The Chant of Savant

Tuesday 19 October 2010

Kanada yaja na mchuma wa kisasa na salama


Aina mpya ya gari lililogunduliwa Kanada Knight XV ambalo limefanya magari maarufu kama Hummer kuonekana viduchu. Lina horse power 400 na uzito zaidi ya tani sita. Hapa chini ni vidokezo juu ya mtambo huu wa bei mbaya. Sijui watawala wetu wasiopitwa na kitu watanunua mangapi kwa kodi ya wafa njaa? Wauza unga wamelitaka sana lakini wazalishaji wamewatolea nje. Je haitakuwa busara zaidi kuwatolea nje hata watawala wetu ambao tofauti yao na wauza unga ni kwamba wauza unga hawashiriki uchaguzi?

A magnetic detector attached under the vehicle can also alert the driver when a remote-control bomb or a tracking device has been attached to the Knight XV.

And don’t worry if the bad guys shoot out your tires, the Knight XV can run flat on rims made of steel that is the same strength as that used in the wheel rims on massive passenger jets.

“No matter what happens,” says Conquest president and founder William Maizlin, “you’re in an armoured plated cocoon. You’re safe.”

A fully loaded Knight XV costs nearly US$800,000, and oddly as it sounds this armoured-clad behemoth is being built in Toronto, far from violent destinations like Iraq where its blast-proof plating just might come in handy.

One Saudi sheik was so anxious to get his hands on one that he demanded it be shipped in a week’s time. The shipping costs alone came in at $50,000

8 comments:

Anonymous said...

Je haitakuwa busara zaidi kuwatolea nje hata watawala wetu ambao tofauti yao na wauza unga ni kwamba wauza unga hawashiriki uchaguzi?

umesema yote

Anonymous said...

Je haitakuwa busara zaidi kuwatolea nje hata watawala wetu ambao tofauti yao na wauza unga ni kwamba wauza unga hawashiriki uchaguzi?

umesema yote

Anonymous said...

MH Mpayukaji.

Wauza unga wanashiriki uchaguzi kwa namna moja au nyingine,tena kikamilifu.
Hawasimami wao wenyewe moja kwa moja; bali hutumia fedha yao chafu kuwapa nguvu wanasiasa uchwara, ili wapige kampeni haramu zilizo jaa ngwala na vikumbo kwa maana kwamba wakishinda himaya zao(Maharamia) zilindwe kwa bei yeyote.
Jiulize Fedha itumiwayo na CCM kupiga Kampeni inatoka wapi??

Madai yetu ni kwamba mahabithi hawa nambari 1 wanaiba fedha ya serikali, ni ukweli lakini si ukweli mzima.
Ukweli mwingine ufichwao uvunguni ni kwamba fedha ya kampeni ya CCM ni fedha haramu kutoka katika viganja vya majambazi wanao inajisi nchi yetu Tanzania kwa kila jambo haramu katika mtiririko wamaisha yetu yote ya kila siku.

CCM wanafurahi sana tukiwatuhumu kuiba fedha serikalini, kwa sababu hiyo ni tuhuma hafifu kwao. Kwanini? Kwa sababu wizi wa mali ya umma ni jambo linaloshabikiwa sana na karibu asilimia 10 ya Watanzania wasomi wenye nafasi na upeo wa kielimu. Tukiwatuhumu kuendesha kampeni kwa fedha itokanayo na michango ya maharamia wakubwa Tanzania na nje ya nchi,jambo ambalo ni kweli tupu, tuhuma hizo zitawakera ki kwelikweli.

Kuhusu hilo gari la kifahari. Fedha ni tamu sana, wakifikia bei watawauzia tu.

Wauza unga wapo nyuma ya CCM zaidi ya kutoa mshiko,sijui wanawafanya nini CCM!

MADELA WA MADILU

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

MADELA WA MADILU umemaliza yote. Sina ya kuongeza nisiharibu ujumbe ambao nadhani wahusika wameupata barabara.
Ubarikiwe kwa busara na uoni wako wa mbali dhidi ya upofo wa mafisadi na genge lao liitwalo chama.

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Hummer ililalamikiwa sana kwa "kunywa" mafuta kwa wingi. Hili nalo linakunywa lita ngapi kwa km. moja?

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Bwana Masangu umeuliza swali zuri. Nimepitia kwenye mtandao wa hawa jamaa. Bahati mbaya sijaona details zote za kifaa hichi zaidi ya picha nyingi tu. Sijui wameficha au wamesahau.
Nitazidi kuzama zaidi.

Anonymous said...

Nyinyi wakanada hamna maana kabisa. Mnavumbua mtambo wa kuwafanya hawa wasenge wetu watumalizie pesa kwa kisingizio cha usalama. Mhango umefanya kosa kubwa kutangaza dude hili. Kesho yataagizwa ya Kiwete, Riziwani, Salma, Rahma, Rostam, Lowassa hata mbwa wao tena kwa pesa ya wabongo wapumbavu. Kesho kutwa utayaona ya akina Patel, Chande, Dewji na wasenge wengine wa kihindi!

Anonymous said...

Kuvumbua au kutengeneza chombo chochote imara haijawahi kuwa dhambi au nusu dhambi.

Kiwanda cha mapanga na mashoka kimejengwa kwa nia ya kuzarisha zana za kazi mashambani.

Utashangaa sana ukiambiwa bin adam wamegundua kutumia mapanga na mashoka kutoana Roho.

Lakini hata hivyo mapanga na mashoka mengi hutumika kufanyia kazi ambayo ni mlengwa tangu awali.

Pengine ni vema tukikumbushana kwamba mfumo wowte ule, uwe imara kwa sana udhaniwao haupenyeki au hafifu ni lazima sambamba ujijengee udhaifu mkubwa sana uwezao ku u ua mara moja.

Fedha nyingi ndani ya mfumo wowote ule hutumika zaidi katika kuulinda mfumo kuliko kuudumisha.

Ndiyo maana katika mifumo ya Computer kuna sofware nyingi za kulinda mfumo mzima wa computer usiingiliwe software hizi ni gharama sana.

Wana siasa hutumia fedha nyingi kuhonga na kununua vyombo vya ulinzi na usalama wakiwamo watu wadhaniwao ni hatari kwao kimaslahi ili kudumisha mfumo wao.

Usilalamikie wavumbuzi, kaa chini piga bongo na kuchambua udhaifu wa mfumo wa kifisadi.

Mra uutambuapo udhaifu wa mfumo wa kifisadi piga msumari wa moto na kutia chumvi yenye mchanyiko na pilipili kwa uwingi.
Uwiiii!

MADELA