The Chant of Savant

Tuesday 29 May 2012

Pamoja na vita bado Ivory Coast wanatuzidi!

Rais Jakaya Kikwete  akiwa na mgeni wake rais wa Ivory Coast Allasane Ouatara (pichani).

Kwa mtu anayejua hali ngumu ya vita na kutokuelewana liliyopitia taifa la Ivory Coast anashangaa kuona bado wana ndege ya maana kuliko sisi ambao tumekuwa na amani miaka yote. Ningekuwa rais Kikwete hapa bila shaka ningeona aibu hata roho kuniuma na kulifufua  Air Tanzania badala ya kuacha wezi wachache walimalize. Ni bahati mbaya kuwa viongozi wetu wamekosa roho ya kujisuta hasa wanapoendekeza ufisadi na uomba omba wakati mali wanayo lakini wanaikalia na kuigawa kwa wawekezaji na matepeli wachache kwa hongo ndogo ndogo.

No comments: