The Chant of Savant

Tuesday 31 May 2011

Nigeria recalls diplomat over wife-beating claims



Nigerian High Commissioner to Kenya Chijioke Wigwe (centre) and his wife Theresa dance at a past function

Nigerian High Commissioner to Kenya Chijioke Wigwe, has been recalled over allegations of wife battering.

Nigerian media, quoting the country’s foreign ministry official reported on Tuesday that the “ministry had decided that the diplomat should go home as part of its investigation and disciplinary measures.”

The wife of the Nigerian envoy, Ms Tess Iyi Wigwe, was examined on Monday by a police doctor over assault claims. (READ: Police doctor to examine wife of Nigerian envoy)

Ms Wigwe recorded a statement with the Diplomatic Police Unit in Gigiri after reporting that she was assaulted by her husband, Dr Wigwe.

The Nigerian High Commission has, however, termed the allegations against Dr Wigwe as “malevolent, far from the truth and unsubstantiated.”

The Nigerian Bulletin quoted the spokesperson of the Ministry of Foreign Affairs, Mr Damian Agwu saying: “He will first of all be recalled and then be handled from there.”

In Nairobi, the Foreign Affairs ministry remained tight-lipped, only indicating that acting minister George Saitoti will issue a statement on Thursday over the matter.

Kenya chapter of the Federation of Women Lawyers chairperson Naomi Wagereka had called on the Kenyan and Nigerian governments to immediately withdraw all diplomatic immunity and status of Dr Wigwe.

Ms Wigwe displayed serious injuries on the face, which she claims were inflicted on her by her husband.

Police sources also revealed that her daughter was also injured as she tried to protect her mother. It was not clear whether the woman intends to prefer any charges.

Police Commissioner Mathew Iteere said they had written to the Ministry of Foreign Affairs regarding the lifting of Dr Wigwe’s immunity.

Being a diplomat, he is not liable to any form of arrest or detention by Kenyan authorities.

Nigeria had the option to recall the diplomat or have him face trial here should his diplomatic immunity be waived.

Source: Daily Nation

Friday 27 May 2011

Kenya moves from paradox to paradigm

Since the inception of the Government of National Unity (GNU) in Kenya, there have been many squabbles. In effect, squabbles have direct or indirect affected the lives of Kenyans. When GNU was ushered in there were dreams of huge leap forward that ended up becoming a too-often lie culminating from squiggles of success especially the making of the new constitution.

Though this marriage of convenience between Mwai Kibaki and Raila Odinga that brought GNU in has soldiered on, despite all drawbacks, there are many positive signs at this eleventh hour after the duo decided to embark on face lift for their marriage.

At essence, the mesmerizing way the duo quickly and expediently offered to their consent to the appointment of the candidate for Chief Judgeship the revolutionary-cum-resolutionary Dr. Willy Mutunga and his deputy Nancy Barasa is commendable and applaudable altogether. Indeed, this is but a new spirit that is likely to bring a lot of change in Kenya shall it be maintained.

Mr Kibaki and Odinga, never again allow you to be played off of being swallowed by narow ethnoegoistic political miasmas. Open a new page of reconcialiation and delivering. Verily, you know as well as I. This new realization of the duo is inspirational. For none of them can ably go solo politically without the other otherwise one wants to cascade into oblivion and historical dustbin. The duo is like the two side of the coin. Thus working together nicely for them is not an option but an obligation to their goals, nation and legacy.

Given that time is quicly lapsing for two principals, the paradox they make should come closer and closer reasonably and deliver Kenya. To know what this means, refer to the two antagonistic forces that generate electricity. This is the right way Kibaki and Odinga can make use of their paradox.

Notably, kibaki is currently laying some bricks for his legacy whiulst Odinga is gaining more qualification and expartize for yet another big job. The duo needs each other. Kibaki cannot leave a very bright legacy without Odinga who can not shoot up without Kibaki. In this situation whoever hampers another is but sabotaging himself. To know how this works, refer to the battle for the new constitution. When the duo opposed each other the draft constitution was shot down easily. If anything, this was the worst-case scenario. But when the duo worked together, the new constitution was ushered in easily. This is a positive and reasonable work of paradox whose benefits can end up becoming a paradigm in the future. Cooperation among the people making paradox undergirds achievement. So there is an urgent and permanent need for the duo to keep on working together mutually and amicably.

Shall the duo succeed in delivering Kenya from archaic rivarlies and political anarch; theirs will be a precedent for others that are still under the yolk of dictatorship and experimental politics in the region and far beyond. Therefore, the slogan of the duo should be: “Yes we can where they said we can’t.”

Let me cite another constructive paradox. As a constructionist, Mandela-De Klerk stance was a paradox. After they buried their differences and allowed common sense to reign in there came what is refered to as Truth and reconcialiation paradigm. From paradox to paradigm this is what it became. What a legacy for both! We need to learn to turn conflicts to constructive forces based on peace, justice and deliverance. This is but the biggest lesson from Mandela-De Klerk paradox-turned paradigm.

In a word, Kibaki and Odinga can still deliver and erase all negatives and past mistakes under their watch. Time is only now. After all, this has been a ground gristmill experience for the two. Conflicts even differences are but natural phenomena that make us think and meet our challenges. What is not natural is the drawbacks of giving a conflict intractability and permanent abode.

As for my friend Dr Mutunga, Kenya has a lot of expectations and hope all pinned on you. Please understand. Don’t go the way your former comrades in Arms went. I am not going to name names. But again when most of your friends and comrades got power, they drank a lot of it so as to end up intoxicated and licking their vomitase. This should not happen to you.

Your friends like Kiraitu Murungi, James Arengo even Koigi wa Wamwere know this too well. I am sure you’ll not embark on moribund politics of revenge and vengeance. Thus abhor all petit politics of this is our turn to eat and the likes. Like the two principals who endorsed you expediently without any squabbles, you too have a legacy to leave behind after your tenure comes to an end.

In sum, many precious metals and honorifics are there to pass but not the legacy that one leaves behind. You can see this in the oft-citing Plato, Socrates, Sophocles, Cicero and many more.

My last word of advice quotes this. “Doing justice is paramount to restoration, rectifying wrongs, and creating right relationship based on equity and justice.” John Paul Lederach in his book Preparing For Peace: Conflict Transformatio n Across Cultures.

To summize and reiterate, there is that culture of ethnicentricism, nihilism, impunity and corruption in Kenya judiciary being one of them. it is time for changes. Let us turn a paradox into a paradigm.

Source: The African Executive Magazine May 25, 2011

Serikali ya CCM imechanganyikiwa

SERIKALI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kama si kuishiwa basi imechanganyikiwa, imeishiwa hata uhalali wa kutawala kutokana na matendo yake.

Kashfa zote kubwa za wizi na matumizi mabaya ya fedha za umma zinaihusu na haijitetei zaidi ya kukiachia chama tawala CCM kufanya usanii ambao nao haufui dafu.

Hebu tujikumbushe kashfa kama EPA, Richmond, uchakachuaji na wizi wa kura, matumizi mabaya ya fedha za umma yanayofichuliwa na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), uwekezaji wa kijambazi na hovyo na baya zaidi ya yote, mauaji ya watu wasio na hatia.

Hivi karibuni watu wapatao sita waliuawa na polisi wilayani Tarime mkoani Mara. Na hii si mara ya kwanza kwa wananchi wa Mara kuuawa wakipigania haki zao zilizobinafsishwa kwa wawekezaji ambao kimsingi si wawekezaji kitu, bali wachukuaji waliokula njama pamoja na serikali kulihujumu taifa.

Badala ya serikali kutoa utetezi wake hata kuomba msamaha, ilidandia upinzani kudai kuna mbunge alikuwa nyuma ya kadhia ya Tarime.

Rejea tuhuma za kizushi za Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Hamis Kagasheki, akidai kuwa wahanga walikuwa wahalifu na aliyewatuma ni mbunge wa chama fulani.

Hivi watu wasio na uwezo hata wa kutumia busara wanafikiaje kwenye ngazi kubwa kama hizi bila kuwa na namna? Au ni yale ya kuwa mkwe wa rais wa zamani? Kama kuna mbunge wa upinzani nyuma ya kadhia hii, basi huyu ndiye anawafaa wananchi. Maana anaongea lugha wanayoelewa.

Na si kama hawa wabunge wa CCM ambao wako tayari kuuza watu wao kulipa fadhila ya kuwezeshwa kuwa wabunge kupitia uchakachuaji.

Kama huyu mbunge alichofanya ni kuvunja sheria, kwanini asichukuliwe hatua? Maana kwa anayejua siasa na sera za visasi za CCM, kama madai ya Kagasheki yasingekuwa uzushi, huyu mbunge wake angekuwa katika hali mbaya.

Kagasheki anangoja nini? Au ni yale kuwa watawala wetu hawana roho zenye kuwasuta na wako tayari hata kujiuza na kuuza watu wao ili wabakie madarakani? Hakika hii ni changamoto kwa Kikwete na serikali yake yote.

Je, Watanzania wataendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mlevi kujifunzia kunyoa hadi lini? Waguswe wapi au wauawe wangapi ndipo mikoa yote kwa umoja wao iamke na kuipiga teke serikali hii habithi?

Kuonyesha kuwa serikali imechanganyikiwa, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alikaririwa akitoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu.

Huyu ni bosi wa Kagasheki na kinachoendelea hapa ni serikali moja kupingana.

Huyu anasema ni wahalifu. Mwenzie tena bosi wake anatoa mkono wa rambi rambi! Je, huku si kuchanganyikiwa kwa serikali na kupingana kunakoiondolea uhalali wa kutawala?

Hili lingetokea kwenye nchi zenye viongozi wenye akili na si watawala wa wasanii, serikali yote ingetimuliwa bila mjadala.

Kituko kingine, eti polisi waliotuhumiwa kuua ndio wanatumwa kuiwakilisha serikali na kushauri wahanga wazikwe. Tangu lini polisi wakawa wawakilishi wa serikali wakati wanapaswa kutokuwa na upande?

Polisi wa Tanzania licha ya kuwa vinara wa ufisadi, kusaidiana na majambazi, wanasifika kwa kuua wananchi. Ni juzi juzi waliua kule Arusha, Shinyanga, Mbeya na sasa Mara. Halafu hawa hawa wanajiletaleta kwa kutumia kodi za wahanga hao hao kujifanya waelekezi wa nini kifanyike.

Huyu Mkuu wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja na wenzake wanapaswa kujiuzulu badala ya kujifanya washitaki, waendesha mashitaka na mahakimu.

Hata Waziri Kagasheki aliyekaririwa akisema wahanga walikuwa wahalifu anapaswa kuachia ngazi bila kujali ni mkwe au mtoto wa nani.

Je, haya ndiyo matokeo ya chama kuiweka serikali mfukoni huku kikitumia taasisi za umma kama polisi kufanya kazi zake chafu?

Polisi wetu siku hizi wamegeuka walinzi wa migodi ya wawekezaji huku sisi tukikabwa na vibaka waliowatengeneza kila uchao!

Je, Watanzania kwa sasa ni salama? Je, waende kwa nani zaidi ya kujipigania wenyewe? Je, polisi wa namna hii wanapaswa kulipwa kodi zetu kila mwisho wa mwezi? Kwa kazi na sifa gani?

Ajabu, wakati watu wanaonewa kutokana na sera chafu na chovu za serikali ya Rais Jakaya Kikwete, yeye alipata mshipa wa kwenda Namibia kutanua!

Nasema kutanua kutokana na kulinganisha umuhimu wa alichokwenda kufanya na uhai wa binadamu.

Isitoshe, nasema alikwenda kutanua kutokana na kuficha majina ya watu alioandamana nao, tabia ambayo imeanza kuota mizizi.

Je, kwanini anaficha ujumbe wake kama hakuna watu wenye kutia shaka? Je, huyu kweli anawajali Watanzania?

Kuna haja ya kuendelea kuipa serikali ya Kikwete ushauri wa bure kutokana na umahiri wake wa kuvurunda badala ya kulikwamua taifa.

Wakati kadhia ya Tarime ikiendelea, Shirika la Habari la Uingereza (BBC) liliripoti kuwa Tanzania imeuza ardhi kwa kampuni la Kihindi kufanya shughuli za kilimo.

Najua serikali itakanusha kwa kusema imewakodisha ardhi kwa miaka 99 sawa na inavyowafanyia Watanzania. Kwa wageni huku ni kuuza.

Kabla ya kashfa hii hata kutolewa maelezo, ilifumka kashfa nyingine ya utoroshwaji wa nyara zetu kwenda Uarabuni.

Ajabu wanaofanya hivi ni Wakenya na Wapakstani wakishirikiana na Watanzania. Baada ya habari hii kutoka serikali imefanya nini? Kimya kama kawa!

Serikali yetu inajulikana kwa ubingwa wake wa kunyamaza ili mambo yajifie. Je, Watanzania wataendelea kuuawa, kuuziwa mali zao na nchi yao hadi lini? Kwanini wenzetu wa Kenya na Uganda wanahamanika kulinda masilahi yao huku sisi tukijifanya kila mtu alimhusu na kuishia kulalamika? Je, Watanzania wataendelea na serikali yenye tabia sawa na kuku alaye mayai yake hadi lini?

Tumalizie kwa kuuhimiza upinzani kushikia bango jinai hizi. Kadhalika tunawapa changamoto Watanzania kuachana na ukondoo unaowafanya wageuke wahanga wa kila jinai inayotendwa na kundi dogo la wahalifu wenye madaraka.

Haya ndiyo matokeo ya serikali zitokanazo na ufisadi. Ziko tayari kufanya lolote inayoamriwa na mabwana zake, yaani mafisadi na wawekezaji walioiwezesha kuwa madarakani.

Kwanini watu hata kama ni wachache wasiwe na uchungu wa nchi yao na watu wake? Anayetaka kujua ni kwanini Watanzania hawapaswi kuogopa kundi dogo la wahalifu, ajiulize serikali anayodhani ni yake wakati si yake imefanya nini kujibu tuhuma za wizi wa pesa za umma, kuanzia uliotajwa hadi ule wa rada na ndege mkangafu ya rais?

Ajiulize majibu na utekelezaji au tuseme urejeshaji wa nyumba za umma zilizoporwa na genge hili la wezi umefikia wapi?

Ajiulize zaidi kwanini deni la taifa linaumuka kila siku huku hali ya maisha ya Watanzania ikizidi kuwa mbaya? Jibu la yote ni moja, serikali fisadi na isiyo na visheni wala ajenda ya kulikwamua taifa bali kuliibia kila uchao.

Serikali hii inaingia kwenye vitabu vya historia kama taasisi iliyoiuza Tanzania.

Hakika CCM imechanganyikiwa kiasi cha kutoa matamshi na misimamo inayokinzana na yenye kuiacha uchi. Damu ya Watanzania wa Tarime haipaswi kupotea.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 25, 2011.

Kumbe bei ya mlevi mmoja ni vipande vitatu!

MWENZENU nina mipango bab kubwa ya kuwakomboa walevi na wadanganyika kwa mpigo. Ingawa Geronimo EKIA, mie napanga kuwa mkaidi. Sitalala kitanda kimoja na mafisadi wala kujigeuza changu kwa bei yoyote.

Sitatishwa wala kuhongwa hata kwa mabilioni ili niwauze walevi wangu. Mie ni maskini jeuri na si changu kama wale wanaofakamia uchafu wa mafisadi wa nje huku nao wakigeuka mafisadi wa ndani hata wawe na power.

Tofauti na wale magaidi uchwara wanaotumia dini, mimi nasema wazi kuwa nataka kuanzisha kundi liitwalo al-Kaidi. Nimechagua jina hili kuonyesha ukaidi wangu na si ugaidi.

Mimi kama kiongozi wa mtandao wa al-Kaidi sitajificha kwenye mahekalu huku nikiwahimiza walevi wajitoe mhanga wakati mie natanua na washirika wa bedroom kama Osami bin Burden aliyepunyuliwa hivi karibuni. Huu kwangu ni woga na unafiki. Lazima jemadari aongeze mapambano badala ya kuwatuma wengine wateketee yeye akitanua. Jemadari wa namna hii kwangu ni mwoga na changu wa kawaida.

Mie nitatumia watu wenye uchungu na kaya yao badala ya majuha waliochoka kuishi wakitafuta pepo kwa kuua wenzao. Mungu si mpuuzi kiasi hicho kuruhusu uue ndiyo uingie peponi. Pia Mungu si mchovu kiasi cha kutegemea ngurumbili wasio na maana kama hawa ninaosema. Mungu wa kweli ahitaji msaada wa binadamu kufanya mambo yake.

Mungu wa namna hii ni mchovu na kuogopwa kama ukoma. Leo sitaongelea sifa za Mungu. Kwa hicho kiduchu ngoja niachie hapo na kuelekea mambo mengine urgent.

Hakika, matandao wangu hauna dini kama ipo si nyingine zaidi ya uzalendo. Pia, sitawaahidi wafuasi wangu kwenda peponi zaidi ya kutengeneza pepo hapa hapa kayani. Napanga kufanya mambo yanayoingia akilini badala ya wendawazimu kama wale wachovu wa madevu aliyepunyuliwa hivi karibuni.

Lengo la kundi langu ni kudai haki ya wabongolalalanders wa Danganyika kwa kukaidi upuuzi wote kuanzia propaganda, hongo, vitisho na ujambazi mwingine. Hivyo, hata kama nikiitwa gaidi roho haitaniuma kwa vile ninachopanga kufanya si uganga njaa wa kumtumia sir God.

Mie nasema wazi. Nitapambana na mafisi na mafisadi wakiongozwa na Njaa Kaya na ukoo wake na walamba viatu wake wakiongozwa na Rostitamu na shangingi la kinshomile Silvia Rwependekezamu.

Hakuna kitu kimenichochea kuanzisha al-Kaidi kama mauaji ya kinyama waliyofanyiwa walevi wa kule kwa kina Mura Msama wa mbuye ori tata? Nimeamua kufanya hivi kutokana na kuona kuwa jamaa hawa wanaosifika kwa kujiamini na kulipiza kisasi kushindwa kuwanasa angalau vibao wale wakubwa wa genge la mauaji walioongozwa na Po Chagonjwa kwenda kuwahadaa eti wakubaliane na upuuzi wa lisirikali wazike wafu wao.

Hata hivyo nawapongeza kwa kunusuru kumnyotoa roho msaliti wao mkuu Nyambwari Nyangwile. Kitendo hiki kitaandikwa kwenye historia ya ukombozi wa kaya kwa maandishi ya dhahabu na vito vya thamani. Tusibweteke na hili. Tuwafanyie kweli ili tujikomboe kweli.Nasema tusibweteke kutokana na ujinga tunaofanyiwa. Watu wanauawa halafu wahalifu na wauaji waliofanya hivyo wanasema waliodedishwa ni wahalifu! Hivi kuna tusi baya kuliko hili wandugu zanguni?

Yaani tumekuwa wa hovyo kiasi cha kuvumilia matusi kwa marehemu zetu waliorudisha namba wakipigania heshima na haki ya kaya yetu! Je hawa maiti si bora kuliko sisi?

Twazidiwa na hayawani mdogo kuku ambaye yuko tayari kufa akipambana kuokoa vifaranga wake kuliko kuendelea kunenepeshwa kwa mahindi ya amfugaye! Hata kondoo hufikia mahali wakakereka na kutembeza kichapo. Duh! Hata hayawani wanatuzidi. Je, sisi ni hayawani kuliko hayawani?

Mandata wakae mkao wa kula. Maana zali langu lazima lianzie kwao ili waache kujigeuza mbwa wa kutumia na genge la mafisadi wenye power.

Tujikumbushe. Ji jitu limoja liitwalo Kangacheki lilikaririwa na vyombo vya umbea likisema kuwa watu waliouawa kule ni majambawazi. Mie nasema walionyotolewa roho ni mashujaa. Anayesema ni wahalifu ni mhalifu na kumbaff.

Hebu tutumie common sense japo kwa chati. Sasa kama kweli hawa watu walikuwa majambazi mbona lisirikali lilitoa madau milioni tatu kwa kichwa ili maiti wafukiwe na ushahidi wao?

Ingawa msiba huu umeniumiza na kuniathiri kisaikolojia, umenifumba macho kuwa kumbe bei ya walevi ni ndogo kuliko hata babaj!

Ya kwa akina Mura Msama tisa. Wajua kuwa kaya sasa inauzwa kwa maponjoro na magabacholi? Kama hujui jua sasa. Bado wake zenu na mama zenu. Bahati nzuri bi mkubwa wangu alishakufa.

Nimeamua kuanzisha kundi langu la al-Bamiza kuhakikisha mshirika wangu wa bedroom na dota wetu hawapigwi mnada na hawa mahabithi. Hivi wakija nanyi mtauzwa?

Je, wajua? Hawa mahabithi wanafanya kufuru zote hizi kwa imani kuwa walevi na makondoo na njiwa. Mie simo. Maana wanatuuza sisi na ardhi yetu ili wao na wabwana zao waendelee kutanua siyo?

Loh! Nilitaka kusahau. Umesikia tangazo hili? Mheshimiwa alhaji Mpayukaji anafurahi..sorry anasikitika kutangaza kifo cha shehe Yaya Hoseni kilichotokea Mwembamaziwa na habari ziwafikie washirikina wote wakubwa na wadogo.

Misiba wa sheheha shehe Yaya Hoseni nilioutabiri. Nawashauri wenye mamlaka waliokuwa wakimtumia waje kwangu mara moja maana mie natabiri ukweli. Mkuu upo? Chama cha manonihiino mpo?

Je, vais tue quelque granuile qui voleur nos argents. Je crois que je vais success vraiment. Usishangae na kuuliza hii lugha gani. Hiki ni kifaransa na tafsiri yake ni simpo:nitaua chura yoyote anayeiba pesa yetu niamini.

Nimalizie kwa kitendawili. Je bei ya mlevi ni gani? Just madafu milioni tatu.

Naona wale ndata wanafanana na wale waliodedisha watu wangu kule Tulime. Acha nikawazabe vibao. Bahati yao leo sikuvaa milipuko ningekufa nao. Duh! Kumbe wana bunduki. Acha nitoke nduki asije kunitarime.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 25, 2011.

Sunday 22 May 2011

Tuwalaumu au kuwaamini wakenya? EA si bomu kwa wabongo?

Kenyans capitalise on ‘Babu’ herbal cure

KENYAN authorities have started promoting the herbal 'magic cure' at Samunge Village in Loliondo Division, Arusha Region, urging foreigners to go there through Nairobi.

The Ngorongoro District Commissioner, Mr Elias Wawa-Lali, told the Arusha Region Consultative Committee over the weekend that the neighbouring country was reportedly advertising Samunge Village as if it were in Kenya.

The village is where the retired Lutheran Pastor, Rev Ambilikile Masapila, administers his herbal concoction in a single cup, which is said to cure various conditions including diabetes, cancer, heart ailments and HIV/Aids.

Over 3.5 million people had as of May 10, travelled to the village for the cup, according to Ms Margaret Martin, the Arusha Region Chief Statistician.

''From May 8, Rev Masapila started attending to about 10,000 people on daily basis,'' said Ms Martin.

The Arusha Regional Commissioner, Mr Isidori Shirima, said the Bank of Tanzania intends to conduct a survey on economic impact of the 'Loliondo cure' to Samunge village.

''Loliondo is now very popular after Babu Masapila came up with the cure. Digo-Digo ward as well as the entire remote Sonjo plains is now live on Airtel and Vodacom," the RC said.

The Meru District Commissioner, Ms Mercy Sila, said it was high time for the region to promote the Samunge Village and the herbal clinic.

''Kenya is now benefitting from Samunge village by promoting the 'Loliondo cure' abroad, attracting foreigners to Nairobi from where they begin their journey to Sonjo while here in Arusha we are just sleeping," she said.
Source: Daily News

Wednesday 18 May 2011

Tanzania yaanza kupigwa mnada kwa Magabacholi


Bangladeshi companies say they have leased thousands of hectares of farmland in Africa as part of their efforts to avoid future food shortages.

Two Bangladeshi companies have already signed deals to lease unused cultivable land in Uganda, Tanzania and Gambia.

Another agreement to lease around 30,000 hectares for 99 years will be signed with the Tanzanian government later this week.

Officials say African countries have huge amounts of unused cultivable land.

At the same time they say that Bangladesh has the manpower and expertise to produce staple crops all year round.
'Food security'

Under the plans, the Contract Farming System will enable Bangladeshi companies to get at least 60% of the produce.

In return Bangladesh will train African farmers in rain-fed rice cultivation, seed conservation and irrigation.

It is hoped that the new arrangement will increase food productivity and enable the country's expanding workforce to be deployed in Africa's farming sector.

"Basically this idea is mainly for proper management of our food security," said Wahidur Rahman, a senior Bangladeshi foreign ministry official.

"We are thinking of expanding our agriculture, but we do not have enough land to cultivate. Because of this we are thinking Africa may be the destination for our agriculture production."

Bangladesh is the world's fourth largest producer of rice and it harvested around 34 million tonnes last year.

Although the country produces enough to feed its population of 160 million people, it faces shortages at times because of natural disasters.

Officials say apart from rice there is also scope to cultivate other crops such as wheat and cotton in Africa.

Chanzo: BBC

Dogo, acha kutishia watu wazima nyau

NI muciare Kristo ni muciare,
(ni mzaliwa mkombozi)
Ni muciare yaciaritwe itura lya Daudi (ni mzaliwa kazaliwa nyumbani kwa Daudi)
Ni muraika akyuga (Ni malaika asemaye hivyo)
Ni muciare muhonokyia witu (Kazaliwa mkombozi wetu)
Mutuhoyeri mututhaithaneri (Mwombezi na mtetezi)
Mengine utamalizia mwenyewe. Ni lugha gani? Not important so far.

Ngoja niimbe kwa lugha baba na mama ya lugha Afrikani, ambayo aihitaji tafsiri.

Ni fisadi Dogo, ni fisadi,
Ni fisadi kwa mgongo wa dingi,
Bilionea mtoka shuleni!

Ni fisadi kama baba yake
Ni fisadi kama mama yake nanihinoo
Ni fisadi hata akanushe vipi.

Ninininininhhhhi hiyo tena, pombe hizi siku moja zitanifunga.

Leo nina hasira nusu ya kulipuka kama bomu. Nina hasira ingawa mara nyingine huwa napafa furaha ya hasira. Upo hapo?

Fungua masikio usikie unabii huu kwa wadanganyika waliwao na kila fala kuanzia yule wa Kiajemi, kunyantuzu na kimeru ajiitaye morani wa Kimmasai.

Juzi nilicheka nusu kunonihino kwenye salawili. Wajue ni aje? Si baada ya huyu dogo tuseme mtoto wa nyoka ambaye naye ni nyoka kuanza kuleta nyodu kwa kutishia watu kuwa atawapeleka kwa pilato kwa kumvua gamba.

Kwanza nimwambie huyu bwana mdogo asiye na lolote zaidi ya kudandia mgongoni mwa dingi yake. Hawa anaowatisha ni watu wazima wasiotishiwa nyau. Wamemshinda dingi wake yeye kinyamkera mchanga aliyeko mberekoni atawaweza?

You know what? Baada ya Daktari Willy Silaha kudai kuwa Riz-One Kikwikwi ni bilionea, eti alijitutumua kuwa atampeleka kwa pilato asijue mafisadi na waliomuumba baba yake waliahidi hivyo na kuishia mitini!

Wako wapi wanasharia kama Nimrozi Mkononi, Endelea Chenga na mafisadi wenye nazo kama Eddie Ewassa ambaye alikubali yaishe huku watu kama Grey Mugonjoka eti wakitishia kumfikisha Silaha kwa pilato wasithubutu.

Dogo, dingi wako kafyata mkia itakuwa wewe yai! Kumbaff sana. Nasikia eti nawe ni mwanasharia. Kama ni wale wa chuo kikuu cha Manzese nakuonea huruma. Maana miprofwesa mingi pale imechanganyikiwa kiasi cha kuonea watu na kuwanyenyekea mafisadi.

Kama ulishinda mtihani wa sharia si kwa sababu you are competent. Indeed, so to speak, if I may and if all laws and rules are employed, you passed just because you are the son of the prezzo. Finito. Like or lick it. Shauri yako.

Najua you can not reciprocate to this as a quid pro quo knowingly that I am but a prof of juris. Jaribu niku-bang legally.

Kwanza dogo, inapaswa unishukuru kwa kukupa somo bure. Maana nikilinganisha somo ninalokupa wewe Dingi yako, mama yako hata hao ndugu zako na wapambe wa wao na kiasi nilichokuwa nikilipwa nilipokuwa nafundisha Chuo Kikuu cha Havard, naona kama nimekupenda sana.

Nikupe lau fununu. Dokta Willy Silaha na mchunaji sorry mchungaji wa kujipachika Kris Mtikisa ni al-shindikanaa kwa lugha za kitaalamu. Laiti
Pia ni vizuri ukafahamu kuwa wabongolalalanders wanajua ulivyo bilionea atokanaye na wizi. Wanajua kuwa hata mama yako ni bilionea.

Wanajua kuwa hata Freddie Ewassa ni bilionea. Wanajua nani ameiba nini, kiko wapi, kwa namna gani na anakula na nani. Unadhani kuwa hawajui? Lol! Wanajua kuwa utawala wa dingi yako umegeuka mali ya ukoo na kujuana.

Wanajua kuliko unavyojua na unavyodhani hawajui. sema. wananyamaza wakiacha historia baadaye ifanye vitu vyake.

Ama kweli ulaji tena wa dezo hulevya. Yaani mara hii umesahau yaliyowakuta akina Morinyo watoto wa Ben Makapu wa tunituni na nkewe mama Ana-tamaa! Ama kweli la kufa halisikii.

Kama historia ya Bongolalaland inakutia woga kwanini usisome ile ya Zaire ya Mobutu ambaye alijegeuza kila kitu yeye na watu wake akaja kufa kifo cha mbwa na kuzikwa kwa aibu tena kwa siri ughaibuni utadhani mbwa.

Kama anaona historia ya Mobutu ni ngumu kupata basi aende kwa Joe Makambale aliyevuliwa hivi karibuni ona anavyoanza kupotea utadhani hajawahi kuwapo!

Hata Dingi yako kuna siku atatokomea kama walivyotokomea wengine isipokuwa mzee Mchonga aliyeacha legacy inayong’ara.

Laiti Dogo angekuwa msomi lau wa kawaida na si kihiyo anayeitwa msomi, basi angefunga domo lake ili angoje njeo hapo baadaye ipitishe hukumu yake.

Hata kina Mubarak wa Kibaraak kule kwa Farao walikuwa na kiburi kama cha baba yake huku watoto wao kina Ala kumbe na Gamal wakijiona kama wasioguswa. Uliza. Sasa wako wapi? Wananyea debe bila huruma huku baba yao akingoja apatikane na hatia anyongwe kama mbwa kama alivyofanyiwa Saddam Hussein habithi wa mahabithi.

Nimalizie na semini endekezi ya wizi iliyofanyika hivi karibuni kule Idodomya. Nani anakumbuka rafiki yangu alivyokuwa akijiliza na kuwawekea mkwara wezi?

Wengi tunajiuliza bila majibu. Kama dingi mzima mwenye kaya unalia lia hao wa chini yako wafanye nini? Kwani hayo maulaji ni yanini kama siyo kuwatoa watu wanapoboa?

Hata hivyo tusishangae. Wapo wanaomuona kama mnafiki na msanii wa kawaida anayepiga mkwara ili muda wake uishe atimkie kizani.

Niwachekeshe. Juzi niliona video ya bi mkubwa Shari Njaa Kikuku akihutubia kule kwa Joji Kichaka! Du kumbe mtupu ung’eng’e haupandi. Alivyokuwa akitokwa jasho na lafudhi yake ya kimachinga huku akikosea maneno ya kimombo sina hamu. Wapelekeni wake zenu shule.

Nimalizie kwa kumuonya kuwa Dogo asipofunga domo lake tutamvua nguo na si magamba.

Kama amesomea taaluma yoyote mbona haifanyii kazi na anajificha nyuma ya umoja wa vitegemezi wa kiama cha baba yake.

Ngoja nisogee karibu na hili hekalu. Naona shangingi lile kama la Dogo. Huyu mlinzi naona hana heri nami acha nijikate kabla sijaitiwa mbwa wa Fanya Fyoko Ukome. Khalas kweisine.

Sunday 15 May 2011

Better or Bitter Life for all?





When I deeply muse on how an arrogant and brutal cabal of hoity toity (Coverted Con Men (CCM)) is tirelessly hoodwinking and dividing the hoi polloi of ill-fated Africa, like a bomb, I feel like exploding.

I’m not a medical doctor. But thanks to my knowledge in psychology, education, journalism, law and conflict resolution studies, I can easily predict the gloomy future of Africa shall things remain as they wrongly are today.

Look at how menacingly hunger, corruption, selfishness, dictatorship and all maladies are clobbering our people. We recently witnessed some of people being killed, beaten and jailed simply because they did the right thing at the right time. In Uganda, the authorities brutalized the citizenry just because they voiced their anger. Instead of solving their problems, the authorities responded with bombs, gunshots and tear gas! Is this the food people wanted? Can violent and brutal silencing of Ugandans solve the problem or escalate it?

Currently hunger, joblessness, inflation, mega corruption, impolicy and sick economies, among others, are the only things we know. But again, the cabal of rulers that are looters is not affected. They have a lot of money they rob from us by the way of taxation. Even the budgets of their dockets and those protecting them are not affected. Our education systems are clogged with ignorance and impolicies thanks to producing unthinking rulers that cannot envision the danger they are blindly inviting.

Life almost everywhere in Africa is becoming useless and meaningless for the poor. All essential items are exorbitantly expensive. Who suffers? The common person of course.

But again, whilst the common bin-Adam is in limbo, the top dogs are increasing their emoluments and yum-yum. This is why Ugandan authorities did not see any logic in complaining about price surging, hiking of items, maladministration and what have you. They have their tummies full.

Sadly though, the same guys beating and jailing people are the same that promised people the whole heaven on earth! So too, they are the same honourable theives behind all these miseries hoi polloi is facing. Ironically, they still have the guts to kill, beat and jail! Can Yoweri Museveni hear and understand me? Zing.

Importantly, it should be underscored. Hosni Mubarak and Zine Adine Ben Ali faced the same situations and acted exactly the same way.

My shew stone tells me that the same people they mistake of being coward and docile will one day turn tables against them, and their illusion and brutality will be the good sources of their cascade.

People will nary live in lies wrapped in sweet and many promises of better life for all that turn out to be but sheer fiction. Though this is done as the process of waxing, in essence, it is but waning. Look at what transpired in Egypt, Ivory Coast and Tunisia just recently. Do these brigands think our people are zombies that can nary learn? This is but the “sign of the times” that needs to be read carefully and honestly. For the above mentioned countries are economically better off comparably.

Nonetheless, many provoking questions still boggle my mind. Is it better life or bitter life for all? How can life be better for all, whilst a few of us is living in heaven, whilst others (majority) are living in a hell on earth? Does this post-colonial promise of better life for all include slum dwellers, beggars, unemployed and all those suffering in the miseries for decades in Africa? Here is where the metaphor of waxing and warning comes in.

How can better life stop being bitter if at all, if a few of our venal rulers and their sycophants are able to steal billions of hard-earned dosh without facing the music? Aren’t we sick even feeling sarcastic of the ennui for being in bed with this inimical lot? What can such moral-bankrupt braggarts do apart from self-serving competitions as evidenced almost everywhere in Africa? How long shall we remain their victims in bondage?

To do away from all this bullshit, indeed, we need to hit them where it hurts, as James Hadley Chase once put it in one of his masterpieces. Take on them like Egyptians, Tunisians and Libyans did. Our venal rulers, or call them looters, pretend to be an island so as to maltreat already maltreated people with deceit and tear gas.

Going on smooching them shows nothing but malady and demise altogether. For how long are they going to gang rape us like sick minions? Happiness and life were created for all equally. We, thus, need to erase this anomaly so as to enjoy these beautiful rewards from the creator. After all, we have a short time to live. For we’ll one day die. Why were Egyptians and Tunisians able to boot their tyrants out not us? This is but our challenge.

People are afraid of death. Yet they die of and in miseries. It is better to die fighting for honourable life than living in a miserable one. Though death is the same, the way we die makes a difference. The death of a self-made slave is different from the hero. Who wants to live and die like a dog?

No dog can boast of better life. Being a dog and being tamed are two miserable things a human being should nary become. A dog is a dog whether it is fed or starved. Fat and starved dogs are all called dogs. Dogs that live in the castles are more humiliated than those put up in the wilderness. No human being should think or live or be treated like a dog by another human being.

When one accepts “dogness”, indeed, “he” is done. Such a person is chronically sick just like the one torturing him or her. Sick are all that live in the miseries they see and know without taking actions. So too, are those that cause those miseries simply because they’ve power. Peppery relationship with tormentors is better than peaceful acceptance of exploitation and humiliation.

Likewise, sick is everybody that exploits another. Those that exploit, cheat and take others for a ride are dogs despite being overfed on the toil of their victims. So we are talking about two types of dogs: overfed and over-starved dogs! Dogs are dogs. For they all have masters. Without masters, a dog is a mere wild dog. It is either a better or bitter life. But again a dog is a dog. A human being should nary be.

Source: Afro Spear May 14, 2011.

Friday 13 May 2011

Hivi huyu mi mzima kweli? wake 107 watoto 185!

Meet the Nigerian Islamic faith healer who married 107 women and has 185 kids!
Meet a Nigerian Islamic faith healer and polygamist man who has made marriage a full-time job, taking 107 brides and fathering 185 children.

According to the Los Angeles Times, Bello Maasaba, now 87, is currently married to 86 wives between the ages of 19 and 64. He has buried nine spouses and divorced 12 and his youngest child is one month old.

"I get a revelation from God telling me any woman I'm going to marry," the New York Daily quoted Maasaba as telling the Times.

"If it wasn't from God, I wouldn't have gone beyond two," he added.

The polygamist lives with his family in an 89-room house in the city of Bida. His extended family including in-laws, cousins, nieces, nephews now numbers about 5,000.

Maasaba was arrested three years ago for his audacious act, when he refused an order from Islamic authorities to divorce all but four of his wives.owever, when the case went to trial, dozens of his spouses testified they were married of their own free will. After hearing from 57 women, the court ordered Maasaba's release.

Chanzo; Internet

Wednesday 11 May 2011

Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu

KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujambazi wao. Viumbe hawa wachafu kama uchafu wao hawana hata aibu.

Kwa wanaosoma magazeti vizuri wanawajua kwa majina wachumia tumbo waliovaa majoho ya kiroho wenye uroho. Hapa lazima tuelewane. Ninaposema magazeti namaanisha magazetisi yale ya kifisadi ambayo yamejaza mikanjanja inayotumika kama nepi.

Pia simaanisha magazeti yaliyonunuliwa kwa pesa ya HEPA. Na yale ya kiama yanayounga mkono kila upuuzi kama yale ya utumwa (kinyume), mamluki (kinyume), fumba macho (kinyume), Mbongo na mengine mengi ya mifukoni.

Hata ninaposema runinga simaanishi zile za kifisadi na kibubusa kama vile BCT, VTV, NTC na nyingine nyingi ambazo ni zana za ufisadi.

Matapeli hawa wa kiroho wamejaa roho mtakakitu na mchafu chini ya kisingizio cha roho mtakatifu. Hawa si wachungaji bali fisi na mbwa mwitu wawararuao watu wa Mungu.

Hawa walafu hawana tofauti na wale mbwa mwitu aliotahadharisha Bwana Yesu. Hawa jamaa hawana Mungu zaidi ya matumbo yao na mafisadi. Hawana dini zaidi ya ufisadi na utapeli.

Matapeli hawa waliojivisha vyeo vikubwa na vitukufu kama uaskofu, uchungaji hata uijilisti, wameanza kuwa tishio na kero. Ni wa kuogopwa kuliko hata ukimwi na ukoma. Wamekuwa wakiwaibia watu maskini, wajinga na wenye matatizo kwa njia ya kudai sadaka na kula wao na kutajirika.

Wengine walipoona biashara zao za wizi wa sadaka hazitoshi, sasa wameamua kutafuta mbinu nyingine chafu zaidi ya kuongeza wafuasi ili sadaka iongezeke. Wanahubiri tumtolee Bwana wakati hakuna cha bwana wala bibi bali matumbo yao. Walibuni utapeli na sanaa ya kuomba na kufanya miujiza.

Kwani hamuowani kwenye runinga na kwenye hata magazeti na radio wakitangaza uchangudoa wao wauitao kuomba na kufanya miujiza. Kama wanaweza kutenda muujiza lau mmoja si mwingine bali kuwaibia walevi maskini wa Bongolalaland.

Kwa kula na kuiba sadaka hawajatosheka. Sasa wameanza kujipendekeza kwa mafisadi. Wamekuwa wakisikika wakiomba eti amani bila kukemea ufisi na ufisadi. Wamekuwa wakishambulia watu wanaofikiri sawa sawa wanaosema mfalme yuko uchi. Je, hawa ni nini zaidi ya kuwa chui kwenye gamba la kondoo?

Hawa nao wanapaswa kujivua magwanda au tuseme gamba. Niwajuavyo viumbe hawa laanifu hawawezi kujivua gamba. Ni jukumu la farasi wanaowabeba yaani walevi kuwavua gamba.

Ndiyo, wanafaa wavuliwe majoho na hatimaye magamba. Tusiwaruhusu watuombee na kutuomba bali tuwaombee na kuwaumbua. Maana nijuavyo, hivi karibuni mtawasikia wengi kama chiriku wakiimba nyimbo kwenye kambi mbili.

Wapo watakaomuunga mkono Mkuu wa Kijiwe kwenye kila upuuzi atakaoufanya. Pia wapo watakaomuunga mkono Ewassa ili kumsafisha. Katika makundi yote haya mawili hakuna mwenye nia ya kuunga mkono bali kuwatumia mafisadi hawa wakuu kujineemesha.

Niwape kisa kimoja ili mkumbuke na kujua viumbe hawa laanifu walivyo. Mnakumbuka mmoja wa waganga njaa hawa watumiao jina la Mungu aitwaye Zakkie Ka-tortoise alivyomsifia Mkuu wa Kaya kuwa ni mpole sana wakati akitetea genge lake la biashara lisipitiwe na mitambo ya unishati?

Kutokana na elimu na busara haba, jamaa alidhani akijipendekeza na kumsifu, angemtetea asijue naye ni kama yeye kwenye suala zima la usanii. Baada ya Mkuu kutoingia mkenge nadhani mnakumbuka jamaa alivyomgeuka na kumshambulia si kawaida.

Jamaa huyu aligufu na kudhani kuwa Mkuu wa Kaya ni kama Lyatongolwa ambaye akihadaiwa kidogo huchemka na kutoboa kila siri. Japo naye ni tapeli lakini hamfikii mkuu wetu kijiweni. Hakujua kuwa Lyatongolwa ni tapeli na kihiyo kama yeye. Angejua kuwa mkuu ni zaidi kwenye sanaa hii asingepoteza muda kwa kujipa matumaini yaliyoishia kuwa kilio na aibu.

Juzi nilimsikia fisidini Godfala Muhogo-lolo akihanikiza kujikomba na kujiuza kama changu kwa Njaa. Pia hata Mozes Kuloa naye nilimsikia akijinadi gulioni kwa mafisadi. Mzee huyu anatia huruma. Alianza kuwatapeli watu kuwa anatenda miujiza. Baada ya kumshtukia aliwamba ile mbaya na sasa ameibuka na uchangudoa wa kiroho na kisiasa. Hata Chris Mtikisa msimwamini. Murongo huyo hana lolote bali njaa na kujikomba. Anarusha makombora ili aandikiwe cheki na azame na kutuguna na akiishiwa arejee.

Inashangaza sana. “Askofu” mzima unajikomba kwa wezi tena wanaosababisha mauaji ya halaiki. Sorry sina haja ya kukulaumu. Maana wewe si askofu bali askopo au tuseme muasipofu. Ajabu maaskofu hawa wa kujipachika hata hawaoni aibu tunavyowavumilia kwa uaskofu wao wa kujipachika!

Kuna vijiaskofu uchwara vingi vilivyojipachika uaskofu vinavyoibuka kila uchao vikijifanya vinamtetea mkuu ili avitupie mabaki. Viogopeni na vizodoe na kuvifichua vijue mambo vinayofanya ni kinyaa kwenu.

Siku hizi hawa maaskufuru wa kujipachika wamekuwa kama waganga wa kienyeji. Hamkuwasikia wengi wakipambana na babu wa Loliyondo baada ya kuwafunika kwa ujiko na mihela? Wote lao moja. Wangetaka nao wawapate kama babu alivyowapata hadi wazito kiasi cha kugeuka serikali ndani ya serikali.

Wanajikomba kwa kila mtawala bila kujali miiko ya nafasi walizodandia. Hata hivyo huwezi kuwashangaa sana kutokana na ukweli kuwa wao si watumishi wa Mungu bali muungu-mali na madaraka.

Zamani dini zilikuwa zinaheshimika kabla ya kuibuka kwa maaskufuru na mashehena kiasi cha kuzifanya ziwe biashara na ugaidi wa kawaida.

Bad news ni kwamba mzee mzima nilinusurika kurejesha namba mnamo tarehe sita mwezi huu kutokana na mtambo wangu kupinduka nilipokuwa nakwenda kumpa hongera Obama kwa kumnyotoa Osami bin Burden. Nitaongea kwa kirefu wiki ijayo.

Yule changu namkumbuka. Niliwahi kufaidi ulodi wake na kugoma kulipa fadhila. Ngoja nijikate asijenitoa jasho bure watu wakajua kuwa nasi wakubwa ni waasharati.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 11, 2011.

Hawa si wachungaji bali ni fisi na mbwa mwitu

KUMEZUKA mtindo mchafu na wa rejareja wa baadhi ya wachumia tumbo na matapeli kumtania hata kumtumia Mwenyezi Mungu kufanya utapeli na ujambazi wao. Viumbe hawa wachafu kama uchafu wao hawana hata aibu.

Kwa wanaosoma magazeti vizuri wanawajua kwa majina wachumia tumbo waliovaa majoho ya kiroho wenye uroho. Hapa lazima tuelewane. Ninaposema magazeti namaanisha magazetisi yale ya kifisadi ambayo yamejaza mikanjanja inayotumika kama nepi.

Pia simaanisha magazeti yaliyonunuliwa kwa pesa ya HEPA. Na yale ya kiama yanayounga mkono kila upuuzi kama yale ya utumwa (kinyume), mamluki (kinyume), fumba macho (kinyume), Mbongo na mengine mengi ya mifukoni.

Hata ninaposema runinga simaanishi zile za kifisadi na kibubusa kama vile BCT, VTV, NTC na nyingine nyingi ambazo ni zana za ufisadi.

Matapeli hawa wa kiroho wamejaa roho mtakakitu na mchafu chini ya kisingizio cha roho mtakatifu. Hawa si wachungaji bali fisi na mbwa mwitu wawararuao watu wa Mungu.

Hawa walafu hawana tofauti na wale mbwa mwitu aliotahadharisha Bwana Yesu. Hawa jamaa hawana Mungu zaidi ya matumbo yao na mafisadi. Hawana dini zaidi ya ufisadi na utapeli.

Matapeli hawa waliojivisha vyeo vikubwa na vitukufu kama uaskofu, uchungaji hata uijilisti, wameanza kuwa tishio na kero. Ni wa kuogopwa kuliko hata ukimwi na ukoma. Wamekuwa wakiwaibia watu maskini, wajinga na wenye matatizo kwa njia ya kudai sadaka na kula wao na kutajirika.

Wengine walipoona biashara zao za wizi wa sadaka hazitoshi, sasa wameamua kutafuta mbinu nyingine chafu zaidi ya kuongeza wafuasi ili sadaka iongezeke. Wanahubiri tumtolee Bwana wakati hakuna cha bwana wala bibi bali matumbo yao. Walibuni utapeli na sanaa ya kuomba na kufanya miujiza.

Kwani hamuowani kwenye runinga na kwenye hata magazeti na radio wakitangaza uchangudoa wao wauitao kuomba na kufanya miujiza. Kama wanaweza kutenda muujiza lau mmoja si mwingine bali kuwaibia walevi maskini wa Bongolalaland.

Kwa kula na kuiba sadaka hawajatosheka. Sasa wameanza kujipendekeza kwa mafisadi. Wamekuwa wakisikika wakiomba eti amani bila kukemea ufisi na ufisadi. Wamekuwa wakishambulia watu wanaofikiri sawa sawa wanaosema mfalme yuko uchi. Je, hawa ni nini zaidi ya kuwa chui kwenye gamba la kondoo?

Hawa nao wanapaswa kujivua magwanda au tuseme gamba. Niwajuavyo viumbe hawa laanifu hawawezi kujivua gamba. Ni jukumu la farasi wanaowabeba yaani walevi kuwavua gamba.

Ndiyo, wanafaa wavuliwe majoho na hatimaye magamba. Tusiwaruhusu watuombee na kutuomba bali tuwaombee na kuwaumbua. Maana nijuavyo, hivi karibuni mtawasikia wengi kama chiriku wakiimba nyimbo kwenye kambi mbili.

Wapo watakaomuunga mkono Mkuu wa Kijiwe kwenye kila upuuzi atakaoufanya. Pia wapo watakaomuunga mkono Ewassa ili kumsafisha. Katika makundi yote haya mawili hakuna mwenye nia ya kuunga mkono bali kuwatumia mafisadi hawa wakuu kujineemesha.

Niwape kisa kimoja ili mkumbuke na kujua viumbe hawa laanifu walivyo. Mnakumbuka mmoja wa waganga njaa hawa watumiao jina la Mungu aitwaye Zakkie Ka-tortoise alivyomsifia Mkuu wa Kaya kuwa ni mpole sana wakati akitetea genge lake la biashara lisipitiwe na mitambo ya unishati?

Kutokana na elimu na busara haba, jamaa alidhani akijipendekeza na kumsifu, angemtetea asijue naye ni kama yeye kwenye suala zima la usanii. Baada ya Mkuu kutoingia mkenge nadhani mnakumbuka jamaa alivyomgeuka na kumshambulia si kawaida.

Jamaa huyu aligufu na kudhani kuwa Mkuu wa Kaya ni kama Lyatongolwa ambaye akihadaiwa kidogo huchemka na kutoboa kila siri. Japo naye ni tapeli lakini hamfikii mkuu wetu kijiweni. Hakujua kuwa Lyatongolwa ni tapeli na kihiyo kama yeye. Angejua kuwa mkuu ni zaidi kwenye sanaa hii asingepoteza muda kwa kujipa matumaini yaliyoishia kuwa kilio na aibu.

Juzi nilimsikia fisidini Godfala Muhogo-lolo akihanikiza kujikomba na kujiuza kama changu kwa Njaa. Pia hata Mozes Kuloa naye nilimsikia akijinadi gulioni kwa mafisadi. Mzee huyu anatia huruma. Alianza kuwatapeli watu kuwa anatenda miujiza. Baada ya kumshtukia aliwamba ile mbaya na sasa ameibuka na uchangudoa wa kiroho na kisiasa. Hata Chris Mtikisa msimwamini. Murongo huyo hana lolote bali njaa na kujikomba. Anarusha makombora ili aandikiwe cheki na azame na kutuguna na akiishiwa arejee.

Inashangaza sana. “Askofu” mzima unajikomba kwa wezi tena wanaosababisha mauaji ya halaiki. Sorry sina haja ya kukulaumu. Maana wewe si askofu bali askopo au tuseme muasipofu. Ajabu maaskofu hawa wa kujipachika hata hawaoni aibu tunavyowavumilia kwa uaskofu wao wa kujipachika!

Kuna vijiaskofu uchwara vingi vilivyojipachika uaskofu vinavyoibuka kila uchao vikijifanya vinamtetea mkuu ili avitupie mabaki. Viogopeni na vizodoe na kuvifichua vijue mambo vinayofanya ni kinyaa kwenu.

Siku hizi hawa maaskufuru wa kujipachika wamekuwa kama waganga wa kienyeji. Hamkuwasikia wengi wakipambana na babu wa Loliyondo baada ya kuwafunika kwa ujiko na mihela? Wote lao moja. Wangetaka nao wawapate kama babu alivyowapata hadi wazito kiasi cha kugeuka serikali ndani ya serikali.

Wanajikomba kwa kila mtawala bila kujali miiko ya nafasi walizodandia. Hata hivyo huwezi kuwashangaa sana kutokana na ukweli kuwa wao si watumishi wa Mungu bali muungu-mali na madaraka.

Zamani dini zilikuwa zinaheshimika kabla ya kuibuka kwa maaskufuru na mashehena kiasi cha kuzifanya ziwe biashara na ugaidi wa kawaida.

Bad news ni kwamba mzee mzima nilinusurika kurejesha namba mnamo tarehe sita mwezi huu kutokana na mtambo wangu kupinduka nilipokuwa nakwenda kumpa hongera Obama kwa kumnyotoa Osami bin Burden. Nitaongea kwa kirefu wiki ijayo.

Yule changu namkumbuka. Niliwahi kufaidi ulodi wake na kugoma kulipa fadhila. Ngoja nijikate asijenitoa jasho bure watu wakajua kuwa nasi wakubwa ni waasharati.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 11, 2011.

Monday 9 May 2011

Kikwete na mkewe mbona wanachezewa sana?





Hebu angalia hizo picha hapo juu ulinganishe na ukweli. Inashangaza mke na mume hawako makini kwenye kila wanachofanya. Ajabu ni kwamba hata wanaowadhalilisha au tuseme kuwapima hawajali kuwa kuna macho makali pembeni! Je wahusika wanasukumwa na tamaa na ujinga kiasi cha kupokea madudu kana kwamba hawana macho wala akili? Je hao wasaidizi na wapambe wao wanalipwa kwa kazi gani kama wote ni sawa? Je mtu wa namna hii anafaa kuaminiwa madaraka makubwa kama urais? Hakika aliyohofia marehemu Baba wa Taifa mwalimu Julius Nyerere yanajitokeza kila uchao.

Sunday 8 May 2011

Wanadamu tuogopeni sisi siyo Mungu


Hivi karibuni kumetokea wimbi la baadhi ya matapeli wanaojitangaza kuwa watetezi wa manfisadi. Wamedangaya na kuumiza wengi hasa wajinga na maskini wenye matatizo ya kimaisha.

Hivyo usishangae kusikia "askofu au mchungaji" fulani akitetea fisadi wake mwenye madaraka. Mara nyingi, matapeli hawa hawatumwi na wanayemtetea bali kutaka kujipendkeza kwake ili awatupie mabaki ya fedha zitokanazo na ufisadi.

Yesu aliacha busara moja kuhusiana na matapeli hawa wanaotumikia matumbo yake kwa kisingizio cha neno la Mungu. Hawa hawamtumikii Mungu bali kumtumia kuneemesha tamaa na matumbo yao. Tuwaogope kama ukoma. Tukimbie makanisa yao na kupuuzia mahubiri yao.Yesu aliwalinganisha hawa na chui wenye kujivika ngozi ya kondoo ili wawararue kondoo.

Yesu aliwajua vizuri. Alisema kuwa utawajua kwa matunda yao. Ni muhimu kuwatahadhari. Wanatamka maneno mazuri na kutenda shubiri.

Hawa matapeli wa kiroho hawako peke yao. Wapo waandishi wa habari mitondoo ambao wako tayari kujidhaliiisha wao familia zao, taifa na taaluma zao ili washibe kwa mabaki yatokanayo na ufisadi. Tuliwaona wakati wa uchaguzi mwaka 2002 hata 2010. Wamejiweka rehani na kuhatarisha usalama wa jamii ili wajazwe makombo na uchafu vitokanavyo na ufisadi jinai inayosaliti utaifa na jamii.

Bahati mbaya sana, baadhi ya mafisadi wanamilki hata vyombo vya habari na waandishi uchwara wenye roho zilizokaa mifukoni mwao badala ya vifua vyao. Je hawapo? Hebu soma magazeti ya kila siku uone ukweli wa haya yanayoandikwa. Kuna wahariri na waandishi ambao ni vigumu kuwatofautisha na dodoki au nepi. Wanatumiwa na hawastuki wala kuangalia mbele wala nyuma bali mifukoni.

Kinachokera ni ile hali ya wananchi kutoa pesa yao ya maana kusoma uchafu wa maajenti wa mafisadi. Vyombo vyao vya habari vinajulikana kwa majina na mahali vilipo bila kusahau hata hawa mafisadi wanaovinunua na kuvitumia.
Kuna kipindi unashindwa kutofauti kichwa na kiuno cha mtu viko wapi kutokana na anavyojirahisi na kutumiwa.

Turejee kwa wanaojipachika uongozi wa kiroho wakati ni waroho wa kawaida. Ni wangapi sasa wanatumia kila mbinu kutangaza uongo na utapeli wao kwa mfano wanaouita ufanya miujiza wakati ni upuuzi wa kawaida? Juzi kulitokea ugomvi baina ya mbweha hawa waliovaa majoho na babu wa Loliondo. Babu anatafuta kula kwa kutumia mawazo na shuhuda za ndoto akitetea uganga wa kienyeji kwa kuupa umungu. Wao walipoona anatikisa wakaanza kulia lia.

Ni wangapi tulikuwa tumezoea kuwaona wakijisifu kutenda miujiza ya kupata utajiri wakati ni wauzaji wa kawaida wa madawa ya kulevya?
Baadhi yao walipopata vyeo vya kisiasa hatuwasikii wala kuwaona! Tunaowaona na kuwasikia ni wale vidhabu wachungaji wa kujipachika na wanasiasa wa msimu ambao huibuka na kutokomea wanapopewa chao. Je hawa wanaweza kweli kuwa watu wa Mungu au muungu pesa na mafisadi?

Tutawalaumu matapeli hawa kwa kujipendekeza kwa watu wachafu huku wakimtumia Mungu. Vile vile waumini wanaoshindwa kuwapiga teke au kutowapa hizo sadaka wanazotumia kupata umaarufu na kutaka kuwaridhisha mafisadi ili wawakati kitu kidogi hata kibwa. Maana bila ya waumini hawa matapeli ni bure.

Kimsingi waumini ndiyo mtaji mkubwa umaarufu na ndoto za kuwa karibu na mafisadi wakubwa ili wawatumie kupata mabaki.

Hivyo, siri ya kuwamaliza ni kuwakimbia na kutosikiliza ulaghai wao. Waumini wanaweza kujikuta wakichangia kuenea na kutamalaki kwa ufisadi bila wao kujua. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Matapeli hawa wa kiroho waliojaa roho mtakakitu bwanayemuita mtakatifu wanalijua hili. Ndiyo maana huendelea kuwalewesha mateka wao ili wawatumie.
Tumalizie na kisa cha hivi karibuni ambapo gaidi wa kimataifa Osama bin Laden licha ya kuuawa kama mbwa alifichuliwa unafiki na woga wake. Alikuwa akihimiza watu wampiganie Mungu na wasiogope lakini yeye aliisi kwa kujifungia nyuma ya kuta na walinzi. Je kwanini hakumuacha Mungu wake amlinde kama kweli alikuwa akiamini katika Mungu? Bin Laden aliwahimiza watu kuwa mashahidi tena wasioogopa! Ajabu ya maajabu yeye akikuwa mwoga kuliko hata panya! Ajabu nyingine watu wenye mtindio wa akili walimwamini, kumuabudia na kumtumikia bila kutumia hata chembe ya akili.

Ajabu nyingine ni ile hali ya mahasidi wa Bin Laden-Marekani kuonewa huruma wakati wao ndiyo walimtumia na kudhulumiana naye. Nani anajali kupoteza muda kidogo kutafuta ukweli hata kama mchungu umuweke huru.

Tumalizie kwa kusema wazi kuwa hatuna kundi wala upande linapokuja suala la utapeli na kugeuza na mabwege. Viongozi wa kidini wanaojipendekeza kwa mafisadi wanaweza kuwa ima mafisadi wenyewe na wabaya kuliko hata hao mabwana na miungu yao waitwao mafisadi. Je hamkuwsikia wengi wakiwatetea kwa kisingizio cha amani na kuwambea?
Tunawahimiza waumini na wananchi kwa ujumla kuwaogopa mbweha hawa waliojivisha majoho kuliko hata ukoma na ukimwi.
Chanzo:Dira ya Mtanzania Mei 9, 2011.

Friday 6 May 2011

Siku nilipokiona kifo kinakuja

Hapa naangalia madhara mke wangu alipokuja kunichukua toka kwenye eneo la ajali
Hapa ni eneo la ajali ambapo mke wangu anaangalia madhara kwenye eneo la tukio asiamini


Wapendwa wasomaji nachukua fursa hii kumshukuru Mungu kuwa leo nimenusurika kwenye ajali ya barabarani ambapo gari langu limepinduka na kubiringika kama mara tano. Nimetoka mzima bila mchubuko wala maumivu. Ni muujiza.

Thursday 5 May 2011

Was Bin Laden a crusader or lunatic?


The world did not know the most vilified and hunted person, Osama Bin Laden, until August 7, 1998 when simultaneous bombs exploded in US embassies in Dares Salaam and Nairobi respectively. Over 200 innocent people were killed in these attacks.

Intelligence world took note of him and started devising the methods of dealing with him. The good or bad thing about Bin Laden is the fact that he’s not new to America and vice versa.

In essence, Bin Laden was the creature of the US created during cold war. Thanks to USSR invasion to Afghanistan, the US had to team up with Mujaheddin to defeat the then Soviet Union. In this courtesan marriage of convenience, everybody tried to use each other to attain his goals. This is when desperate Bin Laden, after being stripped off his Saudi citizenship, came into the big picture.

If anything, the US regrets its negligence for not disposing Bin Laden after using him in Afghanistan. So too, Bin Laden regretted to, blindly, render his service to the guys that have no permanent enemy or friend.

Thanks to the umbrella or covert of Islam Bin Laden used to use, he easily fooled many so as to have sycophants and sympathizers in the intelligence world, especially in countries like Afghanistan and Pakistan where he lived and died. Living in Pakistan for long without being detected or dealt with speaks volume regarding this conspiracy and double standard.

Going back to Bin Laden hallmarks, though these attacks on America’s establishment in East Africa were conducted by Al Qaeda, the world, for the first time, knew of Al Qaeda and its leader and founder Bin Laden. But thanks to the minor status of the victims and locality of the embassies (Africa), Bin Laden was not taken seriously. He did not even become a legend.

One important link that connected Obama with this crime is the fatwa he had issued earlier saying that Muslims are duty bound to kill Americans and this would be translated as jihad.

Bin Laden became an icon-cum-devil-incarnate on September 11, 2001 when Al Qaeda struck one gain. This time America’s symbol of power and prosperity, the twin-tower-World Trade Center (WTC) in downtown Manhattan New York, became a target. What transpired is but dirty history and a scar on humanity. The anger that emanated from hither is too known everywhere.

In actual fact, the September 11 attacks gave Bin Laden a new look among the world. Those hoodwinked by his megalomania, that of fighting for Islam revered him, whilst those who knew his devilish megalomania hated him next to no one.

Now that Bin Laden is no more, was he a hero that deserved reverence or a mere lunatic that was supposed to be flashed out earlier than it took? Bin Burden, the thorn in a shoe for America is no more than a dark and lunatic history.

Though Bin Laden pretended to stand for Islam, there are those who doubted his legality and fitness as far as Islamic cause is concerned. They urged, how could a bastard as per Islamic law, fight for its cause? Islam allows a Muslim, under strict conditions of extreme fairness and equality to marry up to four wives.

Koran 4:3 “And if you fear that you will not deal justly with the orphan girls, then marry those that please you of [other] women, two or three or four. But if you fear that you will not be just, then [marry only] one or those right hand possesses. That is more suitable that you may not incline [to injustice].”

Many eminent psychologists and sheiks agree that a human being can nary be fair by nature. Thus, whoever marries many wives, in other words, is going against Islam and the law of nature. No ontocratic possibility between these. Osama’s mother, Hamida al-Attas was a tenth wife of Mohammed bin Awad bin Laden.

Even if one looks at his last moment will find something fishy. Reports have it that one woman was killed along with Bin Laden. This woman is said to be one of Bin Laden’s guard. Why a woman? Wasn’t she his mistress knowing that if he brought his known wife or wives in, they would blow his cover? Is this Islamic?

Even if you look at his father’s hyper touted wealth, you’ll find it highly suspicious. For he had to befriend King Faisal to secure tenders. This means he did not use merit to win those tenders of building government buildings. Is this Islamic? For those conversant with how corrupt the Saudi regime is, will agree with me that what they do is contrary to what they preach and pretend to stand for, hype hypocrisy. One empirical fact is the kingdom. Islam presupposes that Muslims should be ruled under caliphates, not kingdoms or ayatollahs as it is in Iran.

More on unfitness of Saudi regime. Last year one of the grandsons of the King Abdullah, Saud Bin Abdulaziz Bin Nasir al-Saud, was jailed in Britain for murdering Bandar Abdullah Abdulaziz on February 15. The media had it that the deceased and his killer had homosexual relationship. This is intolerable in Islam. But again, thanks to being the prince, even if his un-Islamic behaviour was known, nobody would punish him. But if this were committed by a commoner, he would face the noose of a hangman.

Who was Bin Laden actually? A lunatics just like Paul Kibwetere, who on 17 March 2000, killed over 500 followers at Kanugu in Uganda. This killer promised his victims that they would go direct to heaven.

He was a megalomaniac using the word of God, just like Vernon Howell (David Koresh) who on 28 February 1993 at Mount Carmel, US, killed over 70 followers including 20 teens by duping them that they would go to heaven.

True, many lunatics and con men and women use religion to dupe and rob people. Sadly though, all these famous lunatics like those mentioned above were not captured so as to have their brains examined. This would give us a clue as to how religious lunatic think so as to avoid future miseries.

Though Bin Laden has taken many blames, the US too has its share. So too is double faced ally Pakistan that used to receive billions of dollars aimed at tracking down Bin Laden and his gang, but still sheltered him. Now that the world is under one order, it should abolish its double standard policies of exploiting others.

Now that Bin Laden is gone, will peace prevail? Hopefully yes if we study what happened to Red Brigade or what happened after the apprehension of Carlos the Jackal.
Source: Afro Spear May 4, 2011.


For more comments from readers CLICK HERE

Sasa ni vita kuvuana magamba

Kuna usemi maarufu kuwa kumbikumbi akikaribia kufa huota mbawa na kupaa ili kunguru wamtafune. Hili ndilo linalokikabili Chama Chama Mapinduzi (CCM) baada ya kuja na usanii uitwao kujivua gamba.

Sasa tujiandae kushuhudia mnyukano na mpambano baina ya CCM hasa yale makundi ya kimaslahi maarufu kama mitandao. Huu ni ushahidi kuwa hata ajivue magamba vipi nyoka atabaki kuwa nyoka. Isitoshe hakuna kuishiwa kama huku ambako ni kiashiria cha mwanzo wa mwisho wa CCM. Tumpongeze Rais Jakaya Kikwete kuwa wa mwisho kupigilia msumari kwenye kaburi la CCM. Ama kweli waliosema yeye ni chaguo la Mungu, hawakukosea!

Turejee mitandao. Kimsingi, mitandao hii ya wasasi wa mali na madaraka ndicho chanzo kizuri cha kuporomoka na kuchukiwa kwa CCM. Maana, iliundwa mahsusi kutafuta madaraka. Ili kupata madaraka lazima uwe na fedha ya kuhongea wapiga kura hasa wakati ule takrima ikiruhusiwa. Ili kupata pesa lazima ushiriki ufisadi. Nani hakutumia kanuni hii kuanzia mwenyekiti na wale waliotimuliwa?

Kimsingi, mitandao ndilo chaka la ufisadi wote tunaopigia kelele bila kusikilizwa. Tulisema hadi sauti zikakauka. Wahusika walitupuuzia na kutuona wazushi na wenye wivu wa kike. Waliendelea na business as usual kulindana, kufadhiliana na kuzidi kushikamana katika jinai. Maskini hawakujua kuwa mambo hubadilika. Baada ya umma kuwastukia, hatimaye nyufa zilianza kujitokeza na kukisambaratisha Chama bila kuiacha serikali yake.

Kinachoshangaza ni ile haya ya sasa ambapo mitandao, yenye ama madaraka au ukaribu na wenye madaraka, kuanza kuitafuna ile inayotishia madaraka kutoka mikononi mwake ama kutokana na kuchusha au kuliana njama.

Hali inazidi kuwa mbaya hasa ikichangiwa na ulevi wa madaraka kiasi cha watu kujihisi na kujiona hawagusiki, ndiyo CCM ilizidi kutota.

Sasa baada ya wenye (wana) nchi kuiadhibu kwenye uchaguzi mkuu uliopita ikanusurika kwa kuchakachua, CCM, hatimaye, imezinduka na kutia akili ikiwa imechelewa sana. Kutaka kuendelea kuwaridhisha na kuwaibia wale iliowadharau na kuwaibia kwa muda mrefu, CCM ilikuja na usanii wa kujivua gamba. Katika kufanya hivyo ilijivua kigamba kidogo cha mkiani huku ikiacha gamba lenyewe liendelee kutuna! Je tatizo la nyoka ni sumu au gamba?

Kwa wanaojua mshikamano na ushirika wa CCM katika kutenda jinai kama vile wizi wa fedha ya umma toka Benki kuu chini ya fuko la EPA, watakumbuka jinsi jinai hii ilivyo kama mduara. Si mkubwa si mdogo wote wamo- (mtego wa panya) wamechafuana. Hakuna msafi CCM kuanzia mwenyekiti hadi mfagia ofisi.

Baada ya kukaa Dodoma na kufanya kile wazungu huita Cosmetic Changes (CC) kwa kutoa shinikizo kwa vigogo wake waliotaja sana waachie ngazi, CCM , kama mtoto mchanga ajipakae maji tumboni akiamini ameoga, ilikuja na majigambo kuwa imejivua gamba wakati gamba bado linaonekana.

Kwa vile CCM wamejifanya vipofu kiasi cha kudhani na watanzania ni vipofu, hatuna shaka sasa wale waliojeruhiwa na sanaa hizi watatwambia mengi. Hii maana yake ni kwamba nguvu ilivyokuwa ikitumika kuwahonga wanahabari wenye roho na tamaa za fisi, itaelekezwa kuwarudi waliowajeruhi. Sitashangaa kuona yale magazeti yaliyonunuliwa kwa pesa ya EPA kuanza kuwashughulikia walioidhinisha wizi huu.

Na hii ni matokeo ya watu kufanya maamuzi bila kuangalia matokeo yake. Tunajua CCM baada ya kuona umma umewastukia na hasa ikichangiwa na kinachotokea kwenye baadhi ya nchi, walikurupuka na kutosana kama walivyozoea wasijue, si jibu. Hili haliwezi kuwa jibu lenye kuingia akilini kutokana na umma kujua yote yanayofanyika chamani na serikalini. Watu wanajua nani ameiba kiasi gani akimtumia au kusaidiana na nani. Wanajua kuwa chanzo cha mchezo huu licha ya ufisadi ni kulipana fadhila, kujuana, kulindana na kutoona mbali.

Haiingii akilini, kwa mfano, watuhuhumiwa wa EPA watolewe kafara wakati waliofaidika na wizi huo wakiachwa wawe ndio waamue nani atoswe na nani abaki. Hapa ndipo wenyeviti wa CCM yaani Benjamin Mkapa (mwenyekiti mstaafu aliyeasisi skandali ya EPA) na Jakaya Kikwete hawana jinsi ya kupona hata kama watatumia maguvu ya madaraka yao.

Wengi watauliza Mkapa naye alinufaika vipi? Bila kuasisi EPA unadhani angenusurika kufikishwa mahakamani? Wakipona ni kwa muda. Ukweli wa matokeo haya utajulikana mwaka 2015 ambapo CCM piga ua itajikuta kwenye benchi la upinzani huku kesi nyingi zikifumka.

Kwa kosa walilotenda CCM wajue fika, kufikia kwenye uchaguzi wa 2015, watakuwa wamechafuka zaidi ya sasa kutokana na wale waliotemwa kumwaga mboga ili wote wakose. Hii ni silka ya binadamu. Na hili litakamilisha utabiri wa mwanzilishi wa CCM marehemu baba wa taifa kuwa atakayeibomoa CCM atatoka CCM.

Na hakika huyu si mwingine bali Kikwete na genge lake la washauri na waramba viatu.vyake, ataibomoa CCM sawa na wenzake wakishirikiana naye walivyoanza kuibomoa walipotelekeza maadili ya uongozi na kushabikia madili. Je mwanzo wa mwisho wa CCM upo nasi? Hata wajivue ngozi achia mbali gamba unyoka na sumu yao vitaendelea kuwaandama.
Chanzo:Tanzania Daima Mei 4, 2011.

Wamevuana magamba, sisi nguo

BAADA ya Chama ambacho wabaya wake wamekipa jina la Chama Cha Majoka (CCM) wengine wanakiita cha magamba, kujivua gamba, kijiwe nacho kimekuja na mpya. Kwanza ieleweke. Huu si usanii kama wa CCM bali kutaka kufanya kweli.

Si yametokea mafyatu yanayojifanya yanachukia ufisadi kusema eti tuvuane nguo ili kila mtu abakie alivyozaliwa tumuone! Sikuwa najua kama kahawa inalevya kama maulaji. Baada ya walevi kupwakia kahawa na kashata wacha wachachamae kama siafu!

Ikichukuliwa kuwa ni muda mrefu nimekuwa nikikwepa kuitisha vikao vya kijiwe, walevi walikuwa na usongo sina mfano. Kila mtu alipania kunivaa mwenyekiti ili waje na mkakati wa kuvuana nguo na kunitosa.

Sababu kuu iliyotolewa ni kwamba sisi si majoka wala mijusi bali watu. Hivyo magamba yetu ni nguo tuvaazo. Mijamaa hii mishenzi sina hamu. Moja si lilisema eti majoho, mipete, micheni, misuti na makorokoro yangu ya bei mbaya ndiyo magamba hasa yatokanayo na ufisadi. Mingine ilisema eti NGO ya bi mkubwa ya kashata nayo ni gamba!

Kijiwe kilikaa kikao cha dharura tena bila idhini ya mkiti na kutaka kujadili ufisi na ufisadi. Kwanza walevi wote walipitisha kauli moja kuwa Mgosi Machungi wa Makambale atimuliwe ukatibu mkuu wa kijiwe.

Mzee Maneno ndiye alikuwa wa kwanza kulitibua. Alisema, “Waheshimiwa wajumbe tusipoteze muda. Leo lazima tusafishe kijiwe chetu kwa kuwatimua mafisi wote.”
Inaonekana hii ilikuwa imepangwa. Maana wote waliitikia kwa pamoja isipokuwa washirika wangu waliokuwa wamepigwa na bumbuwazi.

Kuona wanataka kunipindua nikiwepo niliingilia haraka, “Hili ni jambo jema kwa mustakabali wa kijiwe. Natoa baraka zote tuwasulubu mafisi wa kijiwe hiki. Kwanza, watajeni hao mafisi. Mie sitaki unafiki.”

Kabla sijamaliza mzee Maneno alidakia, “Mwenyekiti acha unafiki. Unajifanya hamjijui mko mafisi wangapi? Mbona kwenye kuiba njuluku za kijiwe kupiga kampeni iliyokupa ulaji mlikuwa pete na chanda. Leo unajifanya kuwasahau!”

Kabla ya kumaliza, Msomi alipayuka. “Basi tunawataja. Kwanza mkiti, Mgosi, Ewassa, Roasttamu, Chengee.”

Kabla ya kumaliza Mchunguliaji anakwanyua mic, “Mbona humtaji bi mkubwa wa Mkiti na NGO yake na kitegemezi chake Riziki ambao ni wakwasi wa kutupwa kutokana na kutumia madaraka ya mkiti?”

Makambale alivyo mbishi msambaa huyu si alikataa kufa peke yake. Alisema hawezi kuachia ngazi hadi waganga njaa wenzake wa Kamati kuu ya Kijiwe yaani Kijiwe Central commetee (KCC)nao watimke naye isipokuwa mie mkiti.

Wakati Makambale akipiga mkwara mie nilikuwa nimeishaanza kunonihii kwenye sarawili yangu. Baada ya kujitoa mhanga kufa na wenzake huku akinisaza mimi, nilianza kupumua.

Msomi Mkata Tamaa alikwanyia mic na kutoa wazo la kipumbavu kuwa wa kwanza kuvuliwa nguo na ulaji niwe mimi mwenyekiti. Toba! Nilijisemea moyoni. Mie na kutotahiriwa kwangu si itakuwa shughuli!

Nikiwa natafakari la kusema lau kujiokoa ingawa kiakili sina ujanja wala mshipa, si fyatu wangu Pio Mchekwa akajaribu kuokoa jahazi.

Bila kuomba ruksa Pio alisema kwa kujiamini, “Mkiti ni mtu safi sema anaonekana mchafu kutokana na kushauriwa vibaya na akina Mgosi.”

Kabla ya kuendelea fyatu Andramani Kinamna alikwapua mic na kusema, “Msomi tukubaliane umevuka mipaka. Mkiti ni mtu safi na hata kama ni mchafu inakuwaje atoswe na sisi wenzake bila kutoa wengine sadaka ili apone?”

Kabla ya kuendelea mzee Maneno aling’aka, “We kinamna nyamaza. Uchafu wako wa kutorosha nyara za kijiwe unajulikana. Hivyo funga domo lako hata kama unapewa makombo na mkiti.”

Bila kungoja waende mbali niliingia kati, “Mzee Maneno nakuheshimu sana. Futa kauli yako na uniombe msamaha kabla sijakutoa kafara.”

Mzee Maneno hana subira. Anadandia mic na kusema, “We ni mwizi wa kawaida tu hata kama ni mwenyekiti. Unadhani hatuoni mkeo na vitegemezi vyako wanavyotuibia kashata na kahawa kila siku? Nyamaza mwenyewe kabla sijakuvua nguo kabla hata ya kupitisha azimio la kufanya hivyo.”

Kuepusha shari ilibidi ninywee na kufunika kombe ili mwanaharamu huyu mzee apite nipete.

Kumbe mzee Maneno alikuwa amepania! Pia baadaye niligundua kuwa mpango ulikuwa umesukwa muda mrefu bila sisi kujua. Mzee Maneno alishikilia uzi na kusema lazima tuvuliwe nguo.

Kuona mambo yanazidi kuharibika, nilimtonya kijana wangu Mapepe Ninaye aharibu hewa. Bila kufikiri wala kujivunga ili kunifurahisha akijua nitampa ulaji Mape alinyanyuka na kusema, “Tukubaliane. Hatukuja hapa kupanga jinsi ya kumvua nguo mkiti bali Ewassa, Endelea Chenga na Roast Tamu ambao wanajulikana walivyokwanyua mimali ya kijiwe. Ndiyo siyo?”

Kijiwe wala hakikumsikiliza zaidi ya kuanza kumvua yeye nguo huku akizabwa vibao kama mwizi. Ilisika sauti ikisema, “We Mape ni kinyoka kichanga lazima tukushughulikie ili ufe na joka lenyewe yaani mkiti.”

Bila ajizi kijiwe kilipitisha pendekezo hili na kuamua kutuvua nguo. Tulivuliwa nguo. Tulilambwa vibao kuzomewa na nusu kuchomwa moto kama si busara ya Msomi Mkata Tamaa. Yaani ilikuwa tufe tunajiona!

Wanakamati waliliripuka kwa shangwe kutokana na kujua kuwa nilitaka kuwavua nguo hawa mapacha watatu nisijue ningevuliwa. Hawakungoja niidhoofike kama wengine walivyodhani. Isitoshe, huu ulikuwa kama mtego kwangu kuona nitawanusuru au kuwatosa vipi mabesti zangu. Ilibidi nitumie kanuni ya Yesu ya kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe ingawa haikusaidia.

Sasa Msomi ambaye ndiye mkiti alisema, “Tuweni wakweli. Dawa ya jipu ni kutumbua siyo kuligusagusa. Nashukuru leo mkiti kavuliwa nguo sambamba na watu wake.”
Hii imetutofautisha na wale wasanii wa magamba, wao walivuana magamba. Sisi tumewavua nguo na mmewaona walivyotimka uchi. Hali ilikuwaje, we acha tu sikia hivi hivi.

Kwa sasa niko kijiweni naganga njaa bila joho la uenyekiti. Ushauri wa bure, ukitaka kujivua ufisadi vua nguo badala ya magamba hata kama inauma na kutia fedheha.

Naona wale mafisadi wa magamba wanapita. Acha nikawahi kijiweni tupange jinsi ya kuwavua nguo hasa mkiti wao.

Khalasi kweisine Rais Mtarajali.
Chanzo: Tanzania Daima Mei 4,2011.

Sunday 1 May 2011

Breaking news! Osama bin Laden auawa



Habari zilizotufikia ni kwamba kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda, Osama Bin Laden aliuawa kirahisi nchini Pakistani. Taarifa kutoka ikulu ya Marekani na vyanzo vya habari ni kwamba Osama aliuawa kirahisi na mwili wake uko mikononi mwa serikali ya Marekani. Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA

Eheee! Gadaffi kumekucha mwanae auawa!


Habari ni kwamba mtoto wa mwisho wa imla wa Libya aitwaye Saif al Arabi Gadaffi aliuawa nyumba yao iliposhambuliwa na majeshi ya NATO usiku wa kuamkia jumapili ya tarehe mosi Mei.

Habari zinatonya kuwa katisha shambulizi hili makini, Muamar Gadaffi na mkewe walikoswakoswa kimiujiza. Saif al Arabi ameuawa sambamba na wajukuu watatu wa kiume wa Gadaffi.

Hakikia hii ni hatua muhimu kwa wapinzani na NATO. Kwani anaanza kudhoofishwa kisaikolojia kama ilivyotokea kwa mwenzake wa Iraq Saddam Hussein walipouawa watoto wake wawili katili.
Je Saif al Arabi alikuwa nani na alifanya nini? BONYEZA HAPA