The Chant of Savant

Friday 28 October 2011

Aibu serikali kutolewa vyombo nje


Habari kuwa wizara ya Habari Utamaduni na Vijana na Michezo ilitolewa vyombo vyake hivi karibuni baada ya kutolipa pango la nyumba kwa mwenye nyumba yaani NHC ziligonga vichwa vya habari. Wengi wanajiuliza. Inakuwaje wizara inayopangiwa bajeti kila mwaka kushindwa kulipa pango la nyumba kama hakuna ufisadi? Je pesa inayotengwa kwenye bajeti kwa ajili ya kulipia pango inakwenda wapi na kwa nani? Ajabu utashangaa kusikia kuwa wakubwa wa wizara wanaishi kwenye mahekalu ya serikali ukiachia mbali kuporomosha mahekalu yao binafsi? Je pesa ya pango inaishia kwenye mifuko na miradi ya wakubwa wa wizara?

Tumejuzwa deni la pango. Vipi madeni ya maji, simu umeme na mambo mengine? Maana kwa hali ilivyo, ni kwamba kila mtu anajifanyia atakavyo ilmradi ni wakati wa madili uliopindua maadili. Anayebishia hili ajiulize ni matajiri wangapi anawaowajua tena watu walioanza kazi jana kwa vyeo vya chini lakini wana mimali ya kutisha. Nenda ukachunguze wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere au KIA utajua ninachomaanisha. Usiishie hapo. Nenda bandari, uhamiaji, mita za mafuta, TRA hata mbuga za wanyama utajua nimaanishacho. Ukitoka hapo malizia benki kuu na wizara ya biashara utaona ninachomaanisha. Tunaipeleka wapi nchi? Ajabu hakuna anayejali. Hata wakubwa wanaotuaminisha kuwa wako makini hawastuki wala kushangaa!

Turejee kwenye kashfa hii ya wizara kushindwa kulipa pango la nyumba. Kwa ufupi ni kwamba NHC, Kama Tanesco haipaswi kuwa maskini kama ilivyo. Nani hajui kuwa wapangaji wengi ni watu wa mbari fulani tena wenye uwezo lakini wakilipa kiduchu ukilinganisha na wapangaji wa Kiswahili wanaopanga uswahilini? Ingawa NHC inaitwa Msajili wa Majumba, kimsingi si msajili wa majumba bali msajili wa Wahin… malizia tusijeambiwa tunahubiri ubaguzi. Ajabu ubaguzi kwenye upangaji wa nyumba na umilki wa biashara tena zitokanazo na ufisadi si ubaguzi! Nani hajui kuwa wezi kama akina Chavda na wengine wengi wanaendelea kutanua huku vibaka wakimalizwa kwa moto?

Hii maana yake nini? Serikali inaona uchungu kwa wizara yenye kutumia pesa ya walipa kodi, kutimuliwa kwenye nyumba wakati serikali hiyo haioni uchungu pale makapuku wanaponyanyaswa na kunyonywa na wenye nyumba wanaoweza kujipangia kiasi cha kodi bila kubughudhiwa. Hivi nani hajui kuwa wapangaji wengi mijini wamegeuka watumwa wa wenye nyumba wenye tamaa wanaodai kiremba hadi kodi ya mwaka kwa mtu anayelipwa kwa mwezi? Hii ndiyo maana hatuna uchungu na wizara kutupwa nje ya nyumba. Tungeshauri na Tanesco na DAWASA wawakatie huduma hadi walipe. Maana kwa kuendelea kuwavumilia tunaumiza watu wetu. Kwanini kuwavumilia wakati ni hao hao wakwepa kodi ya pango wanaoingia mikataba ya kipumbavu na wezi kama Dowans na kuishia kugawana mabilioni ya kodi zetu huku tukilazwa kwenye kiza kama mende?

Wenye uchugu na taifa letu wana hasira na kisasi na watendaji wanaotumia mamlaka yao kuzidi kuwaibia maskini kodi zao. Kwanini wizara inapata pesa ya kulipa posho za vigogo wake, pesa ya kupitisha bajeti, kujipongeza hata ya kukirimu wageni lakini wizara hiyo hiyo ikakosa pesa ya kulipa pango la nyumba? kunani hapa? Ingawa Afrika inasifika kwa umaskini na uomba omba wake, ukweli ni kwamba hivi havijaumbwa na Mungu bali ombwe la uongozi na vipaumbele uchwara. Inashangaza nchi inayoweza kutumia mabilioni kwenye jimbo moja la uchaguzi kushindwa kulipa pango la wizara yake na hakuna anayewajibishwa.

Nani hajui kuwa tatizo letu ni kuvipa umuhimu vitu vya hovyo na kuvipuuzia vitu vya muhimu? Hebu angalia tunavyowekeza kwenye siasa badala ya huduma za jamii. Jiulize ni helkopta ngapi zilitumika Igunga lakini kura zikasafirishwa kwa mikokoteni na punda? Je hapa tatizo ni raslimali au busara akili na utashi katika kuweka vipaumbele? Kwanini, kwa mfano, serikali inapata pesa ya kununua mashangingi mawizarani, mikoani na wilayani lakini ikashindwa kulipia pango, umeme, simu, maji na huduma nyingine?

Ajabu nchi isiyo na pesa ya kutosha kulipia pango, inaruhusu majambazi wachache kutorosha madini na wanyama na hakuna anayestuka? Nani hajui kuwa pesa nyingi ya kodi inaishia kwenye mifuko ya watendaji wachache wa umma kama tulivyobainisha kuhusu TRA, viwanja vya ndege, mipakani na kwingineko? Kwani hili halijulikani au kwa vile waajiriwa kwenye maeneo haya ni watoto wa wateule au vibaraka wao wanaokula nao? Nani hajui kuwa wengi wa matajiri kwa mfano wa viwanja vya ndege ni waajiriwa wa serikali na wauza unga? Kwani siri? Ajabu utasikia TAKUKURU ikitoa kila maigizo na kushindwa kuwachunguza watu ambao utajiri wao haulingani na vipato vyao. Lakini TAKUKURU itafanyeje hivyo wakati watendaji wake wengi nao wana mali nyingi zilizopatikana kifisadi sawa na wenzao wanaopaswa kuwachunguza.

Leo askari wa usalama barabarani wamegeuka askari wa balaa barabarani kutokana na kula na wahalifu wanaoendesha magari kinyume cha sheria huku polisi wakila na majambazi, wanasiasa na wafanyabiashara haramu na majambazi wakubwa na wananchi wakiendelea kuwa mashuhuda.

Tumalizie kwa sakata la wizara kufungashiwa virago. Ajabu ni kwamba wakubwa watang’aka na NHC itanywea na wizara kuendelea kufanya vitu vyake. Nani anajali kwenye taifa ambalo halina mwenyewe na kila mtu anatesa kwa zamu. Hivi kweli haya nayo yanahitaji rais kuingilia au wananchi wenyewe wanaweza kufanya hivyo kwa kushinikiza serikali iwajibike vinginevyo waitimue? Hata kama wananchi kwa ujinga, ukondoo na kuishi kwao kwa matumaini ni waathirika, wasipopaza sauti nani atawasaidia badala ya wao kujisaidia wenyewe? Tieni akilini.
Chanzo: Dira Oktoba 2011.

Wednesday 26 October 2011

Al Shabaab War: Did Kenya Count the Cost?


Since its independence, in 1963, Kenya has nary embarked on any war with any country. Now the “Ordnung” or unchallenged order has been broken.

Almost all Eastern Africa countries, except Kenya have had war either with neighbours or within their boundaries. Kenya has however known small scale riots namely, the shifta uprising (1967) and post-elections chaos (2007). The country has been relatively peaceful but the Al-Shabaab incursions are putting this record to test.

Should Kenya ignore all realities and shun taking on Al-Shabaab or let her security hang in the balance? Logically, the choice is obvious. However, before making it, there were some issues that needed analysis and consideration.

First, before going to war with Al-Shabaab, Kenya ought to have secured support from neighbouring African countries. Unfortunately time and circumstances did not allow this. So too, neighbours are duty bound to support Kenya militarily and politically simply because Al-Shabaab’s activities in the region have always affected all countries. Refer to the piracy in the Indian Ocean that has badly affected the economies of the region, the Uganda attack during the World Cup games as well as the Dar es Salaam and Nairobi Al-Qaeda bombings in 1998.

For other African countries to come into the big picture, they must obtain consent from the African Union (AU) which should have declared war against Al-Shabaab. This would avert the danger of other countries blaming Kenya for invading the failed state of Somalia. Countries such as Britain, United States and other that have already been affected by terrorism, must not sit back and watch.

Secondly, Kenya whose shilling is now in a free cascade should have ensured that the war will not damage the shilling further. Remember, Tanzania lost her economic stability in 1978 when it took on Idi Amin. The economy of Tanzania has never recovered even though this is not the only reason for the country’s sick economy and currency.

Kenya’s economy depends heavily on tourism. Therefore, when Kenya is taking on Al-Shabaab for attempting to sabotage and suffocate tourism and security in Kenya, it must have ensured that the war does not stifle tourism.

As for national security, this is sine qua non. Nobody can discuss or put a choice on this. Kenya has to fight to make sure that Kenyans and their visitors are secured so as to enjoy their lives. This, if anything, is non-negotiable.

Kenya is not facing Al-Shabaab only. She has looming wars almost in all her boundaries except the boundary with Tanzania. On the west there is Migingo Island crisis with Uganda while in the north, Ethiopian bandits have always put Kenya on alert. Now that Kenya has decided to take on Al-Shabaab, the message for the rest will be crystal clear: a peaceful country can turn to war if it is forced to do so.

The Al-Shabaab spokesman recently warned that Kenya's beautiful buildings and tourism would be badly affected for engaging Al-Shabaab. Such verbiage must agitate Kenya even more to make sure that Al-Shabaab is exterminated soon. How can Kenya allow Al-Shabaab to keep on spitting on it and get away with it under the strength of issuing threats? Nunca mas, (never again)!

Going to war depends on the seriousness of provocation especially when it has to do with national security; the personal behaviour of a country’s commander in chief and the economy. Nobody wants to go to war games. But if you are forced as it is in this case, you have no choice but to go to war. It is not an easy choice, this is why Kenya is currently vacillating amidst many battles.

Source: The African Executive Magazine October 26, 2011.

Sitta anataka kumdanganya nani?


Hakuna ubishi kuwa Waziri wa Jumuia ya Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo, Samuel Sitta, ni mmojawapo wa wanasiasa wakubwa nchini tena wenye historia ndefu na pana ya taifa letu.

Sitta, ni kati ya wazee walioonekana kama wenye msimamo wa kuleta maendeleo kwa taifa hasa kwa jinsi alivyoendesha Bunge alipochaguliwa kuwa spika wake.

Hakuna kitu kilimpatia sifa na heshima kubwa kama kuridhia kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye ni Naibu Waziri wa Ujenzi.

Maana ni kupitia maamuzi ya Kamati ya Mwakyembe, kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa, waziri mkuu aliweza kulazimishwa kuachia madaraka yake baada ya kubainika kuwa nyuma ya kashfa ya Richmond. Leo hatutaongelea maana ya Richmond maana wengi wanaijua kutokana na kuwa sehemu ya kongwa shingoni mwao.

Tunachoweza kusema ni kwamba tutaongelea kampuni mtoto wa Richmond yaani Dowans ambayo imeshinda tuzo la shilingi 111,0000,0000,0000 ambazo zinapaswa kulipwa na Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) kwa kuvunja mkataba na kampuni hii.

Tuzo hili lililotolewa na mahakama hivi karibuni limeigawa nchi baina ya watu wachache wenye madaraka na wanaodhaniwa kuwa nyuma ya hujuma hii na wengi wasiopenda kusikia neno kulipwa Dowans.

Mmojawapo wa watu wanaotaka Dowans isilipwe ni Sitta. Kupinga pesa ya umma kulipwa kwa mafisadi si jambo baya. Ila kwa mtu wa aina ya Sitta kusema Dowans isilipwe pekee hakutoshi.

Wapo wanaouliza: Yeye kama mwanasheria kitaaluma na waziri kwenye serikali yenye kuonyesha kasi ya ajabu kuilipa Dowans anachukua hatua gani binafsi? Hivi kujiuzulu nako kunahitaji ushauri zaidi ya uzalendo na utayari kuwa serikali husika haifai?

Je, mtu anayekaa ndani ya serikali hiyo hiyo na kuwaaminisha umma kuwa anaichukia si mbaya kuliko hata wale wanaokaa kimya?

Wapo wanaokwenda mbele na kuhoji: kwanini Sitta asijiuzulu toka kwenye serikali inayoonyesha wazi kulalia ufisadi badala ya kukaa humo humo na kupiga mdomo na kulalamika?

Wengi wanashangaa kwanini Sitta hataki kujua kuwa kikwazo cha kila kitu ni bosi na rafiki yake Rais Jakaya Kikwete. Je, Sitta anadhani watanzania wamesahau yeye na Dk. Mwakyembe walipowasaliti kwa kutotoboa ukweli wote kuhusiana na walioko nyuma ya Richmond?

Leo anakuja na maneno kuwa waziri mkuu akijiuzulu serikali yote inaanguka. Kama ni kweli mbona kamati yake na Bunge lake hawakushinikiza serikali ijiuzulu na badala yake walidandia kupewa vyeo vidogo kwenye serikali hiyo hiyo?

Namheshimu sana mzee Sita. Heri ajinyamazie na kuendelea kusutwa na nafsi yake kama ana udhu kiasi hicho au aendelee kutetea mkate kwa kutetea serikali legelege iliyoshikwa na mafisadi.

Katika hali hii you must either be pregnant or not pregnant but not both.

Ajabu Sitta hivi karibuni alikaririwa akisema kuwa hakutegemea Lowassa aachie ngazi na kama angefanya hivyo basi alijua serikali nzima ingeporomoka. Hii maana yake ni kwamba sifa inazopewa Kamati Teule ya Bunge haizistahili ikichukuliwa kuwa haikuwa imedhamiria kumtimua waziri mkuu na kama ingekuwa imedhamiria, alipojiuzulu kwanini kamati haikushinikiza serikali nzima iachie madaraka.

Hili ni swali ambalo Sitta na wenzake litawaandama daima huku nafsi zikiwasuta kuwa walisaliti umma kwa ajili ya vyeo tena vidogo vya muda.

Wanaokumbuka kashfa ya Watergate iliyomuondoa madarakani rais wa Marekani Richard Nixon watakumbuka jinsi mambo yalivyokwisha tofauti na ilivyotegemewa kama ilivyotokea kwa Lowassa.

Je, Lowassa alijiachia madaraka kwa hiari yake kama sehemu ya uwajibikaji? Kama ni hivyo mbona alilalamika baadaye? Kama ni hivyo kwanini aliendelea kutoelezea alichojua kuhusiana na Richmond? Kama ni hivyo kwanini Lowassa hakutaka kuongelea tuhuma mbali mbali za ufisadi hata kabla ya Richmond zinazoendelea kumwandama?

Je, Lowassa alilazimishwa na bosi wake yaani rais Kikwete kuepuka siri zote kumwagwa hadharani? Je, aliachia ngazi kuokoa serikali akitegemea angerudishwa kwa mlango wa nyuma? Je, Lowassa alifanya uamuzi kutokana na hasira au kuogopa hatari ya kuletewa ushahidi zaidi na kuishia kifungoni?

Ingawa Lowassa ana zigo lake la tuhuma, spika aliyeunda tume iliyommaliza Lowassa, Sitta hawezi kuendelea kujionyesha kama mtu mwema wakati anatumikia serikali hiyo hiyo inayonuka.

Hawezi kueleweka kuiambia serikali isiilipe Dowans wakati anaendelea kubaki kwenye serikali ile ile.

Laiti Sitta angekuwa mkweli pamoja na mwenzake Dk. Mwakyembe wangeeleza yaliyofichwa na kamati teule ya Bunge na kuomba msamaha yakaisha. Bila kufanya hivyo nao wataendelea kuwa wanafiki na mfisadi wa kawaida waliohongwa vyeo uchwara kwa kuisaliti nchi.

Tatizo kubwa la wanasiasa wetu wengi ni kudhani kuwa umma hauna akili wala kumbukumbu kujua nani ni nani katika nini.

Mwakyembe na Sitta wamekuwa wakiisakama serikali lakini ajabu hawataki kutoka kwenye serikali hiyo hiyo! Wamekuwa wakitaka waonekane kama wapiganaji dhidi ya ufisadi kwa kuendelea kutumikia serikali wanayoituhumu kuwa fisadi!

Huwezi kusema kuwa serikali ya Kikwete ni ya kifisadi lakini bado ukasema eti Kikwete si fisadi. Ni ajabu hata Kikwete anawavumilia au ni kwa vile wote wanatumiana? Yale yale ya Magomeni! Aliyeuza dhahabu feki kapewa noti feki. Mchezo kwisha!

Je, Sitta anataka kumdanganya nani wakati kila kitu kiko wazi? Heri mzee Sitta angejinyamazia na kuendelea na cheo chake kitokanacho na kazi pevu aliyofanya kuinusuru serikali anayoishambulia kila siku.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 26, 2011.

Badala ya kujivua gamba Ewassa amejivua nguo


INGAWA amejitahidi kula kobisi, kwa wale wenye kufuatilia mambo watakubaliana nami kuwa Eddie Ewassa aliyependa kujionyesha kama kidume kumbe ni mwoga.

Jamaa si alitupata wanywa kahawa lilipopigwa talalila kuwa angefanya kweli na kutoa somo kwa dunia tusijue atageuka mwoga!

Tukiwa hatuna hili wala lile si wambea wakatangaza kuwa Ewassa angeitisha kigwena na kumwaga mtama kwa kuku ili watafune! Usiambiwe! Kila mnywa kahawa na mlevi alijiweka tayari kupokea ufunuo huu wa kumwaga mtama.

Mpayukaji kama ada nilinunua kabrasha kubwa tayari kuchoronga yote ambayo yangenenwa na kigogo huyu.

Wengi tulijiandaa hata kumuuliza maswali mazito juu ya mambo mazito na tuhuma nzito. Wapo waliojiandaa kuzomea zomea huku wengine wakijiandaa kwenda kwake kujipendekeza ili awape mshiko kama ilivyotokea kwa wasomi uchwara hivi karibuni. Jamani kujigonga kwa fisadi ni uchangudoa wa kimaadili hata kama wahusika wanaona ni dili.

Hauchi hauchi kuchile. Kule Richmondoli nyasi zilitandazwa tayari farasi kufungiana nyama na nyangwa. Saa ilipowadia tukamuona jamaa akiingia ukumbini na waramba viatu wake kina EF. Kibondemaji na Kayaanda waliokuwa wakihanikiza kwenye runinga kutukana watu kwa vile eti wanamsakama mungu wao.

Huku viroho vikitweta na kijasho chembamba kikituchuruzika tayari kusikia yasiyosikika jamaa si alianza sanaa .

Hatukuamini masikio yetu kutokana na yale aliyoanza kusema. Ilibidi tuvumilie maana mvumilivu hula mbivu ingawa wakati mwingine aweza kuambulia mbovu kama sisi.

Wajua nini? Badala ya kumwaga mipwenti si alianza kumsifia mshikaji wake wa barabarani wa Chama Cha Mafisadi (CCM), Sio CCM unayoijua, hii ninyine kabisa. Wengi hatukuamini macho na masikio yetu.

Tulizidi kuvumilia tukifiri kuwa yale yalikuwa maroroso na makando kando ya kutuandaa tayari kupokea injili. Hola! Jamaa alizidi kujiweka karibu na mshikaji wake hadi muda ukazidi kuyoyoma huku mie nikitamani niamke nimwulize swali baya.

Jamaa aliendelea kujivua gamba kiana katika kila mstari aliosoma toka kwenye hotuba yake uchwara. Mara aseme, “ sie ni damudamu na hatukukutana baharini wala relini. “Mara wanatuzushia kuwa sisi si wamoja na ulaji wetu si mmoja. Mara namheshimu na kumhusudu Njaa Kaya. Mara hivi mara vile.

Nilitamani nimwambie akajiunge na akina Isha Mashauzi na Hadiji Kopo akaimbe mipasho badala ya kujiita mwanasisasa. Maana maongezi yake haikuwa siasa bali mipasho tena mipasho kwa Nepi Nnaunge.

Wengi walianza kujiuliza nani kamroga huyu. Utadhani alikuwa ameambiana na habithi Kashafi wa Libia aliyekuwa akijidanganya na kuudanganya ulimwengu kuwa walibia walikuwa wakimpenda hadi kumfia asijue wakimpata wanampiga hadi kumdedisha kama ilivyotokea.

Hakuna aliponiacha hoi pale alipojua ukweli mchungu pale walipomtia mbaroni na kuanza kuzoza akiuliza eti alikuwa amewakosea nini NTC asijue walibia walijua kila janja na ukatili wake. In the end walimdedisha kwa kichapo cha mwizi.

Tuendelee na huyu, kusema ukweli hajarogwa. Kama niliyosikia ni kweli basi nasikia anasumbuliwa na Richmonduli.

Wapo wanaosema eti alilaaniwa na mzee Mchonga pale alipomtolea uvivu. Iwe kweli au la mie simo. Tuendelee na stori zake. Kadili alivyozidi kuchafua hewa kwa mipasho uchwara tulizidi kukodoa mimacho huku mshawasha na hamu vikizidi kuongezeka jamaa asiongee hata pwenti moja!

Wenye akili tukajua tumeingizwa mkenge kuletwa kusikiliza rongorongo za mfa maji. Kwa ufupi ni kwamba jamaa tuliyetegemea ima avue gamba au kumkaba mtu shati si aliishia kujivua mwenyewe na kubaki kama alivyozaliwa kiakili!

Tafsiri ya haraka iliyonijia ni kwamba jamaa alikuwa anaandaa mazingira ya kujivua gamba kwa kujionyesha ana heshimu genge lao.

Najua. Siku ya kufanya kweli atasema, “kwa kuheshimu genge na mwenyekiti wake, ingawa sikutenda kosa lolote, nimeamua kujivua gamba ili kuleta mshikamano wa genge.” Wengi wataguna. Jamaa hatajali miguno. Badala yake atabwabwaja sifa za genge lililomlea na kumpa ulaji hadi akawa mkwasi.

Kama haitoshi, wenzake watatuma salamu za pongezi kwa kuonyesha ukomavu wa kisiasa na uzalendo. Ebo, wengi wataguna. Uzalendo gani wa kuleta Richmonduli?

Hata hivyo, radio mbao zimenitonya kuwa alikuwa ana usongo wa kumwaga mtama lakini akiwa amebakiza dakika tano na ushei simu ilipigwa toka Vigogoni kumuonya kuwa akimwaga mtama atashughulikiwa kwa kupelekwa mbele ya pilato.

Nasikia simu ilitoboa wazi kuwa Ewassa anapaswa kujua wazi kuwa ana kigwena ingawa wameamua kumnyamazia. Jamaa kusikia hivi, nasikia alianza kunonihino kwa presha.

Naona gari lile kama la fisadi linakuja, acha niwahi nikalimwagie maji machafu.

See you guys!
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 26, 2011.

Saturday 22 October 2011

Bad start for Libya


Bad start for Libya
Although former Libya strongman Muammar Gaddaffi was almost hated by everybody except those who were closer to him, what the new regime did to display his remains for public to ridicule was unreasonable.

The author personally needs to divulge his interests-in short he did not like Gaddafi not just he hated him because of being a human being but a tyrant. Again, despite author’s freedom to hate or love, he did not like the way Gaddafi’s remains were abusedly maltreated so to speak. Gaddafi is still a human being even posthumously. This is the fact like it or not. Gaddafi, therefore, deserved to be treated humanly just like any other human being. What the new regime did is to punish the corpse whereby the law is clear that once someone is dead, his sins or offences are forgiven. This is why you cannot hear ICC baying for Gaddafi’s blood anymore. Actually there was no logic or necessity to dress down a desperate dead body. Indeed, this is a bad precedent NTC has set for its leaders in the future.

For whoever with rational thinking that saw how Gaddafi’s body and those of his defence minister, Abu Bakr Younus and security advisor who also was his son Muattassim hated the act of displaying the copses for people to photograph and scoff at.

Half naked and bullet ladden, the bodies were displayed for longtime against Islamic practices. Though many Libyans said Gaddafi was not a Muslim thanks to their pent-up anger, he was a human being and the head of the state. This is the fact that no sane person can dispute. Why then did the new regime allow this inhumane treatment to dead bodies? Dead bodies are no flowers or something good to look at given that everybody will die; and nobody knows when and how. Even when Gaddafi took power, abused it and clung to it, he did not know he would end his life the way he did. If he knew, he’d not have behaved the way he did.

Looking at how Gaddafi’s body was ridiculed and abused, reconciliation for Libya will become very difficult if we face it that Gaddafi still has sympathizers especially those that used to benefit from his rule however brutal it was. What adds insult to injury is the fact that even children were brought in the supermarket where the bodies were for long displayed. Indeed, if anything, this is but abusing children and teaching them such bad behaviuor and cruelty.
We all know that Libyans suffered a lot under Gaddafi. It is obvious they had vengeance against Gaddafi. Yet again, one must avoid behaving like a madman so that people onlooking at him should nary fail to notice the difference.
Ironically, most of people forming a transition government, apart from working with Gaddafi before ditching him, are the same people who made Gaddafi a stinking dictator. They don’t ask themselves what would happen to them shall the mass decide to completely scrap Gaddafi’s legacy. This is possible given that Gaddafi’s autocratic rule was defined by many cheerleaders and bootlickers among who are in the current regime.

Friday 21 October 2011

Watawala wetu na ufisadi wa kielimu


Zamani shahada ya heshima haikutolewa hovyo hovyo. Siku hizi, hata hivyo, rais wa nchi anaweza kupewa shahada kama njugu kiasi cha maana ya kusoma na shahada husika kupokea. Ajabu ya maajabu rais anayepewa shahada za heshima hupenda kuitwa daktari utadhani kasomea! Hii matokeo yake ni kuzuka kwa madaktari wa kughushi wengi sawa na waganga wa kienyeji. Tumefikia mahali kuwa na mawaziri walioghushi shahada za udaktari huku rais akiwafumbia macho. Je atawezaje kuwashughulikia iwapo gonjwa lao la kupenda sifa hata wasipostahili ni moja?

Vyuo vyetu vikuu vimeanza kugeuka vyoo vikuu. Maana vinatoa shahada bila kufuata hata vigezo wala utaratibu. Inakuwaje mtu mmoja hata kama ni rais kupewa shahada za juu za heshima karibu kila mwaka na kusiwepo kuvunjwa taratibu? Je ni kwanini vyuo vyetu viko tayari kupinda kanuni na kujishushia heshima kwa kutoa shahada kama njugu.

Hapa Kanada mkuu wa nchi ni Malkia Elizaberth anayewakilishwa na Governor General of Canada. Sikumbuki kusikia au kuona malkia au mwakilishi wake hata waziri mkuu wakigawiwa shahada. Je kwanini watawala wetu wanapenda shahada za dezo?

Watafiti tafitini mjue chanzo cha ugonjwa huu. Je yaweza kutokana na wakuu wengi wa vyuo kuwa marafiki na wateule wa rais au rais anatumia watu wake kulazimisha apewe shahada kama njugu? Hakika huu nao ni ufisadi wa kielimu.

Thursday 20 October 2011

Breaking News Gadaffi ameuawa


Habari zilizorushwa na kituo cha Televisheni cha Al Jazeera zinasema kuwa imla wa zamani wa Libya Muamar Gadaffi ameuawa leo baada ya kustukiwa na wapiganaji wa serikali ya mpito (NTC). Hata hivyo habari za uhakika hazijatolewa na serikali. Hivyo habari zinazozidi kutoka zinachukuliwa kwa umakini mkubwa. Habari za uhakika ni kwamba msemaji wake Musa Ibrahim yumo mbaroni baada ya kuanguka mji wa Sirte ambao ni nyumbani kwa Gadaffi na ngome ya mwisho ya imla huyu.

Wednesday 19 October 2011

Hatimaye Lowassa afikia mwisho


Kwa waliosoma u kusikiliza hotuba ya mbunge wa Monduli na waziri mkuu wa zamani aliyetimuliwa, Edward Lowassa, watakubaliana nasi kuwa sasa amefikia mwisho. Wengi walitegemea Lowassa angekuja na jipya. Ajabu alikuja na mipasho dhidi ya waandishi wa habari na maadui zake wa kutengeneza.
Hakuna kinachochekesha kama Lowassa kujigonga na kujikomba kwa Kikwete akirai na kubembeleza. Anaendelea kushikilia msimamo wake kuwa yeye na Kikwete hawakukutana barabarani.
Kwa ufupi ni kwamba hakuna jipya alilosema Lowassa zaidi ya kuiangukia CCM. Kimsingi, alichofanya ni kuihadaa CCM kuwa yeye ni mtiifu huku akimwaga sifa kwa Kikwete ili abadilishe uamuzi wa kumvua gamba. Hakuongelea ufisadi wala tuhuma yoyote ya kifisadi dhidi yake. Kabla ya kuandaa mkutano huu, wengi tulimuona Lowassa kama jasiri.Lakini baada ya kumalizika mkutano tumemuona kama mwoga wa kawaida. Na hii ni mara ya tatu Lowassa kuonyesha kuwa ni mwoga wa ajabu. Mara ya kwanza aliionyesha mwaka 1995 pale marehemu Mwalimu Julius Nyerere alipomrushia kimondo kuwa amejilimbikizia utajiri usioweza kutolewa maelezo ambao ni matokeo ya rushwa na wizi. Mara ya pili ni mwaka 2008 alipokurupuka na kuachia madaraka ya Uwaziri mkuu ambao anaendelea kuulilia. Na mara ya tatu ni leo tarehe 19 Oktoba 2011. Kama huyu ndiyo Lowassa wa sasa, kwisha kazi. Maana hana ubavu tena zaidi ya kutumia na kutegemea sanaa ku-survive.

Tuesday 18 October 2011

What is Wrong with Mutharika?


When Malawi’s president, Bingu wa Mutharika won elections after a lot of scuffles with his boss former president Bakili Muluzi, many thought: at least fresh air had come to Malawian politics. Those who thought fresh air was coming into Malawi’s political landscape goofed badly. For, before long, Mutharika was at loggerheads with his vice president Dr. Cassim Chilumpha who was his running mate thus automatically Vice President.

After the Mutharika government was sworn in, it did not take long before Mutharika found a hunch to start machinations to get rid of his VP. The situation worsened so much so that Mutharika alleged that Chilumpha attempted to kill and overthrow him. These allegations against Chilumpha sparked off a legal battle that saw Mutharika sacked Chilumpha. However, Mutharika’s tricks did not hold water. Chilumpha went to court in 2006 to seek interpretation of the constitution of Malawi. The court ruled against his firing. The government however refused to re-instate Chilumpha but arrested and charged him for treason.

Chilumpha’s fate was sealed on 28 April 2006 when he was arrested at his home and sent to Lilongwe where he was put in the custody. It was alleged that Chilumpha conspired with another person to have Mutharika assassinated.

Now that Vice President Joyce Banda is doing the same after her boss wanted to flush her out the way he did with her predecessor, what is going in the Malawi power struggles? To begin with, Mutharika sacked his Vice President Banda from the ruling Democratic Progressive Party (DPP) after finding that Banda was a threat to his brother, Peter who Mutharika would have liked to see succeeding him.

Will Mutharika succeed where former president Bakili Muluzi failed? Does Mutharika intend to appoint his wife VP or his brother? This is the question many Malawians are asking after Mutharika appointed his wife minister of Safe Motherhood in a hurriedly cobbled up ministry - a very unique ministry all over the world. Mutharika went ahead and appointed his brother Peter minister for Foreign Affairs.

After finding no hunch to fire his VP, Mutharika is now asking the high court to rule on how the VP can work against her own government and constantly fail to attend cabinet meetings and still be considered a legitimate and continuing vice president.

Malawians are keen to what the High Court will rule as far as this impasse is concerned. The hope of the majority is that the High Court will never allow itself to do Mutharika and his Dynasty’s dirt laundry.

A holder of a PhD in economics, Mutharika ought to know and appreciate rule of law that does not accommodate cronyism, nepotism and nihilism. It does not require one to be an astrophyist or a guru in science to know that Africa is abaft in development just because of being manned by people like Mutharika. One does not need to know Fibonacci sequences, number and rabbits or first second and third newton’s laws of motion to fault Mutharika and the like.

Source: The African Executive Magazine October 18 ,2011.

Huu ni mtihani mzito kwa Rais Kikwete



KADIRI siku zinavyokwenda Watanzania wanangoja kwa shauku kubwa kujua mwisho wa tishio la Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watuhumiwa wake wa ufisadi yaani Andrew Chenge, mbunge wa Bariadi Mashariki, waziri na mwanasheria mkuu wa serikali wa zamani na Edward Lowassa, mbunge wa Moduli na waziri mkuu waliong’olewa madarakani na kashfa ya Richmond.

Kumekuwa na vuta ni kuvute na kurushia vijembe na tambo kwa muda mrefu. Baada ya kujivua gamba kwa mbunge wa zamani wa Igunga na mmojawapo wa watuhumiwa wakuu wa ufisadi Rostam Aziz, wengi walijua Chenge na Lowassa wangefuatia. Lakini wapi! Kimsingi, huu ni mtihani mzito kwa Rais Jakaya Kikwete mwenyekiti wa CCM na CCM yenyewe. Je, nani ataondoka kwenye kitanzi hiki na kicheko ama kilio.

CCM na Kikwete wako kwenye kitanzi ambacho ni Chenge na Lowassa huku Chenge na Lowassa nao wakiwa kwenye kitanzi yaani kujivua gamba. Kitanzi cha Chenge na Lowassa kilifanywa kuwa dhahiri na hatari na uamuzi wa Rostam kujivua gamba.

Hivi karibuni “magamba” haya yalisikika yakikejeli miito ya kuwataka waachia ngazi. Bahati mbaya au nzuri, CCM haikutaka kutoa majibu kwa kejeli hizi. Je, huu ulikuwa mwanzo wa CCM kukubali yaishe iishie kulamba matapishi yake na kuendelea kuonekana kama chama cha mafisadi?

Joto la uchaguzi mdogo wa Igunga lilileta nafuu ya muda kwa CCM hata watuhumiwa. Lakini sasa uchaguzi umebakia kuwa historia. Je, CCM itakuja na kisingizio kipi kuacha kuwachukulia hatua watuhumiwa? Je, CCM na mwenyekiti wake wanaogopa nini? Je, wanaogopa yale aliyosema mwenyekiti wa kamati teule ya Bunge iliyomng’oa Lowassa, Dk. Harrison Mwakyembe kuwa kama wasingeficha baadhi ya mambo serikali yote ya Kikwete ingetimuliwa? Je, umma wa Watanzania utegemee usanii mwingine au ukweli kuwekwa wazi kiasi cha yale yaliyofichwa kufichuliwa na wahusika kuwajibika zaidi?

Huo ni upande mmoja wa habari. Je, kina Mwakyembe na spika aliyesimamia uundwaji wa kamati teule ya Bunge, Samuel Sitta wataendelea kuficha ukweli ili waendelee kufaidi ulaji wa uwaziri waliopewa kama fadhila kwa kuikoa serikali? Je, Watanzania ambao, kimsingi, ndio waathirika wakuu wa kashfa hii kutokana na kuwekwa kwenye kiza miaka nenda rudi huku pesa yao ikiendelea kuchotwa kuwalipa wezi wachache wataendelea kuwa mbuzi wa shughuli? Hakika maswali ni mengi kuliko majibu.

Nadhani huu ni wakati muafaka kuwakumbusha CCM na mafisadi kuwajibika maana hawakulazimishwa kufikia uamuzi wa kuvuana magamba. Kuna haja ya wananchi kushinikiza haki itendeke tena haraka sana iwezekanavyo kabla taifa halijaangamizwa na mdudu huyu mchafu wa tamaa, uongo na woga.

Je, watuhumiwa wataiheshimu CCM na kujivua gamba au kuidharau na kuendelea kupeta? Je, CCM itaendelea kuwagwaya na kuendelea kuonekana kama kikaragosi kinachoweza kutishwa na mafisadi wachache? Je, upinzani ulioibua kashfa hii nao utaendelea kuwa kitanda kimoja na CCM ili kuwaokoa mafisadi wake?

Kinachozidi kuiweka CCM pabaya ni ile hali ya mahakama hivi karibuni kuridhia kampuni yenye utata ya Dowans ambayo ilirithi mkataba tata wa Richmond ilipwe tuzo . Wengi wanashangaa uhalali wa Dowans kulipwa mabilioni ya Watanzania. Pia inashangaza ni kwanini serikali iko tayari kulipa kampuni ambayo ni zao la biashara haramu!

Wanasiasa wana kitu kinaitwa presumption- sina Kiswahili chake ambapo husema kuwa kitu chochote hata ni kizuri namna gani kilichopatikana kutokana na njia au kwa kitu haramu nacho ni haramu. Inashangaza kwanini wanasheria wa serikali hawakutumia presumption hii.

Je, hawakujua au walijua lakini kwa vile walikuwa na masilahi kwenye wizi huu waliamua kuuchuna hata kutoa msaada wa kuepuka hili? Maana tunaambiwa Mwanasheria mkuu wa serikali hakuhangaika hata kuweka pingamizi kwenye shitaka husika.

Kitu kingine kinachoshangaza ni ile hali ya wahusika wa Richmond ambayo kimsingi ndiyo Dowans yaani Rostam, Chenge na Lowassa wanashughulikiwa kisiasa badala ya kisheria.

Hii inajenga hisia kuwa kuna wakubwa serikalini ambao wamo kwenye racket hii bila shaka. Je, hawa ni nani? Je, tutayajuawaje majina ya watu hawa iwapo kina Mwakyembe hawataki kuwataja kwa faida zao?

Ajabu nao wanataka kutuaminisha kuwa wanapingana na ufisadi wakati wanaukingia kifua hadi kuufichia siri!

Wengi wanadhani kuwa hawa walioko nyuma ya pazia mmojawapo ni Kikwete. Maana aliwahi kuwahakikishia wananchi kuwa angetatua tatizo la umeme na alikuwa akifuatilia mazungumzo baina ya Lowassa na Richmond.

Na si hilo tu. Kama hana anavyonufaika, ni kwanini hataki kuwashughulikia watuhumiwa vilivyo? Je, Kikwete ana ubavu wa kuwashughulikia Lowassa na Rostam wakati ndio waliomweka madarakani?

Nani mara hii kasahau kuwa, licha ya Rostam kuwa Richmond na hatimaye Dowans ndiye Kagoda wa EPA? Je, kwa Kikwete aliyenufaika na pesa ya EPA anaweza kumkamata mwezeshaji wake?

Je, anaweza kumshughulikia Lowassa naye akawa salama? Hapa ndipo kitendawili cha nini kitatokea kuhusiana na kitendawili cha kujivua gamba kitakapoteguliwa.

Watanzania wengi wangetaka kujua hatima ya nchi yao. Wanataka kujua kama itaendelea kuwekwa rehani kwenye mifuko na mikono michafu ya mafisadi au kurejeshwa kwao.

Kama watafikiri sawa sawa, kadhia ya Dowans-Richmond inaweza kuwa kitufe cha kufyatua hasira zao na kurejesha taifa lao kutokana na wale waliowaamini kushindwa kutimiza wajibu wao na badala yake kuwa washirika wa uangamizaji wa taifa.

Tukubaliane. Kuna ombwe kubwa la uongozi. Tumekuwa na ombwe kubwa kiasi cha kukosa hata utawala achia mbali uongozi. Maana viongozi walikufa zamani. CCM imeshinda ubunge Igunga. Je, itashinda gamba itakapokaa Dodoma au Dar es Salaam au kwingeneko? Time will surely tell. Tia akilini.

Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 18, 2011.

Tathmini ya Mpayukaji kuhusu uchaguzi

MWENZENU ndiyo nimerejea kutoka Igunguli kwenye kampeni za kamupani za uchafuzi wa uchaguzi. Nilikuwa chama gani zaidi ya UNM yaani Ugali Nyama na Maharagwe usiniulize tafadhali. Je, chama change kimepata kura ngapi? Please don’t ask. If you do I shall commit suttee.

Ingawa nimechelewa kutoa tathmini yangu ya uchaguzi wa Igunguli, bado sijachelewa sana. Hivyo ifuatayo ni taarifa yangu na tathmini ya uchafuzi sorry uchaguzi mzima.

Kwanza, Chama Cha Mafisadi kilitembeza pesa chafu hakuna mfano. Ukiachia mbali kuhonga pesa, Chama Cha Mafisadi (CCM siyo CCM chama tawala), kilihonga ubwabwa, gongo hata fulana na kofia. Mtonyaji wangu amenitonya kuwa chama cha wasanii kilitumia zaidi ya madafu bilioni thelathini katika uchaguzi mdogo hivi! Ajabu hawa wanaotapanya pesa kama hizi, wanaendesha kaya isiyo na hata pesa ya kulipia pango la wizara zake! Hebu niulize kwa herufi kubwa.

Inakuwaje wizara inashindwa kulipia pango lake wakati kila bajeti inatengewa pesa ya kufanya hivyo? Au ni yale yale ya kuchukua pesa ya pango na kwenda kujenga mahekalu binafsi.

Kuna mnywa kahawa alisema kuwa hizo wizara furushwa hazidaiwi pango tu bali bili za maji, umeme hata simu. Ajabu wizara hizo hazikosi pesa ya posho ya wakubwa zake, pesa ya kukirimu wageni, pesa ya kupitisha bajeti, pesa ya kuandaa tafrija za kujipongeza na upuuzi mwingine.

Pili, CCM ilitumia vyombo vya dola kama ndata na Uhasama wa Taifa kuhujumu vyama vingine. Hebu uliza yule mama aliyekamatwa akipanga kuhujumu uchaguzi kwa kutumia madaraka yake hadi akanyofolewa mtandio na kukabidhiwa kwa polisi amefanywa nini zaidi ya kungojea kuteuliwa kuwa mkuu wa nkoa? Je, hapa vyombo vya dola la kaya havijatumika kuwabeba wachovu na mafisi na mafisadi? Ndiyo. Hebu jiulize. Kwenye uchaguzi Fanya Fyoko Ukome wa nini? Kwenye uchaguzi bastola kiunoni za nini?

Hamkusikia wahuni wasio na heshima waitwao waheshimiwa walifikia hata kufyatua risasi? Mwenzenu nina bahati tena ya mtende. Si yale mapumbavu na malimbukeni ya silaha yalirusha risasi utadhani mawe! Kama siyo kutumia mbinu zangu za kikomandoo nilizojifunzia Kyuba nilipoarikwa na kugharimiwa na rafiki na komandoo mwenzangu Fidel Castro ningekuwa al marhum wallahi! Una habari risasi moja ilipitia sikioni kwangu na kuangukia pembeni yangu? Hivyo ndiyo ilivyokuwa niaminini.

Ukiachia mbali uhuni na ushamba wa watu wazima, kulikuwa na sakata la ngono nje nje. Ngono zilipamba moto hadi kada mmoja wa chama hicho hicho cha mafisiduni akamkada mke wa kada mwenzake wakafumaniwa. Nadhani kisa cha yule Mchembe Mwingilu hamjakisahau. Aibu sina mfano.

Hawa kweli wanaweza kupambana na ukimwi wakati wao ni wa kuogopwa kuliko ukimwi wenyewe? Achene kupenda chini hata kama mna madaraka ya juu. Mgoni na mzinzi aliyefumaniwa hapaswi kuendelea kuwa madarakani.

Maana atayabaka na kuyanajisi madaraka haya kama anavyonajisi na kubaka wake za wenzake wenye nafasi za chini akitumia madaraka ya juu. Kweli cha maskini huliwa na tajiri! Walijisemea wahenga. Mie nasema wazi. Ukimmendea mshirika wangu wa bedroom navaa bomu na kukulipua kama al Kaidi.

Ukiachia mbali ngono, udini nao haukubaki nyuma. Bila shaka mnakumbuka wale viherehere mashehena waliojiita mashehe wakati si mashehe walivyotishia kumtoa mtu roho eti mkuu wa wilaya alivuliwa hijab wasijue mwezao si dini yao bali mtawala.

Mnaweza kudhani ninawasingizia au kuwakandia na nina chuki za kidini. Hasha. Wako wapi baada ya kugundua kuwa kumbe waliyekuwa wakimtetea si mwenzao? Si wameishia mitini kwa aibu. Watu wengine bwana kupenda kujikomba na kununua kesi. Nani aliwaambia kuwa yule mama ni wa dini yenu wakati ameolewa na mla kiti moto? Achene kudandia mambo dandieni magari. Hayo!

Yaone yanavyotoa toa mimacho. Tumeishawastukia nanyi ni mafisadi mnaotumia dini sawa na wale wanaotumia siasa. Komeni na mkomae nyang’au wakubwa.

Pia kulikuwa na kampeni za uongo mtupu. Nilimsikia mpuuzi mmoja akipanda jukwaani na kusema eti ameleta maendeleo wakati ameleta maanguko. Jamaa mwenyewe wamjua? Si Tunituni aliyeiba hadi migodi na kuuza nyumba za walevi halafu anasema eti hayo ni maendeleo.

Mwe! Njomba hii hunipati na chikuchapoti kwa hili njomba. Huwezi kuamini, Igunguli iligeuka uwanja wa uongo na upuuzi. Hata lile gamba lililojivua hivi karibuni eti nalo lilikuwa likiwahimiza wananchi walisikilize wakati ni jizi la kawaida! Kaya hii! Kweli imegeuka danguro la kila changu wa kisiasa kufanyia ufuska wake.

Ukiachana na uongo, kulikuwa na mashindano ya vyama kama vitatu kuonyeshana utajiri. Vyama hivyo sitavitaja leo. Huwezi kuamini kuwa vilikuwa vikishindana kutua kwa helkopta huku wanaohutubiwa wakiwa maskini hata wasio na makubazi miguuni!

Nani angeamini kuwa wakati wapiga domo walibebwa kwa mahelkopta, kura zilisafirishwa kwa punda na mikokoteni! Akili au matope? Cha muhimu nini kati ya walaji wachache na wababaishaji kibao na kura zenyewe? Hata hivyo siwalaumu. Kwao kula ni bora kuliko kura na kura ikiwa bora basi iwezeshe wao kula. Hizo ndizo siasa uchwara alizosema Roast Tamu bin Gamba bin Fisadi bin Kagoda al Ajemia.

Lol! Nilitaka kutenda dhambi isiyo na kitubio wala msamaha! Wiki iliyopita nilighairi kwenda Mwitongo kumkumbuka Mchonga baada ya kuona wezi, majambazi, wanafiki na maadui zake wakijaza kule kumsanifu eti wakimuenzi. Tangu lini mbwa akamkumbuka samba? Tangu lini juha akamkumbuka mwenye busara zaidi ya kumkumbuka juha mwenzake?

Akifanya hivyo jua anasanifu kama jamaa zangu waliojazana Mwitongo kumsanifu Mchonga. Hata wale walioghushi shahada eti nao walikuwapo! Kweli simba akifa mzoga wake waweza kuliwa na hata panya.

Nitaendelea na tathmini ya uchafuzi mwaka 2015 baada ya kuwachunguza hawa wanaojipitisha pitisha eti tuwachague wakati hawana maana wala udhu.

Naona kali la Mwiguli linaelekea mtaani kwangu. Acha niwahi nikamfumanie na yule mke wa kada mwenzake. Au naye ana powers of attorney kuwanonihino wake za wenzake?

Imetoka hiyo! Ikirudi? Mtajaza wenyewe.

Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 18, 2011

Monday 17 October 2011

Kumbe wanyama ni bora kuliko watanzania!


Tarehe 5 Oktoba vyombo vya habari vilimkariri waziri wa Waziri wa Maendeleo Mifugo na Uvuvi Matayo David akisema kuwa serikai itawachukulia hatua watakaosafirisha wanyama kikatili. Waziri alibainisha kuwa watakaovunja sheria hii ya ustawi wa wanyama watafungwa mwezi mmoja au kutozwa faini kati ya shilingi 20,000 na 100,000. Hiki si kiasi kidogo kwa mtanzania anayeishi kwa kubangaiza kama vile kuchinja kuku na kusafirisha wanyama wake kwenda sokoni.

Inashangaza kugundua kuwa waziri hajui kuwa baada ya kuua Mamlaka ya Reli, watanzania hawana namna ya kusafirisha mifugo yao zaidi ya kuwaswaga na kuwatembeza makumi ya kilometa. Kama wanafunzi wa vijijini wanajiswaga kwenda kurundikana madarasani kama vifaranga huku wakikalia mawe, itashindikanaje wanyama kuswagwa?

Inasikitisha na kufedhehesha sana. Je wanaosafirisha wanadamu kikatili kama wale waliopoteza maisha kwenye meli ya Islander mbona hawakupata kinga hii? Je ni wangapi wanasafirishwa kikatili kwenye dala dala, mlori, na mabasi ya vijini na serikali inaona na kukaa kimya? Kulikoni kujali wanyama na kupuuzia wanadamu?

Je ni watoto wangapi hawana mahali pa kuchezea kutokana na sehemu za wazi kuvamiwa na wezi wachache wenye pesa na ushawishi na serikali ikikaa kimya kwa miongo mingi? Je hawa hawafanyiwi ukatili? Je ni sehemu ngapi za beaches pwani zimevamiwa na vibaka wajiitao wawekezaji na kuzizungushia seng’enge wakiwaacha watanzania wakitamani kwenda kuogelea? Rejea mauji ya Kigamboni ya kijana wa kitanzania yaliyofanywa na mwekezaji uchwara wa kihindi hivi karibuni. Je ni kwanini serikali inaona mateso ya wanyama na kutoona ya watanzania? Je ni watanzania wangapi wanababanishwa kwenye magereza na kutunzwa kikatili wakati serikali ikiangalia?

Japo wanyama wanahitaji kuonewa huruma iwapo wananchi wa kawaida hawaonewi huruma? Nani hajui kuwa watanzania kwa sasa wanaishi kizani kama wadudu huku serikali hiyo hiyo inayohusika na kiza hiki ikiendelea kujifanya kama aihusiki na jinai hii! Kama serikali aihusiki inakuwaje inawavumilia watendaji wabovu kama mawaziri husika wa wizara ya Nishati na Madini au wale wa Wanyama na Utalii?

Ni jambo na kusikitisha na kushangaza kwa serikali inayoruhusu kutoroshwa kwa wanyama wa mamilioni kujifanya inajali wanyama wa kufugwa. Ingawa lengo letu hapa si kutetea ukatili wa wanyama, ila ukiangalia kiwango kikubwa cha utesaji wa wanyama kilichofumbiwa na macho wakati wa kuwatorosha, unashangaa hii huruma, kama kweli ipo, inaanzia wapi na itaishia wapi? Je kuna wafadhili waliolalamikia hili au wanaotaka kutoa pesa kwa serikali hivyo inajenga mazingira ya kujipatia pesa kwa kujifanya inawajali wanyama? Huwezi kuwajali wanyama kabla ya kuwajali watu. Hivi wagonjwa wanolazwa watatu kitanda kimoja au wanafunzi wanaokalia mawe au kwenye sakafu hawafanyiwi ukatili hasa ikizingatiwa kuwa nchi yetu imejaliwa utajiri wa kumwaga ingawa tunautapanya kutokana na upogo na uroho wa watu wachache?

Safu hii huwa haina muda wa kumtetea mtu au kikundi cha watu zaidi ya kumwanga ukweli kama ulivyo hata kama unauma ili wahusika waelewe na kuchukua hatua. Hivyo, tuseme wazi. Badala ya serikali kuja na mipango ya alinacha ya kuwajali wanyama ianze kuwajali wanadamu ambao wamepewa umilki juu ya wanyama.

Waziri Matayo aabiwe bila woga kuwa kipaumbele chake hakina maana iwapo waziri huyo huyo anashindwa hata kuwashauri mawaziri wenzake wanaohusika na utalii kuacha ukatili wa wanyama na wanadamu. Maana unapowatorosha wanyama bila kupitia mikondo ya kisheria, licha ya kuwahujumu watanzania, unawaongezea umaskini ambao mwisho wake ni ukatili kutokana kushinda wakihangaishwa na maisha wasipopaswa kufanya hivyo.

Serikali yetu ni ya ajabu wakati mwingine. Hebu tutoke nje ya mada kidogo. Nani amesahau ilivyoweza kuandaa uchaguzi mdogo wa Igunga kwa kuweza kusafirisha wapiga kampeni kwa helkopta huku kura zikisafirishwa kwa punda na baiskeli. Hii kweli ni akili? Nani hajui kuwa kuna vyama vimetumia mabilioni ya shilingi yakatwayo kwenye kodi za wananchi maskini kwenda kuwapigia kelele na wengine kuzini na wake zao? Nani hajui kuwa pesa nyingi imetumika kuwarubuni wananchi ili mtu wa chama apite na chama kiendelee kuzoa ruzuku huku wananchi wakiendelea kusota? Je hawa na wanyama ni wapi wanapaswa kuonewa huruma kwanza?

Hivi nani hajui kuwa wananchi wa Igunga wametapeliwa mchana kweupe? Kwanini wasitapeliwe iwapo tunaambiwa waliojiandikisha kupita kura walikuwa zaidi ya 150,000 lakini walipiga kura ni theluthi moja, kwanini? Je waligundua baadaye kuwa ulikuwa ni upotezaji wa muda kwenda kupiga kura wakati maisha yao hayabadiliki kama ya wanyama? Imebidi tuunganishe kisa hiki na hiki cha wanyama kuonyesha jinsi vipaumbele vya serikali yetu vilivyo vya hovyo.

Leo waziri anapata jeuri ya kutangaza hadharani kuwa atakayewatesa wanyama atatoza faini au kufungwa huku waziri huyo huyo akishuhudia wamachinga wakiteswa na wezi wa baadhi ya halmashauri za miji. Waziri huyo anajua fika kuwa wakati wamachinga wapiga kura wakinyanyaswa, kuna wamachinga toka ima India au China wamejaa kwenye miji yetu wakilindwa na serikali hiyo hiyo inayovunja sheria kuwaruhusu wafanya umachinga wakati sheria hairuhusu. Je haya hayafanyiki? Kama ni kutimiza wajibu na kutekeleza sheria basi serikali ifanye hivyo bila kubagua wala kuendekeza pale kwenye maslahi yake tu. Hii nchi ni ya wananchi wote hata kama hawana sauti wala mamlaka zenye uzalendo za kuwatetea. Ni aibu kufikiri kulinda haki za wanyama kabla ya kuanza kulinda za wanadamu.

Chanzo: Dira Oktoba 17, 2011

Saturday 15 October 2011

Tanzania inapoathimisha zoezi la kunawa mikono bila maji!

Salma Kikwete akiongoza watanzania kunawa mikono kwa maji yasiyokuwepo!

Tumeona picha nyingi zikiwaonyesha watanzania wakiadhimisha siku ya kunawa mikono duniani. Ni jambo bora kiafya kunawa mikono kila wakati. Je watanzania wangapi wananawa mikono kila mahali wakati maji ni tatizo?

Bahati mbaya sana, nchi zetu huwa zinadandia kila jambo bila hata kutafakari. Huwezi kuadhimisha siku ya kunawa mikono kwa kunawa maji yasiyokuwepo. Mie nadhani maadhimisho haya yangeelekezwa kutoa maji kwa watanzania wote. Hivi jijini Dar es salaam, kwa mfano,ambalo ndilo uso wa nchi ni wangapi wana maji ya uhakika? Ni ajabu kwa nchi inayoruhusu hata watu kufungua biashara bila kuwa na vyoo kuwa na jeuri ya kusherehekea siku ya kunawa mikono.
Kuna haja ya kuelekeza vipaumbele vyetu kwenye matatizo ya kweli badala ya kuwa wadandizi wa kila kitu hata kile kinachotusuta.

Mpayukaji apewa ‘Power of Attorney’ kuibia taifa

BAADA ya wakubwa fulani kuingizwa mkenge na Mpayukaji na kuunda kampuni ya ujambazi ya Richmonduli iliyobadilisha jina na kujiita Downs, anazidi kufanya vitu vyake kama hana akili nzuri!

Msichanganye na TRA tuliyoongelea wiki iliyopita ambapo tulikuwa tukisaidia wafanyabiashara maarufu kukwepa kodi na kugeuka matajiri wa kutupwa kiasi cha kuwa na ushawishi juu ya nani awatawale walevi.

Ili kufanikisha azma ya kuliibia taifa kiulani, mimi na washirika wangu wenye madaraka ambao ni top secret, tutanzisha miradi ya kijambazi mmojawapo ukiwa ni kusambaza kiza nchini. Tutafanikiwa sana hasa kwa kusingizia ukame ingawa ukame wenye haukuwa wa mvua bali uadilifu na akili. Mradi huu tutaupa jina la Downs. Hii ni baada ya wanoko fulani kustukia jina la kwanza la Richmonduli. Ili kufanikisha ujambazi wetu, tuna mpango wa kujipa tenda ya kusambaza zana zote za kuzalisha kiza nchi nzima.

Na kwa kutumia kampuni yangu ya TRA, tutahakikisha tunakwepa kodi. Ili kuhakikisha hili halikwami, tutaagiza mitambo mikangafu toka kwa Joji Kichaka ili itusaidie kufua kiza ambacho kitaenezwa nchini mapema zaidi. Ili kuhakikisha mambo yanakwenda tulivyopanga, tutaipa sirikali shea kwenye kampuni yetu hewa ili kuwafumba macho walevi wapendwa wa Danganyika.

Ili kufanikisha hili, tutasema kuwa taifa linahitaji kiza cha dharura hivyo kila kitakachofanyika kitafanyika kwa dharura. Hii itatusaidia kukwepa vyombo vingine vya dola kama Bunge, tume za manunuzi na vingine kupata muda wa kuchunguza na kupitia michanganuo yetu. Maana bila ya taifa kuwa kizani, wananchi watapata shida ya kukosa usingizi au kulala kwa taabu. Hatutaki wananchi wetu wateseke wakati tuna uwezo wa kutengeneza kiza hata mvua hapo baadaye.

Tunajua katika kufanya vitu vyetu, kuna vyombo vya dola ambavyo havitaridhika kutokana na kutokuwemo kwenye ulaji huu. Hivyo, hima vitapiga kelele kupinga mradi wetu au vitatia veto. Katika kukwepa hili au kulitumia kwa faida, tumeajiri wanasheria mahiri kuandika mikataba ambayo inatupa nguvu kubwa kuliko asasi nyingine za umma. Hivyo kwa kutumia uchochoro huu, tutahakikisha kuwa kama mashirika mengine ya serikali au vyombo vyake vitapinga au kutusimamisha kusambaza kiza, tunakwenda mahakamani na kushinda mabilioni.

Pia tuna mkakati wa kwenda banki kubwa kuchukua mikopo ya mabilioni ambayo yatalipwa na serikali kwa vile ndiyo itakayotudhamini mikopo hii. Hii inatokana nasi kutokuwa na mtaji zaidi ya akili na hila zetu na usuhuba na wenye maulaji kama vile waziri mkubwa. Ambaye tutamwita Eddie Ewassa Ngoyali.

Ili kuhakikisha hatustukiwi, mmoja wetu ataachana na siasa ili kuanzisha mjadala kumhusu huku mambo yetu yakienda bambam.

Hapa tutahakikisha tunawahadaa walevi kuwa nimeacha siasa uchwara kwenda kushughulikia madili yangu. Wao wasivyo na akili waliponiona Igunguli nikitwanga kampeni ya uchafuzi wala walishindwa hata kunizomea!

Kweli walevi ndiyo waliwao! Yaani hawakuwa na hata ubavu wa kuniuliza ni kwanini nilikuwa nikishiriki kwenye kutafuta mrithi wangu kwenye siasa uchwara kama kweli ni uchwara! Laiti wangeniuliza swali hili ningeumbuka hakuna mfano.

Hakika nawasikitikia walevi kila uchao ingawa sina huruma nao. Yaani wanachagua mtu kula na kuwala tena kwa kuhongwa upuuzi kama ubwabwa bado wanashangilia! Hivi nani aliwaroga viumbe hawa wasiotaka kujifunza kukubali ukweli? Tangu lini mtu anayewakilisha tumbo lake akawawakilisha wenye njaa wakati kuna matajiri wa kujaza tumbo lake kama nilivyofanya mimi?

Siku hizi uwakilishi na uishiwa ni madili mtindo mmoja. Mnakodishiwa madege na makampuni ya madini na kwenda kuhomola mkirudi mnawaweka sawa waliwa.

Mnasaini mikataba uchwara na hatari halafu mnahomola kama tutakavyohomola kwenye Richmonduli baba Downs. Upo hapo mshirika? Nani wa kunizuia iwapo nina Powers of Attorneys and attorneys, judges and whatnot? I have tweaked my strategies. I am using the court of law to steal from wajinga. Woooii! Nimesahau na kumwaga umombo nisijue kuwa nilishahama uingerezani na kurudi ulevini Danganyika Danganyatoto Bongolalalaland ya Mafisi na Mafisadi.

Nashukuru Mungu imelipa huku ikila kwao. Si juzi pilato alitoa tuzo la vijisenti kwa mradi wetu wa kiza tuliouanzishia kule Monduli tukauita Rich-Monduli. Mungu anipe nini sorry Mungu atupe nini? Maana nikisema Mungu anipe nini wenzangu wa nyuma ya pazia ambao ni mabosi na waajiri wangu wanaweza kudhani nina mpango wa kuwaacha Solemba. Msihofu wakuu mie ni wenu na bila nyinyi si ningenonihino kwenye debe kule rupango.

Kwa taarifa ya wanoko wote popote mlipo, huu ni mwanzo. Baada ya jaribio letu kufanikiwa na kukwanyua mabilioni, kaeni mkao wa kuliwa. Mtaliwa wote bila kujali mkubwa au mdogo mwanamke au mwanamme na mengineyo. Tutahakikisha tunaingia kwenye orodha ya akina Warren Buffet na Bill Gates kupitia migongoni mwenu. Mbuga za wanyama na wanyama tele, madini, mabenki na madili vipo kwa sana. Mungu atupe nini zaidi ya wadanganyika na walevi?

Acha niwahi nikagawane mabilioni na Ewassa na tukapange jinsi ya kukwanyua mengine.

Are you there guys?

Washirika na wawezeshaji wengine ambao bado wako kwenye powa siwataji.

Imetoka hiyo!

Jamani, leo tusameheane. Nawahi kwenda zangu San Fransisco kwenye mazishi ya genius mwenzangu Steve Jobs muasisi wa Kampuni ya Apple ambayo huwa naihusudu. Pia jamaa huyu naye alikuwa mlevi mwenzetu.

Chanzo: Tanzania Daima.

Thursday 13 October 2011

KUMBUKUMBU MAALUM YA MWALIMU NYERERE


Mwalimu Nyerere sikia

Mpendwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere baba wa taifa letu,

Naadika ujumbe huu kwako maalum nikiamini kuwa utausoma na kuwasomea mashujaa wenzako kama vile Edward Sokoine, Horace Kolimba, Jenerali Imran Kombe na wahanga wengine waliouawa na watu wachafu wenye chuki na yale yote uliyopigania, kusimamia na kutekeleza.

Mwalimu,
Leo ni siku maalumu kwa wapenda haki nchini na duniani. Kwani ndiyo tunaadhimisha miaka 12 ya kifo chako. Ingawa kimwili hatuko nawe, kiroho tuko nawe. Ingawa miaka 12 inaweza kuonekana mingi. Sisi wapenzi wako tunaona ni kama jana ukiachia mbali mateso kutufanya tuone kama ni karne moja imepita baada ya kurudishwa nyuma kwa mamilioni ya miaka. Najua mwalimu kuna mengi yametokea ambayo huyajui. Yapo ya kuudhi na kufurahisha.

Cha mno ni kwamba kile Chama chako ulichokiasisi na kukifanya kiwe kipenzi cha watanzania ni kama kiko ICU kikipumlia mashine tayari kwa kukata roho wakati wowote. Hakipendwi tena wala kuheshimika. Kila mtu anajisemea na kujifanyia atakavyo kana kwamba hakuna mwenye nyumba. Wale mafisi wenye uchu wa pesa uliokuwa ukipigana nao vita sasa wameshika kani kama alivyowahi kuseme Profesa Issa Shivji. Wezi siku hizi wanaitwa wafanyabiashara maarufu huku mafisadi wakiitwa magamba ya nyoka. Ni juzi juzi kimetoka kwenye uchaguzi na ushindi wa aibu. Hakiitwi cha mapinduzi bali majina mengi ya ajabu ajabu. Mara wakiite chama cha magamba, maangamizi, mafisadi, wauzauza na mengine mengi.

Mwalimu, katika hili la magamba, hata yule jamaa uliyemtolea uvivu kuwa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi za wizi yumo. Kwa sasa yumo msambweni kuvuliwa kama gamba ingawa anasitasita. Hayuko peke yake. Wapo wengine kama vile Andrew Chenge na Rostam Aziz ambaye amejivua gamba siku za hivi karibuni ingawa kwenye ulaji hajavuliwa. Umma unatamani ungekuwepo uwatimue kama mbwa au kuwapa vipande vyao kama ulivyowahi kumpa jamaa mmoja uliyemuita mhuni. Maana hali ilivyo ni kwamba kuna watu wanasitasita sijui kwa kuwaogopa wasitaje uchafu wao. Sijui ni kwanini, ambao wanamwambia leo toka na kesho wananywea kama hamna namna nyuma ya pazia?

Mwalimu, unakumbuka? Siku hizi uadilifu na maadili ulivyokuwa ukipigania na kusisitiza hakuna. Kuna ubadhilifu badala ya uadilifu na madili badala ya maadili. Mambo yamezidi kuchacha. Nakumbuka mpendwa mkeo mama Maria hakuwa na shea kwenye uongozi wako. Siku hizi ni tofauti. Kijana wako Yoweri Museveni siyo yule mwanampinduzi wa zamani. Ni king’ang’anizi na dhalimu hakuna. Una habari yeye na rais wa Malawi Bingu wa Mutharika wameishawateua wake zao kuwa mawaziri? Najua hutaamini lakini hivyo ndivyo hali ilivyo.

Mwalimu,
Nakumbuka mkeo hakuwa na ASIZE. Usiniulize Asize na ugonjwa au mnyama gani. Ni vifaa fulani watumiavyo wake za wakubwa kukusanyia pesa na kuchuma utajiri kupitia migogoni mwa madaraka ya waume zao. Una habari mwalimu? Siku hizi yale madini uliyokuwa umekatalia kuchimbwa yamegeuka balaa badala ya Baraka. Watu walioko kando kando yake wamegeuka watumwa na wageni katika nchi yao. Wanazuiliwa kupita karibu na machimbo ili wasiibe madini na wakipita wanapiga risasi. Mazingira ndiyo usiseme. Mito imechafuliwa na mashimo makubwa yamechimbwa kiasi cha huko tuendako kuwa jangwa kama hali haitabadilika. Nani aibadilishe?

Mwalimu,
Kile chama alichoanzisha Gavana wako wa benki kuu Mzee Edwin Mtei kiitwacho CHADEMA kama ulivyokitabiri kinaanza kuonyesha makali kiasi cha kukubalika nchini hakuna mfano. Kimeishafichua ufisadi ambao ulifikia mahali pa kutishia kuiangusha serikali hadi waziri mkuu Edward Lowassa akatimuliwa. Najua mwalimu unamkumbuka mtu huyu ambaye ulimsemea mbaya alipokuja Msasani kutaka Baraka zako ili agombee urais. Ulisema wazi kuwa wengine wananuka na wamejilimbikizia mali za wizi. Rafiki yako Lowassa alitimuliwa na kashfa iliyoiacha nchi kizani huku ikipoteza mabilioni ya shilingi. Mpaka ninavyoandika, kampuni hii iliyojivua gamba na kuvaa jingine kwa kujiita Dowans inakaribia kufilisi nchi yako. Maana mahakama juzi iliipa tuzo la kusababisha kiza la shilingi 111,000,000,000.

Kitu kingine mwalimu, mambo yamebadilika sana. Serikali imefilisika huku watu binafsi wakitajirika. Unaweza kuamini kuwa kuna wizara zimeishafungashiwa virago na kutupiwa vitu nje kwa kushindwa kulipa pango la nyumba zile ulizotaifa? Hizi ni zile zilizonusurika kuuzwa na kijana wako Ben ambaye baada ya wewe kufa aligeuka na kuwa kituko cha mwaka. Huwezi kuamini kuwa alipokuwa akiondoka madarakani alifikia hatua hata ya kujiuzia mgodi huku akigeuza ikulu yako pango la wezi na wanyang’anyi. Siku hizi yupo yupo tu na haonekani kutokana na watu kutokuwa na hamu naye.

Mwalimu,
Itakuwa ni utovu wa nidhamu kumaliza waraka huu bila kukupa habari mbaya za kifo cha swahiba yako Simba wa vita. Alikuwa miaka miwili iliyopita akiwa amesononeka kutokana na kuona machukizo yakifanyika mbele za macho yake. Halafu mwalimu, unamkumbuka yule tapeli mmoja wa Magomeni karibu na nyumba yako ya zamani aliyejiita mtabiri? Jamaa aliharibikiwa akaanza kutabiri maafa hatimaye yakamkumba yeye. Ajabu alipokuwa akitabiri upuuzi wake hakuna aliyekuwa tayari kumkabili na kumnyamazisha. Kitu kingine mwalimu, siku hizi biashara ya uga imekuwa kero kwa taifa. Huwezi kuamini kuwa kuna hata viongozi wa kidini na wa kiserikali wanafanya biashara hiyo. Haya si maneno yangu. Ni maneno ya rais Jakaya Kikwete. Nadhani mwalimu unamkumbuka. Ni yule kijana uliyemwambia mwaka 1995 kuwa asubiri akomae aongeze nchi. Kwa sasa ndiye rais.

Mwalimu nadhani unamkumbuka kijana wako Samuel Sitta. Miaka michache alichaguliwa kuwa spika wa bunge na kufanya mapinduzi yaliyosababisha Lowassa auteme uwaziri mkuu baada ya kuteuliwa huku kukiwa na shinikizo la kutaka rais asimteua kwa vile ulivyomuacha unajua na wananchi wanakumbuka. Hakudumu. Uliyosema hayakukawia. Yalijitokeza na jamaa akajikuta anatupwa nje kwa aibu huku mkewe akiangusha chozi kama kichanga. Hayo tuyaache mwalimu.

Mwalimu kuna mengi ya kukwambia ila nafasi haitoshi. Nimalizie kwa kukutaarifu kuwa siku hizi uongozi haupatikani kwa ambaye hana pesa wala jina kubwa au kuwa mtoto wa wakubwa. Hiyo ndiyo hali tuliyo nayo watu wako tunaoendelea kukumbuka na kuteseka hasa kwenye kiza na ufisadi.

Naomba nimalizie hapa kwa kukutakia mapumziko mema ya milele.

Chanzo:Dira Oktoba 13, 2011.

Mnywa gongo amkumbuka Mwalimu

Siku ya leo, walevi wote wamkumbuka shujaa wao

Wamkumbuka shujaa wao mwalimu Nyerere

Wanalia na kusononeka kwa kumkosa mtetezi wao

Hasa wakati huu ambapo mafisi na ngedere

Wameamua kuuza na kurarua utu wao

Rudia mara mbili kabla ya kupiga funda tatu za gongo

Pamoja na jeuri yangu ya kunywa gongo na ubishi wa kisomi kutokana na usomi wangu kuhusiana na haya mazabe yanayoendelea, bado namhusudu marehemu mzee Mwalimu Juliyas Mchonga Kambarage Mussa Nyerere kwa jeuri, utaua na uadilifu wake. Hakuwa fisi wala fisadi. Hakuwa kihiyo wala bwege. Jamaa alikuwa amepiga vitabu hadi kunyakua Masters yake. Kwa sisi wenye Masters na PhD tunajua ugumu wa kupata vifaa hivi. Wengi wanaviogopa hasa kama akili hazichemki kama zangu na Mzee Mchonga. Mwalimu hakuwahi kutumia shahada ya heshima hata siku moja ingawa alikuwa nazo utitiri acha hawa wenye kimoja pale na kingine pale tena vya kulazimisha. Ndiyo maana pamoja na usomi wake hakufa na cheo cha dhuluma cha kujiita Daktari wakati udaktari wenye ni wa heshima. Mwalimu hakupenda makuu wala kupenda kupewa shahada hata na vyuo ambavyo havina sifa kama wale wengine muwajuwao wapendao kuitwa madaktari wakati hawataki kwenda shule wala kufikiri kisomi.

Juzi nilikuwa nikisikiliza hotuba yake ya Mei 1995 kule Mbeya alipotabiri kuwa uongozi wa Bongo utakuja kugeuka biashara, ujambazi na kila aina ya jinai, niliridhika kuwa kumbe hotuba zake bado ni bora na zenye mantiki kuliko za walio hai. Kwa hiyo hapa nikiongelea usomi wa Mwalilmu hata kama mimi ni mnywa gongo na mvuta bangi, tunaelewana. Hebu ukitaka kujua ninachomaanisha, chukua hotuba moja ya Mwalimu uichambue ki maana na maanawia halafu ulinganishe mihotuba mirefu ya wengine utajua ninachomaanisha vilivyo.

Leo nani ana ubavu wa kuwafokea wezi achia mbali kuwatimua badala ya kula nao? Leo nani anaweza kupata madaraka bila kuhonga, kuiba kura, kudhaminiwa na fedha chafu na upuuzi mwingine? Mwalimu aliweza kuyaepuka na kuyatabiri haya pale aliposema kuwa Ikulu si sehemu ya kufanyia biashara ya njugu, ubwabwa, bwimbwi wala sanaa.

Ukiachia mbali usomi, kuona mbali, uadilifu na ushujaa, Mchonga alijenga nchi wengine wakabomoa. Wangeshindwaje kuibomoa wakati hawana uchungu nayo? Kujenga nchi kunahitaji moyo na kuibomoa kunahitaji uchoyo na upgo. Hii ndiyo tofauti ya Mwalimu na wahujumu wa kazi zake. Alilinda raslimali za umma mafisi wakatapanya. Wengi wa mafisi na mafisadi unaowaona wakiibukia ni matunda ya fikra na sera za mwalimu hata kama ni wezi wa fadhila. Wengi baba zao hawakuwa na uwezo hata wa kuwapeleka hata mama zao kujifungua hospitali hao wezi wao. Ndipo mwalimu akaleta huduma za bure za jamii. Baada ya kuanza kutembea akawapeleka shule bure wengine wakasoma hadi kupata PhD wanazotumia kuibia umma. Wakati wa mwalimu hapakuwa na mawaziri wa kughushi shahada kama ilivyowahi kutokea huko nyuma. Hapa kinachotukera hasa sisi wanywa gongo ni kuona jinsi vitegemezi vyetu vinaposumbuliwa na kunyimwa au kupewa mikopo wakati wanaofanya hivyo walisoma bure. Huu nao ni ufisadi na ujambazi wa aina yake. Kwanini, k ama kulipia elimu ni mali, wao wasilipe pesa iliyotumika kuwasomesha?

Mwalimu alikuwa kiboko. Hakujilimbikizia wala kuabudia mali kama jamaa zangu magamba. Hakuwa mpuuzi wala msanii bali mtoboa siri kama mimi. Mna habari kuwa ingawa mwalimu hakuwa mlevi wa gongo alilewa utu? Mna habari mimi nimechukua tabia zake kuliko hata watoto wake? Naona niishie hapa msije kuanza kumpakazia kuwa alizaa mwanaharamu nje ya ndoa ambaye ni mimi kama yule jamaa chovya chovya mwenye watoto wa kuokota hapa na pale mia kidogo. Hayo tuyaache.

Leo ni siku maalum ya kumuenzi nguli mwalimu Kambarage Burito baba wa Tanzania. Hivyo nitaongea kilevi lakini kwa heshima na taadhima vya namna yake kwa ajili ya heshima ya nguli huyu.ninapoandika wanywa gongo pale Uwanja wa Fisi walishajiandaa kukaa kimya kwa dakika kumi kabla ya kunywa gongo ili kumkumbuka Mwalimu wa walimu.

Tunajua mwalimu alipotutoka hakuacha baadhi ya misamiati kama vile mafisi, magamba hata wasanii. Hivyo tunachukua fursa hii kumuomba na kumshukuru Mwenyezi Mungu amuweke mahali pema peponi kwani alimpenda zaidi kwa kumchukua kabla ya kushuhudia kufuru na uchafu ambavyo kama angeviona huenda angejitoa roho kama siyo kuzimia.

Kwa namna ya pekee, juzi walevi wa Buzwagi, Mara, Shinyanga na kwingineko ambako mbwa mwitu wameshambulia walituomba tushirikiane kumkumbuka na kumuombea nguli huyu wa uadilifu na baba wa ujamaa. Kweli mwalimu alikuwa baba wa ubinadamu na adui mkubwa wa ufisi na ufisadi. Hakutufanyia biashara wala kutuchuuza kama ilivyokuja kutokea. Pamoja na mapungufu yake, leo ukitamka jina Mwalimu kila mmoja anatia akilini hata sisi wanywa gongo na wavuta bangi. Jina la Mwalimu ni machukizo na tishio kwa vibaka wakubwa wakubwa na wale wote wanaokula bila kunawa kwa miguu na mikono huku wakivuna pale ambako hawakupanda.

Manadhani Mwalimu angekuwa hai hawa majambazi kama hawa wanaotaka kulipwa mabilioni kwa kusambaza kiza wangefurukuta? Hakuwa na mchezo wala kuchekacheka mbele ya maafa. Kweli paka akiondoka panya hujitawala. Shujaa Mwalimu ameondoka, mafisi, mafisadi, mapapa, vinyamkera na kila kinyama cha kizani vinatuchezea mahepe. Hata hivyo kuna siku yao isojina vitalia na kusaga meno.

Natamani niandike hadi kesho. Acha niende kwa Mama Betty nimlilie Mwalimu wetu hata kama ni kwa kupiga funda moja. Mwalimu we shall miss you greatly even though those hyenas you left behind have tried unsuccessfully to founder your name.

Chanzo: Dira Oktoba 13, 2011.

Sunday 9 October 2011

Kikwete kweli kiboko!


Wachambuzi hata wanasiasa wamekuwa wakimshauri rais Jakaya Kikwete kufanya maamuzi magumu ili kuondokana na ulegelege unaoikabili serikali yake na chama chake. Wengi wameandika na kunakiriwa wakifanya hivyo. Kwa kumbukumbu ni kwamba walioanzisha msamiati wa maamuzi magumu ni Mwalimu Nyerere Foundation (MNF) pale walipoona mambo yakwenda siyo. Hawa si wengine bali mzee Joseph Butiku na hatimaye waziri mkuu mstaafu Jaji Joseph Walioba. Wazee hawa hawakutaka kuwa mashahidi wakati mambo yakiharibika ima kwa kuendekeza woga ua takrima na fadhila kama wazee wengine walivyoonyesha. Hawakukubali kuendeshwa na matumbo yao bali vichwa.

Wazee hawa walipomtaka Kikwete afanye maamuzi magumu hasa kuwashughulikia wenzake wanaotuhumiwa ufisadi walisakamwa. Bahati mbaya wazee hawa walipotoa rai hii walizomewa hata na wazee wenzao chamani hasa wale wanaoshabikia mfumo uliopo kutokana na kunufaika nao. Mmojawapo wa aliyewashambuliwa wazee hawa wenye busara ni mzee Peter Kisumu ukiachia mbali waramba viatu wengine wasio na majina.

Hivi karibuni mmojawapo wa wale waliokuwa wakiwakejeli hawa wazee, waziri mkuu aliyetimuliwa na kashfa ya Richmond na swahiba mkuu na mshirika wa Kikwete, Edward Lowassa alibadili mwelekeo kwa kumshauri rafiki yake afanye maamuzi magumu. Alikaririwa akisema: "Mheshimiwa mwenyekiti hivi sasa kuna ugonjwa umezuka nchini kwa viongozi wa serikali kushindwa kutoa maamuzi magumu, bora ukubali kuhukumiwa kwa kutoa maamuzi magumu kuliko kuogopa kuyatoa. Tukitulia, tukiamua naamini tunaweza."

Kwanza hayo maamuzi magumu ni yapi? Na kwanini Lowassa ameliona hili na si wakati alipokuwa waziri mkuu na mtendaji mkuu wa serikali? Je ni kutaka sifa, kulipa visasi au unafiki wa kaiwada?

Japo maneno ya Lowassa ni kweli tupu, uongo ni yeye kusema haya leo wakati akiwa nje akikabiliwa na shinikizo la kuvuliwa kama gamba la chama chake. Kwani Lowassa ni msafi? Mbona yeye na rafiki yake Kikwete wamekataa hata kutaja mali zao? Hili mar azote limekuwa likifutikwa ikiwa ni ishara ya ufisadi wa wazi wa watawala wetu ambao mali zao zinatia shaka. Hakika nao ni uamuzi mugumu japo hasi.

Hapa chini tutaonyesha kuwa Kikwete alishafanya maamuzi magumu japo hasi. Hakuna maamuzi magumu yaliyotaka roho ya mwendawazimu kama kumteua Lowassa kuwa waziri mkuu huku akipuuza historia na miito yote iliyomtaka asijitie kitanzi kwa kutenda kosa hilo. Ajabu alilitenda kabla ya ukweli kumuumbua yeye na mshirika wake ambaye siku hizi amemgeuzia kibao.

Yafuatayo ni maamuzi magumu yaliyofanywa na Kikwete:
Mosi, kutumia hovyo mali na pesa za watanzania na kuweka upenyo kwa makampuni ya kitapeli kama Dowans kuchota pesa ya umma. Rejea ahadi ya kurekebisha mikataba ya kijambazi ya uwekezaji. Aliishia kuingia mingine tata ambayo inaendelea kulisumbua taifa. Nani haoni nchi inavyozidi kuzama kwenye kiza huku kukatwa umeme mara kwa mara ukisababisha maisha kuwa magumu bila sababu za msingi?

Wakati pesa ya kuzalisha umeme tunaambiwa hakuna, rais na wenzake wanapata pesa na muda mwingi kwenda kutumia ughaibuni huku akikwepa matatizo ya ndani. Nani mara hii amesahau alivyotimkia nje wakati wa mauaji ya Arusha?

Pili, kuruhusu familia yake ijiingize kwenye biashara kwa mgongo wa ikulu. Rejea mkewe kuendelea kutumia asasi yake isiyo ya kiserikali lakini yenye kufanya shughuli za kiserikali ikibebwa na serikali kama alivyofanya mke wa mtangulizi wake. Rejea kutajirika kwa haraka kwa mwanae Ridhiwan aliyetuhumiwa hivi karibuni akashindwa hata kujitetea. Isitoshe ni maamuzi magumu sana kuruhusu Ridhiwan aendelee kuuvuruga umoja wa vijana wa chama cha baba yake bila kujali madhara yanayoweza kutokea na matokeo yake huko tuendako.

Tatu, kuweka nchi kizani na asijali huku akiendelea kutoa uongo usioingia hata kwenye akili ya kuku.

Nne, kuanzisha uchakachuaji kwenye uchaguzi ukiachia mbali kuunda mitandao iliyokisambaratisha chama chake.

Tano, kuendekeza visasi kwenye utawala wake. Rejea kuenguliwa kwa spika wa zamani wa bunge Samuel Sitta na kutubambikizia kibaraka wake Anna Makinda ambaye amedhihihirisha udhaifu wake kama ilivyotokea kwa Lowassa.

Sita, kuendelea kuwateua na kuwakumbatia watuhumiwa wa ufisadi mmojawapo akiwa Peter Noni aliyemteua kuwa mkurugenzi wa benki ya Raslimali (TIB) huku akikabiliwa kuasisi na kutekeleza wizi wa EPA kama ilivyodaiwa na mwanasheria Michael Bhyndika Sanze aliyesajiri wizi huu.

Ni maamuzi magumu kiasi gani kwa kiongozi kujiruhusu kuingia na kubakia madarakani kwa kutumia pesa chafu zenye kutia kila aina ya shaka? Anayebishia hili amuulize Kikwete ni pesa kiasi gani alitumia na zilitoka wapi zaidi ya kwenye taasisi za umma hasa benki kuu kupitia EPA?

Nane, kufanya uteuzi wenye kila utata wa watendaji mbali mbali kwa kuzingatia kujuana. Rejea kumteua Mwanaidi Maajar kuwa balozi ilhali anatuhumiwa kuwa mmojawapo wa waliofanikisha wizi wa EPA.

Tisa, kuanzisha jinai ya kutumia vyombo vya habari na wana habari kuwachafua wenzake huku wakimpamba. Rejea kuendelea kumuweka ofisini mtuhumiwa wa ufanikishaji wa kashfa ya Richmond aliyepewa jukumu la kuisafisha Richmond bila mafanikio Salva Rweyemamu. Huyu pia alitumika wakati wa kusaka urais kwa kumjenga Kikwete huku akiwapakazia wengine. Hapa hatujata waandishi wengine kanjanja na nyemelezi waliojazana kwenye ofisi za CCM ngazi ya wilaya. Hapa bado hatujataja magazeti yaliyohongwa kumsafisha Kikwete na kuwachafua wengine yatokanayo na pesa ya EPA.

Kumi, kumkingia kifua mtangulizi wake Benjamin Mkapa marafiki zake na familia yake wasishitakiwe kwa ufisadi waliotenda. Ni maamuzi magumu kiasi gani kwa Kikwete kufanya madudu yale yale aliyofanya Mkapa? Rejea mke wa Kikwete kuendelea kutumia NGO sawa na ile ya mke wa Mkapa kujipatia utajiri binafsi. Rejea Kikwete kuendelea kuzurura nje sawa na alivyokuwa akifanya Mkapa bila kujali maonyo toka kwa watanzania.

Kumi na mmoja, Kikwete amefanya maamuzi magumu kuamua kuwatumikia mafisadi badala ya wananchi. Rejea anavyozidi kuwakingia kifua majambazi wa Kagoda na Richmond huku akiwapumbaza watanzania kuwa atawapeleka Kanani ambako nako hawapeleki zaidi ya Misri. Rejea wale mafisadi na watoa rushwa waliokataliwa wakati wa mchakato wa 2000 walivyorejea kwa kishindo na kushinda ubunge. Je hawa wanaweza kulisaidia nini taifa zaidi ya kuliuza kwa mabwana zao?

Kumi na mbili, pia kuendelea kutotangaza mali zake na wakubwa wenzake ni maamuzi magumu hata kama ya hovyo. Bila roho ngumu nani angeamini kuwa Kikwete huyu huyu ambaye hajawahi kutangaza mali zake angeruhusu serikali yake eti iwahoji ambao hawajajaza fomu! Ni unafiki na maamuzi magumu kiasi gani?

Kumi na tatu, Kikwete kuendelea kutawashughulikia wauza unga, majambazi na wala rushwa ambao alisema ana orodha zao? Je anazuiliwa na nini kama si kufaidika na kadhia hizi?

Kumi na nne, atapaswa afanye maamuzi mengine magumu kutokana kuanza kuumbuliwa na maswahiba zake kama ilivyotokea hivi karibuni kwa Rostam Aziz kuachia ngazi akithibitisha madai yote dhidi yake yalivyo kweli.

Kikwete ameishafanya maamuzi mengi magumu hata kama hayana maana kwa watanzania. Laiti angetumia ithibati hiyo ya kufanya maamuzi magumu ya hovyo kufanya maamuzi magumu ya kweli!

Haya ni maamuzi magumu hata kama ni hasi. Hebu angalia Dowans inavyoendelea kuhomola pesa yetu utadhani hatuna akili wala shida na pesa hiyo.

Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 9, 2011.

Friday 7 October 2011

Moi Visit: CJ Mutunga on Right Track



Kenya's Chief Justice Dr. Willy Mutunga visited his arch foe former president Daniel arap Moi recently. This drew a lot of ire and tirade that Mutunga was doing a very nasty thing. Some of Kenya's bills have the image of Moi. Can Mutunga's accusers boycott these bills simply because they have Moi's face? If you think you don't need Moi's face, go to the parliament and vote against using these bills.

Sadly though, people whose cases against Moi are before the court rushed out accusing Mutunga of compromising justice. They wrongly think Mutunga is betraying them. How if he is not the only one to look into the matter? Does this hold water legally?

Mutunga has said categorically that he is the CJ of all Kenyans. Moi is a Kenyan senior citizen who needs to be taught what justice is and how it works. Even if his legacy and past deeds are tainted and stinking, still Moi has the right just like any Kenyan to meet his Chief Justice. Mutunga and other activists were jailed, tortured and exiled by Moi's regime. How do we erase this? Should we embark on retributive justice or reconciliation and starting afresh?

Mutunga's visit to Moi, apart from being a lesson to Moi and others alike, is a blow to injustice and power winos. Those interested in Transitional Justice, will agree that Kenya needs healing. Healing cannot be attained by vengeance and fear of each other but by taking such bold steps. You must encounter or face your enemy and tell him that what he did is wrong, forgive or prosecute him. Dr. Mutunga's meeting with Moi is a first step to reconciliation and healing for the nation and individuals.

First of all, Moi, just like any Kenyan citizen, has the right to have audience with his CJ to air his views. This if anything is a challenge to Mutunga, Moi and Kenyans so to speak. How do we reconcile the country without finding the middle ground?

The big lesson this take has is the fact that power belongs to the people; not rulers. Mutunga who used to be a fugitive is now honourable person Moi can entertain and talk to. What a precedent!

Again, Moi did not rule Kenya alone. Even those in power today were with him at one time. PM Raila Odinga was once jailed by Moi. But again, he teamed up with him to topple his regime democratically. Kaunda says: ‘talk to your enemy to know how he regards you.’

By introducing a new constitution, Kenyans aimed at forging ahead. How will they do so if Kenyans do not have equal rights? I think if it convinces Kenyans, they should prosecute Moi for atrocities committed under his watch or forgive him. Moi too needs to be congratulated for humility and taking a bold step to accept defeat.

When Nelson Mandela met with Fredrick De Klerk (former Head of Apartheid South Africa) those who did not get it had their tongues wagging. Futuristic leaders see things others do not see.

Who knows? Mutunga's mission can be studying what Moi thinks of a new judiciary especially if there are plans to bring him or his accomplices to justice. Bravo Dr. Mutunga for taking such unique and bold step to reconcile Kenyans.

Source: The African Executive Magazine October 5, 2011.

Hili la Dowans na vibaraka wao litatufilisi


WATANI wake humwita Jiwe Kubwa (JK). Mie huko siko maana huyu mhusika si mtani wangu bali mtesi wangu. Ataachaje kuwa mtesi wangu iwapo ananifanya ninywe kama samaki kwa kukimbia mazonge na adha zitokanazo na vitu vyake na wenzake?

Zamani nilizoea kulewa kahawa. Siku hizi baada ya mambo kuzidi hasa mgao, nimevamia gongo kiasi cha kuchengua akili yangu. Wakati nikiendelea na masahibu yangu binafsi kama bi mkubwa kuniona mtoto si riziki, walevi nao wana yao. Wanaishi kizani kama mende huku wakiendelea kuaminishwa kuwa hayo ndiyo maisha yenyewe-maisha bora!

Juzi kijiwe kilikaa na kutafakari mambo mbali mbali likiwamo la kunitaka nigombee urahisi ili niwakomboe walevi wahangaika wa Danganyika ya Bongolalalaland.

Yote haya yasingetokea kama siyo mapilato kutangaza kuwa sasa kaya inaamriwa kuwalipa wezi wa Dowanis mabilioni ya madafu. Mwenzenu natamani kunyotoa roho au kuvaa mibomu na kuwavamia hawa washenzi wa Dowanis na watumwa wao wanaotumika kuifilisi kaya yangu.

Sitaki niitwe gaidi. Badala yake sasa natangaza rasmi kuwa nitagombea urahisi ili kuwakomboa wanakaya walevi wanaoendelea kuhangaika. Hatuwezi wote kuwa woga. Lazima nijitokeze kidume niwakabili hawa majambazi wakubwa wapendao kujionyesha kama waheshimiwa wakati ni wezi wakubwa tu wa kawaida.

Nimegundua kumbe nami mlevi naweza kuwa rahisi nikatawala watu na wanyama hata kama ni kwa sanaa bila sera wala uchungu nao! Naweza kuwa rahisi kirahisi kutokana na kuwahonga wapiga kura kahawa na kashata kama siyo ubwabwa kama ilivyotokea hivi karibuni kule Igunguli. Nitashindwaje kuwa rahisi iwapo walevi wanachojali ni hongo badala ya haki zao? Kwani urahisi unasomewa?

Pia siku hizi urahisi auhitaji elimu wala uadilifu bali ujanja na lugha tamu ya kuvulia kura za kula. Kwani nitakuwa wa kwanza kufanya usanii huu iwapo wasanii kibao wamejaa kwenye maulaji hadi kukuu ambako kumegeuka pango la wezi kama Dowanis AIPITIELO, Richmonduli na majambazi wengine kujivulia pesa ya walevi?

Kwa vile kaya yetu imevamiwa na njaa kiasi cha kusababisha utapiamlo wa mawazo, naamini nikiingia jukwaani na mishale na pinde watanipa tu. Nitawatishia kama yule al shabaab Rege alivyowafanyia jamaa wa Igunguli. Mikwara ya Rege ikishindikana natumia ile ya Hayaishi na Ulaya walioamua kuzifyatua ndude zao ili kuwatisha wagawa kura ya kula. Mpo hapo washirika? Mie sitatumia bastola bali mishale na pinde. Mie sitajaza masanduku ya kura za wizi bali madeli ya kahawa na makapu ya kashata tayari kuwahonga.

Katika kampeni zangu nitahimiza kuondoa njaa ya ubongo na maadili nikiwekeza kwenye madili ya uchukuaji wa rasilimali za walevi ili watanue vizuri. Ukiachia mbali njaa ya ubongo, nitapambana na njaa ya matumbo ambayo, kutokana na utawala dhalimu yamegeuka vichwa. Kila mtu siku hizi isipokuwa mimi, anafikiri kwa masaburi na utumbo. Lazima nianze na kampeni za kufufua vichwa nikizika njaa na kupiga marufuku kufikiri kwa masaburi.

Katika kampeni zangu nitawafungua macho walevi kuwa lazima wawe na mwanga badala ya kuishi kwenye kiza kiasi cha bongo zao kujaa kiza. Bila kufanya hivi kaya itaangamia naona halafu kesho Mwenyezi Mungu aniweke motoni bure kwa kushindwa kutumia kipaji change.

Kwa vile naona njaa kila kona na kila mmoja, nitahuburi siasa za ukombozi huku nikiwataka walevi wawajibike kujipigania badala ya kusubiri wajomba toka mbinguni kuja kuwapigania. Najiuliza. Kwanini wengine wameweza kuwatimua wezi wenye madaraka wakati kwenye kaya yetu wanalelewa na kuenziwa?

Ni nani huyo amuabudiaye chatu asimmeze? Jamani, niseme mara ngapi na kwa lugha gani rahisi mnielewe enye walevi wapumbavu? Nani aliwaroga nyinyi ambao kila kitu kiliwekwa wazi mbele yenu na nabii Musa bin Mchonga aliyekataa kushiriki makufuru haya?

Nani aliwaroga nyie mnaodhani kuwa kiza kinaweza kuwa zana ya ukombozi? Tazama mnakazana kuzaa watoto wenye kiza kichwani.

Je, hawa watawasaidia nini baadaye? Heri kuacha kuzaa kama mimi mkapambana na kiza na waleta kiza wanaochota mabilioni kukinunua kiza.

Hakika hizi ndizo siasa uchwara alizosema Rosti Tamu la Aziz ambazo kila uchao zinamlipa mabilioni. Kwenye Kagoda alihomola mabilioni. Baada ya kunogewa akaanzisha Richmonduli akishirikiana na Ewassa. Baada ya kustukiwa akiegeuza kuwa Dowanis ambayo sasa inaingiza mabilioni kila uchao. Ama kweli wajinga ndiyo waliwao!

Wakati upuuzi huu ukiendelea utawaona mashehena waliosheheni njaa na majoho yao pamoja na wachunaji wa kondoo waitwao wachungaji wakipanua midomo yao michafu kutetea uoza huu kwa kuingiza imani zao na ibada za vitu na utajiri. Hawa nawambia wazi kuwa nikipata madaraka nawatia panga bila kujali haki za binadamu au wadudu. Kwani hawa wanaoteswa na mabwana zao si binadamu?

Juzi niliwaona mashehena njaa wakimtetea mama wa kikatoliki aliyevuliwa kilemba wao wakakiita hijab. Acheni njaa na ulimbukeni. Mnamtetea mama yule utadhani nyanyaenu, mnapiga mikelele utadhani nyie ndiyo mliovuliwa hijab. Mbona Nchembela alimvua mke wa shehe nonihino Guest House na hamkumlaani au kwa vile wote ni chama moja?

Nasema wazi kuwa nikishinda uchaguzi sitaruhusi wabunge au Waishiwa kuhongwa na Jero na mic kuhongwa posho za makalio. Serikali yangu itatoa posho ya kufikiri na kuwajibika vilivyo. Mie si mpumbavu wala limbukeni.

Nitahakikisha raslimali za walevi zinaliwa na walevi wenyewe. Hata kama kutakuwa na madili kwenye serikali yangu, yatashughulika na kile Wazungu huita mpowerment na siyo disillusionment kama ilivyo sasa.

Leo sitaki niseme mengi zaidi ya kutangaza rasmi kuwa nataka kuwa rahisi wa kutawala na si rahisi wa kuwaibia walevi.

Naona umeme umekatika. Acha nikavamie ofisi ya Dowanis na kumkata shingo Dowanis mwenyewe. Sitampa nafasi ya kujivua gamba kama danganya toto kwa walevi.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 5, 2011.

Tuesday 4 October 2011

Hongera Lowassa kuivisha gamba CCM


Mpendwa Edward Lowassa, salaamu,

Naomba tena nitumie fursa hii adimu na adhimu kuwasiliana nawe tena. Nafanya hivyo kutokana na baadhi ya mambo kunichanganya kiasi cha kusikia umbea mwingi. Nakuandikia angalau kutaka kujua ukweli na uongo ni upi.

Kwa mara nyingine nimepata fursa ya kutimiza ahadi yangu ya kukuandikia tena kuhusiana na mvutano uliokuwapo baina yako na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pale kilipokutuhumu kuwa gamba (fisadi papa kwa kuazima usemi wa Reginald Mengi).

Hata wauiteje, kitendo cha kuendelea kushikilia nafasi ulizoamriwa kuachia ni ushindi mkubwa kwako na kuivisha gamba CCM iliyotaka kukuvua gamba. CCM walishazoea kujigamba kwa kufunga magoli ya kisigino wasijue wewe umewafunga na mkono!

Juzi nilisikia wambea wakisema eti wewe ni fisadi wa kunuka ndiyo maana hukuhangaika kujibu wala kujitetea bali kunyamaza na kupanga mipango ya kuwashikisha adabu CCM kabla hawajakushikisha adabu.

Kuna washenzi wanasema eti ulinyamaza kwa kuogopa CCM wasikunyime marupurupu na makandokando ya uwaziri mkuu mstaafu kwa sababu wewe hukustaafu bali kulazimiswa kuutema ulaji. Katika wambea hao kulikuwa na wanasheria waliosema kuwa kwa muda uliokaa kwenye uwaziri mkuu huna sifa ya kuitwa mstaafu wala kulipwa marupurupu ya ustaafu. Wambea walikuwa wanasema kuwa pesa unazopewa kama si fadhila basi ni aina nyingine ya ufisadi wa kimfumo. Mie napingana na hawa kwa vile cha mlevi huliwa na mgema kama wewe. Na pia hawa hawakujui vizuri. Ulipewa miezi mitatu, ukapangua. Uliongezewa mwezi na ushei, nao umepangua. Sasa wanataka uonyeshe umwamba gani zaidi ya huu?

Bwana Mkubwa,
Wengi wanakumbuka tambo na kujipiga kifua za CCM huku baadhi ya vinara wake wakikukamia wasijue wewe ni gari kubwa. Yako wapi sasa? Si wamefyata mkia. Walisema eti wanakupa mwezi mmoja ujivue gamba wasijue watanywea kama konokono aliyenuswa na simba.Hivi hawa hawakujua kuwa wewe ni morani? Hata yule Bwana mdogo aitwaye Nape siku hizi simsikii akikoroma na kuapa kuwa lazima uvuliwe gamba. Je ulimuita na kumpa vipande vyake au una maswahiba chamani waliomtonya na kumwabia aache kuharibiana ulaji?

Mpendwa,

Katika waraka wangu niliokuandikia mwezi jana, ingawa hukuujibu moja kwa moja, nilifurahi kukumbuka vipande vyako ulivyotoa kwenye kata ya Moita hapo mwezi Julai alipojivua gamba Rostam Aziz mshirika wako wa zamani kwenye maulaji ya Richmond. Nakumbuka ulisema kuwa kama wangekutimua kwenye chama basi ungeondoka na wabunge 11 na mawaziri wanne ambao hukuwataja. Mwanzoni mie nilidhani ulikuwa mkwara nisijue ni ukweli.

Naona nimeongea mengi kiasi cha kusahau hata kukupongeza kwa ushindi wako wa kishindo dhidi ya CCM ambayo ilitaka kukatiza mbio zako za kugombea urais mwaka 2015.Nakumbuka pale Moita ulisema lazima ugombee urais mwaka 2015 hata kama ni kusimama kama mgombea binafsi.

Leo sitauliza maswali mengi isipokuwa machache. Je bado unaamini kuwa hata ukigombea nje ya chama chochote unaweza kushinda? Je kama wapiga kura watakuuliza kilichokutoa CCM utawajibu nini? Na je kama utaendelea kuwa kwenye CCM kama ambavyo hali inaonyesha, kama waliotaka kukuvua gamba watakataa kukupendekeza kugombea utafanya nini? Ina maana utawapiga mkwara kama uliowapiga kwenye kujivua gamba wanywee? Je ombi langu la kutaka utangaze mimali yako na kupangua shutuma za kashfa ya Richmond, Dowans, kujilimbikizia mimali na nyingi umelifikiria vipi?

Juzi nilizinyaka kuwa CCM inakuvutia pumzi. Wambea wanasema kuwa baada ya kumaliza kibarua kigumu cha Igunga ambapo mambo si mazuri kwa CCM, kuna uwezekano wa kukuita na kukupa talaka yako. Je kama watafanya hivyo una mpango gani wa kupangua? Je ukweli ni upi, umewagomea na kuwabwatukia wakanywea au wanakuvutia pumzi ili wamalizane cha Igunga?

Je ule mtandao wako bado una bao? Kuna kitu nilikuwa nimesahau. Vipi zile shutuma kuwa mwanao Fred alihojiwa na mamlaka za Uingereza kwa kuingiza mabilioni ya shilingi bila maelezo? Je ni kweli Fred ni mfanyabiashara maarufu? Je anafanya biashara yake au ya familia?

Je kwanini hukwenda Igunga kumpigia kampeni mgombea wa CCM wakati swahiba na mwenzio Rostam alifanya hivyo? Je uligoma, kuzuiliwa au? Pia kabla ya kusahau, bado ule mradi wa kujenga ofisi ya bei mbaya kwa ajili yako mjini Monduli bado unaendelea?

Kabla ya kusahau, vipi ule ushauri wako kwa CCM, hasa viongozi wake, kufanya maamuzi magumu mojawapo likiwa kukutimua, je walikujibu au wanaendelea kukuvutia pumzi ili wakufanyia maamuzi magumu yaani kukutosa bila kujali kuwa ulikuwa mwenzao? Je kama mojawapo ya maamuzi magumu itakuwa kukushikilia hadi ujivue gamba, utaendelea kuwashauri wafanya maamuzi magumu tena? Hivi kati yako na wale wanaosema uvuliwe gamba nini adui wa CCM anayeiangusha mbele ya jamii? Je ni wewe unayekataa kuachia ngazi au wale wanaozungushazungusha mambo wakati kila kitu kiko wazi? Je mwoga ni yupi, wewe unayeogopa kutoka au wao wanaoogopa kukutoa?

Nauliza maswali hapo juu si kwa kejeli. Ni kwa sababu nimechanganyikiwa kwa hiki kinachoendelea ambapo mnapimana ujogoo huku wapiga kura wakiendelea kusota na kuhisi kama wamesalitiwa.

Nimalize kwa kukupongeza tena kwa kuishinda CCM. Swali ni je, hizi zitakuwa mbio za sakafuni au wataendelea kukugwaya huku wewe ukitesa na kujiandalia kuutwaa urais mwaka 2015 come shine come rain?

Chanzo : Dira Oktoba 2011.