The Chant of Savant

Thursday 23 August 2012

Wenye swimming pool mngefanya nini hii ingewatokea?



Nchini Afrika Kusini ndama wa kiboko mwenye miaka miwili amekuwa mgeni asiyetegemewa kwenye swimming pool ya mtu mmoja. Ndama huyu aliyeandamana na mama yake aliyekuwa akienda mateneti kujifungua, aliachwa na mama yake kiasi cha kupotea. Mama alikwenda hospitali (mwituni) kujifungua na kurejea na kichanga chake huku akimpoteza ndama yake mkubwa. Hivyo, ndama alilazimika kuzurura hadi alipofanikiwa kupata bwawa la kuogelea la mtu na kujichimbia mle. Je mgeni huyu ungemkuta kwenye bwawa lako la kuogelea ungefanya  nini? Kwa habari zaidi BONYEZA hapa.

No comments: