The Chant of Savant

Sunday 28 February 2010

Rada imefunga luku watawala

UTHIBITISHO kwamba kampuni ya BAE Systems ya Uingereza imetembeza rushwa ili kupata kuiuzia Tanzania rada ya kijeshi (Plessey Commander Fighter Control System), unatupa changamoto kama taifa kuhusu uwajibikaji na utayari wetu kukomesha ufisadi.

Hiyo imetokana na ripoti ya Shirika la Uchunguzi wa Jinai la nchi hiyo, Serious Fraud Office (SFO) kuthibitisha BAE Systems ililipa pauni 30 milioni kwa baadhi ya vigogo wa Tanzania waliotajwa waziwazi.

Mauzo hayo ambayo aliyekuwa waziri wa ushirikiano wa Uingereza, Claire Short aliyaita kuwa ni uozo na harufu ya ufisadi, yalifanyika mwaka 2002.

Kati ya waliotajwa ni mwanasheria mkuu wa zamani wa Tanzania, Andrew Chenge na gavana wa zamani wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Dk. Idris Rashid wanaosemekana waliificha fedha waliyokatiwa kwenye benki nchini Uingereza.

Ajabu watuhumiwa hawa hawajawahi kukiri wala kukanusha ingawa ushahidi wote unaonyesha walitenda makosa na kuhujumu nchi.

Kibaya zaidi, mamlaka za uchunguzi za Tanzania zimekuwa nzito kuwashitaki kwa hofu ya kudhalilisha vigogo wengine wa serikali walioidhinisha ununuzi wa rada.

Taarifa mpya ni msumari wa mwisho kwenye jeneza kwa wale wanaosita kushitaki achilia mbali watuhumiwa wenyewe.

Watanzania na Waingereza wanangoja kuona mamlaka sasa zitatoa kisingizio gani mbele ya ufunuo huo.

Kwa kuthibitishwa kukosa, BAE Systems imepigwa bakora. Je, washirika wake watanusurika au kuendelea kulindwa na wakubwa wenzao? Na je, Watanzania walioibiwa wataendelea na ukondoo?

Kisheria, kama mamlaka zetu zisingekuwa na tabia ya kulindana, kesi yake ni rahisi; si BAE wamekiri kutoa? Iwapi nafasi ya kuendelea kugeuza Watanzania ni majuha?

Je, rais Jakaya Kikwete ambaye amekuwa akijenga imani watu kwamba anapambana vilivyo na ufisadi, naye atakubali kuendelea kuumbuka na serikali yake kuonekana kumbe ina ubia na watu tofauti na alivyowahi kukana?

Wakati muafaka wa kumshinikiza Mkurugenzi wa Mashitaka wa Serikali (DPP) kuchukua hatua za kiutu uzima ndio huu.

Tunajua shahidi. Watuhumiwa ni vigogo wenye ushawishi katika ngazi za juu kutokana na kuwahi kushika nyadhifa nono walizozichafua na kuzitumia vibaya.

Lakini je, Watanzania wataendelea kufumbia macho uoza na dhulma hii? Vyama vya mageuzi vitanyamaza kama wananchi wataendelea na ukondoo? Tutarajie maandamano ya kushinikiza haki kutendeka kwa watuhumiwa kushitakiwa mahakamani.

Tuhuma za ubadhirifu kwenye tenda ya kijambazi waliyopewa BAE zilipofumuka, kwa makusudi watawala wetu walizikejeli. Sasa ukweli umedhihiri. Wanasemaje?

Uzuri wa tukio hili la kihistoria ni ukweli kwamba BAE hawakuzungusha kitu wala kushangaa. Wametaja wezi kweupeni.

Wakati tukisubiri hatua, vema kukumbuka kwamba kuadhiriwa kwa wakubwa kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na viongozi adilifu wa Uingereza.

Wangetaka wangenyamaza tu na fedha zetu zikawa zimeliwa na kampuni yao. Hawakufanya hivyo. Hawa kesho watatudharau na kutukejeli iwapo serikali yetu itashindwa kushughulikia vigogo waliolishwa asali.

Tunatakiwa kukua na viongozi wetu watie akili sawa na wafadhili wanaotusaidia. Walisita kwa kuwa uthibitisho haukuwepo, leo imeshathibitishwa hakuna cha kufanya wazubae. Ni kuchukua hatua na sasa siyo halafu.

Ningekuwa DPP ningeficha uso kusudi nyani wa kumuua asinilaghai. Ni kumuua tu maana muda wake umefika. Angeharakisha kupata ripoti kamili ya uchunguzi kutoka SFO ili kutumia taarifa hizo kufungulia watuhumiwa mashitaka.

Ajabu kusikia waziri anashinikiza fedha ziletwe haraka na kukabidhiwa serikali lakini haelezi ni lini watuhumiwa watashitakiwa.

Hakueleza ni vipi wanawasiliana na serikali kutaka fedha walizoficha watuhumiwa baada ya kuhongwa zirudishwe nchini.

Hivyo hatua ya BAE kukiri inajenga mazingira kwa serikali kurejesha heshima iliyokuwa imeipotea kutokana na kutowashughulikia wezi.

Miezi michache imebaki kabla ya uchaguzi. Kwa kuwa serikali inaogopa kushitaki watuhumiwa, upinzani uchangamke kwa kuzidi kuamsha umma maana yawezekana watuhumiwa wakalindwa hadi mwisho.

Kazi ya kuhamasisha wananchi kuitia adabu serikali ifanyike sasa. Hakuna sababu ya kutumia nguvu, wenyewe wanajua wapi pa kusemea.

Ndio wakati wa kuwaeleza kwamba ufisadi hauna nafasi Tanzania. Anayeutenda, asulubiwe badala ya kupokewa kwa shangwe.

Wananchi wasijali pilau wala pombe ya kienyeji au upande wa kitenge. Wajue wakichekelea takrima leo, ni majuto ya miaka mitano kwao.

Kwa vile watawala wanahubiri utawala wa sheria bila ya kuufuata, wanapokosea wao, bakora yao ni kuwanyima kura.

Hebu tuangalie fedha zile zingetumika kujenga shule na kuipatia vifaa vyote watoto wangapi wangenufaika?

Fedha zile zingenunuliwa dawa na vifaa tiba na kugawanywa kwenye zahanati za vijijini masikini wangapi wangenufaika?

Ni fedha kama hizo hutafunwa kila siku na watumishi wasiokuwa waaminifu na hakuna kinachofanyika kuzirudisha.

Bado utasikia rais wetu anashindwa kutoa jibu akiulizwa nini sababu ya Tanzania kuendelea kuwa masikini.

Nchi itaendeleaje wakati viongozi wanaibia wananchi na kutumia vibaya madaraka waliyopewa?

Nchi itapiga vipi hatua ya maendeleo wakati rais anaona fakhari kila siku kufanya ziara za nje na kuomba misaada?

Nini kama siyo upungufu kukubali kuomba huku rais akidiriki kuitwa ombaomba aliyevaa suti ya bei mbaya au mlafi anayetapika kwenye viatu vya wafadhili kama alivyowahi kusema balozi wa Uingereza.

Inataka mtu kuoba aibu na kutambua utu wake na maslahi ya watu wake. Vinginevyo serikali isingeshindwa kushitaki watu waliolamba asali.

Hivi kama matapeli wachache wanaweza kuiba kiasi kikubwa cha fedha tusishtuke si wakitaka hata kuangusha serikali wataweza?

Umma unataka walionufaika na ununuzi wa rada wakamatwe na kushitakiwa maana wakati wa kutafuta mchawi umepita.
Chanzo: MwanaHALISI Feb. 24, 2010.

Tanzania, Afrika, nani ameturoga?

KAMA siyo kuibuka utata na mabishano juu ya pendekezo la kutumika kitabu kimoja kwenye shule za sekondari, huenda nisingeandika makala hii.

Tunaambiwa kuna utafiti umefanyika na kukuta wanafunzi wanafeli kwa kusoma vitabu vingi. Je, hata wakisoma hicho kimoja wakafeli itabidi kiondolewe?

Je, hili ndilo jibu la tatizo au sehemu ya tatizo? Huu ni uhuni unaofanywa kwa watoto wetu na mfumo wetu wa elimu. Mbona hawa wanaotushauri kuanzisha utaratibu wa kitabu kimoja walisoma vitabu vingi na havikusababisha kufeli?

Mbona huko wakubwa wanakokimbizia watoto wao wanasoma vitabu vingi? Naona ajabu sana. Binti yangu wa darasa la tano hapa Kanada ameishasoma noveli zaidi ya tano, ukiachia mbali nyingi za mwingine wa darasa la tisa ambaye ameishasoma novei nyingi na hawalalamiki wala hawafeli.

Tunajenga jamii gani ya wasomi isiyofikiri na kulinganisha, kupambanisha mambo na kupembua? Je, ule msemo kuwa ukitaka kuficha ukweli kwa mswahili ficha kwenye vitabu, unaanza kujirudia?

Akina Jumanne Maghembe wanaosingizia kufeli kutokana na kusoma vitabu vingi, wao wamesoma vitabu vingi na hawakufeli. Hata hivyo tusiwashangae sana.

Kwanza, wana uwezo wa kusomesha watoto wao nje, ukiachia mbali kusoma bure na kuwauzia wengine elimu waliyoipata bure.

Hata huko Kenya na Uganda wanapokimbizia watoto wao, baadhi ya Watanzania wenye kipato hawasomi kitabu kimoja.

Laiti wangejua kuwa wakati Kenya wakiwaletea walimu wao feki; wao wanapeleka watoto wao Uganda, wasingepoteza pesa na muda wao hivyo.

Badala ya kujenga shule na kuimarisha mfumo wetu wa elimu, tunaubomoa na kuwekeza kwenye upuuzi kama grosari na nyumba za kulala wageni.

Nani ameturoga? Msipoangalia hata Rwanda itatupita hivi karibuni. Tatizo letu ni kuwa na tawala zilizopatikana kwa njia za rushwa; zinazoendeshwa na matukio badala ya mipango mikakati.

Leo utasikia kelele juu kuhusu “Kilimo Kwanza.” Utashangaa hata hayo matrekta ya kulimia tunayoahidiwa yanaingia utata hata kabla ya kufika.

Tuna uwezo wa kuingiza mashangingi ya wabunge na watendaji wengine wasiopaswa kuwa nayo; lakini hatuna uwezo wa kuingiza matrekta.

Watawala wanalenga kuwahadaa wapiga kura. Lengo lao ni leoleo na kura na siyo mstakabali wa taifa. Je, hawa si rahisi kuuza ardhi hata watu wetu ambao wanaendelea kufanywa wajinga? Nani ameturoga?

Leo watu wazima na akili zao wanasamehe kodi ilhali wakiwalangua elimu tena dhaifu watoto wetu. Ukilinganisha kiwango cha kodi zinazokwepwa, kusamehewa na kufujwa, kama tungekuwa na mfumo na utawala bora, zingetosha kusomesha hata kutibia watu wetu bila taabu.

Je, ni wangapi wana ubavu wa kuwasomesha watoto wao nje kwenye elimu nzuri tunayoiabudia? Nani ameturoga?

Wasomi gani hawa? Leo watu wetu wanakufa njaa ilhali tunakodisha ardhi kwa wageni kuzalisha chakula kwa ajili ya watu wao; hata kutulangua sisi, kwa vile wanaweza kuwahonga asilimia 10 baadhi ya waroho walioko madarakani.

Hivi unaposoma makala hii, watu wengi wa Ethiopia wanakabiliwa na tishio la njaa. Lakini wakati hili likiendelea, makampuni ya kigeni yamo nchini humo yakikodisha ardhi na kuzalisha chakula kwa ajili ya watu wao.

Kampuni la kihindi la kuzalisha maua la Karuturi limo likizalisha maua wakati Waethiopia wakiendelea kufa kwa njaa.

Kadhalika nchini Sudan, ambamo watu yapata milioni tano wanaishi kwa kutegemea mashirika ya kimataifa kuwalisha, kuna nchi za kiarabu zinalima mpunga na kusafirisha kwao.

Abu Dhabi yenye watu milioni nne imeishawekeza nchini humo kwa ajili ya kulisha watu wake wakati Wasudani wakiendelea kuteketea. Nani ameturoga?

Kenya yenye idadi kubwa ya watu wasio na ardhi nayo imo kwenye mchakato wa kuridhia ukoloni huu kwa kukodisha ardhi yake yapata heka 40,000 kwa kampuni moja ya Qatar kando ya mto Tana ili ilime chakula kwa ajili ya watu wao.

Ajabu Kenya hiihii inataka kutuhadaa tuungane nayo ili itumwagie watu wake wasio na ardhi; waje kuzoa yetu baada ya watawala wao na walowezi wa kizungu wachache kuipora yao. Wanatulaumu kwa kutoharikisha mchakato wa kuungana.

Lakini hao hao wanapinga kuharakishwa mchakato wa kuwa na sarafu moja ya Afrika Mashariki. Wao wanataka ardhi yetu na kulinda sarafu yao. Kwetu wanasemaje? Tusiogope Wakenya wala Wanyarwanda; bali tushindane nao bila maandalizi. Nani ameturoga?

Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) Dk. Jacques Diof ameishaonya kuwa hii ni aina mpya ya ukoloni. Leo tunafukuza watu wetu kuwapisha wageni wazalishe chakula.

Rejea taarifa ya kijiji cha Namwala inayozunguka kwenye intaneti ikionyesha aina hii mpya ya ukoloni. Maana hakuna sheria zinazolazimisha wageni kuuza chakula kwa nchi zinamozalisha chakula hata wakati wa baa la njaa.

Ajabu habari hizi zinafichwa kwa vyombo vyetu vya habari hadi kutangazwa na vyombo vya nje. Habari hii ilirushwa na Shirika la Habari la Kijapani (NHK).

Nchini Madagascar utawala wa Rais Victor Ravalomanana ulidhoofishwa na kuangushwa na kashfa ya kutoa ardhi kwa kampuni ya Korea nchini humo mwaka 2008.

Rovalomanana alikodisha ardhi kwa miaka 99 yenye ukubwa wa eneo sawa na nusu ya Ubelgiji, tena bila ya kulipwa hata senti moja.

Si kwamba hawakulipa kitu. Nchi haikulipwa lakini wapenda rushwa waliokuwa na madaraka walilipwa badala ya nchi. Nani ameturoga?

Leo tunapata taarifa za kuhuzunisha kuwa mzungu mmoja huko Kagera ametangaza jamhuri yake kwa kuwanyang’anya watu wetu ardhi akisaidiwa na mgambo. Tunachekelea na hatuchukui hatua haraka.

Watu wanakodisha ardhi yetu hata kulima maua wakati watu wetu wanakufa kwa njaa au kutegemea jembe la mkono. Nani ameturoga?

Leo hii biashara zote za maana na tenda hata za ulinzi zinafanywa na kupewa watu wa nje, tena wanaoishi ughaibuni.

Leo nyumba nyingi za Msajili wa Majumba (sasa chini ya Shirika la Nyumba la taifa – NHC), zinakaliwa na raia kutoka nje wakati wafanyakazi wa serikali inayozimiliki wakiteseka huko “madongo poromoka” wanakolanguliwa pango. Nani ameturoga?

Leo watoto wa wafanyabiashara wenye kutia mashaka wananunua ubunge sisi tunaangalia tu. Tusishangae hata kesho wakinunua urais na sisi tukiwa tumekodoa macho tu. Jamani nani alituroga?
Chanzo: MwanaHALISI Feb. 2010.

Thursday 25 February 2010

Africa: The Coup Era Returns


Tandja cornered.



I abhor undemocratic means of ascending to power. When Capt. Mousa Dadis Camara survived an attempt on his life by his aide Boubakar Diakite, many thought it was just an isolated incident and a passing cloud. To the contrary, thinkers had a different take of this. Is this the beginning of a new era whereby marksmen are likely to usher democracy in?

After Diakite shot Camara, his grip on power started to shrivel where it would have thrived. His sober deputy Sekouba Konate came into the big picture to arrest the impasse the country was in under Camara. Thanks to his efforts and bravery, Guinea may have a democratic elected government soon shall what has been agreed upon be adhered to.

The recent development whereby the army in Niger staged a successful coup tells how the army that used to be regarded as the means to power has made a U-turn that, if maintained- is likely to get Africa rid of tyrants and strongmen. Won’t it bring back military juntas? This is the big question many have to ponder on cautiously and carefully.

Mamadou Tandja a former army chief annoyed the world last year when he embarked on a controversial referendum that abolished the presidential term limit and gave himself more leeway to bulldoze Niger after his second-five-year term in office expired last December. His paid stooge maintained their bagatelle that Tandja had special work to complete as if the country was his private estate.

The turning of tables against Tandja must send signals to all African potentates clinging to power by depending on the armies. What transpired in Niger must open eyes for other dictators who think they are smart. Tampering with constitutions has become an in-thing for African tin-pot dictators. It has been done in Senegal, Uganda and Rwanda. This proved to be a hard nut for opposition and civil organizations to break given that it was supported by armies. Now, the new breath is likely to come from the men and women in uniform. They are tired of being a tool in one’s hand.

Given that all tyrannical regimes in Africa depend on armies, this new move –shall it aim at restoring democracy- is likely to succeed and spread pronto. Nigeria is currently democratically stable thanks to the realization of the army that it can play a great role in restoring democracy. Though Madagascar is still frangible, the role the army played during the power struggles between former president Marc Rovalomanana and current one, Andry Rajoelina, is commendable and apable.

Though military juntas are coming to plunder just like those they depose, opposition needs to give them a heck so that their stint in power should restore democracy instead of transforming themselves into civilian aspirants for presidency as recently evidenced in a failed bid in Guinea.

It is time for the opposition to agitate that Niger be steered back to true democracy. The good name the junta gave itself: Supreme Council for the Restoration of Democracy (SCRD) must mean exactly that.

Africa was trying to soldier on without coups. But given that our democratically elected dictators don’t want to honor their promises and the constitutions of their countries, slowly we’re relegating back to dark days of tyranny and dictatorship. What even pains is the fact that our sitting duck-AU, has always been backing dictators. That’s why when the army pulled Tandja down, it quickly suspended Niger. The irony though is when Tandja tampered with Niger’s constitution; it did not take such stern measures!

Nigers are upbeat though it is early to speculate. One of the junta leaders, Harouna Djibrilla Adamou, was quoted as thus: "We call on national and international opinions to support us in our patriotic action to save Niger and its population from poverty, deception and corruption."

“I hope the soldiers restore some order ... clean up the political environment,” said taxi driver Moussa Issa. “We need to start from scratch, without being compromised by the current political class which has been discredited over the last 20 years.” Issa added.

Is the junta going to meet the expectations of the people? Time will tell.
Source: The African Executive Magazine Feb. 24, 2010.

Mapenzi ya ulaji na kuokoa Valentine Idodomya

WAKATI watu wengi walisherehekea Valentine Day na wapendwa wao, mzee mzima nilisherehekea na kina Mbwa Mwitu aka Ewassa, Rost Time aka Kanji na washikaji wengine.

Tulikutana kwenye kijiwe cha kahawa cha mtaa wa Dodoma pale Ilala kuweka mambo sawa. Hii ni baada ya Sammy Sixx na wenzake kugeuka mwiba. Ila washikaji msikonde kwani tuliwasilimisha na kurejea mapenzi yetu ya zamani tukiwa kitu kimoja.

Kabla ya kuchonga vilivyo ngoja nikupe kidogo. Una habari mzozo huu ulinichelewesha kwenda zangu Umangani kujirusha na Shosto wangu?

Jingine, kwenye msafara wangu niliandamana na mafisadi papa wa nguvu ambao hata hivyo sikutaka watajwe zaidi ya kusema, niliandamana na wasasi ngawira kadhaa. Unajua maana ya kadhaa? Basi kama hujui kadhaa ni kadhia kwa walipa kodi wa kijiwe. Maana tulipunyua ndululu zao na kwenda kujinoma na washirika zangu. Bila usanii dunia hii huishi ukiishi utageuzwa punda na wasanii. Hayo tuyaache.

Mambo yalikuwaje? Tulivalia kijani kama alama ya kuzika tofauti zetu na kumalizia na nyekundu, alama ya mapenzi ya ulaji wetu na maafa kwa waliwaji na walevi wetu.

Wakati wengine wakienda kusambaza ukimwi, sisi tulisambaza ufisadi.

Kama siyo mzee Maneno pamoja na mzee Machale aka Mchekwa, kijiwe kingegeuka jehanamu baada ya akina Sammy Sixx kutaka kuwasulubu washirika zangu akina Mbwa Mwitu na Kanji.

Kwa vile sisi ni wanasiasia, tulisia sia mikakati na kuamuru ugomvi baina ya makundi mawili ufe vinginevyo tungewanyima jamaa nafasi za kugombea ulaji kwenye uchafuzi ujao. Upo hapo? Hii ndiyo siri ya akina Sixx kugeuka mbwa na kulamba matapishi yao.

Ile kashfa ya mkaa tuliyoibatiza Richmonduli nusu ikidedishe kigwena chetu cha UNM yaani Ugali Nyama na Maharagwe aka Chama Cha Maulaji kama wakiitavyo watani wetu.

Kuweka mambo sawa, mzee mzima niliteua kamati ya watu watatu kusuluhisha mafisadi na wasimafisadi. Nilimteua mkuu wa zamani wa kijiwe Ali Assaani Mwi..we koma we, Pio Mchekwa na Abdalaman Kiaina kusuluhisha tatange hili.

Wengi hawakustuka ni kwanini nilimchagua Pio wakati ana usongo na nongwa na Sixx. Nilimteua ili kwenda kuvuruga njama zozote za kuwawajibisha akina Mbwa Mwitu. Na ilikuwa hivyo. Kwani alifanya kazi ya kupigiwa mfano ya kuja na mapendekezo ya kuwaminya akina Sixx na hatimaye kuwageuza ndondocha wa hoja.

Kuwapata vizuri, alitumia Baibo huku Ali akitumia Al Koroani.

Najua waumini wa kweli wa dini watakuwa wanashangaa ni vipi shetani anaweza kutumia vitabu vitakatifu kulinda ushetani wake. Msishangae. Hizi ndizo siasa za kijiwe. Bila rongo rongo unafiki na hila hufiki popote.

Kama nilivyowamegea last week, Ewassa na mafisadi wenzake waliangusha pati ya kufa mtu. Mpaka tunaondoka mtaa wa Dodoma, akina Sixx walikuwa wanaonekana kama vyangudoa wa kawaida baada ya kuzimwa kama mshumaa wasifurukute. Unafanya mchezo na ulaji wa dezo? Hata hivyo walinifurahisha kitu kimoja; kusema kuwa wameamua kufyata mikia kwa kuogopa kunitia mzee mzima kwenye matatizo wasijue mie ndiye baba wa matatizo yote!

Jamaa niliwaona wajanja mwanzoni. Sikujua ni weupe kiasi cha kutojua kuwa mradi mzima wa mkaa niliuanzisha na kufaidika mimi! Au kwa vile jamaa wamelemewa na ulaji kiasi cha kutojitafutia habari na maarifa. Ukiwasikiliza wakipayuka utadhani wajanja kumbe kanjanja watupu. Viko wapi viapo vya akina Mwakiwembe kuwa kama tungeendelea kuwapuuzia wangetoboa siri? Utapeli mtupu. Nani hajui kaya hii ya wasanii na vyangu wa kisiasa?

Nakupa siri. Ingawa wameingia mkenge kuwa wakiacha uhasama watarejeshwa kwenye ulaji, nani afanye kosa hili? Hawa mambo yao kwisha. Harudi mtu wala nini. Afadhali wangekuwa wajanja siyo majuha wangeendelea na mkakati wao wa Chama Cha Jeuri ambacho tumekisambaratisha hata kabla ya kuzaliwa. Hakuna cha Chama Cha Jeuri wala Chama Cha Kupambana na ulaji wetu.

Tumewafanyia kitu mbaya baada ya wao kutaka kutufanyia kitu mbaya. Watoto wa mjini husema tumewafunga goli na sasa wana mimba za mafisadi wa kijiwe. Sie vidume ati. Kwanza tunajua kaya yetu ilivyo ya woga na wabangaizaji. wanaoendeshwa na matumbo yao badala ya vichwa hata wawe na elimu kiasi gani.

Mara hii mmewasahau wale madaktari akina Kusumbuka wa Miayo na Hasidi Kaboro! Walipojifanya wanajua huu nasi tukawaonya kuwa tunaujua ule. Tulisema beekhe! Hao wakanywea na kihoro mavi debe kama mbwa waliojaribu kuiba mafuta!

Wako wapi? Ni watoto wa watu sasa na wako kwenye kiama wametulia.

Muulize Meku wa Kilema. Siku hizi anaimba utukufu wangu baada ya kuexpire na kuishiwa. Naye kama wao analamba matapishi yake na kuyakoga kama nyoka baada ya kunyimwa miguu. Laana hiyo jamani. Laana hiyo! Imeandikwa. Kila mti utaujua kwa matunda yake.

Sisi chata kubwa bwana. Hamkusikia akinisifia kila siku utadhani yeye ni mgosi Machungi wa Makambale! Baada ya meku kupigwa na kisukari nasi tumempa sukari sasa analamba, aam! na kusahu aliyosema juzi. Unacheza na sukari nini?

Kwa kutumia sukari tumeua upinzani kiasi cha waliokuwa wapinzani kijiweni kugeuka wapambe na makada wa chama changu.

Kutokana na mapenzi ya Valentine hakuna anayefanya fyoko. Akifanya fyoko tunamwambia nyoko na kumkata mkia.

Hata akina Sammy Sixx wangefanya fyoko tungewapa talaka bila “haq tamat” kwa wanaojua kiarabu. Utampaje “haq tamat” changudoa? Hata ukimpa ni shiliingi mbili si maelfu sawa na mama mwenye kujiheshimu. Maana kwa kukubali yaishe wamejidhalilisha sawa na vyangu. Tumefanya hivyo kwa makusudi kuepuka kuchukuliwa na wapinzani wetu kijiweni.

Ukitaka kumkomesha mbwa mkate pua. Kwa tulichowafanyia hawa hata ukiwategeshea fisi bingwa wa uroho hawezi wagusa. Tumemaliza kazi na tukiingia kwenye uchafuzi tunapeta. Kwa maneno mengine hawa ndiyo wafu aliowatabiri shehe Ubwabwa.

Hakuna watu nawasikitikia kama wale waliokuwa wakiwaamini vyangu hawa. Maskini hawakujua kuwa kwenye fani ya usanii na mazingaombwe haaminiwi mtu bali ulaji! Sasa yamewakuta. Tutaona tambo na majigambo yenu yataishia wapi kama siyo kula jeuri yenu kama Chama Cha Jeuri ambacho tumekinyonga hata kabla ya kuiona mbeleko.

Tumalizie kwa kuowaonya walevi wanaoshabikia neno la God. Juzi tulimuona jamaa yetu Ka-tortoise pale Menge menge akiwashushia kibano Tanisiko. Kumbe kaya hii inaruhusu kila tapeli kujifanyia atakavyo! Haya ndiyo matokeo ya umbwe na kuendeshwa na mafisi na mafisadi. Mie simo. Ila tufikiri.

Ukija mgao wa umeme tunalalamika. Wakija mafundi tunawachapa! Mbona hatuna jema jamani? Mpaka kesho sijaamini kama tapeli wa mchana kama huyu angezuia shughuli za maendeleo kwa kaya. Ka-tortoise, elewa. Kumbi kumbi akikaribia kufa huota mbawa ili aruke na kunguru wamfanye kitoweo. Zako zahesabika ati.

Valentine Day mtaa wa Dodoma ilifana hasa kwa kuwapata wapenzi wapya akina Sammy Six na kundi lake. Walikuwa wanatubania. Sasa hawatubanii tena. Tunafaidi mavituz kama kawa. Naona gari la Sammy Sixx. Ngoja niende kuzomea na kumzodoa!
Chanzo: Tanzania Daima Feb. 24, 2010.

Tuesday 23 February 2010

Richmond, MPs and fix-it-yourselves gesture

WHEN our ‘brave house’ of August turned tables on itself when it put Richmond
scam down, many appallingly wrote to me asking for comments little knowing that I was
chirking this milestone up!

Don’t get me wrong. I’m not a napkin-like scribe like those who did the dirty laundry
for Richmond. Didn’t you know that by trusting politicians you’re trying to square the
circle and these are the results?

Because the mails were many more than I’d reply, I decided to write this epistle to: Firstly, fault all those condemning honourable MPs and their stance. Cheer them for
showing you who exactly they are and what they do and stand for.

Secondly, thank the parliament for its good soap opera. Indeed, it made our nation
proud and happy. How could MPs put their colleagues in shame in this hank where
nobody is clean? Don’t you remember! Sofia Simba the minister of bad, sorry, good
governance once warned that: he who’s without sin must be the first to throw a
stone? She knew them. They understood her.

Thirdly, thank the government for its resilience to see to it that its big hitters are not crucified. Fourthly, the hoity toity that enabled the top secret (sirikali) to put sense into those that wrongly thought our sacred cows committed any wrongs. Mali ya umma
haiumi.

Fifthly, thank the hoi polloi for letting the government off the hook, especially those
supremos whose ulaji were threatened by this stinking scam. Yes. Those MPs represent
them well and whatever they do good or bad has their blessings. That’s why they’ve
nary acted decisively.

So too, I must bid and reprimand all those blaming our good topdogs. They must understand: the case is closed. So, whoever pokes their noses into it, they’ll be dealt with by PCCB the way it dealt with MPs who wanted to spoil the deals.

I’m still wondering. Who charmed people of this hank of honey and milk? How could
they loathe the blood of those they wrongly thought are big thieves or sharks, even whales, while the rule is open? Didn’t they know that Lord Jesus said it plainly that he who has will steal from he who has not and there won’t be any crime?

Why do they forget the cardinal law that when big freebooters steal big money they are
not supposed to be jailed or be disturbed in anyway? The rules of the jungle are
simple and clear. Petty thieves will be condemned to life imprisonment even being
set on fire alive whilst the big footpads will be spared even by using poor taxpayer’s money.

If any of you reading this epistle thinks I’m sick with regard to spending kapuku’s
money on freeing freebooters, ask yourself: Where did MPs get their sitting,
sleeping, even gossiping allowances if not from your tax?

Let me now delve into Richmond. Honestly, Richmond wasn’t a bogus project-cum-company. How could it be if money was made and now you see nobody is to be crucified? Don’t you know? This is how the power-that-be makes money especially
at this time near elections.

If you can’t comprehend this simple mathematics, let me give you yet another one.
Have you ever asked the rationale for MPs and other politicos receiving huge amounts
of money in emoluments and what not whilst doctors and other professionals are
receiving peanuts? Go and think again.

But one thing is obvious. Richmond has robbed MPs all gains they realized when they
defeated the government by ousting PM Edward Lowassa and company thanks to his role
in the Richmond scam.

And don’t tell me the opposition is the minority and thus had no girth to act. Vacating the house for those that don’t consent to this broad-daylight-light corruption would add up. What will they tell the people that had already cultivated trust in them? Doesn’t this blackmail portray them in bad light just as CCM MPs? If anything, this is the point at which the so-called opposition and ruling kit and caboodle of swindlers meet and become one thing.

Importantly, you need to know that if there had not been such deals nobody would aspire by heavens and skies to become a mheshimiwa.

For us privy to the upper echelons of power knew was déjà faire when the president
briefed the nation during his one-hundred-days-in-office talk. Do you remember what
he said? He averred that thanks to their connectibility, especially with some smart
guys in the land of Obama, power rationing would become a thing of the past. And
indeed it is. So what else did you want him and his friends to do?

The other day I was irked and piqued, so as to start capering like a Masaai warrior, when I heard a certain stupid guy saying that those that stashed money abroad after purchasing fake radar must be trussed! How can you hang such heroes who forced the Britons to give us the radar free? After all, in our palatinate, larceny pays. Importantly, one must loot big dosh not chickens and chains.

Guess what, Richmond and even Dowans made away with billions of shillings of taxpayers’ money. The fault wasn’t of those honourables you call big time cossairs but that of our rotten system.

So to cut the story short, I must say: We don’t need to blame MPs, even honourable
Richmond suspects, players and movers behind the curtain. Who dares cut the hand that
Feeds, him especially at this time party consent is needed to stand again for parliament?

Secondly, in lieu of passing the buck, guys, you need to upbraid yourself. You know
what? Thievish society fashions, thievish captaincy. I don’t mean yours is a thievish society. But if we fully truly hate graft, will you really have any stomach to vote back such people you think and believe are thieves?

What’s more, by 'taking' the bull by the horns, surely, voters will reward the government and the party that capacitated all this for their peril. When your fat cats sup, they do it on your behalf. That’s why voters in Bariadi, Monduli and Rombo threw big parties for their people after being sacked for ‘chopping your dollars.’

Japes aside, this way, we’re killing future generations. Indeed, if anything, what the House did is nothing but a fix-it-yourselves (wananchi) gesture. The big jigsaw’s how are you to fix it? Your vote counts. Or you can take to the streets to send a clear message that you understood their brain games.

By the way, when will hyenas meet to discuss how to save sheep?
Source:ThisDay Feb. 22, 2010.

Thursday 18 February 2010

Kikwete ajibu tuhuma dhidi yake



RAIS Jakaya Kikwete aliishajijengea utamaduni wa kutojibu shutuma dhidi yake. Kazi hiyo aliikabidhi kwa wapambe wake, Yusuph Makamba, Kingunge Ngombale -Mwiru, George Mkuchika, Sophia Simba na Salva Rweyemamu.

Haikujulikana hasa nini kiini cha yeye kushindwa kujibu kile kilichomhusu, au kilichohusu serikali yake. Lakini sasa Kikwete ameamua kuvunja mwiko wake. Inawezekana ni baada ya kuona wale aliowatuma au waliojipachika, wameshindwa kumsaidia.

Ninampongeza. Ni vema aendelee kujibu tuhuma zote zinazomkabili yeye binafsi, chama chake na serikali yake. Ingawa baadhi ya majibu yake hayakubaliki, lakini kuna kila sababu ya kumshajiisha ili aanze kujibu hoja hata kama amechelewa.

Sasa anapaswa kujibu tuhuma ya kwanza, kwamba ushindi wake katika uchaguzi mkuu wa 2005 uliwezeshwa na fedha za EPA zilizoibwa kutoka Benki Kuu ya Taifa (BoT).

Tunamtaka ajibu kuhusika wake, nyuma ya pazia, katika sakata la mkataba tata wa kufua umeme kati ya serikali na kampuni ya Richmond.

Asiishie hapo. Ajibu tuhuma kuwa aliacha kutangaza mali zake kutokana kuogopa kuulizwa alivyozichuma. Ajibu tuhuma kwamba ameshindwa kutekeleza ahadi nyingi alizotoa wakati wa kampeni zilizomwingiza madarakani, hadi wakongwe wa chama kuanza kupendekeza “apigwe buti.”

Kuna tuhuma kuwa Kikwete anazidiwa nguvu na mitandao na kwamba ni mitandao ambayo inamwendesha na inayolihujumu taifa. Hajakanusha.

Kuna madai kuwa anamtumia mtu aliyejipachika unajimu mkuu Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein kuwatisha wanaotaka asipewe nafasi kubeba bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) au hata kupingana naye. Hajakanusha.

Mlolongo wa tuhuma unaendelea. Kuna madai kuwa anafanya uteuzi mwingi kwa kuangalia mtandao, urafiki, dini na kulipa fadhila. Lakini rais amezidi kuziba masikio huku watu wasio na udhu wa nyadhifa zao, kama Sofia Simba au watuhumiwa wa kughushi vyeti vya taaluma, wanaendelea kupeta ingawa ni aibu kwa rais.

Kikwete anatuhumiwa kukumbatia watuhumiwa wa ufisadi, mmojawapo akiwa mshirika na rafiki yake, Rostam Aziz mbunge wa Igunga anayetuhumiwa kuwa mmiliki wa Richmond, Kagoda.

Tuhuma zinasema hii ndiyo siri ya kutokamatika kwa wamiliki wa Kagoda na wezi wengine kama alivyobainisha mkuu wa jeshi la polisi Said Mwema hivi karibuni.

Hili nalo linataka majibu. Kwanini taasisi yenye kila nyenzo na wataalamu wa uchunguzi wa jinai ishindwe na wahusika wasiachie ngazi kwa kushindwa kutimiza wajibu wao?

Rejea tuhuma kuwa kampuni ya kuzalisha umeme, IPTL ambayo imegeuka donda ndugu kwa uchumi wa taifa, iliingia mkataba wakati Kikwete akiwa waziri mhusika kwenye masuala ya nishati. Tuhuma hii haijajibiwa.

Rais anashutumiwa kukalia kesi nyingi za wahalifu mbalimbali kama alivyowahi kukiri na kutangaza kuwa ana orodha za majambazi, wauza unga, mafisadi, wezi wa bandarini, wala rushwa na nyingine.

Kuna tuhuma kuwa rais anaendesha nchi kirafiki ambapo mamlaka yake yanatumiwa vibaya kuwalinda marafiki zake. Rejea kutofikishwa mahakamani kwa aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, Dk. Ibrahim Msabaha, Nazir Karamagi na Andrew Chenge.

Hawa wanatuhumiwa kushiriki, kwa nyakati tofauti na kwa pamoja au mmojmmoja, kuipa mkataba kampuni ya Richmond, wa kufua umeme wakati haikuwa na sifa wala hadhi.

Tuhuma nyingine ni kuwa ameshindwa kurekebisha mikataba ya uwekezaji ya kijambazi iliyoingiwa na awamu ya tatu.

Kuna tuhuma kuwa, kwa vile alikuwa waziri wa Benjamin Mkapa, alishiriki kujipatia nyumba za umma hata kushiriki “uchafu” wa Mkapa. Akanushe au kutoa maelezo.

Tuhuma nyingine ni kwamba rais amekuwa mateka na mtumwa wa mafisadi. Wanasema nchi sasa ina ombwe la utawala. Haya ni madai mazito yasiyopaswa kunyamaziwa au kupuuziwa.

Pia kuna madai kuwa Kikwete anatawala bila sera kwani ni wachache wanajua sera yake ukiachia mbali kauli mbiu yake ya kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya ambayo imegeuka na kuwa kinyume.

Kuna hili la kukwepa majukumu ya ofisi yake na kupoteza muda mwingi ughaibuni kwenye ziara zisizo na manufaa kwa taifa. Rejea ziara zaidi ya kumi alizofanya kujitambulisha kwenye nchi mbalimbali; utadhani ndiyo walimpigia kura.

Madai mengine ni kuwa siku hizi majina ya watu anaoandamana nao nje yanafanywa siri. Hili nalo linaonekana kama ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Rejea kutotangazwa kwa waliokuwa katika ujumbe wake kwenye ziara yake huko Cuba, Jamaica, Trinidad and Tabago na Marekani ambako cha mno tuliambiwa alibembea na kuonana na mwanariadha maarufu wa Jamaica, Usain Bolt na kuomba makocha wa riadha.

Kuna tuhuma kuwa NGO ya mke wa rais, WAMA, ni bomu sawa na EOTF ya Anna Mkapa; kwamba ipo kutegeneza pesa na wachangiaji na wahisani wake wengi wana harufu ya ufisadi na wanafanywa siri.

Wengi wanahoji, kwanini mkewe awe na uchungu na akina mama mara tu baada ya Kikwete kupata urais.

Rejea mama Salma Kikwete kuonekana karibu kila mkoa na kwenye kurasa za mbele za magazeti akimpigia kampeni mumewe kinamna hata kabla ya tume ya uchaguzi kutangaza kuanza kampeni.

Yanatakiwa majibu yanayoingia akilini na utekelezaji wa kuifutilia mbali NGO hii ambayo umma unaiona kwa jicho baya hasa kutokana na uzoefu wa EOTF (mfuko wa fursa sawa kwa wote ya Anna Mkapa) wa kufanya biashara ikulu.

Kwa vile Kikwete ameamua kujibu mapigo, tungemshauri ajibu hoja na si mapigo dhidi ya madai haya mengi, mazito na ya muda mrefu.

Japo ukimya ni dhahabu, mwingine ni adhabu. Martin Luther King Jr. aliishawahi kusema, maisha yetu huanza kupukutika siku tunapoanza kunyamazia mambo makuu na muhimu (Our lives begin to end the day we become silent about things that matter).

Hizi ni baadhi tu ya tuhuma. Tunangojea Rais Kikwete kujitokeza mbele na kujibu hoja na tuhuma anazotwisha. Kwa njia hii ataeleweka na atakuwa ametoa mwanga au elimu juu kinachojadiliwa.
Chanzo: MwanaHALISI Feb. 10, 2010.

CCM ife, Watanzania wakombolewe

KATIKA harakati za kujinasua (bila mafanikio) kutoka kwenye ufisadi, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekumbwa na migawanyiko ambayo inaonyesha kitazidi kuparaganyika na, hatimaye, kufa.

Huu ni ukweli. Si fikra wala ndoto tena. Hapa ndipo utabiri wa muasisi wa CCM Hayati Mwalimu Julius Nyerere utakapotimia.

Hata kifo cha hivi karibuni cha muasisi mwingine aliyekuwa amesalia, Mzee Rashidi Kawawa, aliyekuwa na mvuto na uwezo wa kufanya mambo nyuma ya pazia, ni pigo jingine kwa CCM.

Hata hivyo, kuna faida kwa mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, hasa kutoka kwa wapenda maendeleo walio wengi. Faida hii itapatikana kama atacha CCM ijifie ili Watanzania, akiwamo yeye, wakombolewe.

Wachache wanaofaidika na utawala wake watamlaumu. Watajaribu kujinasua toka kwenye pigo hili takatifu lisilozuilika sasa, ingawa kwa bahati mbaya, muda umeshewatupa mkono. Walichelewa kusoma alama za nyakati. Wanasukumwa na matukio na si mipango na mikakati.

Kama Kikwete atahakikisha CCM inazikwa wakati wowote kuanzia sasa, atajizolea umaarufu kama alivyofanya kiongozi wa mwisho wa Muungano Kisoshalisti wa Jamhuri za Kisoviet wa Urusi (USSR), Mikhail Gorbachev.

Hapa, kuna shuruti. Salama ya Kikwete itategemea atakavyoshughulikia mafisadi papa waliotamalaki kwenye chama na serikalini, ambao wengi ni washirika, wawezeshaji na maswahiba zake wa karibu.

Lakini kuwashugulikia hakuwezekani bila kurejesha maadili ya uongozi. Hili nalo linaweza kumpatiliza hata yeye; maana watu wenyewe wanajua siri na udhaifu wake.

Ana mtihani sawa na ule alioupata Mfalme Suleiman alipoletewa kesi ya wanawake kugombea mtoto mmoja.

Kuepuka hili anaweza kufanya mambo yafuatayo:

Ama afumbe macho awatose mafisadi ili yeye anusurike, au aanzishe chama chake kama alivyofanya Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika.

Kuacha CCM indelee kumeguka kama ilivyotokea kwa KANU huko Kenya, kimsingi, ni furaha kwa Watanzania maskini. Hii imeshaanza kujitokeza kutokana na kuundwa kwa chama kipya kinachozungumzwa sana sasa (Chama Cha Jamii (CCJ)).

Anaweza kuunga mkono chama hiki kisiri siri kiwe kama mtumbwi wa uokozi kwake hata kama hatakuwa madarakani. Rais Amani Karume amefanya hivyo na hasimu wake mkuu, Katibu mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Seif Shariff Hamad. Hili linawezekana. Kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu bali maslahi ya kudumu.

Kama tetesi kuwa chama hiki kinaundwa na vigogo wasioridhishwa na mwenendo wa mambo ndani ya CCM ni kweli, Kikwete hana jinsi bali kukiunga mkono. Pia hii itategemea kama kitapata usajili na kushiriki kwenye uchaguzi ujao.

Bado kuna upenyo mwingine kama msajili wa vyama atawatilia kauzibe. Kuna vyama kama CHADEMA na vingine. vitawapokea. Na katika anguko hili, CHADEMA, kama alivyotabiri Mwalimu Nyerere, itavuna na kuweza hata kuchukua dola. Huenda hii ndiyo sababu ya mwenyekiti wake Freeman Mbowe na Katibu wake Dk. Wilbroad Slaa kutoonyesha nia ya kugombea kwa vile wanajua yupo aliyetabiriwa atakayekuja na kusimama.

Watanzania wengi waliochoshwa na ufisadi na ubabaishaji wangetaka hili lifanikiwe haraka ili waachane na CCM waliyokwisha kuichoka licha ya CCM yenyewe kuchoka na kuchakaa.

Jaribu kupiga picha ya balaa litakaloikumba CCM kama vigogo wanaokubalika ndani na nje ya chama kama Spika wa Bunge Samuel Sitta, Makamu wa Mwenyekiti wa CCM mstaafu John Malecela, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Philip Mangula, wabunge machachari kama Dk. Harrison Mwakyembe, Lucas Selelii, Fred Mpendazoe, Christopher ole Sendeka, Anna Kilango Malecela, William Shellukindo na wengine wanaotambulika kama vinara wa vita dhidi ya ufisadi wakikihama chama.

Hapa bado hujaweka vigogo kama Joseph Warioba, Joseph Butiku, Juma Nkhangaa, Mateo Qares na wengine wanaoonyesha dhahiri kutoridhishwa na mambo katika CCM. Hawa hawana tofauti na lile kundi la ODM lililokifisha chama cha KANU kule Kenya. Hawa ni lulu na almasi inayouzika kwa wapiga kura wetu maskini walioahidiwa vinono wakaishia kulishwa shubiri.

Hawa si wanasiasa wepesi, na hoja yao (kupambana na ufisadi) si nyepesi pia. Wana mtaji mkubwa. Kama ilivyokuwa kwa Wakenya, Watanzania wemeishachoshwa na CCM na madudu yake.

Vyovyote iwavyo, lazima Kikwete achague mojawapo. Je, muda uliobaki kuelekea uchaguzi na shinikizo lililopo mbele yake vinamtosha kufanya mabadiliko yanayoweza kuzuia chama kuzidi kudhoofika na hatimaye kukata roho? Je, kwa timu aliyonayo anaweza kukiokoa hata kama muda utaruhusu?

Hakuna ubishi. Kwa sasa CCM na Kikwete wanakabiliwa na changamoto kuu nne.

Mosi, kuna ufisadi ambao Kikwete aliacha umuamrie hatima ya utawala wake.

Pili kuna maelewano ya hivi karibuni baina ya Rais Karume na hasimu wake mkuu, Maalimu Seif Shariff Hamad. Licha ya kumtega, yamezaa shinikizo kutaka katiba ibadilishwe ili Karume aongezewe muda kinyume cha matarajio ya wengi.

Huu ni mtihani mkubwa kwa Kikwete na CCM. Maana asipounga mkono tendo hili linaloonekana kama ukombozi kwa Zanzibar, uungwaji mkono visiwani utatoweka.

Tatu, ni Kikwete, CCM na serikali yake kushindwa kukidhi matarajio ya Watanzania ambapo kila kitu ni shaghala baghala kiasi cha kufanya wakongwe wa CCM kung’aka wazi wazi kuwa hafai kuruhusiwa kugombea muhula wa pili.

Nne, ni kushindwa kutekeleza ahadi alizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2005. Hili linakuwa pigo takatifu ikizingatiwa kuwa uchaguzi mkuu uko mlangoni. Maana yake ni kwamba Kikwete hana wala hatakuwa na cha kuwambia wapiga kura.

Maana uzoefu unaonyesha kuwa kugombea na kushinda uchaguzi awamu ya pili hutegemea taarifa ya utekelezaji aitoayo mgombea aliyeko madarakani.

Hili linategemea mambo makuu mawili, yaani mwitikio wa wapigakura na jinsi wapinzani watakavyolielezea kwa wapiga kura.

Je, CCM inaweza kuepuka kikombe hiki? Uwezekano ni mdogo. Rejea kichwa ngumu ya viongozi wa CCM ambao huwachukulia watanzania kama mataahira.

Hebu tunukuu maneno ya Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, akijipa moyo: “Naomba nikuulize, Bwana Augostino Mrema zamani alikuwa chama kipi? …na alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani, na sasa yupo TLP. Pia huyo Bwana Seif Hamad wa CUF alikuwa CCM na alihama. Hivyo sisi tupo na tutaendelea kuwepo.”

Huu nidyo upeo wa Makamba. Kama akili za viongozi wa CCM wa juu ni hivi, tutarajie nini?

Rejea kuchafuka kupita kiasi kwa serikali ya sasa na chama tawala. Pia unaweza kujikumbusha hatari ya mitandao ya kimaslahi ndani ya chama.

Hivyo vyote vikichangiwa na uongozi usio na visheni inayoeleweka, ndiyo basi tena. CCM haiwezi kupona piga ua. Yawezekana huu ni mwanzo wa mwisho wa CCM, na utimilifu wa utabiri wa mwanzilishi wake?
Chanzo: MwanaHALISI Jan. 17, 2010.

Mwamini changudoa lakini si mwanasiasa

Kabla ya kuwaletea za leo, ninayo furaha kuwafahamisha kuwa nimepokea barua toka Sauzi ambapo Bwana mkubwa Jack Zuma ameniomba niache kusiliba na kutangaza upuuzi wake.

Makombora yangu yalimlazimisha kuomba msamaha kwa kuzini na kuzaa na Sonono Khoza binti wa rafiki yake tena yanki kuliko babu huyu kiwembe kama jamaa yangu pale ambaye simtaji.

Taarifa nyingine ni ya masikitiko. Kijiwe kinasikitika kutangaza kifo cha ripoti ya tume ya uchunguzi wa wizi wa pesa ya kununulia mkaa ambayo tuliibatiza Richmondulo ya kijiwe uliosababishwa na Mbwa Mwitu a.k.a Ewassa na Rosti Time.

Sambamba na hili ni taarifa kwamba wakuu wa kaya, hatimaye, wamewazidi nguvu makamanda wa ufisadi kiasi cha kuwasilimisha na kuridhia kulala bed moja.

Sikuamini kama Spika Sammy Sixx angejiingiza kwenye mtego wa Ewassa kiasi cha kugeuka kikaragosi ghafla na kuua sifa zote alizojizolea na imani ya walevi! Ama kweli unaweza kumwamini hata changudoa lakini si mwanasiasa!

Anyaway, wanasiasa ndivyo walivyo hawana tofauti na tuvyangu pale Oh.. lo! Hapa nataka kulikoroga! Kwa ufupi ni kwamba pesa ya walevi imeliwa na yale mapapa na majoka aliyesema meku huku Cheka Cheka akichekelea na mlamba viatu wake Mgosi Makambale wa Machungi. Shenzi nyote kabisa! Mkiambiwa kaya hii mnaliwa mnapandisha ilhali ni ukweli usiopingika. Ole wenu mrudie makosa.

Tuendelee. Juzi nami nilijitutumua pale kwenye mashine ya ATM au Automatic Teller Machine kwa lugha ya kitasha. Nilikwenda pale kuchukua vijisenti vyangu ili kuwazuzua walembo wa Bongo wanaoabudia wenye nazo hata kama ni mafisadi.

Kwanza mimi si waziri wala fisadi. Hili lifahamike kwanza. Ingawa si chochote si lolote ukiachia mbali ukuu wa kijiwe, huwa najiona kama malaika na wengine hasa walalahoi ni takataka mbele yangu.

Kufika nikiwa na kirongaronga changu cha kisasa kiitwacho Broadband, nilibofya machine nikaanza kukamua huku nikichonga na kimada wangu aliyekuwa akiningoja kwenye Hoteli ya White Cliff.

Wanukajasho wengine walikuwa kwenye foleni wakingoja zamu zao kuchukua sabuni ya roho ili waende kukosha na kukonga roho. Upo hapa mshirika?

Niliona watu wanaanza kuchukia huku wakitoa maneno machafu. Hawakujua kuwa kumbe pale kulikuwa na kibopa tena mwenye kaya yake yaani mimi niliyekwenda kuchukua pesa niliyokuwa nimewekewa na Kanji baada ya kumpa dili la kusambaza mkaa kwa kijiwe. Upo hapo ndugu yangu.

Usianze kusema mimi ni yule Ngeleza wa madili ya IPTL na Richmond au Kiwila. Mimi nakula rushwa itokanayo na dili za kijiwe si kaya yenu.

Basi mwanawakwa, kutokana kuendelea kuongea kwa pozi na madenguzi huku umati wa wataka sabuni ya roho ukizidi kuumka, mlinzi wa ATM ile aitwaye Mnoko si alikuja kunipa somo kuwa nifanye chap chap kwa vile kulikuwa na wateja wengine wakingojea. Maskini hakujua kuwa mimi ni nani!

Maongezi yalikuwa hivi: “Bosi, naomba ufanye haraka. Kuna wateja wengine wanangojea kuhudumiwa kama wewe.”

Kwa vile Mnoko ni mtu mdogo sikujihangaisha kumjibu. Niliendelea na kuchonga.

Mnoko hakuridhika sawa na wateja wake. Alirudi tena na kusema; “Bosi, kuna wateja wanangoja huduma hivyo naomba ufanye haraka ili nao wapate huduma.”

Mnoko hakujua amechokoza nyuki. Kwa ghadhabu nimjibu. “Unajua mimi ni nani?”

Mnoko alijibu. “Mie hayo hayanihusu zaidi ya kutimiza wajibu wangu.”

Mimi: “Kijana huna adabu na hujui mimi ni nani. Neno moja linatosha kukufuta kibarua na mke na vitoto vyako vitateseka.”

Mteja mmoja alimnong’oneza mwenzie na kusema: “Yule jamaa ni waziri wa kijiwe anayeshughulikia mkaa.”

Mwenzie alisema: “Sasa anapouliza kama mlinzi anajua yeye ni nani inaingilianaje na biashara?”

Mwingine alidakia, “Yule si fisadi wa kisukusi tena mshamba aliyeukwaa ukuu kutokana na kijiwe kutawaliwa na mafisadi tu.”

Huku Mnoko akiwa amepigwa na butwaa akiendelea kunidai nifanye haraka mteja mwingine alisema tena kwa sauti ya juu, “Huyu anayesema yeye ni nani zaidi ya kuwa mshamba mmoja mwenye kijicheo cha kupendelewa? Hebu sikiliza hata lafudhi yake ya unanijuaga mimi ni nani. Wewe ni nani zaidi ya kuwa limbukeni wa kawaida?”

Kutokana na wanakijiwe kuwa na tabia ya kujichukulia sheria mikononi, sikumjibu huyu mkota kwa kuhofia kuzushiwa na kuchomwa moto kama kibaka. Nilifanya haraka na kuchukua pesa yangu tayari kwenda ofisini kwangu kumfukuzisha kazi Mnoko kwa unoko na ukosefu wake wa nidhamu.

Pia sikutaka kuendelea kuwa pale nikizozana na Mnoko kuhofia wambea wajiitao waandishi wa habari kurekodi maongezi yetu nikaibika. Kweli hasira wakati mwingine hasara. Maana niliumbuka siku ile hakuna mfano!

Nasikia na lisilikali fisadi na jizi liliwahi kumwambia Sammy Sixx: “Unajua sisi ni nani?” Matokeo yake wameichinja Richmonduli tena kwa kutumia mikono ya Sixx mwenyewe ambaye sijui ataweka uso wake wapi kama kweli ana chembe ya roho!

Juzi nasikia Ewassa na Rosti Time, waliangusha bonge la pati kusherehekea kuzikwa aibu zao! Ama kweli kaya hii ni Danganyika tena danguro la mafisadi kutanua na kuiba watakavyo! Sijui hata mantiki ya msanii kwenda akijigamba kuwa atapambana nao ilhali ndiyo wanaoamua akae ukuuni.

Angefanya fyoko wangemtimua na kukichagua kikaragosi kingine tayari kusimamia wizi na ujambazi wao. Kumbe mzee Butuka alipobotuka na kubwatuka akisema mkuu wa Kaya yetu hapa kijiweni ni mtumwa wa mafisadi hakudanganya!

Wengi walikuwa wanamtaka afanye maamuzi magumu wasijue hatafanya. Unadhani ni mchezo kufanya uamuzi mgumu wa kujivua nguo hadharani na kutembea kama hayawani kama kuendelea kutumiwa na kina Richmonduli na Kagodoka?

Laiti walevi wangekuwa wana akili na si kuendeshwa na matumbo yao. Huu ulikuwa wakati wa kumtimua bwana mazingaombwe na kujikomboa. Kwa vile aliyewaloga alikwisha kufariki, ni mganga gani atawasaidia?

Kwa vile walevi na wakubwa zao wameamua kufanyiana uchangudoa, hakuna wa kuwalilia bali wajilaumu na kujililia wenyewe. Ukitaka kujua kuishiwa, aanza kuuliza. Unajua mimi ni nani? Kwani we Mungu au gendaeka wa kawaida ngurumbili mwenye kila mapungufu.

Hata wapuuzi kama Saddam Hussein, Chemical Ali na majuha wengine walizoea kuwauliza Wairaki: “Unajua mimi ni nani?”

Wewe si sawa na inzi anayeshida na kutapika kwenye viatu vya wafadhili kama alivyosema balozi wa Uingereza. Je na Richmonduli na Kagodoka ni nani?

Ngoja niende zangu Idodomya nikawalambe bakora waheshimiwa wa mjengoni.
Chanzo: Tanzania Daima Feb.17, 2010.

Thursday 11 February 2010

AU: Sudan like powder keg!

In an interview with French broadcaster RFI recently, AU commission chairman Jean Ping was quoted as thus: "We have a feeling that we are sitting on a powder keg."

It is true. But who’s to blame in the first place? AU has always sits on many powder kegs such as, Madagascar, Western Sahara Somalia, Sudan and Zimbabwe just to mention but a few. Unfortunately, it hasn’t learned from the past experience in which it always maintained its double standard and flip-flop. Will this prevent a baby from taking a Hoober-Bloober Highway ? Noway. The baby must be born despite all pangs the mummy is to go through.

"Will the independence of Southern Sudan not lead other players in Darfur and in other places, which are currently not asking for independence, to seek independence as Southern Sudan will have done?"

This is but pure water and on whatever foundation this shallow thought is under-girded, won’t move things forward. What emollient claptrap! By the way where was AU, and what constructive role did it play, when things were taking this turn? Why didn’t this happen when Eritrea seceded from Ethiopia ? If it is a solution so be it.

AU was told to intervene fully in Darfur ; it didn’t apart from sending a weak contingent. Instead, many of heads of states making AU are openly supporting Sudanese butcher Omar Bashir. They’ve ganged behind him to see to it that he is not being submitted to ICC for fear of others to follow thereafter.

Ping and all the likes, agog and gaga, tell it to the birds. The people of South Sudan have to decide their destiny and so be it. I know. Many opportunists would like to team up with the top dogs (Bashir) to underrate underdogs (Mayardit). But again, who knows? Today’s top dog can become an underdog and the underdog of today becomes the top dog of tomorrow. We’ll soon see this in Sudan , pronto.

While AU is playing schnook role, Bashir, despite all, is upbeat. He’s quoted as thus: "We will work to make unity attractive to all Sudanese, but we will respect the wish of southerners whatever the outcome and we will be the first to recognize such a southern state."

Bashir said the same at a rally marking the 5th anniversary of the peace pact that ended more than 20 years of civil war between the north and south on 21st January 2010.

This was the first time for Bashir to offer the olive branch to his brethren in south. Was this an accident or claptrap? Is Musumar (nail) -as Darfuris would put it- eating him up? Is his Northerners-are-better-to-rule milieu turning against itself?

He too well knows. He can not stand in the way of the people of South Sudan to decide their future. He knows. Shall he repeat the same mistake; they’ll go back to the bush. He knows how determinedly ready they are. Nobody wants this to reapt. And those saying all this nonsense need to be told to their face that south Sudanese will nary compromise their freedom and resources with anything.

African rulers and their conspirators can nary weigh anything up so as to wish well people suffering under Khartoum bloodthirsty regime they fully support and nourish. If Darfur or Nuba Mountains goes freedom that will bring peace to their people as opposed to current carnage, so be it. It is better to have a peaceful fragmented country than a tyrannically united one.

Those wrongly thinking that South Sudan and North Sudan will not make good neighbours should ask themselves. Why did the duo consent to end a two-decade war? New North Sudan won’t attempt any aggression thanks to having no muscles. Methinks. North Sudan will be weaker than South Sudan politically and economically.

Even if it attempts to assault south, it won’t thanks for what it evidenced during the twenty-one wars with South. This is when the necessity of peace comes in.

There is a season for everything under the sun. There are times for wars and times for peace. There are times for life and times for death; times for fears and times for strengths. Time for strength for South Sudan is approaching. And those worrying about this will soon be proved dead wrong.

Time for the reconstruction and resurrection of South Sudan is indeed now. It won’t pay off to stand in the way for this natural phenomenon to take place. By metamorphosis or symbiosis South Sudan must exist and excel.

You can see this in the words of Kenyan PM Raila Odinga he said at the just ended AU conference in Addis Ababa . He was quoted as thus: "Given the unprecedented advances the CPA entrenched in promoting democracy, it has been distressing to learn that senior-most officials in the two organisations (UN and AU) oppose the referendum’s option of creating a sovereign nation in the South."

Despite AU openly supporting Khartoum regime, the PM did not mince his words. He added: "Having done so much to advance this historic process of self-determination, it is preposterous that anyone would now seek a predetermined outcome."

When it comes to Sudan crisis Botswana and Kenya have called a spade spade. This makes them have high moral authority when it comes to comment on the future of the same. So it is better for those that failed South Sudan to keep their big mouths shout and evidence history being made.

Come shine or high water, South Sudan will nary remain in an abusive and exploitative marriage with the north.
Source: The African Executive Magazine Feb. 10, 2010.

Haiti’s calamity the hypocrisy of African rulers



The world is still grappling with what happened in Haiti recently. On 12 January, 2010 Haiti was hit by a killer earthquake that left tens of thousands dead and millions either injured or their properties destroyed.

After the quake struck, the world, led by US, was racing to Haiti to help the victims. This is a good thing indeed. However, some African countries used it to show their hypocrisy and disregards of their people and their constitutions.

The first African country to chip in was Senegal. Whilst other countries were trying to bolster quake efforts, some African rulers displayed poor and bad judgements. Senegalese president, Abdulaye Wade, interestingly came in with the offer of land or houses to Haitians that were ready to return back home-Africa. How much money or soldiers did he send to help the victims? Zero. Is this what really Haitians need now? Nay!

Senegal’s president says he’ll offer free land and “repatriation” to people affected by the earthquake in Haiti. “The president is offering voluntary repatriation to any Haitian that wants to return to their origin,” said Mr Wade’s spokesman, Mamadou Bemba Ndiaye.

Try to imagine how tormenting such a sickly proposition made by a ruler of dirt-poor country. Wade was quoted saying that Haitians were sons and daughters of Africa, since Haiti was founded by slaves, including some thought to be from Senegal. In other words, the Darfuris are not sons and daughter of Africa! That’s why Wade as an African, ruler and a Muslim has nary bothered to welcome them.
Many people who know Africa well were dismayed and buffed by this make-believe generosity aimed at gaining international notoriety and pizazz. Questions on this were many more than answers. Why should he wait for the calamity to strike? Why promising to offer houses to Haitians whilst many Senegalese have no houses? Was this a political capital or what? Does the constitution of Senegal allow president to offer part of the land to anyone he deems fit? Did he consult with the people? Can this help Haiti and Senegal altogether?

What appalls, those Senegalese suffering from all miseries including having no houses, unluckily, are the ones that voted for Wade apart from their tax giving him the guts of thinking about unthinkable. This proves how Wade has become myopic and a dictator, despite being a professor of law that he’s breaking. Does Wade regard Senegal as his private estate he can offer to anyone? He is totall off rails.

By and large, Haiti is even better than Senegal with the GDP per capital of $1,066 (as per IMF economic outlook database) compared to Haiti ’s GDP per Capital was $1,300 (2008). As of 2008 the population of Senegal was 12,211,181, whilst Haiti was 9,780,064.


Like many African countries, poverty is rampant in Senegal. Also, GDP per capita has actually declined over the past 25 years. The United Nations Development Programme (UNDP), which classifies countries according to their human development index score (HDI), ranked Senegal 155th out of 174 countries in 1998, while the United States ranked third. The HDI is a composite index that examines specific figures on education, health, and standard of living. Senegal’s low ranking reflects the country’s low development in these areas, consistent with its overall poverty.

Africa has nary been bankrupt when it comes to goodies and baddies. So too, hypocrisy was displayed by war-torn DRC that sent $2,500,000 to help quake victims. Surprisingly, this is one ninth of 23,000,000 that Britain offered to quake victims! This left Congolese shocked. They could not understand how a country with the highest number of IDPs could attempt such a thing in the first place!

Answering his critics, Information Minister Lambert Mende was quoted by BBC recently as thus: “Congo isn’t bankrupt… our own problems shouldn’t prevent us from helping a brother country”. This was echoed by Academic Ntanda Nkere, who was quoted as thus: “It’s a contradiction to see a country which is facing serious financial problems giving away $2.5m”.

This is not the first time a begging African country helped another. In 2008, Tanzania, the country that tops the list of begging and poor countries on earth, donated various medicines on top of money. Medicines so donated to Zimbabwe included over forty boxes of Ciprofloxacin, Doxycline, Erythromycin, Sodium Lactate, Sodium Chroride and Cresol. Other parcels in this bragadaccios included Chlorinated Lime, Methylated Spirit, plasta, bandage, wool, etc., that were received by two Zimbabwean diplomats in Tanzania.

One interesting thing did happen. When Tanzania was offering highly needed stuff at home to Zimbabwe, at Mwananyamala, Temeke and Ilala hospitals in Dar es Salaam, patients were sleeping three abed, not to mention paying for their own medicines! Is this love? Bob Marley would have asked. The irony is the other day Kenya will send its army to Darfur to prevent genocide, though the same failed to stop post-election massacres. The same Kenya that neared the verge of self extermination is presiding over seeking peace for Somalia! The Swahili sage has it that the ape does not see its bum.

Africa has nary run out of controversy. Remember Sudan who’s over 5,000,000 in Darfur depend on UN food support, is currently selling sorghum to Middle East. To add more insults to the injury, the same has given a big chunk of land to Arabs to produce food for their citizenry whilst hers are dying day in day out! Kenya too once thought about allowing foreign investors to invest in agriculture in Kenya, whilst the majority of Kenyans are landless. What hypocrisy!

Many still wonder. Neither DRC nor Senegal has ever extended such supports to the people of Darfur that are dying everyday thanks to the man-made calamity. Instead, the same countries, under AU, vowed to openly and fully support their butcher, Omar al Hassan Bashir!

Not only that, ever since Africans Muslims of Sudan, who believe they are Arabs, started killing their brother Africans and Muslims, African Muslims have nary showed any solidarity to fight for them like they do for Palestinians!

Africans, as well as their rules, have a candle love especially where there is popularity to be garnered.

While African rulers were trying to square the circle, a relatively small city of St. John’s, the capital of the province of Newfoundland and Labrador, came up with something possible. It urged all Canadian cities to see to it that they build Haiti .

Back to our rulers… is this generocity or hypocrisy for countries suffering from abject poverty to embark on a candle love? Help your people you exploit time and again in lieu of bragadaccios of helping others. Charity begins at home.
Source: Afro Spear Feb. 2010..

CCM ife, Watanzania wakombolewe

KATIKA harakati za kujinasua (bila mafanikio) kutoka kwenye ufisadi, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekumbwa na migawanyiko ambayo inaonyesha kitazidi kuparaganyika na, hatimaye, kufa.

Huu ni ukweli. Si fikra wala ndoto tena. Hapa ndipo utabiri wa muasisi wa CCM Hayati Mwalimu Julius Nyerere utakapotimia.

Hata kifo cha hivi karibuni cha muasisi mwingine aliyekuwa amesalia, Mzee Rashidi Kawawa, aliyekuwa na mvuto na uwezo wa kufanya mambo nyuma ya pazia, ni pigo jingine kwa CCM.

Hata hivyo, kuna faida kwa mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, hasa kutoka kwa wapenda maendeleo walio wengi. Faida hii itapatikana kama atacha CCM ijifie ili Watanzania, akiwamo yeye, wakombolewe.

Wachache wanaofaidika na utawala wake watamlaumu. Watajaribu kujinasua toka kwenye pigo hili takatifu lisilozuilika sasa, ingawa kwa bahati mbaya, muda umeshewatupa mkono. Walichelewa kusoma alama za nyakati. Wanasukumwa na matukio na si mipango na mikakati.

Kama Kikwete atahakikisha CCM inazikwa wakati wowote kuanzia sasa, atajizolea umaarufu kama alivyofanya kiongozi wa mwisho wa Muungano Kisoshalisti wa Jamhuri za Kisoviet wa Urusi (USSR), Mikhail Gorbachev.

Hapa, kuna shuruti. Salama ya Kikwete itategemea atakavyoshughulikia mafisadi papa waliotamalaki kwenye chama na serikalini, ambao wengi ni washirika, wawezeshaji na maswahiba zake wa karibu.

Lakini kuwashugulikia hakuwezekani bila kurejesha maadili ya uongozi. Hili nalo linaweza kumpatiliza hata yeye; maana watu wenyewe wanajua siri na udhaifu wake.

Ana mtihani sawa na ule alioupata Mfalme Suleiman alipoletewa kesi ya wanawake kugombea mtoto mmoja.

Kuepuka hili anaweza kufanya mambo yafuatayo:

Ama afumbe macho awatose mafisadi ili yeye anusurike, au aanzishe chama chake kama alivyofanya Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika.

Kuacha CCM indelee kumeguka kama ilivyotokea kwa KANU huko Kenya, kimsingi, ni furaha kwa Watanzania maskini. Hii imeshaanza kujitokeza kutokana na kuundwa kwa chama kipya kinachozungumzwa sana sasa (Chama Cha Jamii (CCJ)).

Anaweza kuunga mkono chama hiki kisiri siri kiwe kama mtumbwi wa uokozi kwake hata kama hatakuwa madarakani. Rais Amani Karume amefanya hivyo na hasimu wake mkuu, Katibu mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Seif Shariff Hamad. Hili linawezekana. Kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu bali maslahi ya kudumu.

Kama tetesi kuwa chama hiki kinaundwa na vigogo wasioridhishwa na mwenendo wa mambo ndani ya CCM ni kweli, Kikwete hana jinsi bali kukiunga mkono. Pia hii itategemea kama kitapata usajili na kushiriki kwenye uchaguzi ujao.

Bado kuna upenyo mwingine kama msajili wa vyama atawatilia kauzibe. Kuna vyama kama CHADEMA na vingine. vitawapokea. Na katika anguko hili, CHADEMA, kama alivyotabiri Mwalimu Nyerere, itavuna na kuweza hata kuchukua dola. Huenda hii ndiyo sababu ya mwenyekiti wake Freeman Mbowe na Katibu wake Dk. Wilbroad Slaa kutoonyesha nia ya kugombea kwa vile wanajua yupo aliyetabiriwa atakayekuja na kusimama.

Watanzania wengi waliochoshwa na ufisadi na ubabaishaji wangetaka hili lifanikiwe haraka ili waachane na CCM waliyokwisha kuichoka licha ya CCM yenyewe kuchoka na kuchakaa.

Jaribu kupiga picha ya balaa litakaloikumba CCM kama vigogo wanaokubalika ndani na nje ya chama kama Spika wa Bunge Samuel Sitta, Makamu wa Mwenyekiti wa CCM mstaafu John Malecela, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Philip Mangula, wabunge machachari kama Dk. Harrison Mwakyembe, Lucas Selelii, Fred Mpendazoe, Christopher ole Sendeka, Anna Kilango Malecela, William Shellukindo na wengine wanaotambulika kama vinara wa vita dhidi ya ufisadi wakikihama chama.

Hapa bado hujaweka vigogo kama Joseph Warioba, Joseph Butiku, Juma Nkhangaa, Mateo Qares na wengine wanaoonyesha dhahiri kutoridhishwa na mambo katika CCM. Hawa hawana tofauti na lile kundi la ODM lililokifisha chama cha KANU kule Kenya. Hawa ni lulu na almasi inayouzika kwa wapiga kura wetu maskini walioahidiwa vinono wakaishia kulishwa shubiri.

Hawa si wanasiasa wepesi, na hoja yao (kupambana na ufisadi) si nyepesi pia. Wana mtaji mkubwa. Kama ilivyokuwa kwa Wakenya, Watanzania wemeishachoshwa na CCM na madudu yake.

Vyovyote iwavyo, lazima Kikwete achague mojawapo. Je, muda uliobaki kuelekea uchaguzi na shinikizo lililopo mbele yake vinamtosha kufanya mabadiliko yanayoweza kuzuia chama kuzidi kudhoofika na hatimaye kukata roho? Je, kwa timu aliyonayo anaweza kukiokoa hata kama muda utaruhusu?

Hakuna ubishi. Kwa sasa CCM na Kikwete wanakabiliwa na changamoto kuu nne.

Mosi, kuna ufisadi ambao Kikwete aliacha umuamrie hatima ya utawala wake.

Pili kuna maelewano ya hivi karibuni baina ya Rais Karume na hasimu wake mkuu, Maalimu Seif Shariff Hamad. Licha ya kumtega, yamezaa shinikizo kutaka katiba ibadilishwe ili Karume aongezewe muda kinyume cha matarajio ya wengi.

Huu ni mtihani mkubwa kwa Kikwete na CCM. Maana asipounga mkono tendo hili linaloonekana kama ukombozi kwa Zanzibar, uungwaji mkono visiwani utatoweka.

Tatu, ni Kikwete, CCM na serikali yake kushindwa kukidhi matarajio ya Watanzania ambapo kila kitu ni shaghala baghala kiasi cha kufanya wakongwe wa CCM kung’aka wazi wazi kuwa hafai kuruhusiwa kugombea muhula wa pili.

Nne, ni kushindwa kutekeleza ahadi alizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi wa 2005. Hili linakuwa pigo takatifu ikizingatiwa kuwa uchaguzi mkuu uko mlangoni. Maana yake ni kwamba Kikwete hana wala hatakuwa na cha kuwambia wapiga kura.

Maana uzoefu unaonyesha kuwa kugombea na kushinda uchaguzi awamu ya pili hutegemea taarifa ya utekelezaji aitoayo mgombea aliyeko madarakani.

Hili linategemea mambo makuu mawili, yaani mwitikio wa wapigakura na jinsi wapinzani watakavyolielezea kwa wapiga kura.

Je, CCM inaweza kuepuka kikombe hiki? Uwezekano ni mdogo. Rejea kichwa ngumu ya viongozi wa CCM ambao huwachukulia watanzania kama mataahira.

Hebu tunukuu maneno ya Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, akijipa moyo: “Naomba nikuulize, Bwana Augostino Mrema zamani alikuwa chama kipi? …na alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani, na sasa yupo TLP. Pia huyo Bwana Seif Hamad wa CUF alikuwa CCM na alihama. Hivyo sisi tupo na tutaendelea kuwepo.”

Huu nidyo upeo wa Makamba. Kama akili za viongozi wa CCM wa juu ni hivi, tutarajie nini?

Rejea kuchafuka kupita kiasi kwa serikali ya sasa na chama tawala. Pia unaweza kujikumbusha hatari ya mitandao ya kimaslahi ndani ya chama.

Hivyo vyote vikichangiwa na uongozi usio na visheni inayoeleweka, ndiyo basi tena. CCM haiwezi kupona piga ua. Yawezekana huu ni mwanzo wa mwisho wa CCM, na utimilifu wa utabiri wa mwanzilishi wake?
Chanzo: MwanaHALISI Jan. 27, 2010.

Zanzibar leteni hoja kuvunja Muungano

MAONI ya msomaji wangu aliyejitambulisha kwa jina la Hilal, kutoka Zanzibar, yamenifanya niandike makala hii. Japo msomaji aliniandikia matusi, sikumjibu. Badala yake nimeona nijadili kiini hasa cha tatizo ambacho wengi wanakwepa kujadili.

“We chogo, mambo ya Zanzibar tuachie Wazanzibari, nyie yawahusu nini? Tunapochinjana mnachekelea. Tuachieni hii fursa tuamua mambo yetu,” alisema Hilal.

Mwanzoni nilidharau maoni ya mpendwa huyu. Niliposoma makala ya Salim Said Salim yenye kichwa: ‘Mambo ya Zanzibar waachiwe wenyewe,’ nilizidi kukuna kichwa.

Kabla ya kuzama kwenye kile kinachowashinda wakubwa zetu hata CUF, ngoja nimnukuu. “Baadhi ya waandishi wa habari wa Dar es Salaam ambao hata Zanzibar hawajafika na kuona harakati za uchaguzi ambapo watu kutoka Bunju, Kawe, Bagamoyo huja kupiga kura wamekuwa wataalamu wa masuala ya Zanzibar .”

Wao wataacha mambo ya Bara? Rejea kuwa na wabunge kwenye Bunge la Muungano ambapo hawatoki nje yanapojadiliwa mambo yasiyo ya Muungano.

Nukuu ya pili ya Salim: “Sijuwi wapi baadhi ya viongozi wa bara wamepata ujabari wa kutaka kuwaamulia watu wa Zanzibar mambo yao. Labda walitakiwa ushauri na kama ni hivyo ni nani hao waliowapa kazi hiyo?”

Ni kwa sababu wanatekeleza sera ya CCM chama tawala kilichowapa huo ulaji akina Karume wanaoonekana wa maana sana sasa kuliko chama.

Kwa kifupi, nilipata maoni mengi sana na Bwana Salim, mwandishi mkongwe, naye aliandika mengi.

Chanzo cha yote hayo ni muungano. Muungano ulifanywa na watu wawili. Hii ilikuwa sahihi wakati ule lakini si sasa ambapo umekuwa mama wa matatizo yote (si chaguzi kama tunavyoaminishwa bali muungano ambapo serikali ya muungano hutuma majeshi kuwahujumu Wazanzibari).

Japo ni pigo na aibu kwa taifa kuvunja muungano, kama Wazanzibari na Watanganyika wataridhia na iwe. Maana wakubwa zetu wameshikilia masilahi binafsi kwa muda mrefu na kuacha muungano uoze na kuchakaa kiasi cha kuonekana hauna maana. Ethiopia ilipogundua inatumia muda na raslimali nyingi kupambana na Eritrea iliridhia kuiacha iende kivyake. Na hii iliepusha hasara kubwa katika mali na roho za watu.

Wazanzibari wanaona kama Bara imekuwa kikwazo cha uhuru na maendeleo yao. Ni kweli. Ukirejea kwenye kadhia ya mauaji ya 2001 na mitafaruku mingine, kuna ukweli usiopingika ingawa ukilinganisha faida na hasara za muungano, hili si jibu pia.

Watanganyika nao wanajiuliza. Kwanini kung’ang’ania kijisehemu ambacho hakifikii hata ukubwa wa Wilaya ya Kahama?

Kutokana na haki na shuruti za muungano kutowekwa wazi kwa Watanzania, kila mmoja anamshuku mwenzie hata kwa makosa.

Kama tumeshindwa kuishi pamoja, basi tuachane au kuridhia kukata kiungo kama alivyosema Salim.

Nitatoa sababu: Kwa sasa muungano wetu si muungano kitu bali mgongano uliowekwa chini ya busati na wakubwa wanaofaidi matunda yake.

Pili, bila kuurekebisha (kuurudisha kwa wananchi wa pande zote mbili) utaendelea kutupotezea muda na raslimali. Ingawa waasisi wa muungano waliungana kwa nia nzuri, hawakufuata utaratibu (kuanzishwa na kuridhiwa na wananchi). Ndiyo maana umeshindwa kuwaunganisha vilivyo walengwa. Hata ukivunjika hawatajali japo wapo watakaojutia.

Watawala walizoea kusema: wakati ule hatukuwa na uwezo kielimu kuhusishwa kufanya hivyo. Lakini sheria ya mahusiano huwa haiangalii kiwango cha elimu bali utashi, ulazima na kufuata kanuni.

Tatu, hata baada ya wananchi kupata hicho kiwango cha ‘elimu’, bado hawakuhusishwa hadi leo licha ya kupiga makelele mengi kutaka wahusishwe.

Nne, muungano umeendelea kuwa mali ya watawala huku wananchi wakilazimishwa kuukubali kwa kuaminishwa ni kitu bora kuwa nacho. Ndiyo muungano ni kitu bora. Lakini ni hiari kukipata na kukimiliki.

Wananchi wamekuwa wakiaminishwa na kulazimshwa kuukubali muungano kutokana na watawala kuutumia kusimikana na kugawiana madaraka. Mfano, kama si kutumia kichaka cha muungano, Amani Karume asingekuwa rais wa Baraza la Mapinduzi (SMZ).

Maana kwa anayekumbuka uchafu na wizi uliotembezwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi wa 2005 na hata kabla ya hapo hawezi kuona mantiki ya mtu huyu kuwa madarakani.

Hivyo, kinachofanyika kwenye kivuli cha muungano, ni CCM na kundi la watu wachache kuikalia Zanzibar huku wakiishika mateka. Kwanini umma wa pande mbili uumie kwa ajili ya masilahi ya kundi dogo la watu?

Muungano umeifanya Zanzibar ijihisi kuwa kikaragosi cha Bara. Rejea ilivyotaka kuwa mwanachama wa OIC ikafurushwa na kukaripiwa kama mkoa badala ya nchi yenye mamlaka na haki zake kwenye muungano.

Pia kuna mawazo kuwa Zanzibar inabebwa na ni zigo kwa Bara. Rejea utitiri wa wabunge na wawakilishi ilio nao Zanzibar. Hebu angalia kijisehemu kisicholingana hata na Wilaya ya Kahama kuwa na wabunge na wawakilishi wengi kuliko wilaya za Tanganyika. Hii ni nini kama si kuwabagua Watanzania kwa njia ya sehemu watokako?

Angalia kiwango cha maisha. Wakati ni juzi juzi tu Zanzibar wameanza kulipia ankara zao za umeme wakati mtu wa Mtera akilanguliwa umeme unaozalishwa uani mwake. Lakini mtu wa kilometa zaidi ya mia tatu kisiwani alikuwa akitanua kwa kuufaidi bure!

Kifupi, muungano umechakaa; unahitaji kufanyiwa marekebisho; lakini baada ya kupitishwa kura ya maoni kuona kama wananchi bado wanautaka au la.

Kulikuwa na sakata la Zanzibar kutaka Wabara wabebe vitambulisho kuingia Zanzibar huku Wazanzibari hawafanyi hivyo wanapokuja Bara. Hili linachukua nafasi ya paspoti zilizotumika muda mrefu kama alama ya ubaguzi na ukosefu wa ulinganifu na haki sawa.

Kuna maswali muhimu ya kujiuliza. Je, hii ni tabia ya chako kitamu changu kichungu au ni ile hali ya Zanzibar kuona kama haifaidiki na Muungano? Mwanzo wa ngoma ni lele. Kwa wenye akili, tamko hili lina maana na maanawia. Je, na Bara ikiwataka wafanye hivyo wataridhika?

Jana walitutakisha vitambulisho kuingia Zanzibar bila kujiuliza: hao Wakenya au Waganda watakaotokea Bara si watahitajika kugongesha upya kwenye pasi zao?

Je, ina maana Wazanzibari hawajui haki ya usawa kwa Watanzania ndiyo inafanya kila Mtanzania awe na uhuru wa kwenda popote na kuishi popote ndani ya Jamhuri, uhuru ambao wanautumia kuliko hata hao wabara wenyewe wanaowatakisha vitambulisho? Tunadhani wanajua tena sana.

Who will get the cat out of the hat? Je, Bara, kutaka kuonyesha kuwa inajua kinachoendelea, iwatakishe Wazanzibari vitambulisho kwa ajili ya usalama wake?

Je, huu ndio mwanzo wa kuuchokana na kuanza kuupekenyua Muungano ili hatimaye uvunjike? Je, ukivunjika nani atakosa nini na nani atapata nini? Hatujui nani atakuwa wa kwanza kulia!

Wakati tukitafakari hayo, hebu tuzingatie baadhi ya matukio na hali ambazo zina ukweli na ushahidi wa kutosha juu ya umuhimu wa Muungano, nani ananufaika nao na nani hanufaiki.

Historia ni shahidi. Nje ya Muungano hakuna yeyote kati ya hawa wanaotumbua marupurupu ya ukubwa atakalia kiti alichokikalia. Nje ya Muungano serikali ya Zanzibar itaundwa na Chama cha Wananchi (CUF) na si CCM, taka usitake.

Rejea chaguzi tatu zilizopita ambapo Baraza la Mapinduzi na serikali yake vilishindwa ikabidi Bara iingilie kuwaokoa kijeshi. Je, hawa wamesahau au kuna sehemu wanatarajia kupata masilahi zaidi nje ya Muungano?

Tujalie hao Wabara nao wakianza choko choko wakaanza kuuliza, hivi Zanzibar ina nini cha mno kutubagua kiasi hiki? Je, nani anauhitaji Muungano zaidi ya mwingine?

Je, hili si changamoto kwa Rais Jakaya Kikwete aliyeahidi kuudumisha Muungano uliokuwa umesahauliwa na mtangulizi wake, Rais Mkapa? Je, atakubali kuuona Muungano unayoyoma akibakia kuonekana ameshindwa?

Kupitia chaka la Muungano, wakati dunia inapambana na ongezeko la watu, wao hawana tatizo na hilo maana wana mahali pa kupeleka watu wao wa ziada.

Wakati dunia inapambana na wakimbizi wa kiuchumi, Zanzibar hawana hili tatizo; kuna pa kukimbilia. Si kwa hayo tu. Hebu jikumbushe kadhia zao zote. Walikimbilia wapi kama si Bara? Leo hili halionekani! Tunaambiwa. Tuache wafaidi uhuru wao!

Leo wanatuzushia kuwa kikwazo. Kesho watazusha pesa na baadaye hata uraia huru. Kimsingi, kama tukizingatia maana ya Tanzania kuwa ni Tanganyika + Zanzibar, hakuna haja ya kuwa na Wazanzibari. Kuzaliwa kwa Tanzania kuliua utanganyika na uzanzibari. Kama hali hii itaendelea, watakuja kurejea Watanganyika. Hapa ndipo Christopher Mtikila anapoona mbali zaidi ya watawala wetu.

Ni wakati muafaka kwa wataalamu wa Katiba kutupa namna ya kuvunja huu Muungano ili tuache kulaumiana na kupoteza muda bila sababu.

Kabla ya kuanza kugawana mbao, ni vizuri Serikali ya Muungano na SMZ kutangaza mgogoro wa kikatiba mbele ya Mahakama ya Katiba ili uamuzi utolewe.

Kama siyo, kuna haja kuepuka mizengwe ambayo, badala ya kutatua matatizo ya Muungano, huyalimbika kwa kutimua wanaochafua ‘hali ya hewa’ na matatizo hubakia pale pale yakizaliana.

Lakini kuna haja ya kujua hatima ya nchi hii ambamo kila upande unaona kama unaumizwa na kutumiwa na upande mwingine. Je, haya si madhara na matokeo ya watu wachache kujichukulia mamlaka na kupitisha maamuzi yanayougusa umma bila kuushirikisha?

Je, hii ni changamoto kuwa wakati umefika wa Muungano kupelekwa kwa wenyewe au kuuchinja?

Kwa maana nyingine, kinachofanyika ni ishara kuwa maandishi yako ukutani- Muungano una mshikeli. Muungano ni watu, si watawala na vyama vyao.

Japo Muungano ni mali ya wananchi walioachwa nje muda mrefu kufanya maamuzi, wasiuchukulie kama kitu kisicho na faida bali wapewe muda wa kutafakari njia ya kuchukua kuelekea hatima ya Muungano.

Ni vizuri Muungano ukawa wa Watanzania badala ya watawala. Si kupiga chuku. Kwa sasa, nchi inatawaliwa chini ya Muungano wa watawala unaoitwa Muungano wa Tanzania!

Zingatio: Matatizo ya Muungano hayawezi kuachiwa ama kutatuliwa na watu wawili au vyama viwili bali wananchi wa pande zote.

Tuwatoe wananchi kwenye kiini macho cha masilahi ya Zanzibar yanayowaengua Wabara wakati wa neema na kuwahitaji wakati wa dhiki.

Kwa vile sasa hatuaminiani wala kuhitajiana, basi leteni hoja ya kuvunja Muungano ili kila mtu afaidi vyake, inagawa binafsi bado naupenda Muungano na nauunga mkono.
Chanzo: Tanzania Daima Feb. 10, 2010.

Jack Zumaa umeniponza

Jack Zuma rais wa Sauzi anayetuhumiwa kuzaa na binti wa rafiki yake.
WIKI jana ilikuwa tuandike barua kwa Jack Zumaa kumfahamisha kuwa hatupendi matendo yake.

Kipigo na mauaji ya jamaa yetu yalitufanya tusifanye hivyo. Hata hivyo nina rafiki yangu Sibusiso Sibulele wa Ngubane huko Bondeni. Alinipa mwaliko niende kushuhudia bila kujua nami yangu yanajulikana!

Kwanza naomba vijogoo mnisamehe. Silengi kumnanga mtu bali kueleza ukweli. Nitamnangaje wakati nami ni kijogoo tena kusiri? Ila jina la Jack lapaswa kuchunguzwa kuona ni kwanini kina Jack wanapenda urodi sana.

Ilibidi niende Sauzi kuona wasauzi wanalichukuliaje balaa la uzinzi tena wa mkubwa ili nijiandae kupambana na maswali ya wapiga kura kwenye uchaguzi wa uchafuzi ingawa nilishatabiriwa kushinda kwa kishindo cha radi.

Niliondoka Bongo na pipa la Air South Africa ile iliyoua Air Tanzia. Nilitua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oliver Tambo bila taabu. Huyo! Nilichukua mchuma hadi Kwazulu maeneo ya Mphumalanga.

Stori nilizokuta zinatia kinyaa na kufurahisha! Wasauzi wamegawanyika nusu kwa nusu. Wapo wanaounga mkono uchafu huu kwa vile Jamaa ni mzuluzi mwenzao wanasema; hakuna kosa kwa vile Jack ametoa inhlawulo. Kwa wasiojua lugha ya isizulu, inhlawulo ni faini ya ugoni.

Wapo wanaopinga na kutaka kunywa damu ya Zumaa kwa hasira.

Hakuna kilichonishangaza kama chama cha Zumaa kuunga mkono uzinzi huu unaopingana na sera za serikali kupambana na umeme! Kumbe utumwa mwingine watu huutafuta wenyewe!

Kweli sisi binadamu ni wapuuzi hakuna mfano. Nani angejua kuwa vijogoo wengi wanatucheka sisi vijogoo wenzao kwa vile hawajanaswa? Hata yule DJ aliyefia kifuani angekuwa hai huenda angecheka.

Si ajabu na jamaa yangu naye anachekelea asijue, yake kama yangu, yanajulikana kaya nzima kuwa ana ka-ugonjwa kanakoitwa Tigerwoodiosis karikogundulika huko kwa Joji Kichaka hivi karubuni?

Unajua kijiweni walipopata habari za uchafu na uchafuzi wa Zumaa kabla ya kujua wangu walisemaje? Eti wanataka kuanzia sasa mkuu wa kijiwe hata kaya lazima atangaze idadi ya hawara zake na watoto aliowazaa nje ya ndoa! Hivi wangapi watapona jinai hii?

Kwanza, wanafanya makosa. Hawajui wakuu huwa hatukosei. Hata ukizini, huitwi mzinzi bali dume la mbegu kama rafiki yangu Zumaa.

Hakuna jitu nalichukia kama Msomi. Eti linasema huu ni ufisadi wa ngono! Hivi bila hii kitu lingezaliwa? Linaenda mbele zaidi na kudai ni udhalilishaji wa akina mama utadhani hawapati urodu duniani! Eti linashauri vijogoo wengine wamendee vidosho wa Zumaa hata mimi ili tujue inauma kiasi gani kufanya upuuzi huu!

Bi Mkubwa wangu huwezi kumpata maana nimempa ulaji kwenye NGO. Na kwa vile ana ugonjwa wa gettingrichiosis, sitegemei agawe uroda wangu wala kujali kama ninakula urodi na visichana mitaani hata viwe vibinti vya marafiki zangu au wasaidizi wangu. Penye udhia penyeza rupia.

Halafu eti limsomi linashauri tuokoke! Napiga picha mzee mzima nikianza kujifunga na kusema: Jamani mwenzenu nimeokoka. Lazima nikiri na kutaja dhambi zangu. Kwanza nilizaa na Sofiiii Fyatu wanaharamu wawili ambao nawasomesha Ulaya. Hata huyu bibie napanga kumpa ulaji kijiweni kwa vile ni nyumba yangu ndogo.

Pia lazima niseme wazi na Bwana Yesu anisamehe. Mimi naugua ugonjwa wa ngono uitwao Kwetoisis dogodogozisis.

Pili, lazima nikiri. Huwa nawapeleka dogo dogo zangu nje na kula uroda nao hasa nisipoandamana na bi mkubwa ambaye wabaya wangu wanamwita Shosisto Shari Mpayukaji.

Lazima nizidi kutubu. Mmoja wa nyumba ndogo zangu aitwaye Fatema Allie nimempa ukuu wa kijiwe kwenye wilaya moja ya kijiweni.

Ila mjue. Huyu si mtoto wa rafiki yangu. Mie ni kijogoo hili sipingi. Nina tofauti na Zumaa. Mie siri mayai yangu wala marafiki zangu. Ila yakijileta nalamba. Maana fisi huwa hana mwiko.

Bwana God epushia mbali huyu mdudu wa kufunga kamba watu kuwa nimeokoka asiniingilie. Maana ni aibu! Muhimu lazima nikiri: Bwana hustahili kuja kwangu ila sema neno moja tu roho yangu itapona. Nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa sana. Ndiyo maana namtamani hata Bikira Mari… we koma!

Kuna jamaa mmoja katoa mpya. Eti anasema Jack akimuona ndege jike anatamani ambake.

Hivyo, siku hizi hata njiwa wa Kijiweni wamehama kuhofia kufanyiwa mchezo mbaya! Sijui wamama wanaonyonyesha kama wanaweza kupita karibu naye na vichanga vyao! Eti anasema kwenye ikulu ya Jack kuwekwe ubao wenye maandiko: “Bosi ana ugonjwa wa kubaka baka, chunga sana na polisi hawana uwezo kumpa dawa.” Hayo tuyaache.

Turejee kwenye safari yangu ya Sauzi. Wengi wanalalamika kuwa kodi zao zinatumika kugharimia uzinzi wa Bwana Mkubwa. Hata mawaziri wake wanaanza kuogopa kuhusiana na vidosho vyao ukiachia mbali waume wa vidosho vilivyomo kwenye baraza lake la mawiziii.

Lakini wafanye nini iwapo nao wana ugonjwa uitwao Greedforpowersarcoma? Na Jack analijua hili. Anatumia urahisi kama ulimbo kuwanasa akijua hapendwi mtu bali cheo.

Nimempenda kitu kimoja Jack. Yeye ni kihiyo lakini hana vihiyo kwenye baraza lake la mawizi.

Nashukuru Mungu. Maana kama angesoma na kuwa profesa huenda naye angetoa shahada za chupi kama jamaa zangu waliotimuana hivi karibuni kule Kilimani.

Hivi inakuwaje mtu mzima, tena msomi au unayetegemewa kuitwa msomi ukadai au kutoa rushwa ya ngono? Hamuogopi kujidhalilisha ukiachia mbali miwaya jamani? Naona huyu anasoma na kusonya kwa vile naye alipata gamba lake kwa kuvua chup---sorry nonihino yake. Mtakwisha.

Acha uvivu na tamaa. Soma upate shahada yako. Nawe fanya kazi ulipwe mshahara wako. Kama kufundisha kumekushinda unataka kuwa cassanova, si uache uende ukawatafute vyangu pale Ohio. Nawe dada kama kusoma huwezi si uache uende zako Ohio ukauze hilo balaa lako.

Lo! Nimewananga wengine nikajisahau kuwa nami kwenye kijiwe changu nina mpango wa kumendea kagulo fulani kanakojileta leta. Hata hivyo mimi niko juu ya sheria za kijiwe na hata nikikosea sikosei. Mimi ni mtukufu kama Zumaa.

Sisi ni wakubwa bwana na mambo yetu ni makubwa na wengine tunayafanya siri kubwa ati. Uzuri wa Zumaa hafichi kama mimi ingawa naye anatumia pesa ya walipa kodi kufanya ufuska sorry ujogoo sorry, vituz vyake.

Uzuri yeye anatongoza wavaa gauni si wapiga kura kama mimi. Yeye hana uchaguzi wa uchafuzi mwakani kama mimi ambaye sasa mambo ya kutongoza tongoza wavaa gauni nimeacha.

Sasa najishughulisha na kutongoza wapiga kura ili wanipe ulaji tena. Lazima niseme. Kwenye ziara nitazoanza hivi karibuni kufufua ndoa na wapiga kura sitataka miswali ya kipumbavu ya “Umefanya nini kwa miaka yote mitano kwa kijiwe?”

Mimi ni maarufu kuliko chama changu cha UNM kinachoitwa Chama Cha Mafisadi (CCM) na wabaya wangu. Hata watabiri wameishanitabiria kushinda tena kwa kishindo cha mabomu ya Mbagala ati.

Anyway, acha nimalizie stori ya safari yangu bondeni. Una habari nilikaribishwa chakula cha usiku na mzee Zumaa mwenyewe? Huwezi kuamini. Tulikula na kunywa huku akiwa amezungukwa na vishosto vyake.

Alinishauri nami nitangaze hadharani vidosho vyangu badala ya kujinyima raha kukutana navyo kwa shida na gharama kubwa kwa kuogopa walevi. Nilimkubalia. Lakini we, nikitaja si walevi wengi watakufa kwa kihoro maana wengine ni wake za watu.

Baada ya kula chakula cha usiku na mzee Zumaa, siku ya pili nilikwenda Qunu kumsalimia mzee Madiba ambaye alinionya kuhusu mchezo huu mbaya wa kupenda uroda.

Du! Kumbe niko Bongo tena kijiweni Kwa Mfuga Mbwa! Ndoto nyingine bwana.

Acha nikitoe niende kununua pingu ili niwakamate wenye doshi.
Chanzo; Tanzania Daima Feb. 10, 1010.


Sunday 7 February 2010

Walioghushi vyeti wawajibishwe

OKTOBA mwaka jana ni mwezi wa kukumbukwa kwa wanaharakati wa kupambana na utapeli na ufisadi.

Mwanaharakati mmoja nchini, alikuja na matokeo ya utafiti wake uliodhaminiwa na Tume ya Vyuo Vikuu (TUC). Utafiti ulianika mawaziri na wabunge kadhaa waliogushi sifa za usomi.

Utafiti huo uliofanyika kati ya 25 Juni na 9 Oktoba mwaka jana katika nchi za Marekani, India na Uingereza ambako vigogo walioshutumiwa walidai kuwa walisoma na kupata shahada shukiwa.

Ilitarajiwa baada ya kugundulika, vigogo hao wangechukua hatua zifuatazo: Kuachia nyadhifa zao kama njia ya kuwajibika na kupisha uchunguzi wa kina kufanyika ili ukweli halisi ujulikane.

Au kutoa utetezi unaoingia akilini badala ya kujirusha kimanga. Aidha, wangekwenda mahakamani kudai haki.

Hawakwenda.

Vinginevyo, bunge lingewatimua kazi kama wasingechukua hatua ya kujiwajibisha. Hata rais angewatimua wateule wake ili kutoa somo kwa wengine watakaokuwa wamefanya hivyo au kufikiria kufanya hivyo.

Bahati mbaya, sasa ni mwaka mwingine, hakuna aliyejiwajibisha, kuwajibishwa wala kutoa utetezi. Ajabu ni kwamba waliodaiwa kughushi na uadilifu wao kutoweka, bado wako kazini kana kwamba hakuna kilichotokea. Nchi ya ajabu.

Je, sheria zetu zinaanza kutumika kibaguzi na upendeleo kuwapatiliza wasio na mamlaka zikiwalinda wenye madaraka? Je, ndiko kujuana ambako kumekuwa kukilalamikiwa kuwa ndiyo sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)?

Je, kwa Bunge na rais kuacha kuchukua hatua kwa makusudi mazima si aibu na onyo tosha kuwa wako pale kwa ajili ya marafiki na washirika zao na si umma? Je, umma unaosalitiwa hivi una sababu ya kuziamini taasisi hizi mbili?

Kisheria, kuwasilisha hati za kughushi kwa mamlaka yeyote ni kosa la jinai ukiachia mbali kujipatia marupurupu na mshahara kwa kazi ambayo huna ujuzi wala sifa nazo.

Hapa tutaambiwa ubunge si kazi ya kusomewa. Lakini tukumbuke, ni utumishi wa umma unaotaka usafi wa hali ya juu.

Je, kuwadanganya wananchi, tume ya uchaguzi na taifa kwa ujumla huku ukijipatia mshahara kutokana na sifa usizokuwa nazo si kosa? Kosa hili lingetendwa na wapinzani mambo yangekuwaje?

Tunaanza kuwa taifa lisilo na kumbukumbu kutokana na unyeti wa suala hili na hatari kwa taifa. Tunalirejesha hili kwa hadhira ili umma uchukue hatua baada ya wahusika kugoma kuwajibika. Tulitegemea maandamano ya kushinikiza haki itendeke lakini wapi.

Kama siyo kuandamana kushinikiza wahusika waachie ofisi zetu basi, angalau kwenye uchaguzi kuwanyima kura kama hawatachukua hatua mujarabu. Tuurejeshe mpira kwa rais, Bunge na tume ya uchaguzi ili watende haki.

Maana tunaohujumiwa ni sisi na si wao. Tumkumbushe na ikiwezekana mawaziri sita wanaoshutumiwa kughushi vyeti na sifa hasa za udaktari wawajibishwe.

Tulishinikize bunge ambalo wabunge wake wanatuhumiwa kughushi pamoja na tume ya uchaguzi ambayo waliokuwa wagombea wake walipita ilhali kisheria hawakufaa hata kusimama kutokana na kutenda kosa la jinai linalohusiana na sifa za kuutumikia umma.

Kwa kuendelea kuwa na watu hawa kwenye nyadhifa zao ni taarifa tosha kuwa serikali, chama chao na hata tume ya uchaguzi wameridhika nao. Hivyo hata kwenye uchaguzi ujao watashiriki na kutumia mbinu za porini kuendelea kuula.

Kwanini rais anayetuaminisha kuwa atabadilika na kutimiza matarajio yetu hataki kuliona hili? Kwanini washauri wake hawalioni hili? Kwanini chama chake hakilioni hili? Na kwanini Watanzania hawalioni hili?
Chanzo: MwanaHALISI January 27, 2010.

Tuesday 2 February 2010

Despising Kiswahili Will be East Africa's Undoing

News that the Kenya’s ministry of education declassed Swahili is not a welcome especially at this time East African countries are attempting to unite. Before this denting move, Swahili was mandatory in Kenya’s Secondary schools. Now it has been made optional. Will this help or ruin the spirit of East African unity?

Kenya seems to suffer from a colonial hangover. English is vital. So is Kiswahili. I remember. When I was in Nairobi, many people were irked when I referred to them as Swahilis (meaning Africans (as we’re used in back home). For them, a Swahili is an uncouth and an uneducated fellow.

Again, before their eyes, there was no difference between a Swahili and a Muslim. English was, and still is, erroneously though, highly regarded as a language of educated and civilized people.

I noted this after a hot debate ensued in which the main topic was: Tanzanians do not know English and therefore are not well educated. This did not hold water though after citing two Tanzanian-educated-Kenyan lawyers that steal the thunder. Interestingly, we found that prominent Kenyan lawyers such as Willy Mutunga, Makau Mutua, and others did their law degrees at University of Dar es salaam!

Again, when I started showing them how Swahili people live, slowly but steadily, they started appreciating Swahili life that is built on simplicity and commonality.

To them, Swahili speakers do not know, and cannot speak nice English. They found this illogical after noticing that I had no much more vernacular effects like them.

Even if you watch the Bull’s Eye programme on Kenyas Nation TV (NTV) you’ll find that many Kenyans including the president like to speak Swanglish in that they mix English and Swahili on many occasions. I remember a famous clip when President Kibaki is quoted as saying: “I am sure we shall succeed. We shall succeed. We shall faulu.”

Even Yoweri Museveni of Uganda mixes Swahili and English on many occasion. Addressing Kenyan journalists during the Migingo Island crisis, he said: “...How can we fail to solve this problem ourselves and say UN, wazungu njoo mtusaidie tumeshindwa…”

While Sheng is gaining more momentum in Kenya at this time at the detriment of English than any time in history, Swahili the vital language of the east and central African region is the one Kenya is unnecessarily busting. Even the south region is slowly embracing it. It is widely used in Malawi, Mozambique, and South Africa (thanks to the fact that many South African freedom fighters were based in Tanzania).

Swahili is regarded as a Language of liberation in Tanzania thanks to the vital role it played during the struggle for independence. It would have been difficult for Tanzania to acquire her freedom had she used over a hundred vernaculars spoken in Tanzania. Swahili made it much easier and faster to attain freedom and liberate Tanzanians from all ethnic anathema. Mwalimu Julius Nyerere and his colleagues used Swahili to advertise their policies and the reasons why Tanzania had to be independent.

Using one language built understanding and trust among Tanzanians. Ever since, they are proud of their nationhood as opposed to ethnicity as it is the case in Kenya and Uganda despite aping English. English has nary unified them.

On top of that, it is a language of unification. This is the vital tool Kenya can use to do away with its ethnic hostility-cum-barrier. Tanzania built a higher sense of oneness thanks to Swahili. If anything, Swahili is the only miracle that made 120 odd tribes in Tanzania to live in harmony compared to 40 odd tribes in Kenya that always set off a confusing dance to the nation.

At the conference of commonwealth heads of states 2009 in Trinidad and Tobago, Ugandan strongman, Yoweri Museveni informed the queen of the aim of ‘popularizing Swahili’ as he put it in order do away from ‘putting up’ with interpreters and microphones especially at AU conferences.

Culturally, Swahili people interact easily. This is the reason why life in Mombasa is comparably more peaceful than any part of Kenya. Mark my words. I don’t mean Swahili people are angels while the non-Swahili are devils. You can go about your business in Mombasa even at night without any fear of being robbed or assaulted by police. What is the situation in Nyeri and Nairobi?

Methinks, Kiswahili has something to do with the peace Tanzania enjoys as opposed to Burundi, Rwanda and Somalia that gave their language second place. What’s more, Swahili is easier to learn thanks to interwoven and similar African culture among other things. It also is rich and well established thanks to its open-door nature of taking in some words from other languages. This for its detractors makes it a language dominated by other languages especially Arabic. But they forget one thing. English for example, is hugely dominated by Arabic, German, French and Greek to mention but a few.

Swahili is growing rapidly all over the world. It is taught in many universities and broadcast in many world big radios such as VOA, BBC, DW and others. It ought to be the official language of East African countries. This would help harmonize East African English speaking countries with French speaking Burundi and Rwanda.

By demoting Swahili, Kenya is building a hostile environment. Suppose Burundi does the same. Will East African unity be attainable and tenable? It is erroneous to put Swahili at par with Sign Language. The need for sign language is not at par with that of Swahili. By razing Swahili, Kenya is also putting out its coastal citizenry and it minimizes trust and pride they have taken in Kenya.

Even the outside world that values Swahili is laughing at these braggadocios by an African country to degrade Africa’s more popular and highly growing language, now more than ever, it sounds good to say: please Kenya don’t goof up Swahili.
Source: The African Executive Magazine March 3, 2010.

CCM, CCJ na UUU tutaona nani zaidi

MWENZENU nimo msibani. Nimo mashakani. Ulaji wangu, watu wangu, Bi, Mkubwa na washirika zangu mmo hatarini. Si jamaa wale wenye husda wanaonisingizia kuwa nalinda ufisadi kijiweni wameanzisha Chama Cha Jeuri (CCJ) baada ya Chama Changu cha Ugali Nyama na Maharagwe (UNM) kukibadili jina na kukiita Chama Cha Mafisadi (CCM) na wengine Ufisadi, Ujambazi na Ubabaishaji (UUU)!

Basi mwanawakwa, kijiwe hakikaliki tena hata kahawa hainyweki. Nasikia hata nguo za ndani zinanibana. Presha ishanipanda sana. Majaliwa yangu hadi sasa siyajui. Nimewasiliana na waganga, wapiga ramli hata mashushu wangu. Lakini ngoma bado nzito!

Wapo wanaosema nijilaumu baada ya kutowasikiliza kina Msomi Mkata tamaa aka Daktari Sam Sixx, Mzee Mwaminifu aka Joe Butiko, Msemakweli aka Mat Qarez na wengine wengi.

Unajua hawa jamaa waliniambia sikusikia! Nawalaumu walioniponza hasa mgosi Machungi aka Joe Makambale ambaye alizidi kunisifia nisijue nilikuwa nasifiwa ujuha.

Hata mzee wangu Kimdunge Mwehu anaonekana kupwaya kwenye zali hili. Pamoja na kuwatumia wachumia tumbo kunitabiria ushindi mnono, mambo si mambo. Je ni muujiza gani utatokea nipone na chama hiki cha jeuri bengw’e?

Japo nilishamtonya mtu wangu Joni Tendua akitendue na kukiengua kisishiriki uchaguzi, je hawa jamaa wanaokiunda wakihamia vyama vingine kama CHAKUDEMA nitakuwa mgeni wa nani mwaka huu? Je nikidondoka, nani atanilinda kama nilivyomlinda Tunituni na Anna Tamaa wake?

Hawa jamaa wa CCJ wamejua kutuvua nguo. Wanasema eti sera zao ni kulinda kahawa na kashata na raslimali nyingine kama walevi na wateja wengine! Mbona wanatisha kama ukoma hawa?

Tuache utani, walevi wamechoka, uongozi wangu umechoka na kila kitu kimechoka. Nadhani hata ndege na samaki na wadudu wamenichoka kutokana na ufisadi wangu kiasi cha kuwapa watu jeuri ya kuanzisha chama tena cha jeuri.

Mzee mzima sikubali kufa bila kufurukuta. Nikitoka hapa nawatimua Mgosi Makambale Machungi, Mbwa Mwitu Ewassa, gabacholi Rosti Tamu Kanji na mafisadi wengine ili kurejesha imani ya walevi. Hapa sina ujanja. Nisipofanya hivi nimekwisha. Maana hata rafiki yangu Karumekenge ameingizwa mjini na Madevu kiasi cha kuhatarisha ulaji wangu. Lakini huyu simlaumu. Anatetea ulaji wake na madhambi yake na kila mtu lazima abebe salaba lake ati.

Hata huyu mama aliyejiunga na kijiwe chetu hivi karibuni Wa Kupayuka Sofii Yanga naye namfukuza. Maana domo lake litakuja kuniponza zaidi. Mama linapayuka utadhani halina ubongo! Kwa nini niliache liendelee kujambisha domo lake na kuhatarisha ulaji wangu?

Hebu kwanza nijaribu kutafakari. Kwa nini hawa wadudu wameamua kuanzisha chama cha jeuri? Ahaa nimekumbuka! Ni kwa vile sera yangu ya ufisi, ufisadi na kulindana imetoa mwanya. Maana kwa sasa kila mwizi anajinywea kahawa na kujilia kashata atakavyo kana kwamba mali yenyewe haina mwenyewe. Pia Rost Tamu kanirostisha kwa kuzidi kuiba pesa kwenye fuko la kijiwe chini ya mradi wangu naye wa WEPA ambao watani wangu huita We Panya Acha kutoboa fuko la kijiwe.

Pia nadhani huu mradi wa makaa ulioletwa na Mbwa Mwitu Ewassa na gabacholi wake umezidi kunirostisha. Nimejaribu kupiga chenga kashfa hii ili ijifie bila ufanisi. Wabunge wa kijiwe nao wameshupalia kiasi cha baadhi yao kuniundia chama cha jeuri!

Hapa anayeniponza zaidi ni Mgosi Makambale ambaye inaonekana ana maslahi binafsi kwenye uchafu huu. Kila wakija juu yeye anaongeza mafuta kwenye moto kwa kuwakejeli na kusema ni wahuni. Sasa yamekuwa wameanzisha chama tena kwa jeuri. Je huyu atanisadia au atazidi kuharibu mambo? Lazima nimtimue kabla walevi hawajanitimua.

Ngoja kwanza niongee anisikie. Maana namuona anakuja yuleee! We mshenzi Mgosi Machungi mjukuu wa Kambale uitwaye Makambale, koma na ukomae. Nenda shule ukasome hata kama umebakiza miezi minne kukata roho. Wewe ni fisadi ambaye nilikupa cheo kwa bahati mbaya. Lazima mwaka huu nikutimue na mabwana zako.

Kabla ya kuendelea Mgosi kashatia timu. Anaanza: “Osie, hata kuti naakuzidi umri, nakuheshimu saana mia sikuogoha. Iituka zeze utaanza kunkank’a na ulimi wako bia hata kuitanga kikao cha sii tishezageana shoni want’hu wagima.”

Tafsiri :

“Bosi hata kama ninakuzidi umri nakuheshimu sana ila sikuogopi. Imekuwaje unaanza kunitukana tena kwa ulimi wako bila hata ya kutaka tuitishe kikao faaagha tusije kuumbuana wazee wazima?”

Anatoa leso yake mfukoni na kujifuta jasho na kuendelea: “Mgosi tiheshimiane eeehe! Kama titageukana sisi kwa sisi maadui zetu watatishinda kiahisi uje hio. Kwanini tisikae tikazungumza na tizungumze tikapata suuuhu badaya ya kutukanana hazaani bosi?”

Nami najitutumua na kusema. Hivi haujasikia wapuuzi hawa waliounda chama cha jeuri tena kwa jeuri ya kutaka kutia mchanga kitumbua changu! Hapa hakuna cha kuheshimiana tena.

Mmenitumia na sasa sikubali kuendelea kutumiwa tena. Badala ya kutekeleza sera umekuwa ukifanya maigizo na vichekesho. Sasa unaona matokeo yake? Hawa walevi tutawafunga kamba gani tena iwapo miaka mitano iliyopita hatukufanya chochote zaidi ya kila mtu kuiba mahali pake?

Kabla ya kuendelea, Mgosi alionekana kuchukia wazi wazi na kusema: “Lakini umesahau kitu kimoja. Wakati wewe na bi Mkubwa mkizuua ughaibuni ni mimi aliyejibu mashambuizi dhidi yako. Sasa kosa langu hapa ni nini bosi? Naona titume mashushu wakisambaatishe.”

Bila kufikiri nilimjibu. Kumbe nawe sasa una jeuri ya kuanza kunitisha siyo? Mashushu wa umma watumiwe kusambaratisha chama cha umma? Sasa tutaona. Kama mnajifanya mna jeuri basi mimi nitawasaidia chama cha jeuri niue chetu cha UNM tuone.

Nitafanya mazungumzo ya faragha nao kama alivyofanya Karumekenge na Madevu halafu nione nyinyi kama mtakula jeuri yenu. Mmefulia msijue. Hata best wangu Ewassa Mbwa Mwitu naye nampiga peni na kila mtu lazima hapa abebe msalaba wake.

Mara nilimuona Mgosi amenyong’onyea asijue la kufanya. Kumbe nilikuwa na safari ya kwenda zangu Uswizini. Ziara hii niliweka wazi majina ya watu nilioandamana nao. Ilibidi nianze kutafuta jinsi ya kuachana na Mgosi.

Akiwa anajiandaa kuendelea kujitetea si waandishi wa habari walituzonga. Niliwaona akina Martin, Mchunguliaji kiboko ya matrafiki na makofia meupe, Jeni Mura na wanoko wengine ikabidi niingie kwenye shangingi langu nikitoe kabla hawajaniandika vibaya.

Khalas kweisine.
Chanzo: Tanzania Daima Machi 3, 2010.