muda na kuzidi kujiaibisha zaidi.

Muhimu, tukubaliane. Richmond ni balaa la taifa. Kama upuuzi huu unaoendelea utaachwa uendelee, matokeo yake yatakuwa mabaya kuliko ilivyotarajiwa. Ila ijulikane.

Hawa wanapoteza muda. Siku itafika watanyea debe tu, vinginevyo wajiue. Hivyo basi, kitu muhimu na cha maana kufanya ni kwa serikali kuwafikisha mbele ya mahakama.

Huko basi, kuna nafasi kubwa tu ya kujitetea kama wanadhani wamechafuliwa au kuonewa. Kwanini hawaipokei changamoto hii kama kweli hawana hatia? Hii ndiyo njia pekee ya kuwasaidia.

Mwisho, kuendelea kutumia njia za mwituni hakutaisaidia serikali wala watuhumiwa. Badala yake, kutaongeza hasira kiasi cha ufa kuzidi kutanuka na madhara kuwa makubwa.

Je, wanangoja nguvu ya umma kuingilia kama ilivyoanza kufanya kazi kwenye mamlaka ya Reli (TRL) ambako imeripotiwa hivi karibuni kuwa wafanyakazi wameamua kuchukua uendeshaji wa shirika baada ya wawekezaji kubainika ni wababaishaji na watafutaji ngawira wa kawaida?

Hakika hakuna upuuzi kama madai kuwa Spika wa Bunge, Sitta ni fisadi kirahisi hivyo tu, kwa sababu aliwasiliana na Gire.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 18, 2009.


Simba alna hoja , lakini..............

INGAWA hoja ya ‘udumavu wa akili’ iliyoletwa na Idd Simba, yule Waziri wa zamani katika Serikali ya Awamu ya Tatu, inayosifika kwa kuuza nchi, ilileta kasheshe, bado hoja hii ni nzuri.

Simba, alikuwa na hoja yenye mashiko; kilichoiharibu ni namna alivyoitoa na kuitetea. Kilichomwangusha na kumponza ni aina ya maneno aliyotumia na sifa alizotoa hasa kwa wasomi.

Tuanze kuidodosa hoja. Je, si kweli kuwa Watanzania wana udumavu wa akili kulingana na ushahidi wa kitakwimu alioutoa? Kama zaidi ya nusu ya watoto wetu wana udumavu wa akili, basi na wazazi wao hali kadhalika.

Tukiangalia hata hili balaa la kughushi mitihani kwa wanafunzi na wanasiasa kughushi shahada, tunapata ushahidi wa pili. Je, si kweli kuwa wasomi wetu wengi wamekariri tu na wengine kupata shahada za hongo?

Je, msomi anayeongopa kusoma hadi kuiba mtihani au kughushi cheti si dumavu kiakili? Rejea mawaziri wengi hata wabunge kubainika wana shahada na vyeti vya kughushi na serikali isichukue hatua za kisheria dhidi yao.

Mfano mzuri ni kesi ya Mbunge wa Buchosa, Samuel Mchele Chitalilo, aliyebainika - kwa mujibu wa taarifa za uchunguzi wa polisi kuwa alighushi vyeti na hadi tunaandika hajachukuliwa hatua.

Kimsingi, mfumo wetu umedumaa kiasi cha kuendekeza na kupogelea uchakavu na nyongea ya mawazo mgando kama ilivyothibitika kwenye kupambana na ufisadi.

Kitu kingine kilichomponza Simba ni kuwatuhumu wasomi kuwa wamedumaa kiakili kiasi cha kutoshiriki siasa. Hapo hapo Simba amesahau kuwa yeye na wengine kama kina Masumbuko Lamwai ni wasomi waliojiingiza kwenye siasa wakaishia kudumazwa mawazo na wanasiasa kutokana na mfumo chakavu.

Je, ni msomi gani wa kweli atakuwa tayari kujipeleka huko akadumazwe kimawazo? Je, ni wasomi wangapi wamejaribu kuubadili mfumo huu mchafu hatimaye wakaishia kubadilishwa wao?

Je, usomi ni nini? Ni ile hali ya kuwa na vyeti vingi au utundu wa kuibadili jamii kutoka pabaya kwenda pazuri? Augustine Lyatonga Mrema, si msomi wa kupigiwa mfano kama Benjamin Mkapa au hata Jakaya Kikwete.

Lakini, kwa usomi wake wa kujiendeleza aliweza kutoa changamoto wakati wa uwaziri wake wa mambo ya ndani kiasi cha kupunguza kero zilizokuwa zimewashinda tunaowaita wasomi, kwa sababu walifika vyuo vikuu.

Hata ukimchukulia mtu kama Shaaban Robert, ambaye elimu yake ni ya msingi. Aliacha utajiri mwingi katika fasihi kiasi cha vitabu na mawazo yake kutumika kuwapatia watu shahada ingawa yeye hakuwa nayo.

Je, hapa msomi ni nani kati ya Robert na hawa wenye shahada zitokanazo na kazi zake? Hebu linganisha Frederick Sumaye, aliyekaa kwenye uwaziri mkuu kwa miaka 10 na Edward Lowassa ambaye hakumaliza hata miaka miwili.

Hata ukiwadurusu wana falsafa kama Plato, Academus, Sophocles na wengine, hawakuwa na shahada hata moja. Lakini, waliacha utajiri mkubwa katika dunia ya sasa.

Hivyo, kimsingi tunapoongelea usomi, tusiangalie makaratasi na tambo za ‘nimesoma’ bali mchango wa mhusika katika jamii.

Kama usomi wetu wa sasa ungekuwa na tija, basi watu kama Mkapa, Andrew Chenge, Dk. Idris Rashid na wengine walioingiza nchi kwenye uwekezaji wa kijambazi wasingefanya hivyo; akiwamo Simba aliyekiri na kutubia kwa dhambi hii.

Kinachokera zaidi ni ile hali ya Mkapa kusifia udumavu wake kiutawala akiwatuhumu Watanzania kuwa na uvivu wa kufikiri tofauti naye mwenye uchapakazi wa kufikiri kiasi cha kuiuza nchi ukiachia lile la yeye, mkewe na marafiki zake kujimegea Kiwira. Hawa ndio wasomi na watawala wetu!

Hapa bado huangalia shutuma kuwa pesa ya wizi wa EPA iliyotumika kwenye kampeni na harakati za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuingia madarakani 2005, huku madaktari kama Daudi Ballali, akizidiwa kete na vimada wake na wafanyabiashara na wanasiasa mbumbumbu na matapeli hadi kujiletea mauti kipumbavu.

Kama kweli kuna udumavu wa kiakili kwa Watanzania, je, ni nani wa kulaumiwa kati ya wananchi na watawala wao walioupa mashiko ukoloni na ukale wa kimwazo?

Hebu fikiria. Chini ya Waziri Profesa Jumanne Maghembe, Wizara ya Elimu imedorora kiasi cha kukabiliwa na migogoro ya kiuendeshaji ukianzia kwenye mikopo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, kutolipwa kwa walimu kwa wakati, kughushi na kuvuja kwa mitihani, kuharibiwa mitaala na mengine mengi.

Je, huyu usomi wake uko wapi? Hapa bado hujarejea kwenye uoza aliouacha huko SUA alikochomolewa.

Nadhani. Kwa kuangalia madudu kama haya, wasomi wenye kupigiwa mfano kama Profesa Issa Shivji, wamekataa kujichafua na kujiingiza kwenye siasa za kidumavu na kijambazi.

Tutoe mfano mwingine. Ukilinganisha dhamira na uthubutu vya rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Aman Karume, hasa maghorofa ya Michenzani na waliofuatia, hasa Dk. Salmin Amour, unakosa mantiki ya usomi wetu wa sasa unaoendekeza makaratasi hata kama ni ya kughushi.

Hata ukilinganisha mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Mwalimu Julius Nyerere, ambayo haikuwa na wasomi-bobezi kama zilizofuatia, utagundua: kuwa ilikuwa na mafanikio mara mia ya zote.

Rejea kutolewa elimu na huduma za jamii bure huku kwa sasa vitu hivyo vikibakia kuwa vya wachache wenye pesa itokanayo na ujambazi ima wa kisiasa au kimaadili.

Ni ushahidi wa udumavu wa mawazo kwa hawa waliopata elimu bure kutaka kuifanya biashara kwa kuwakamua maskini waliowatengeneza kwa kusikia kauli ya bwana zao wa Ulaya.

Turejee kwenye wasomi wetu walioko kwenye taaluma. Je, wao wamenusurika na udumavu huu wa kiakili? Nani hajui kuwa wasomi walioko vyuoni wakinoa bongo za wataalamu wa baadaye wanalipwa mshahara kiduchu ikilinganishwa na wanasiasa?

Je, wamefanya nini kujinasua na wizi huu? Je, kwa wao kuridhia kuendelea kunyonywa na kudhalilishwa na wanasiasa si udumavu kimawazo? Maana ukomavu wa kimawazo ni kuliona tatizo na kulipatia ufumbuzi mjarabu.

Imefikia mahali wana taaluma wetu vyuoni wamegeuka watunza nguruwe na bustani ili kukidhi mahitaji yao huku kashfa nyingi za wizi wa mabilioni zikilipotiwa kila uchao wasifanye kitu.

Je, hawa kweli hawajadumaa kiakili? Maana ya usomi ni uasi ulengao kuikomboa jamii kutoka kwenye midomo ya makupe wachache.

Wasomi wasioasi wala kuthubutu kufanya hivyo si wasomi kitu bali makasuku waliokariri nadharia wasizoweza kuziweka kwenye vitendo. Usomi wa namna hii ni hasara.

Leo, eti nchi iliyopata uhuru takriban miongo mitano iliyopita inaagiza wataalamu kutoka ughaibuni! Je, hawa wasomi tunaozalisha kila mwaka wanakwenda wapi au kwanini hawawi wataalamu wetu?

Je, hawa wanaowabagua wasomi wetu kiasi cha kuridhia wageni waje kujichotea mishahara mikubwa si mbumbumbu hata kama ni waheshimiwa na wana shahada kubwa?

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 18, 2009.

Mipasho, vimbwanga na kunga za Idodomya

UNA habari kwamba nilialikwa kigwena zengwe kusuluhisha miparurano baina ya mafisadi fulani na wenzao wanaoingilia ulaji wao? Unaweza kuchukulia huu kama utani. Ni kweli. Nilialikwa ingawa sikutoa pwenti hata moja.

Nilialikwa na rafiki, classmate na mpambanaji mwenzangu, Sam Six ili tuwaumbue mafisidi mbele ya mzee Ruxsa.

Nikiwa nimejificha pembeni tayari kurusha madongo, si yule mwanamke fyatu aitwaye Sofi Yanga akatia mikono michafu desteni na kuamsha kinyaa sina mfano! Hali ilichafuka kiasi cha wabaya wangu kushindwa kunistukia.

Sikujua kuwa alikuwa na lake na yule mama wa chuma aitwaye Anae Machale. Mambo mengine yanaweza hata kuwa wivu au kugombea mabwana.

Kuna viumbe duniani hata wapige miswaki kila nukta si rahisi kuondoa uvundo moyoni na vinywani mwao. Huwezi kuamini. jamaa yangu mkuu ana waimbaji taarabu kwenye kabuneti lake wakiongozwa na chiriku Sofi.

Mara nilisikia wimbo uitwao ‘Fisadi Mwenyewe’ ukitumbuiza. Ulianza kama ifuatavyo:

Nakuonea huruma kiumbe uso haya.
Wasema si mafisidi bibie hauna haya!
Jaribu kwenda kinyume ukumbuke ya nyumayo,
Mbona yote twayajua yalojiri kwa ndoayo.
Kwani bila mfadhili ungeifunga ndoayo?

Kama wewe si fisidi humu wangojeani?
Kama wewe si fisidi kitoe upoteeni.
Usitujazie mbu tukila kwa ulaini.
Kaa kimya ja nune upate mlo laini
Kama wewe si fisidi humu ndani wangojani?

Bibie uache wivu wamuonea Ewassa,
Yeye ni dume la mbegu alochuma siyo sasa,
Uone wake ung’avu alivojaa mipesa,
Acha watu wafaidi sie hatutaki visa.

Shoga siye twala vyetu,
Twavila kivyetu vyetu,
Mnatoka wapi fyatu,
Kuja watukana watu.

Mwawaita mafisadi,
Na mkome nyie fyatu,
Halo halo halo! Na mwakani twala tena.

Akiwa amehanikiza mwimbaji wa taarabu wa kiume aitwaye Makorongo wa kujitoa Muhanga alitia nakshi kwenye beti.

Shutuma zenu ni feki, sisi tutawafichua,
Sisi n-dio breki wengine wajishaua,
Ewassa hana kisiki, na wala hana mawaa,
Ninasema kulaleki, Ewassa bado kifaa
Ambao hamumtaki, jijueni sasa mwafa.

Nacho kile kibabu kiongozi wa mipasho kilitia nakshi zaidi. Kilianza kuimba:

Tatizo sasa ni Six, lazima tutamsix.
Mshakikwaa kisiki, msije kutumix
Sasa nasema si fix, Six tutakufix.
Mwasema tunawahini, ndani mwangoja nini,
Fanya hima kitoeni, aliyewaita nani?

Kabla ya kumaliza, alidakia mwimbaji mkongwe Sam Machale.

Sofi umekumbwa nini? Hebu mama kapimeni.
Najua kinokuhini, Mirembe ujiwahini
Vinginevyo niamini, utaumbuka ugani.

Kabla ya kuendelea, Anae Machale alitumbukiza ubeti wa nasaha. Aliimba hivi:

Alianza kuhanikiza, mwanaketu ni aibu.
Njoo kwangu utubu, mbona unajisulubu,
Heri uwe kama bubu, twayajua maghusubu,
Ulopewa mengi mengi.

Mipasho ilikuwa mirefu kama barabara, ikijaa makubwa kama nyumba. Muhimu ni kwamba jamaa zetu wamefichua maradhi. Kwani wako mahututi ingawa walituaminisha kuwa mambo yao bam bam wakati ni bomu bomu.

Tuliodhani ni simba kumbe mbwa! Waliowahadaa wenzao kuwa watawapeleka Kanani kumbe Kanani yenyewe ni mifukoni mwa mafisadi!

Jambo moja la kuvunja mbavu lilitokea. Eti bwana mmoja mkubwa hivi anataka achunguzwe na mapilato kama yeye si Richamondu au la! Hivi kuna ubishi kama nguruwe ni halali au haramu?

Jaduong Obama alijisemea. Hata apakwe lipstick, shedo avikwe vipuri na majaribosi, nguruwe hataacha kuwa nguruwe.

Bwana huyu anadhani vijipesa vyake haramu vinaweza kumnunua kila mtu. Kama ni mapilato si ukubali upelekwe kwao uone watakavyokusulubu. Jaribu uone janja ya nyani itakavyokwisha baada ya kuonja jiwe ya joto.

Nikiwa nashangaa ya Musa kabla ya kuona ya Firauni mara nikasikia upuuzi mwingine. Yule mwimbaji nyemelezi Makorongo si alitoa mpya! Eti alidai tume iliyomsulubu Rich ni feki.

Ebo! Kama tume ni feki kwanini walioridhia iundwe na kutekeleza mapendekezo yake wasiwe feki? Hapa hakuna kuficha Njaa Kaya ameshindwa vibaya sana. Anapaswa atimuliwe maana naye ni feki.

Huyu bila shaka kama yule muimbaji mwenzake wanatumiwa na majambazi wakubwa ambao wasipofungiwa kule Ukonga au Segerea watakisambaratisha kijiwe kabla ya kuiuza kaya. Wengine wana shida gani iwapo wakikipiga mnada kijiwe hiki watarejea kwao?

Hivi kama yule kibaka mkubwa ambaye babu zake walikuja kufanya biashara ya utumwa wakaloea ana hasara gani hata kama kijiwe kikitupwa motoni?

Ana hasara gani iwapo urithi wa babu zake umetimia? Wao waliwauza babu za walevi tena wajinga; naye anawatumia watumwa tena wanaojiita wasomi ingawa inasemekana usomi wao ni feki.

Kinachosikitisha ni kuona na ndugu zangu wa kizaramizi, kikwerere na likawaga nao wameingizwa na kutumiwa kinyume nyume! Huko nyuma hawakuwa hivyo. Je, huu si uchangudoa ingawa wanajiona wajanja?

Heri watumwa wa enzi zile waliuzwa kwa nguvu na hawakuwa wakiitwa wasomi, waheshimiwa wala hawakughushi vyeti kuliko hawa wa hiari ambao ni dhalili kuliko hata mbwa na panya walao mabaki.

Mtumwa wa hiari ni mbaya kuliko hata jambazi mwenyewe. Kwani, kama kijiko anaweza kutumiwa na yeyote kuchota chochote. Kama bomu anaweza kutumika kujiangamiza hata yeye mwenyewe.

Wale ndugu zangu waathirika wa Mbagala, ninaposema bomu, wanajua nimaanishacho. Sijui katika upuuzi huu kuna mtu anawakumbuka kujua kuna watoto na vikongwe wanasota kulala nje wasijue watakula nini!

Juzi nilisikia wasanii fulani wakitumbuiza wimbo wa Kilimo Kwanza! Nani anataka kulima? Nani punda apende kulima? Siku hizi hakuna cha kulima kwanza wala nini bali mipasho.

Nani alime wakati unaweza ukachora mchoro ukaenda pale Bunch of Tembo (BoT) ukakwapua mabilioni na kuitwa mfanyabiashara maarufu, mfadhili na upuuzi mwingine? Kwanini kufikiria kulima wakati Ze Komedi ya siasa inalipa kuliko hata mihadarati?

Nani alime kwanza kabla ya kuiba kwanza au kula kwanza? Mie kijiweni kwangu nawambia ukweli. Kilimo mwisho na usanii kwanza.

Huwezi kulima wakati uchuuzi wa roho na rasilimali unalipa kuliko kitu chochote. Utakuwa mpumbavu na mwendawazimu. Na ni hatari kuwa mpumbavu na mwendawazimu mtawaliwa.

Utakuwa huna maana kabisa sawa na wana mipasho vigogo wanaovuana nguo hadharani tena mchana mbele ya watoto. Na huu ni mwanzo. Unacheza na laana hasa laana yenyewe inapokuwa ya marehemu?

Waulize wasaliti wakuu kina Yuda. Wafaransa wana methali moja tamu isemayo: A barbe de fol le rasoir est mol. Waingereza husema: A foole brookes any disgrace; A foole's not sensible of any wrong.

Naona gari la mama fyatu linakuja ngoja niishie kabla hajaniingiza kwenye uchafu wake.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 18, 2009.

Nani ataokoa Kikwete?

UKIANGALIA jinsi mambo yanavyokwenda, utaona kama vile Rais Jakaya Kikwete hajali kutumbikiza serikali yake katika kashfa.

Angalia jinsi watendaji wa serikali wanavyotafuta kila njia kuokoa watuhumiwa wa ufisadi na kujiokoa wao wenyewe. Angalia jinsi ambavyo serikali ilivyobeba kampuni tata ya kufua umeme kati ya serikali na kampuni ya Richmond Development Company (LLC) ya Marekani.

Angalia jinsi serikali inavyoshindwa kushughulikia ufisadi uliofanywa na kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, iliyochotewa na serikali na washirika wake mabilioni ya shilingi miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Hata pale wakili wa Mahakama Kuu, Byidinka Michael Sanze aliponukuliwa katika hati yake ya kiapo, kwamba Rostam ndiye aliyemtaka kushuhudia hati za mikataba ya Kagoda, Kikwete ameshindwa kuchukulia hatua madai hayo.

Kampuni ya Kagoda ilichota zaidi ya Sh. 40 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Hii inaonyesha kwamba taifa hili limekumbwa na gonjwa hatari la wakubwa kuonea wadogo katika karibu kila mahali.

Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU inasifika kwa kuwaandama wafanyakazi wa kada ya chini, hasa polisi, mahakimu wa mahakama za mwanzo, walimu, manesi na wengine.

Tuhuma hizo tayari zimefanya baadhi ya wanachi kuona kuwa taasisi yao hiyo nyeti, inatumiwa na wakubwa kulinda watuhumiwa na kutisha wale wanaothubutu kufichua maovu.

Na kwamba Takukuru kama ilivyotaasisi nyingine za umma, mkurugenzi wake anateuliwa na rais, na kwamba ni rais mwenye uwezo wa kumfuta kazi.

Acha hilo. Angalia hili la mgawo wa umeme. Rais haonekani kulishughulikia kikamilifu. Amesahau kuwa “Maisha Bora kwa kila Mtanzania” hayawezi kupatikana kama nchi yote itakuwa gizani kila siku na kwa wakati mmoja.

Maisha bora yatapatikana iwapo taifa litakuwa na nishati hiyo muhimu kwa uchumi na maisha ya kila siku ya mwanadamu.

Ni aibu kwa mfano, nchi ndogo kama Uganda yenye raslimali na vyanzo vidogo vya maji kuuuzia umeme Tanzania.

Kama kuna nchi ilipaswa kuwa na mgao wa umeme kama kweli tatizo lingekuwa ni upungufu wa maji, basi ni Kenya. Lakini wakati tukiishi kama bundi kwenye giza wenzetu wa Kenya wanatucheka hadi kutukumbusha la kufanya kwa kutoa vibonzo vyenye manufaa kwetu.

Lakini achana na hilo. Angalia hili lililoibuka sasa ambapo baadhi ya mawaziri wa serikali ya Kikwete wanatuhumiwa kughushi vyeti vya taaluma.

Kisheria, kujitambulisha tofauti na ulivyo ni kosa la jinai. Hata kuwasilisha hati za kughushi kwa mamlaka yeyote ni kosa kisheria ukiachia mbali kujipatia marupurupu na mshahara kwa kazi ambayo huna ujuzi wala sifa nazo.

Hapa tutaambiwa ubunge si kazi ya kusomea. Je kuwadanganya wananchi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na taifa kwa ujumla na kujipatia mshahara kutokana na sifa usizokuwa nazo si kosa?

Hili la kugushi vyeti lilianzia kwa mbunge wa Bushosa, Samwel Chitalilo (CCM). Chitalilo anatuhumiwa kughushi vyeti na kuwadanganya wapiga kura kama ilivyothibitishwa na Jeshi la Polisi.

Kinachokera ni Chitalilo kujifedhehesha kama mbunge, ukiachia mbali wapigakura wa Buchosa.

Tuhuma za Chitalilo ziliibuliwa na mshindani wake wa kisiasa ndani ya chama chake. Huyu ndiye aliyekusanya nyaraka na kuziwasilisha kwenye vyombo vya dola.

Hata hivyo, pamoja na ushahidi wote uliokusanywa, Chitalilo hajawahi kuonywa wala kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Badala yake, Rais Kikwete alisikika akiwa akiwa jimboni Bushosa akisema, “kelele za wapangaji haziwezi kumnyima usingizi mwenye nyumba.”

Hivyo, kutokana na uzito wa rais na mwenyekiti wa chama kesi iliishia hapo. Ajabu, umma wa Watanzania haukuchukua hatua kumshinikiza rais kuomba msamaha kwa kushiriki jinai ukiachia mbali kutochukua hatua kama mwenyekiti wa CCM – chama ambacho Chitalilo anatoka.

Tufike mahali tumkabili rais bila woga. Kashfa dhidi ya serikali yake na chama chake zimezidi. Rais amekaa kimya na anaonekana hataki kuchukua hatua.

Sasa mawaziri sita wanatuhumiwa kughushi vyeti na sifa hasa za shahada ya uzamivu ya falsafa (Ph.D), wakati hawajawahi kusomea shahada hizio. Lakini rais haonekani kuguswa na jambo hilo.

Je, taifa linaweza kupata maendeleo wakati linaongozwa na watu walioghushi au matapeli huku mamlaka za juu katika nchi zikiwa zimenyamaza bila sababu? Katika mazingira haya serikali itawezaje kutimiza ndoto ya kuwapa Watanzania “Maisha Bora?”

Tayari madai mapya yameibuka na rais haonekani kuyashunghulikia. Kwamba hatua ya mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hoseah kutaka kuhoji wabunge kwa kile kinachodaiwa kuwa wanalipwa posho mbili kwa wakati mmoja, “kumelenga kuwanyamazisha wawakilishi hao wa wananchi.”

Kama alivyosema Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta, kama akili ikitumika vizuri, tukalinganisha hujuma na hasara zitokanazo na Richmond na EPA, wabunge kupokea posho mbili ni sawa na kulinganisha kichuguu na mlima.

Sasa swali la kujiuliza: Kwa nini rais ameamua kukaa kimya ilhali mwakani kuna uchaguzi? Je, anataka kusema kwamba kuendelea kunyamazia tuhuma hizi ndiyo njia sahihi kuliko kukemea au kuchukulia hatua wahusika.

Rais na serikali yake haoni kuwa hatua ya kukalia kimya tuhuma hizi kutatoa nafasi kwa viongozi wa vyama vya upinzani kuendeleza madai yao ya siku zote kuwa serikali hii ni mama wa ufisadi?

Tumeona jinsi serikali ilivyofikisha haraka mahakamani wanafunzi waliotuhumiwa kughushi vyeti. Tumeona jinsi wafanyakazi wa ngazi ya chini wa BoT walivyoburuzwa mahakamani kwa tuhuma kama hizo pia.

Lakini linapokuja suala kama hili kugusa wakubwa, tumeshuhudia vyombo vya dola na serikali kwa jumla ikishindwa kufumbua mdomo.

Ni lazima serikali itambue kuwa hii si nchi ya mabwege kama alivyosema Dk. Harrison Mwakeyembe, na isitoshe mambo yamebadilika sana.

Tuhitimishe kwa kushauri serikali kuweka nukta kwenye aibu inayosababishiwa na watendaji wake kwa bahati mbaya baada ya kumdanganya rais kuwa huku nje mambo yanakwenda vema.

Chanzo: Mwanahalisi Toleo Namba 161.

Wednesday 11 November 2009

Africa's Democracy a Mockery!





Zine El Abidine Ben with supporters Photo courtesy







AU has lost its relevance and credibility. I came to this conclusion after the conspiracy in Zimbabwe, Uganda, Rwanda, Senegal and Niger where rulers tampered with their countries’ respective constitutions to remain in power. Sadly though, they got away with it. with the stamp of AU.

AU messed in Kenya and Madagascar- not to mention Darfur in Sudan where it openly backs the butcher of Sudan Omar Hassan Bashir (a black slave that calls himself an Arab). AU’s recent nod to charade elections in Tunisia proves how more moribund, irrelevant this club for African leaders is. BBC quoted the head of the African Union observer delegation, Benjamin Boungolous as saying that this (abuse to democracy) was free and fair.

How can elections be free and fair when the ‘winner’ has been in power for over two decades? How can Zine El Abidine Ben Ali, who came to power by means of a coup secure such a landslide- ninety per cent victory ?

This is Ben Ali’s fifth “win”! How can it be

free and fair as the opposition cry foul? This time the winning margin has gone down by five percent. Official figures say 84% of the country's voters turned out for the presidential and legislative polls.

While AU was extolling the elections, Ahmed Ibrahim of the Ettajdid (Renewal) Party, also a presidential candidate, was quoted as saying: "The government is preventing me from getting public platforms to speak to my supporters. The state TV changed my air time slot… they're trying to censor my election statement."

African dictators and winos in power have been fooling the world. Firstly, they convene elections themselves. Secondly, the so-called civilized world recognizes them just because their interests are protected by those potentates. This is the miracle by which dictators in Angola, Cameroon, DRC, Equatorial Guinea, Ethiopia, Gabon, Kenya, Rwanda, and Uganda and elsewhere in Africa survive the wrath of the people.

While this macabre act was unfolding, another dictator in Niger, Mamadou Tandja ‘won’ elections which by AU’s standards were ‘free and fair.’ The same AU did not say anything when the son of a dictator, Ali Ben Bongo in Gabon was declared winner after fixed elections! Who would point a finger whilst almost all African potentates are the products of the same dirty game? If Mandela were still in power, he’d have said something.

Many thought Africa and AU would come of age especially in the 21st century. But nay! The same rudimentary methods former dictators used in the 60 and 70s used are still at work! Africa is sinking deeper as time goes by. The modern dictators spend much more money on their survival than the past ones thanks to the Non Governmental Organization and disgruntled population that give them a heck. Even butchering opposition has slightly dwindled thanks to globalization.

Apart from forming bigger governments consisting of their cronies, they spend big chunks of their budgetary money on private armies. To get away with it, the military budget in Africa is still a ‘top national security secret’ as they call it. The current arch foe-cum-threat for Africa is nothing but her gluttonous rulers and their cronies who steal more many than they offer to social services.

Given that dictatorship helps producing countries to do business, it has become difficult for democracy to thrive in Africa. The world is now blaming Hutus in Rwanda for committing genocide. But the same chameleon-like world does not blame Belgium racists who sired the seed of hatred between the Hutus and Tutsi. It does not want even to turn all stones so as to accuse the current regime that started the same!

Shamelessly, the same hate-planters are blaming Africans for being inhuman! What of missionaries, explorers, merchants, administrators with their hickory dickory dock when paving way for colonialism? Some Western self-declared experts on Africa are saying that we should forget attrocities inflicted upon us by foreigners. How can we do this without being redressed? If Jews can nary forget the holocaust, why should Africa easily and blindly forget her holocaust? Wasn’t slavery worse than the Jewish holocaust?

Africa is accused of tribal wars as if she espoused the whole concept of tribalism! Tribalism is all over the world. If you go to the real meaning of tribe, all those groups you see fighting today are tribes. Al-Qaeda is a tribe. Protestants and Anglicans in Ireland are tribes. So you can choose the way you translate this concept. But when it comes to Africa, it is used with bad connotation just like being black.

Going back to democracy, Africa is hampered by the tribe of dictators and their western allies. Donors and investors are a tribe. Look at how they shuffled a mule-like government in Kenya or a surrogate one in Zimbabwe after noting that their interests were endangered. This new tribe is destroying democracy in Africa. The winner and loser end up becoming winners and cobble a carbuncular government. It recently came to light that most of Kenyan’s ambassadors and high commissioners abroad are related to top government officials. In this feat-cum-nepotism, merit does not add up except blood and political connection. Everybody strives to have his people in power in order to do his show.

Source: The African Executive Magazine Nov. 11, 2009.

Rites na serikali, uwekezaji au ujambazi?

HABARI zilizofichuka hivi karibuni baada ya Mkurungenzi Mkuu wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), Hundi Chaudhary, kuilima barua serikali akiandaa mazingira ya kuvunja mkataba ili waondoke na pesa zetu, haziwezi kupita bila kujadiliwa.

Umma wa Watanzania umeshangaa kusikia aliyosema Chaudhary hasa mazingira na masharti ya mkataba wa uwekezaji ambao kimsingi, si uwekezaji kitu bali ujambazi na uchukuaji wa mchana. Sitaki niongeze kitu.

Mkurugenzi huyu wa TRL inayomilikiwa kwa ubia baina ya serikali na kampuni ya Rites ya India, alionekana akiihimiza serikali itoe pesa ya kuiwezesha TRL kuanza kufanya kazi.

Wengi wanashangaa ni mwekezaji gani anategemea mtaji kutoka kwa serikali ya nchi anayowekeza wakati tuliambiwa: kigezo kikubwa cha mtu kuwekeza ni kwa anayewekeza kuwa na mtaji wa kutosha kuwekeza?

Hebu soma maneno ya Chaudhary hapa: “Serikali kwa kutumia kampuni ya Rahco iliyopewa jukumu la kusimamia mali za lililokuwa Shirika la Reli (TRC), inapaswa kutoa fedha za kusaidia mpango mkakati wa biashara kama ilivyowasilishwa na TRL”.

Bila aibu wala kuficha, Chaudhary anaendelea kuvujisha uoza wa ajabu. Haijulikani kama alijua hatari ya kufanya hivyo au ameamua kumwaga mboga au kuanza kumwaga mtama ili serikali izindukane kwa kuchelea hasira za umma.

Chaudhary alikaririwa akisema: “Fedha nyingine zenye thamani ya dola za Marekani milioni 115 na deni lenye thamani kati ya dola milioni 226 na 300 ambazo serikali ilipaswa kuzitoa kwa ajili ya mtaji katika kampuni hiyo, lakini hadi sasa hazijatolewa.”

Hebu zingatia maneno: ‘Kwa ajili ya mtaji.’ Jiulize mantiki na sababu ya mgeni kuaminiwa, kwanza kufanya biashara nchini na pili kupewa mtaji wa pesa ya wavuja jasho maskini ni nini kama si upunguani, ujambazi na ufisadi? Je, hii ni dharau kiasi gani kwa mwananchi anayehenyeshwa na umaskini wa kutengenezwa?

Kwanini serikali itoe mtaji tena kwa kampuni ya kigeni? Ilikuwaje kampuni lisilo na mtaji tena la kigeni kuaminiwa na serikali bila kuwapo mazingira ya rushwa hata wahusika kuwa mawakala wa mafisadi ninaoamini kwamba wamo madarakani?

Hivi tukisema kuwa licha ya kushindwa huku kwa serikali ya sasa ni ufisadi uliokithiri, tutaambiwa tunaiandama serikali! Je, kwa ushahidi utokanao na mkataba huu mmoja, ukiachia mingine mingi, hautoshi kuwaambia Watanzania kuwa serikali yao ndicho chanzo cha ujambazi na ufisadi unaoendelea?

Je, hawa walioingia mkataba wa kijinga kama hawa, kweli wanaweza kujiita wasomi au ndiyo wale wanaoshutumiwa kughushi ingawa hawajatajwa wote?

Hebu angalia uoza mwingine kwa mujibu wa Chaudhary: “Serikali imeshindwa kulipa kiasi cha dola milioni 0.2 ambazo ni malipo ya mwaka ambayo TRL inapaswa kuilipa Mamlaka ya Kudhibiti Usafiri wa Majini na nchi Kavu (Sumatra ).”

Hata kodi ndogo, TRL inaibebesha mzigo serikali tu? Je, serikali iliposema inajitoa kwenye biashara ilimaanisha kurejea kwa mlango wa nyuma kufanya hivi inaotuaminisha ni uwekezaji wakati ni uchukuaji na ujambazi wa mchana?

Huyu mbia anachangia nini zaidi ya kuhamisha pesa zetu baada ya kuwapa mafisadi asilimia kumi yao? Anayeona tunaishambulia serikali, anisaidie aandike makala au atoe maelezo yanayoweza kumshawishi mtu yeyote kama huu si wizi unaofanya na serikali.

Kama kodi ya Sumatra, yaani dola laki mbili TRL inaitegemea serikali, je hizi kodi za kawaida za mapato, uingizaji wa vifaa na mambo mengine yanayopaswa kukatwa kodi zinaishia wapi kama si serikali na uoza huu kujisamehe huku wananchi maskini wakizidi kunyimwa usingizi ili walipe kodi ya kuwapa wawekezaji uchwara?

Jibu la hili limo kwenye taarifa iliyofichua uoza huu. Kwani ilitaja maeneo mengine ambayo serikali ilipaswa kutekeleza kwa mujibu wa mkataba wao ni pamoja na serikali kusaidia katika malipo ya kodi zote kama ilivyo elekezwa kwenye mkataba wao.

Je, mambo kama haya hayamwaniki Rais Jakaya Kikwete, anayejipiga kifua kuwa ataleta maisha bora kwa wote ilhali muda unamtupa mkono na uoza wa serikali yake ukizidi kufichuka?

Je, hapa itakuwa vibaya kuwambia wapiga kura kwamba wakati wa kuking’oa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM) umefika? Maana licha ya kushindwa kutimiza ahadi zake, kimeongeza sifa nyingine ya kushiriki ufisadi kwa kuibia mabenki yetu hadi kuzitoa kafara mali za taifa letu.

Si matusi kusema serikali yetu ni taahira. Hebu soma maneno ya Chaudhary, akiitishia na kuiamuru serikali ituibie. Anasema: “Tumelazimika kuandika barua hii baada ya kubaini kwamba serikali imekiuka mkataba wetu na endapo hayatatimizwa ndani ya siku 60 ninaweza kuvunja mkataba huo ama kuongeza muda, hivyo tusubiri siku 60 zimalizike.”

Jeuri hii Chaudhary anaipata wapi? Je, haina maana kuwa kulingana na kupindisha sheria na kuridhia upuuzi, kuna vifungu ambavyo Rites inaweza kuvitumia kuifikisha serikali mahakamani na kulipwa fidia nono?

Je, ni vibaya kusema kuwa ‘wataalamu’ mbwa mwitu walioridhia upuuzi huu walijua fika kuwa kama hili litafanyika, watapata mwanya mwingine wa kuliibia taifa na kuambulia asilimia 10 yao?

Je, hawa si wabaya wastahilio kupigwa mawe kuliko vibaka tunaowaua kila siku kwa wizi wa kuku na mabeseni? Je, ni vibaya kusema kuwa Tanzania sasa imani hakuna ama ni kichwa cha mwendawazimu?

Je, huu ndio utawala bora unaowaneemesha wezi wa kigeni kwa kuwatoa wananchi kafara na mali zao? Ningependa kusikia mama utawala bora Sophia Simba, akitoa utetezi wake kuwa serikali yake inaandamwa kwa chuki na uroho wa madaraka.

Bila kusema mengi, ni kwamba kama kuna eneo kuna ufisadi unaonuka, unaowahusisha watawala wetu, si jingine bali uwekezaji ambao kimsingi ni ujambazi wa mchana unaofanywa na wale tuliofanya makosa kuwapa dhamana ya madaraka.

Je, kinachoendelea baina ya serikali na Rites si ujambazi wa mchana? Je, serikali inayofanya ujambazi inayoupamba kuwa ni uwekezaji inapaswa kuendelea kuwa madarakani?

Ili ifanye nini zaidi ya kuuza nchi na watu wake? Ningekuwa naombwa ushauri, ningependekeza tubinafsishe Ikulu kwanza, mengine yafuate. Maana imekuwa muhuri mkuu wa ufisadi na ujambazi huu ingawa haitaki kukiri hivyo.

Rais wetu kama hataingilia kati, hali itazidi kuwa mbaya kiuchumi. Nakuomba Rais Kikwete litizame kwa makini suala la mkataba k ati ya Tanzania na Rites. Kazi kwa wenye nchi ambao wamegeuzwa wapangaji na wakimbizi kwenye nchi yao wenyewe.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 11, 2009.

Friday 6 November 2009

Mie sikughushi, nichagueni mwakani jamani

NAITWA Mpayukaji Msemahovyo PhD (Economics) PhD (Abracadabra and Hoaxes) Masters (Lies and faking) Masters (Corruption and Bribing) Advanced Dip (EPA and Richmond), BA (Performance and Ngonjera) etc.

Kumbuka, tuna uchaguzi karibuni kwenye kaya ya Waliwa Wadanganyika. Hivyo, naanza kupiga kampeni hata kama tume haijatangaza hivyo.

Ukizingatia huu ni msimu wa kuvuna ambacho hukupanda kupitia kura ya kula, nimejiandaa kuwatumikia wanakaya. Hata kama sistahiki heshima, bado nimekamia kuitwa Mheshimiwa Mchumiatumbo. Siwezi kuacha ulaji huu wa bure upite iwapo matapeli wengine wanaweza kuufaidi kwa kutoa kila ahadi za uongo.

Nimeishaweka mikakati. Kwanza, nimeishajipatia shahada saba toka vyuo vifuatayo: Commonwealth Nonexistent University, Havazard, and Edenbug, Quacks’ Open University of the World (QOUW), New York na Make-believe University, Bangalore, India.

Kadhalika nimeishaongea na jamaa zangu (mnaowaita mafisadi) wa Kimanga na Kigabacholi kuchangia kampeni zangu ili nikishaupata uheshimiwa nihakikishe wanawekeza nchini.

Kwa vile nitakuwa mtunga sheria, tutatunga sheria za kuwapendelea kuwekeza na kujimegea neema mnazoita kutorosha mitaji.

Nitaanza na kuchangia miradi ya kinamama na vijana na baadhi ya shule kwenye jimbo langu. Yule rafiki yangu Sheikh Brigedia Ally atamwaga pesa kama hana akili nzuri kuwahonga wanakamati ya uteuzi wa wagombea chamani. Kwa dola 5,000 kila kichwa najua hakuna atakayeruka.

Sikutajwa kwenye EPA, Richmond, Meremeta, Kagoda na ujambazi mwingine. Hata kama nilipata mgawo wangu, inakuhusu nini? We usomaye waraka huu usimwambie mtu. Soma kimya kimya. Kwa taarifa yako, EPA yangu itatumika kuwalainisha walevi na wake zao kwa khanga, T-shirts, nyama choma na upuuzi mwingine. Ila kumbuka. Mimi si papa wala nyangumi. Ni safi kama Enderea Changa, Ewassa Eddie nk.

Kadhalika, nimeishapata makanjanja wenye njaa kama fisi kulipamba jina langu kwenye magazeti yao. Kaulimbiu yangu ni: ‘Mchague mkombozi chaguo la Mungu awavushe kwenda Kanani nchi ya mvinyo na nyama choma’.

Mimi si kihiyo. Pamoja na kutumia karne nyingi bila kuingia kwenye hekalu la Mungu, nimeishajiunga na baadhi ya makanisa na misikiti tayari kunipigia upatu. Kitaalamu naitwa Swindler Conman, PhD Phil, MA (Abracadabra and Hypothetical Thinking), BSc (Lies), Dip (Corruption and Mafia), Masters (Public funds Terrorizing), MBA, Masters (Money-making and Forgeries), etc. Watani wananikejeli eti ni mbunge wa tumbo. Mimi ni mzalendo wa kupigiwa mfano.

Shahada zangu zinahitaji mtu mwenye kichwa kinachochemka ambaye Waingereza humuita genius, hasa zile za MA in Lies and Hypocritical Thinking. Ni wachache waliweza kuzipata kama vile Tunituni, Dany kurap Hoi na wengine kama Bob Mugambe, Jack Zumari, Joweri Msaba na Yahya Jammeh.

Unajua? Mipango yangu ni mikubwa kuliko mlima. Hebu fikiria; nawatwanga Wadanganyika kwa kaulimbinu ya pili isemayo ‘nguvu mpya, mipango mipya uzalendo na mwanzo mpya’. Hakika walevi wataniamini kwa maangamizi yao baadaye.

Kwa kuanzia, nitakunywa nao bila kuwabagua ingawa ni wachafu. Nikisalimiana nao nitawataja majina wajue nawajua na kuwamaindi ingawa zote kamba tupu. Sitasahau kuwakumbatia huku nikikenua kama vile nawapenda. Pia nitahakikisha shangingi langu la VX linageuka daladala ya walevi. Nitawapeleka popote watakapo huku mke wangu akitumia NGO yake kugawa rushwa kwa njia ya misaada kwa akina mama na shule za misingi na sekondari kaya nzima.

Atawafunga kamba akina mama kuwa nikishinda atahakikisha akina baba wanapiga deki na kuosha watoto bila kusahau kuwavisha magagulo huku akina mama wakirejea usiku wa manane wakitoka kufaidi uhuru mpya.

Pia nitaanzisha mfuko wa kusaidia jamii uitwao “Swindler’s Anthropological Society of Thoughts” (SAST) ili kupigania haki za viumbe wote kuanzia mapapa, nyangumi, fisi, mafisadi, vikongwe na albino. Nitaitisha mikutano ya harambee kuchangia wagonjwa na mashule jimboni mwangu. Hapa nitanunua vyandurua 500 kwa ajili ya zahanati jimboni na madawati 200 kwa ajili ya shule za misingi. Pia nitanunua mipira na jezi kidogo huku nikivaa moja na kucheza kabumbu na vijana wa vijiweni wajue mimi ni mwenzao. Ingawa huwa nawaogopa kama ukimwi, mara hii nitakula boli nao huku msaa wangu wa Rolex wa bei mbaya nikiuacha hom maana wanaweza kuunywa wezi hawa wa kutengenezwa nasi.

Kumbuka, nimeishawaweka sawa wazee wa kabila letu kwa kumpa chochote kitu kiongozi wao. Usishangae kuniona nimevalia mavazi ya kiasili nikitawazwa kuwa kamanda wa vijana wa wilaya wa chama changu.

‘Nyumba yangu ndogo’ niliyozaa nayo toto la kiume na kulikana, nitairejea kwa haraka sana ili asitoboe siri zangu. Mwanaharamu wangu huyu atageuka ghafla kuwa mtoto wangu kipenzi na nitamuahidi mama yake kuwa nitampeleka sekondari nchini Uingereza. Kumuweka sawa kwanza, nitatafuta shule moja ya kimataifa ya uongo na ukweli nikifanya maandalizi ya kumrusha majuu. Nitamfunga kamba kuwa namuandaa awe rais wa nchi baadaye.

Wafa na nguna wajinga nitawaahidi kupigania bei za mazao yao. Hapa lazima nikope ujanja toka kwa Mheshimiwa Mizengwe. Nitaahidi trekta kila kijiji bila kusahau maji safi na umeme usiokuwa wa mgawo. Hapa Mwarabu wangu wa Dubai atanipiga tafu. Kuwaua kabisa, nitaalika wanafunzi wa chuo cha maji kuja kufanya tathmini ya mradi wa maji na umeme kwa vijiji vya jimbo langu.

Mbinu nyingine ni kumtetea mwenyekiti wa taifa wa chama changu cha UNM, yaani Ugali Nyama na Maharagwe kwa kila upuuzi atakaofanya. Nimeishatishia na kuapa kwa miungu yote kumnyotoa roho yeyote atakayempinga. Huwa naapa kwa kupandisha mwenembago kama morani wa Kimasai niapapo kwa miungu yote ya uongo na ukweli.

Wengi watadhani naota. Lazima niingie bungeni. Kwanza mie ni handisamu kama Njaa Kaya. Isitoshe ni kijana kinda wa miaka 59 ambaye hutabasamu hata kwenye msiba. Pili, mimi ni chaguo la Godi. Tatu ni mtaalamu wa sanaa hasa lugha tamu yenye kupumbaza na ahadi kem kem. Nne ni mtu wa watu. (Usiulize kama kuna mtu wa fisi). Tano nimeleta amani kwenye kijiwe na mifuko ya wapiga kura.

Nina sifa zaidi ya elfu na moja. Hivyo leo nakumegea. Inshallah nategemea kuelezea sera zangu huko tuendako, hasa jinsi ya kupambana na wizi wa kura na migawo ya umeme hewa na maji. Nitahakikisha natetea haki za wanyonge, hasa kwenye wizi huu uitwao multiparty hoax - samahani siasa za vyama vingi. Pia zingatia. Mbinu zangu ni mpya na hazijawahi kubuniwa wala kutumiwa na mtu yeyote isipokuwa mimi tu. Niachie hapa niende kuandaa nyavu za kuwanasa wajinga. Kaa chonjo saa mbaya! Wajinga ndio waliwao.

Khalas Kweisine

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 11, 2009.

Wednesday 4 November 2009

Dead Aid or Wrong Approach?




The good analysis by Helmut Danner on Dambisa Moyo’s book can not pass unapplauded. It was nice and educative so to speak. I am not going to revisit the same, thanks to the good tour Danner did.

Dambisa’s book “Dead Aid or Wrong Approach?” against the odds, is the recent work from Africa that positively captivated the world. Though the idea is not new, it adds up.In a nutshell, let me add a few points. Much of the moneys offered as aid are squandered by rulers.

Donors’ money is either used to do globe trotting or is used to convene pantomime elections that scoop a lot more money. When ‘winners’ are declared, they steal, abuse office and consent to exploitative and misleading policies that enable western companies to rob Africa of her wealth. It recently came to light that mining companies in Tanzania give not only give false information with regards to the amount of minerals they dig, but also cause a great environmental abuse. If such offences were committed in the developed world, the perpetrators would end up becoming bankrupt and their contracts revoked.

Any African will tell you that aid is meant for rulers and if it is stopped, only rulers will be in trouble. Take, for example, the money that is channeled into supporting the budgets of African countries and compare it to the expenditure of the same as opposed to development programmes. You will see the rationale. Budgetary support money ends up being abused by rulers. They use it to pay their private armies and party carders in order to remain in power (not to mention their gargantuan governments made of their cronies and relatives). This is why the budgets of the ministries of defence have been dubiously kept a top secret in Africa.

In 2005, Tanzania Central Bank was robbed by the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) at the tune of over $ 500,000,000. This is a huge amount for a poor country like Tanzania. The money was spent on bribing voters. Although evidence has been adduced to this effect, donors have turned a blind eye given the current regime, as the former one, allowed Western companies to massively steal minerals and land lucrative tenders. The same donors offered money for the charade elections.

When it comes to the loans they extend to poor countries, the common man in the street pays them in future as he is forced to droopingly bow before robbery as we see in investment in Tanzania currently where much wealth is robbed as the citizenry cascade into abject poverty.

What’s more, aid money is given by the left hand but it ends up being snatched by the right one! To muse on this, try to imagine how bigger and extravagant governments- in Africa compared to donor countries- are. Refer to the sacrilege that came to light recently whereby in Kenya, most ambassadors and high commissioners are kins of a ruling kit and caboodle.

Aid has neither solved Africa's problems nor spurred expected development levels as Moyo observes. This can be easily seen on how the recipients have become chronic beggars and dependent. In fact, much of the money is stolen by thievish rulers to end up being stashed in Western banks. Refer to Mobutu Seseseko, Sani Abacha and Nigeria respectively.

The other venue that used to be effective and reliable as far as utilizing aid is concerned was by the way of channeling it through Non Governmental Organisations. But recently things have changed. Government agents have invaded NGOs and are getting away with it. Imagine. What is an NGO manned by the first lady for if not to scoop this generously given money? Sadly, donors favour these NGOs in order to entice and induce the big man in the state house. This is the breeding ground for corruption. Why should a president’s spouse form NGOs only after her hubby ascends to power?

I fully concur with Moyo when she says that free market based on socialist values is the way forward. Such a proposal needs courage of the mad at this time where capitalism is everything. Was it admitted due to the shake up that resulted from the global credit crunch? Is it welcome simply because the world now needs more cash than democracy? This is when China comes in.

Though we’re told currently that we are under globalization and free market, this concept is a hoax and the beneficiaries are but Western countries whilst Africans lose.Terms of trade are not uniform. Again that’s where China makes more sense to do business- despite its hidden repercussions in the long run. Given that it is geared by profit, China may turn out to be as destructive and exploitative as the West is. How one is going to avert this depends on how one utilizes this competition between West and China.

One thing that demeans China’s reputation is its fake and substandard products. China, like India, exports its people to plunder other countries and sends back home the loot. Currently in Angola and Tanzania, Chinese are doing businesses that are supposed to be done by locals.

Source: The African Executive Magazine Nov. 4, 2009.

Hoseah anapata wapi jeuri hii?


UZOEFU unaonyesha kuwa ving’ang’anizi wanapobanwa huapia miungu yote kuwa hawatajiuzulu kama ilivyotokea kwa Mkurungenzi wa Tume ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah.

Ila mwisho wa siku, ving’ang’anizi hawa kwa nyonde nyonde na aibu, hubwaga manyanga na kutoweka. Tuliyasikia na kuyaona kama haya kwa Nazir Karamagi, alipokumbwa na kashfa ya Richmond mwaka jana bila kusahau kina Basil Mramba na wenzake.

Nchini Kenya, Aaron Ringera, aliyekuwa mkuu wa Tume ya kupambana na ufisadi ya Kenya (KACC) alisema kama alivyosema Hoseah hivi karibuni akiwatolea nyodo wabunge wa Kenya.

Wabunge hawa mahiri, katika kumwaga mboga, walimtaka Rais Mwai Kibaki kuchagua; aondoke yeye au mtu wake. Na mwisho wa yote Ringera amebakia katika historia.

Hivi karibuni Hoseah alikaririwa akisema: “Sasa nakwambia, sina mpango wa kujiuzulu, siwezi kujitia kamba eti ili nionekane mzalendo bila kosa, kwanini unataka nijiuzulu au unataka kuchukua nafasi yangu?”

Bahati mbaya, hakueleza ni mbunge au wabunge ama watu au mtu gani anainyemelea nafasi yake. Kwanza, ile nafasi si yake, bali ya umma ambao ndio wenye ofisi. Inapofikia mtu anaanza kuifanya ofisi ya umma kuwa mali yake binafsi, ujue kuna tatizo.

Wengi wanajiuliza mantiki ya Rais Jakaya Kikwete kuonekana kupwaya hasa wanapotajwa wateule wake wenye madoa. Inasikitisha na kukatisha tamaa. Kwani hii si mara ya kwanza kwa Kikwete kugwaya kumfukuza mteule wake alipotuhumiwa.

Mkakati usiozaa matunda unaoendelea wa kuwasafisha, kwa mara nyingine, watuhumiwa wa kashfa ya Richmond unaofanywa na serikali kwa Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ni ushahidi tosha kuwa TAKUKURU hata serikali hawafai. Wanafanya ‘utoto’ usiolingana na hadhi wala umri wao.

Katika kikao cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma, kuna kila sababu za serikali kutaka kuizima kashfa ya Richmond hata kwa kuwatisha, kuwadhalilisha na kuwanyamazisha wabunge.

TAKUKURU na serikali, kwa makusudi mazima na nia ya kutenda jinai tena, wanataka kuwasafisha watuhumiwa wa Richmond iliyomwondoa madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, mwanzoni mwa Februari mwaka jana.

Mpaka anastaafu, mwanasheria aliyeondoka Johnson Mwanyika, alionekana kuwa mwamba na mbabe mbele ya rais, wananchi hata wabunge. Je, ni kwanini inakuwa hivi?

Je, hawa wateule wa rais wanaozidi kumdhalilisha na kumuumbua wanapata wapi jeuri hii? Je, kuna kitu wanakijua hasa kuhusiana na kashfa zinazowakabili kinachoweza kumweka pabaya rais kiasi cha rais kuwaogopa?

Ingawa Hoseah kaanza, tunajua wabunge watamaliza kama ilivyotokea kwa mwezi wake uliopita huko Kenya, kwa mtu aliyekuwa na nafasi anayoiita yake ambaye alilewa urafiki na ushirika wake na rais kiasi cha kulidharau Bunge.

Wabunge wa Kenya walipomtaka Ringera aachie ngazi, aliwakebehi kuwa anafurahia sarakasi zao, asijue angelizwa na hao hao aliowakebehi.

Tujiulize. Inakuwaje mtu anayemwakilisha mtu mmoja kujiona bora na mwamba mbele ya wawakilishi wa umma? Zaidi ya tumbo lake na rais, Hoseah anamwakilisha nani?

Zaidi ya kutegemea kuteuliwa, Hoseah ana ridhaa gani ya umma kuwa pale alipo kiasi cha kupatumia kuhujumu umma? Rejea, Hoseah kwa kutumia TAKUKURU, alivyowahi kutaka kuwasafisha wezi wa Richmond, kwa kudai hapakuwa na mchezo mchafu wakati dalili zote zilionyesha kulikuwa na rushwa achia mbali mchezo mchafu ambao unaweza kupunguza makali ya jinai.

Je, tutaendelea na kuwa na watu wababe kwenye ofisi zetu hadi lini? Je rais ana nini na Hoseah kiasi cha kujiruhusu na kumruhusu awadhalilishe wawakilishi wa wananchi?

Ni muhimu Hoseah akaonyeshwa kuwa nchi hii ni ya wananchi wala si ya rais na wateule wake. Je, wabunge wetu wataufyata mbele ya mtu asiye na mashiko kwa sababu tu ni mteule wa rais?

Kwa vile Hoseah katia mkia wake kwenye kundi la siafu, umma unangojea kuona atakavyoondoka kiasi cha kuondoka akilia. Kwanini kuwahoji wabunge sambamba na kujadiliwa kwa kashfa ya Richmond ambamo Hoseah amehusishwa?

Kama kweli alivyosema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuwa TAKUKURU iliamrishwa na Ikulu iwadhalilishe wabunge, basi kuna uwezekano wabunge wakatumia kura ya kutokuwa na imani kwa rais na Hoseah.

Maana huu ni ushahidi kuwa TAKUKURU haiko huru na haipambani na kuzuia rushwa bali wale wanaotaka kupambana na wala rushwa kama inavyojidhihirisha kwenye hoja uchwara ya kuwahoji wabunge juu ya kula unbuge ili kuwaokoa waliokula mabilioni.

Haiingii akilini na inasikitisha sana kuona mamlaka zenye kuheshimika kuwa nyuma ya ufisadi.

Licha ya watu kuhoji anakopata jeuri Hoseah, wengi wanangojea kuona Bunge litakavyolinda heshima yake na kutenda haki kwa umma wa Watanzania wanaohujumiwa na wezi kama wale wa Richmond.

Wapo wanaoshauri hata TAKUKURU ivunjwe au kuondolewa chini ya Ikulu ili iwe huru na iweze kupambana na ufisadi kweli.

Je, Hoseah anapata wapi jeuri hii na rais anayempa jeuri hajui kuwa wabunge wakichachamaa wote wawili wanaweza kuishia kula jeuri yao badala ya mahanjumati ya ukubwa wanayofaidi na familia na marafiki zao?

Nijuavyo, ndivyo ilivyo. Hakuna aliyewahi kuwashinda wabunge hata angekuwa rais katika nchi yoyote yenye demokrasia.

Chanzo: Tanzania Daima Nov. 4, 2009.