The Chant of Savant

Thursday 2 June 2011

Tutaendelea kudanganywa na walevi hadi lini?

LEO nina hasira kuliko hata wiki jana wakati nataka kujilipua. You know what. Kwanza yale mauaji ya Tarime yamenifanya nichukie lisirikali na mandata kuliko wakati wowote katika ma-life yangu.

Pia mauaji haya yamefanya niwachukie walevi hasa wadanganyika kwa umbwa na ukondoo wao. Hivi mtauawa hadi lini wakati mkiona? Mwadhani kuna mjomba wenu atakayekuja kupambana na geshi la mambwa mwitu linaloamrishwa na mafisi kuwaueni?

Hayo ya Tarime mtajiju au kumalizana wenyewe. My concern today is showing my dismay regarding the whole bragadaccio ya kujivua gamba.

Najua viherehere wanaosoma hapa wanasema kuwa najidai kujua umombo. Mie najua lugha zote duniani isipokuwa ile ya mafisadi na matapeli wa kiroho wenye uroho.

Hivyo nikimwaga ung’eng’e uvumilie hata kama roho inakuchonyota. Hii ndiyo faida ya kwenda shule kuongeza ujinga-sorry elimu. Hata kuongeza ujinga inawezekana. Maana ukiangalia maprofwesa waliojazana serikalini wanavyofanya mambo ya kipuuzi kama Dokta Muinyi ambaye wizara yake ilifanya upuuzi kule Mbalaga akashindwa inshu ndogo tu-kuwajibika au madaktari uchwara wa kughushi kama akina Emmy Nchinvi, Mere Nyago na wengine, kuna ukweli kuwa kuna watu walikwenda shule kuongeza ujuha si ujinga.

Hawa leo sina mpango wa kuwananga. Maana tabu lao liitwalo Education for Ignorance liko mekoni likikorogwa ili nao baadaye wakorogwe na kupakuliwa wakati ukifika. Hivyo my friend Diddie Massamburi na PhD yako feki na Makorongoro Muhanga, Vickie Mwambalashwa kaa mkao wa kuliwa na kupakuliwa mambo yenu.

Leo nina hasira kama nilivyotonya hapo juu. Nina hasira sawa na wale vijana wa chama cha mafisadi wa kule AR waliotaka Mere Kitanda atimke baada ya kuzua noma kutokana na ujuha wake.

Japo wapo wanaosema kuwa wanatumwa na Ewassa ili kulikoroga, kama mbaya mbaya. Kwanini Ewassa awe fisadi pekee wakati na swahiba wake, mkewe hata mwanae ni mafisadi wa kunuka?

Kwenye ufisadi Njaa Kaya anamtoa knock out Ewassa kwa sababu Ewassa anatuhumiwa yeye na kitegemezi wake Freddie huku mama yake Regi akiwa nje ya ulingo wa unyakuzi. May be mambo yake hayajajulikani.

Ukija huku ni mess. NjaaKaya mwenyewe yumo kwenye First Eleven ya Dk. Silaha Kali, huku bi mkubwa Sisalama na Riz-One wakichukua nafasi ya juu kwenye tuhuma za ufisi.

Ziko wapi tambo za hichi kitegemezi uchwara kudai kitakwenda kwa pilato? Kimenywe kama dingi wake. Mama yake ndiyo usiseme. Anaendelea kusanya kama Anna Makapi. Jamani kuna haja ya kubadili methali zetu na kusema: walevi ndiyo waliowao na wadanganyika ndio waibiwao.

Hapa ndipo maana ya looting au tuseme lulling or bullying party yanapojitokeza. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba chama ongelewa ima ni cha majambazi, wasanii au wanyanyasaji hata wauaji. Kama nimewaongopea msikonde bali kwenda shule na kujua bila kutegemea tafsiri yangu. Alright! Kulaleki!

Hebu niwaulize walevi tena huenda wanaweza kutia akilini. Hivi mtaendelea kuongopewa huku jua likiwaka hadi lini? Ni juzi tu mmeletewa upuuzi wa kuvua gamba na kuvaa jezi za kulindana na kuwahadaa. Mmeendelea kuwa watazamaji na waathirika huku mkiishi kwa matumaini! Hadi lini?

Kabla ya moto wa changa hili la machoni kuzimika mara Dk. Silaha akafichua kuwa kitegemezi cha mkuu wa kijiwe ni kibilionea.

Mmesikiliza na kuendelea kutoatoa mimacho kama kunguru aliyenaswa kwenye ulimbo! Nashangaa mlivyoridhia kila ujambazi. You know what? Dowanis mmeliwa tena.

Kwani walioinunua wameishapata hakikisho toka lisirikali kuwa watazalisha na kuwauzieni hapo hapo. Na kwa taarifa yenu muelewe.

Dowanis haijauzwa kitu bali Rostitamu na wenzake wamebadili mikakati yao kwa kuleta sura ya mtasha baada ya mmanga tapeli kutofua dafu. Yule alikataa kupigwa picha. Mtasha kapigwa nyingi tu.

Najiuliza, hivi Dowanis kama hawajalipwa pesa yao waliyopewa na mahakama ya kimataifa, wamepata wapi uhalali kisheria kuuza mitambo yao kama siyo usanii wa kipumbavu kwa vile wana dili na walevi na wadanganyika?

Siku hizi sisikii Rostitamu akidai amepewa Powers of Attorney na Dowanis kufanya kila kitu hata kuibia Danganyika. Amenywea baada ya kugundulika. Hata kile kitegemezi cha Mgosi Makambale Machungi ninchosikia eti kinapigiwa debe kututawala miaka 20 ijayo kimenywea!

Kweli walevi wanatukanwa kila matusi ya nguoni. Eti Jannie Makambale anaandaliwa kuwa rais! Mwe! Hii kali! Yaani harufu ya maziwa ya mama yake haijatua eti tuletewe kinyago kingine cha mpapure kama kile cha Mzee Musa kilichoingizwa majaribuni na Dellila Anae Tamaa wa Kishumundu!

Ama kweli Hassan alisema: wadanganyika ni kichwa cha mlevi mwendawazimu kujifunzia kunyoa. Mzee Ali alijua. Maana alifanya kila ufisadi na kuumba huu unaotusumbua bila kushtukiwa. Kwani unadhani NjaaKaya aliumbwa na nani kama si mzee Ali?

Loh! Nshasahau! Lengo la kuandika unabii haikuwa kushughulika na vijifisadi uchwara wala mafisadi wakubwa bali genge liitwalo Chata Cha Mafisadi. Walevi mbona siwasikii mkilishinikiza lijivua gamba kama lilivyowahadaa au ndiyo mmekubali kuliwa kama kawa ingawa huko nyuma hamkuwa hivi?

Niulize swali simpo. Ni fisadi au mafisadi wapi watawatimua mafisadi wenzao? Sitaki mseme nina wivu na rafiki yangu. Rejea ile orodha ya aibu au List of National Shame ya Dk Silaha kule Mchungwa Simba Meteke.

Nimalizie kwa kuuliza swali la kilevi. Sinema ya Loliyondo imekwisha. Je tutegemee ipi ili kuendelea kuwalewesha na kuwadanganya walevi na wadanganyika?

Au ni yale yale ya Zenj ambapo siku hizi baada ya ngunguru kufunga ndoa na ngangaru ni ulaji kama kawa?

Nimalizie na angalizo na kipuuzi. Una habari kuwa yule kijana Mapepe Tunaye anaanza kuishiwa kama Willy Mukami? Naona wameishiwa sera baada ya kujikuta wakichekwa hata na ndege na vyura kwa ujuha wao kudhani wanaweza kutumia Kiama cha Majambazi eti kulipiza kisasi kwa mafisadi wenzao.

Yote kumi. Kile kizee kiitwacho Mgosi Jose Makambale kimeishia wapi? Au kiko na Kimdunge Ngumbaru mwehu ambaye naye ametokomea.

Tokomea Makambale. Tokomea Kimdunge. Tokomea CCM. Tokomea. NjaaKaya. Tokomea tokomea tokomea mshirika wa bed. Stop! Maana nawe mpuuzi juzi ulisema nachelewa kurudi una wasi wasi na dogoz. Kumbaff nyote.

Namuona mkuu wa manjago ananijia, ngoja nichomoke maana mdomo huu sasa utaniponza!
Chanzo:Tanzania Daima Juni 1, 2011.

No comments: