The Chant of Savant

Wednesday 31 October 2012

Je CCM watamkumbatia Nagu au kumwangukia Sumaye?



 Chama Cha Mapinduzi (CCM) hujitahidi kuficha aibu zake kwa kuwabana wanaodhaniwa kutaka kukiaibisha, kashfa ya rushwa kwenye uchaguzi wa ndani wa chama uliopita haifutikwi chini ya busati. Hakuna mwiba unaoikabili CCM kama madai ya waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye kuwa uchaguzi ulitawaliwa na rushwa.

Sumaye alipotoa madai yake CCM ilitumia busara ya kuepusha malumbano. Lakini taratibu zilianza kuibuka tuhuma nyingine za dhambi hiyo hiyo ya rushwa hasa baada ya kufanyika uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa (UVCCM). Kuna madai kuwa rushwa ilitembea nje nje. Ingawa rushwa ni jadi ya CCM, kuzudi kwake kulimfanya mwenyekiti wake rais Jakaya Kikwete kusema, “Nawaambieni, mkifanya mchezo ipo siku mtakuja kujuta maana mkishamchagua kiongozi asiyefaa, mtalazimika kuwa naye huyohuyo hadi mwaka 2017 na kama waswahili wanavyosema majuto ni mjukuu,” 
Wengi walimuona Kikwete kama mnafiki na mwenye kutapatapa kutokana na ukweli kuwa ndiye aliyefunga rushwa ndani ya chama na serikali. Rejea kuendelea kuwakingia vifua watuhumiwa wa rushwa kama vile Andrew Chenge na Dk Idris Rashid waliobainika na mamlaka za Uingereza kupokea rushwa ili kununua rada mbovu kwa bei mbaya toka kwenye kampuni la BAE.
Rejea kuendelea kumlipa marupurupu na stahiki za kustaafu waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa hata baada ya kubainika kushiriki ufisadi wa Richmond. Rejea kuwarejesha kwenye baraza la mawaziri watu walioshiriki kwenye kuuza nchi kama vile Dk Abdallah Kigoda.

Yote tisa, baada ya Sumaye kushupaa na kutamka hadharani kinyume na taratibu za chama kuwa aliyemshinda kwenye uchaguzi Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Mary Nagu kutokana na rushwa, CCM imejikuta msambweni. Sumaye bado ana ushawishi chamani. Je CCM itamkumbatia Nagu na kumtosa Sumaye au kumwangukia na kumtosa Nagu. Yetu macho.

Mpayukaji ajiteka ili kuwapakazia ndata

BAADA ya kuona kundi la Uangusho kule Zaainzibaa likimwaga cheche na kupata maujiko huku SZM ikiwafumbia macho ikidhani wataufumuua muunganiko, mzee mzima Alhaji, Dk., Professa, Lt Col. Father, mtaalamu wa kuongea na majini, Mpayukaji Msemahovyo Waambie niliamua kujiteka ili kuanzisha vurugu ambazo nilidhani ni ukombozi wa walevi.
Nilipoona wabangaizaji kama Ismi Juha, Shehena Fuad na Tapeli Pondwa wakipata ujiko hata ulaji nami nikaona nitie guu. Ningeachaje kufanya hivyo wakati nina usongo na nambari kwani ukiachia mbali kuweza kupata wachukuaji waitwao wawekezaji wanaoweza kudhamini fujo zangu ili walevi wapigane nao wavune mali zao? Kwa wasiojua gemu zima wajiulize kwanini DRC imo msambweni? Madini wanangu. Kwanini Mashariki ya Kati imo motoni? Wese wanangu.
Kwa vile na kaya yetu ina madini na imegundua miwese mingi, lazima tulianzishe ili tupate washitili wa kula nao kwa ulaini. Unadhani ulaji mchezo?
Pia kufeli na uroho wa wanasiasia kula peke yao kumetufanya nasi kuona tunaweza kutumia nyenzo yoyote kuanzia bangi, kahawa, dini, hata jinsia kupata ulaji.
Hivyo kesho mkiona bi mkubwa wangu akiingia na chama chake cha Wanawake na Maulaji (WEMA) au Equal Oportunities for First Ladies (EOFL) msishangae, ni mambo ya ulaji.
Twende kwenye dili. Baada ya kuona napiga mikelele kwenye kijiwe na walevi hawapati somo, niliamua kujiteka na kutangaza kuwa nimetekwa na ndata ili walevi waamke na kupambana na ndata hata kuwanyotoa roho kama yule wa kule Zenj alivyofanyiwa na wahuni wa Shehena Fuadi.
Ili kuwapata walevi waliochoshwa na kutolewa chochote na ndata, niliwaambia kuwa badala ya kupigana na ufisadi huu wa ndata, tuanzishe vurugu kudai kuwa mfumo wa maisha wa walevi ndiyo unaopaswa kuendesha kaya. Kama Shehena wa Kupondwa Pondwa nilikuja na mkakati wa kudai kuwa walevi tunaonewa. Badala ya kulaumu ulevi na bangi zetu, nilitupia kila lawama kwa ndata na lisirikali.
Na walevi nao kutokana na ulevi na bangi zao si walikubaliana na mahubiri yangu ya ngoa na usongo. Ila kwa vile walevi ni walevi na hawawezi kuwavaa ndata, niliona nibuni njia nyingine ya kuwaamsha wapambane na ndata. Siku ya siku niliondoka zangu home na mshirika wangu wa bedroom tukiwa tunaendesha baiskeli yetu.
Nikiwa naendesha tulijadili mpango mzima na bi mkubwa wangu. Tulikubaliana kuwa baada ya kujiteka na kwenda kujificha kwenye kijiwe cha Uswekeni, baada ya siku tatu nijitokeze kama aliyeachiwa. Uongo tuliotunga ulisema hivi: Tulipofika mitaa ya Usiniulize, nikamwambia bibi mkubwa aondoke zake. Kwani nilikuwa na miadi na Mgoshi Machungi na maongezi yetu yangechukua muda mrefu.
Hivyo, bi mkubwa alipaswa kuondoka ili awahi naye kwenye miadi yake na shoga yake Salmi Kikwekwe ili ampe mbinu ya jinsi ya kutumia NGO yake kutengeneza ulaji hapo baadaye. Baada ya bi mkubwa kuondoa baiskeli niliingia zangu kichakani kuchimba na kupanda dawa. Wakati narudi si ndata wakaniteka kwa siku tatu!
Ilibidi nifanye haraka kujiteka na kujitokeza hasa baada ya kugundua kuwa kumbe na Shehena Pondwa naye alikuwa amelianzisha ili apate ujiko. Hivyo sikutaka amalize ujiko peke yake. Ilibidi nijiteke ili ukombozi upatikane ingawa niliishia kukumbwa na kesi ya jinai.
Baada ya kujiteka si mambo yalitibuka baada ya walevi kuingia mitaani na kuzidiwa nguvu na ndata. Isitoshe kuna walevi wenzetu waliostukia mpango mzima na hivyo kuupinga wazi wazi jambo ambalo lilinimaliza nguvu nikaamua kutoka nilikokuwa nimejificha kwa aibu.
Pamoja na dili langu kubuma nimejifunza mambo mawili matatu. Ukitaka kujulikana kwenye kaya yetu fanya fujo ukamatwe na ndata. Amini usiamini utapata majuha wengi wa kukuunga mkono kwenye kila bangi utakayokuwa ukiipigia debe.
Pia nimegundua kuwa walevi wengi wana hasira hasa baada ya kunyonywa sana na mafisadi. Ingawa wameshindwa kupambana na mafisadi mmoja mmoja au wote kwa pamoja kutokana na woga, wakipata mtu wa kuwachochea kumbe wanaweza kuwa vifaa huko tuendako!
Pamoja na kuwa na hasira, walevi pia wana kisasi na mafisadi, sema hawajui kupambanua nani wa kushughulika nao kwanza. Mfano mzuri ni juzi tu walipoamua kutaka kupambana na ndata wakati adui wao mkubwa ni mafisadi. Mara hii mmesahau mafisi kama Eddie Ewassa wanavyogawa mifweza ya wizi kwa vijiwe mbalimbali! Hawa ndio wa kufa nao badala ya ndata wasio na tofauti na mbwa na amfugaye.
Pia nimejifunza kuwa hata mafisadi nao hawana mikakati ya kuona mbali. Wakibanwa mbavu wanahaha na kuparaganyikiwa kama jamaa zangu waliofungulia masoja kwenda kufanya kazi ya ndata. Kwanini nasema hivi? Hebu angalia jinsi ambavyo akina Shehena Fuadi na Pondwa Pondwa walivyowajambisha ndipo wakakumbuka kufunga eti vyombo vya umbea vilivyokuwa vikitumika kuhubiri chuki na ngoa.
Kwani hawakujua kuwa vyombo hivi vya udaku havikuanzishwa kuelimisha na kuiburudisha jamii zaidi ya kuichafua, kuijaza ujinga na kuihuzunisha. Hawa jamaa nao wamezidi kwa ujuha na kujisahau.
Unakumbuka wakati wa Ben Tunituni bin Makapu alisemaje vyombo vya umbea vilipombana kuwa alikuwa fisi na fisadi? Aliviambia kuwa kama navyo si fisadi vieleze vilipokuwa vimepata mitaji ya kuanzishwa.
Sasa hawa jamaa walipoona vyombo hivi vya umbea vinahubiri maangamizi, wao wakatumia vyao kuhubiri chuki dhidi ya vyama vya upingaji.
Ngoja nirejee kwenye kisa changu cha kujiteka na kudai nimetekwa. Kwa ufupi ni kwamba nimejilaumu baada ya kugundua kuwa kumbe mambo si rahisi kama nilivyodhania. Pia niligundua kuwa kumbe si walevi wote wanaoniunga mkono. Hata hivyo, sitachoka.
Kama watafanya mchezo kama walivyofanya kwa kufanya mambo kwa nguvu ya soda, nitakuja na mikakati mikubwa ya kuchukua kaya kwa njia yoyote bila kujali kama ni halali, haramu, salama ama hatari. Walevi kaeni mkao wa kuliwa kama hamtajifunza kutokana na haya yaliyopita.
Naona gari la Jei Wii. Acha niishie wasije kunikamata kwa uzushi wangu! Hivi kunguru na mwewe nani kiboko ati? Acha nijikate kabla ya kunikamata na kuninyoa madevu yangu kama yule jamaa!
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 31, 2012.

Sunday 28 October 2012

The bad the ugly and the good and miracle performers of Bongo



Looking at EddieWhitehair Lo- Wash doling money out for whoever that approaches him, one’d see love of the rich to the poor. Again, is this love true or has something else? Since he’s forced out of power thanks to Richman Scam, Eddie’s become a very generous politician Bongo has ever had. He does not budge when it comes to dishing out millions. He loves churches even mosques. Ironically, such places are called the places of God! Which God between god money and God Almighty? Aren’t those dens manned by jackals and hyenas Jesus admonished us to be aware of? Mwl Mchonga added that we’d fear such crass putas like leprosy if we want to be safe. Again, who bothers? 
If you want to get Eddie’s dosh just come with the media guys and invite him to anything you deem fit. He surely will come and make you rich. More often than not, those who don’t know how the media operate have always been quick to accuse the media as part of this sellout. Nay guys; ours as media, is to cover events regardless the one making news is a devil or an angel. This is the bottom line. Again, this does not mean that Kanjanjas are not out there abusing and breaking all rules in the books.  Verily, they’re there selling themselves like twilight girls of Ohio and Kinondoni. Technically, we call this professional prostitution just like political prostitution the money has created recently.  
Back to Mr. Plutonic Eddie, when he rakes money out in his spin nobody bothers to ask if his money is legally or illegally gotten. The power that-be has always mollycoddled him and people have taken it seminally! Aren’t, this way, people blessing thuggery and corruption? Who care if at all money talks?  Baniani mbaya (literary bad banyan’s shoe is a cure). A dead donkey does not fear hyenas. You know who is a dead donkey and who hyenas are. What a systemic malady of corruption so to speak? Why don’t we have such courageous people especially men to take on the guy and tell him to his face that we need our Richmond money back? Are we such gullible and greedy in the first place? Miraculously, even Mr. Prezzo who has always made us believe he is there to fight corruption is silent!   
By and large, people know that this ‘generosity’ is temporal by nature. In a simple parlance, this game is known as kutumiana namely to fool each other. Again, blessed is the hand that giveth than the one that taketh. In future, someone will suffer such a humungous blow.  The equation is so simple.  Recipients will be made to pay dearly. What is evil is the fact that at this moment of truth, major victims will be our children.
Given that people have consented to being bribed and fooled with their own money, whose fallacy is this? Again, dudes, if you’ve blindly and pointlessly accepted this hanky panky generosity, don’t take it for granted. For, from now on to October 2015 it’ll exist. Thereafter, tell it to the birds. If he gives you any coin come jeer at me and call me a liar.  Ironically, since some smart guys invented Uhujumaa na Kujimegea (kleptocracy and Selfishness) to replace Socialism and Self-reliance under Zenj Declaration, all opportunists decided to seek power. Those who still remember and adore Arusha Declaration must commit suttee or hara-kiri.  
Things have changed tremendously. We used to get good leaders based on principles, ethics, vision, handwork and what it takes. Currently, money, dirty money, has taken over all those good virtues. Yeah. Show me just one leader who did not buy his way to power today. Not in this deadly venal hunk of ours. Anybody can become president, bishop even sheikh. For those who aspire to become president just like Eddie, it is simple. Grab money from anybody and spend that money on buying political loyalty. This way anybody can become president. Thus, never wonder when you hear guys like Andy Chenge or mzee wa vijidosh wants to become one. Everybody likes to become president especially at this punkish and thieving era. The zinger is under such rotten atmosphere after becoming president you can steal as much as you deem fit to reimburse yourself the money you spent on getting votes. Nobody will put you to task given that all you are manning are conspirators thus thieves by consent. This is where the root of zilch accountability and performance for many afro-president lie. You can become as Mobutu as you like and nothing will happen to you. You know what? Whoever that will try to lay you bare will be hated and persecuted. Have you forgotten how Jesus was treated while a thief Barabbas was adored?    And don’t buy a pig in the poke. Who’ll douse this fire?
Source: ThisDay Oct,. 29, 2012

Wednesday 24 October 2012

Corruption in Africa: The Dilemma

Almost every African country is currently facing corruption and has an “anti-corruption” body. These bodies are known by various good and serious names such as Takukuru (Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa) Tanzania, Kenya Anti-Corruption Commission (KACC) and Anti-Corruption Coalition Uganda (ACCU). Even DRC despite being tainted with corruption, hopefully had an anti-corruption corps.
Although impunity involving those manning anti-corruption bodies is quite known for many Africans, the recent conviction of Nigeria’s anticorruption agency EFCC’s officials is a slap in the face to the government. Douglas Williams and Abba Ishaku were recently convicted for asking a bribe of $ 630 from a politician in order to stop investigating him. The amount of money is so small. This suggests that even the officials in question are junior. What transpired in Nigeria is but a typical replica of what has been going in Africa. African anti-corruption agents are antithetic to what they say they are fighting. They can deal with “everybody.”
Under every rule, there is an exception - they cannot deal with politicos and sacred cows in the country. Most of the anti-corruption agencies intimidate and dupe the general public and donors that their respective governments are fighting corruption. Most of these carbuncular creatures of corrupt regimes are under the office of president like Takukuru. Their modus operandi towards their masters goes with a proverb: asking me no questions; I’ll tell you no lies. How can a corrupt regime fight corruption? How can a government that came to power by rigging fight corruption?
Anti - corruption agencies are being used by corrupt rulers as diapers to clean and conceal their messes. For example, Africa's minerals are stolen every day but nobody is brought to book. How can anti-corruption agencies tackle corruption while there is no ethical grounding in African governing systems? How can anti-corruption agencies take on corruption while they are doing so in Nigeria style of “give me what’s mine otherwise you face it.” In Africa, any thief can plunder and become super rich for no ethical rules are in place for individuals to declare how they acquire their wealth. 
Power in Africa is a family business. The President’s power is used by family members and friends to solicit loans from the banks and other preferential treatment. Anti-corruption agents neither see them nor take on them. To show how smarter anti-corruption agents are, they make their own killings and this is why many of the officials of anti-corruption agencies are rich due to sound salaries and kickbacks they receive in order to “fight” corruption. 
We need independent bodies that can take on whomever no matter what. This must be stipulated in the law. One can’t fight corruption without pertinent ethics in place. Africa needs the same code western countries use. Everybody must give an account of how he or she made her wealth. By having such accountable and responsible codes, Africa will be able to forge ahead. Are African strategies to fight corruption monkey business or another display of hypocrisy and megalomania?
Source: The African Executive Magazine Oct., 24, 2012.

Tuesday 23 October 2012

Serikali ijilaumu kwa kuufuga udini


HIVI karibuni taifa letu limekuwa gumzo kwenye vyombo vya habari vya kimataifa. Hata hivyo, si kwa sababu nzuri bali uchomaji wa makanisa uliotokea baada ya watoto kufanya utoto kutokana na kufundishwa imani potofu na za kishirikina.
Chanzo cha yote ni ubishi baina ya watoto wawili mmoja mkristo na mwingine Muislam kuwa akojoleaye au kuharibu, kutemea mate Korani aweza kugeuka mjusi hata kufa.
Hakuna anayeunga mkono kitendo hiki hata kama ni cha kitoto. Kadhalika, hakuna mtu mwenye akili na nia nzuri anayeweza kuunga mkono matokeo ya kadhia hii.
Katika utoto huu mmoja wa watoto aliamua kufanya majaribio kujua kama alichoambiwa ni ukweli au la. Baada ya kufanya hivyo bila kufa wala kugeuka mjusi, tunaambiwa mwenzie alichukia na kwenda kuripoti kwa wazazi.
Kimsingi, watoto wamefanya utoto kiasi cha kuwaingiza mtegoni watu wazima kushabikia na kufanya utoto zaidi. Wanaojiita waislam wenye ajenda zao za siri walipata fursa ya kuhubiri kiama huku wakishinikiza makanisa yachomwe!
Je, hii ni busara, elimu au dini aina gani isiyotumia hata chembe ya akili? Akikosa mkristo au mkwere mmoja basi unaadhibu wakristo au wakwere wote!
Ili kuona kama kweli kulikuwa na haja ya kujichukulia sheria mkononi ngoja tuhoji. Je, Korani ni nini? Korani ni kitabu sawa na vitabu vingine ukiondoa kuwa husemekana kuwa kimetoka kwa Allah. Ukiondoa hiki kitabu tunachoona, Korani si vile vitabu tunavyomilki bali ujumbe ambao mtume Mohammad (SAW) alikuwa akipokea na kuwakaririsha wafuasi wake.
Ni ajabu: Mohammad alipokufa, aliacha kila kitu kwenye uislam ambao alisema aliukamilisha isipokuwa kitabu kinachotugombanisha.
Je kwa msingi huu, hii Korani (kitabu) ambayo hata mtume hakuiacha inakuwaje inapewa umuhimu kuliko hata ubinadamu?
Binadamu ameumbwa na Mungu. Korani imetengenezwa na binadamu. Huu ni ushahidi ima wa ushirikina au kutojua mambo.
Nasema hivyo kutokana na ukweli kuwa anapochomwa moto kibaka kwa mfano ambaye ni kazi ya mikono ya Mungu, watu hawaandamani wala kuchoma makanisa.
Ajabu kikichomwa kitabu kazi ya mikono ya binadamu watu wanakamiana na kutaka kuuana! Je hapa kweli tatizo ni kuchomwa kitabu au kuna jingine?
Si uzushi wala upendeleo kusema kuwa serikali yetu imefuga hisia za udini nchini mwetu. Maana kumekuwa na watu wanaoota ndoto za mchana kuwa kuna siku Tanzania itatawaliwa Kiislam au Kikristo.
Ila wanasahau kuwa uislam haujawahi kutawala popote ukiachia mbali baadhi ya watawala kuutumia kufikia malengo yao. Mfalme Constantine aliutumia Ukristo kutawala Rumi, Ezana (Kush) huku watawala wa Ottoman, Mughal na Safavid nao wakiutumia uislam kujiimarisha kwenye madaraka.
Je, chanzo cha manabii wa vita na machukizo kama vile Uamsho na wana mihadhara ni nini? Ni ulegelege wa serikali bila shaka.
Tunao wahubiri wengi wa kiislam wanaotumia Biblia kushawishi watu kuwa waislam pasina kutumia Korani kutokana na kutoijua wala kusoma dini.
Hili ndilo kundi kubwa lenye mashehe wa kuzuka kama huyu anayehubiri machafuko aitwaye Issa Ponda Issa ambaye shehe mkuu Shabaan Simba alisema si shehe wala msomi, bali mhuni wa kawaida anayetafuta riziki kwa kujificha nyuma ya joho la uislam.
Leo tuna makundi yenye kila alama za ugaidi kama Uamsho yakijidai kupigania haki za waislam hata watanzania. Ukiwauliza aliyewachagua na kuwatuma hupati jibu zaidi ya kuvunja sheria ya nchi.
Hawa na wale wa kikristo wamekuwa wakiwapigia watu kelele bila hata kujali kuwa wanahitaji utulivu. Leo, kwa mfano, ni hatari kulelea mtoto kwenye baadhi ya maeneo jijini Dar kutokana na kelele zinazotoka misikitini na kwenye makanisa hasa ya mikesha.
Kinachofanya serikali ilaumiwe ni ile hali ya kuruhusu kila mtu kujifanyia atakavyo bila kufuata serikali. Madhehebu ya dini yalipaswa kusajili kwa sharti kuwa yakienda kinyume na matarajio ya serikali yanafutiliwa mbali.
Leo tuna maaskofu wengi feki wanaotumia dini kuwaibia maskini na kuwadanganya wanamchi kila uchao.
Tuna mashehe wengi wanaoibuka na kutangaza vitu vya ajabu kama hawa wanaotaka kuangusha Bakwata au kutaka kueneza uislam wa kihafidhina ambao hata Mtume hakuuacha.
Hata hivyo, inapaswa watu wa namna hii kuambiwa kuwa tulipopigania uhuru tulipigania uhuru kama watanzania na si waislam wala wakristo. Mtu yeyeto aweza kuingia dini yoyote na kutoka lakini hawezi kufanya hivyo kwa uraia wake kirahisi hivyo.
Kwenye kujiunga na dini hakuna maombi wala masharti sawa na uraia. Mbona wakati tukiingizwa kwenye mfumo wa kikoloni au kupelekwa utumwani hizi dini zinazotaka mamlaka leo hazikutusaidia zaidi ya kuwa wakala wa mateso yetu?
Kuna haja ya kusoma historia kuepuka aibu ya kiakili kama hii. Hivyo, hawa al muthnaka wanaoota mchana kudhani Tanzania inaweza kutawaliwa kidini, washikishwe adabu mara moja.
Ni upuuzi na utaahira ukiachia mbali uchizi kwa watanzania maskini kujificha nyuma ya imani za kimapokezi na kimamboleo hadi kuchelea kumalizana. Ni ajabu leo watu wanahamanika hata kufikia kutaka kutoana roho kwa mambo mepesi wakati mambo mazito kama kupambana na ufisadi wanayafumbia macho!
Kimsingi, Tanzania hakuna udini bali uchovu wa kifikra na umaskini wa kunuka.
Sioni tatizo baina ya wakristo na waislam ukiachia mbali wahuni na matapeli wanaotumia dini hizi kuleta vurugu.Hatuwezi kuwahukumu waislam wote kwa ujuha na ajenda fichi za makundi madogo ya kitapeli yenye kufadhiliwa na maadui wetu.
Tumekuwa mafisadi hata wa kiakili kirahisi hivi? Mbona hatuongelei viongozi mafisadi wa kiislamu wanaowaibia na kuwatumia waislamu maskini sawa na wale wa kikristo wanavyowaibia wakristo?
ACHENI UVIVU WA KUFIKIRI na kulialika janga ambalo hamuwezi kuli-contain. Tukianza vurugu wengi wa watu wetu hawatakufa kwa matundu ya risasi bali, njaa baada ya kushindwa kwenda kuhangaika maana ni maskini mno; hawana hata ujanja wa kutorokea nje-hawana pasi za kusafiria wala pesa.
Tuwaacheni waishi maisha yao ya mahangaiko yanatosha, Tatizo la nchi yetu siyo udini bali ufisadi wa kimfumo hata wa kidini.
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 24, 2014.

Tatizo letu si udini, bali uduni


BAADA ya kunuka au kuumana hivi karibuni kwenye kaya yetu ya amani, mzee mzima nimeona nitoe busara na elimu bure ili kuepuka kujitia kitanzi kijinga na kipofu.
Laiti ndata wasingekuja Kijiweni na kutulipulia mibomu yao ya michozi wadhani ningenena?
Ningewaacha wamalizane kwa vile wamefugana na kufuga ujinga na ujanja ujanja wao wenyewe huku wakitudharau sisi ambao hatuhusiki na ligi yao ya kuaminisha walevi imani zao.
Ni juzi tu watoto wawili wameonesha utoto wao na ushirikina unaoashiria mafunzo mabaya kutoka kwa wavyele wao.
Si mitoto mitukutu ilibishana kuwa mmojawapo akikojolea msahafu atageuka mjusi au kufa. Kutokana na ukosefu wa busara si mitoto ikaamua kufanya kweli. Wallahi naapa angekuwa kijogoo wangu siku hiyo ningemfungia kwenye gunia kwa muda ili ajifunze kufikiri.
Nisingekurupuka na kuanza kuchoma ma-church wala kudhani kuwa Manaswara ndiyo maadui zangu. Nisingefanya hivyo kwa vile adui alikuwa nyumbani mwangu saa nyingine mimi mwenyewe kumfundisha mwanangu mambo yasiyoingia akilini.
Haya ya watoto tuyaache. Huo ndiyo utoto wenyewe. Leo nalonga na wakubwa wenzangu hasa wale walioshika maulaji na madaraka kulea ujinga umaskini na ufisadi kiasi cha watu wetu kuanza kuwa na imani mfu na hatari.
Laiti watu wetu wangelikuwa wamepiga shule wangejua kuwa kwa mfano misahafu ni makaratasi yaliyotengenezwa na binadamu ili kuwawezesha kujitawala vizuri.
Wangejua kuwa miili yao ina thamani kuliko makaratasi. Wangeoogopa hata kuchoma vibaka kuliko kuogopa hata kuwa tayari kutoana roho kwa ajili ya makaratasi.
Kijiweni tulishangaa kusikia eti watu wanafia misahafu. Hawakusoma hawa? Huwezi kunajisi misahafu. Ukijitahidi kufanya hivyo utanajisi kitabu lakini si ujumbe wa Mwenyezi Mungu Subhana Wa, taala. Misahafu siyo tabu bali ujumbe wenyewe.
Kwani mnadhani kipenzi chake Allah Sayyidna Muhammad (SAW) alikuwa juha kama nyinyi siyo? Mnajua ni kwanini hadi anafariki hakuwa ametoa idhini ujumbe wake uandikwe kwenye makaratasi zaidi ya mioyo?
Alichelea uvivu wa kusoma kusababisha watu waache kuhifadhi na badala yake wategemee matabu ambayo sasa yanawagombanisha.
Mnadhani Mtume alikuwa zoba kama nyinyi siyo? Kwanini hakuacha amejenga misikiti ya bei mbaya ilhali alijua hekalu la mfalme Suleiman? Niwasaidie, alitaka dini isiwe mzigo bali nyenzo ya kuwafanya watu kuishi kwa furaha na si karaha na kuchukiana. Ukimchukia mwenzio elewa huna dini tena.
Kweli aliyewaita Bongolaland hakuwaonea. Mnagombea nadharia huku mkiogopa hata kugombea mambo yanayowahusu kila uchao? Mbona hatuoni jazba kwenye kupambana na ufisadi na dhuluma?
Ni walevi wangapi wanalanguliwa na wenye mbavu za mbwa mnazoita nyumba ambao wengi wao tena huapa kila mara bila kujali kuwa wana dini? Je, wezi wa namna hii wana dini au mauza uza? Nikimuona mama mwenye ubavu wa mbwa wangu anavyoapa hovyo hovyo na matendo yake nachukia hizi imani kusema ukweli.
Leo mmeruhusu wahuni wahuburi maangamizi na matusi hata bila kuwaonya! Hao mashehena wanaojifanya walimu na magwiji wa dini hasa Ugalatia walisomea wapi kama siyo kuendeshwa na njaa? Wengi hawana hata kazi achia mbali elimu zaidi ya kupiga mikelele.
Mbona hakuna mahali mtume alihubiri ubovu wa Baibulo la moyo wa chuluka jamani? Si aliikuta na kuiacha? Msitupigie kelele na uongo na ujinga wenu.
Mnadhani tunapenda hiyo mikelele na mikesha yenu? Tafuteni kazi au njooni Kijiweni tuwape misheni ya jinsi ya kupambana na ukwe.. na ukapa huu tulio nao.
Tukikwambia kuwa tunapata bangi ili kuondoa mawazo mnatuona makafiri wakati nyinyi ni wabaya kuliko sisi.
Maana bangi zetu tunavuta wenyewe wala hatulazimishi na wengine kuvuta bangi zetu kama nyinyi.
Hivi kama mwili wote ungekuwa sikio jicho lingekuwa wapi? Kila mtu anatuhubiria uzuri wa dini yake wakati tunaona matendo yao ya kutisha.
Kama mmeshindwa kutatua tatizo la kitoto kama hilo mtatatua matatizo yetu au mnataka kutuingiza kwenye matatizo yenu.
Nyinyi mnapata wapi? Kwanini mnatuletea bidaa mchana kweupe halafu mnataka kutumia bidaa zenu kutugawana. Mshindwe na mlegee nasema.
Wabongolalalanders wana matatizo yao mengi. Wanakabiliwa na ukapa na ukwe.. We stop! Wanasumbuliwa na ufisi na ufisiahadi na siasa za Uhujumaa na Kujimegea.
Kwanza, wengi wa wabongolalalander hawana dini na kama wanayo basi si nyingine bali kutafuta utajiri.
Hamuwaoni wale wachunaji wanaojiita wachungaji au mashehena wanaojiita mashehe. Shehe aweza kuhubiri vita na upuuzi au mchungaji miujiza na kuwadai watu sadaka? Acheni njaa zenu na wazimu wenu tujenge kaya.
Juzi nilisikia wajinga fulani wakisema eti Bongolalaland inatawaliwa kwa mfumo Christ! Toba! Mfumo Christ chini ya shehe! Mnamdanganya nani jamani? Mijitu iliyolewa chuki eti inasema lazima tutangaziane vita! Hivi vita mnaijua au mnaisikia?
Tukianza vita wajua tutakufa si kwa matundu ya risasi bali njaa? Mijitu yenyewe makapuku ya kunuka?
Hamna tofauti na mipumbavu inayokula nyama kila siku halafu ikaanza kulalamika eti haipati maharage.
Wenye nazo wakianza kupanda mipipa kwenda kuishi ng’ambo nyie mtanukia kwenye mbavu zenu za mbwa.
Hivi umaskini au maradhi na ujinga vinajua dini? Mbona kwenye mbavu za mbwa za kupanga hambaguani isipokuwa kwenye vichwa vyenu wana hizaya nyie?
Jamani tupeni fursa tupambane na matatizo ya kweli badala ya haya ya kuumba.
Tuondolee mbu na uvivu wenu wa kufikiri jamani tupambane na umaskini tuliotengenezewa na mafisadi ambao dini yao ni utajiri. Tena kabla ya kusahau.
Mbona mafisadi wote wana dini moja ingawa majina yao ni ya Kizungu na Kiarabu?
Waijua dini ya mafisadi? Inaitwa Almight Money bin Senti bin Fwedhaa. Wamjua Mungu wao?
Matumbo na tamaa zao. Leo mnajitia kiranga halafu ndata wakiamua kuwatia adabu mnaanza kulalamika. Acheni mauza uza tufanye mambo ya maana.
Acha niwape vipande vyenu. Tatizo la Kaya yenu si dini bali uduni na ujinga. Nasikia mibomu. Sijui nani kakojolea nani tena?
Chanzo: Tanzania Daima Oktoba 24, 2012.

Monday 22 October 2012

I love our chummy laws and their enforcement


This is the song of peace
It aims at all S.O.B's and D.O.B's
You guys in fatigues
With your totting guns
Trigger happy as you always are
You the killing machines,
You who violate peace
You who are used by morons
Guys,
When you kill, just kill peacefully
When you rape just do it peacefully
You venal and thievish nobles
When you steal just do it peacefully
Do even your corruption peacefully
For this is the hunk of peace
Peace in everything you do
Cops, officials and all courtiers
When you act, please act peacefully
I am talking to everybody
All sheep and hyenas
Noble and disgraced
Please observe peace
Again I should insist
That those suffering should not accept this
Stand up for your rights
Avoid and hate this elusive peace
Do your pacifism and passivism work hither?
Peace that leave in pieces
Just fight straight on and head on
Fight this Criminal Cabal of Murderers (CCM)
Fight all Coveted Oppressive Parloiners (COPS)
Fight all noble thieves and their majordomos
Fight fight everywhere
The poem above reminds me of the poem I wrote for myself when I found that I can’t do anything to prevent the dooms our people were being driven to.
In our good country and under our gentle laws, if you happen to be smart you can get away with it.
You can rob the public, indulge in capital flight, sabotage, receive kickbacks especially when signing such fat investment contracts and stash your money to offshore banks and nothing sinister can happen to you.
If you happen to use gun especially if you are a cop, you can shoot anybody you dislike under any pretext and nothing sinister can happen to you. You can sleep on the wheel if you are CEO of public business such as government and whatnot and nothing can happen to you. You can rig elections under the science of uchakachuaji and the heavens won’t fall on you. No law can reign on you even if what you are committing is pure impunity. This is why I like our gentle and humble laws. Again, don’t take our laws for a ride. They will not only ride on you but run over you especially if you contemplate stealing chickens or valueless things like receiving small kickbacks or indulging yourself in political ambitions under opposing parties; on this our law will nary treat you gently.
The other day I heard people shouting at the top of their voices that they’re not going to be counted during the national census. No law dealt with them. Others went a mile ahead as saying that they’d like their religion to be included in the census as if we were looking for priests and sheikhs. Again, our generous laws did not bite such people who were trying to use religious wisdom to gain political mileage. Under our generous laws, if you are smart or connected, you can do as you like without fearing anything.
I recently heard that some illegal immigrants came to the country and grabbed land and no law bit them. So too, I heard that some coveted illegals were even able to proselytize and nothing happen especially when they started preaching violence. Motorists enjoy our laws. Break them. The traffic officer calls you aside and you just valorize the law and that is that. Drug dealers know it well. Pay an officer at the airport handsomely and your cargo just passes sleekly.
True, our laws are almost generous to everybody except the wretched of the country. If you are an honourable MP you can sleep in the house, tell lies, do nothing to your constituency and the laws hug you instead of biting.
Sometimes back I heard some ballyhoos that the power that-be would take on thugs and drug dealers. Again, when it came to light that those guys were the funders of a certain powerful party this project was abandoned indefinitely. Who would like to cut the hand that feeds him? You can take this to the bank. Ask chaps like “the old man of vijesenti” Endelea Chenga and his pal Dr Idd Rashid. They’ll tell you how gentle, civilized and generous our laws are. You know what? It came to light that those guys stashed billions of dough abroad. Our laws, instead of biting them, they hugged them so as to be given even more ulaji in the house. Do you think I am making this up? Don’t sweat it. Ask Eddie Luwasha who was openly implicated in the Richman scam. He patriotically relinquished his PMship and went on becoming a chair of a powerful house committee plus being availed with all emoluments, pochopochos and whatnot all former PMs get.
To cut a long story short let me surmise saying long live our civilized and generous laws and the soft way they are enforced to see to it that we remain the hunk of peace.
Source: ThisDay Oct.,22 ,2012.

Saturday 20 October 2012

Serikali inamdanganya nani kuhusu mihadhara

    
   Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Saidi Meck Sadiki alikaririwa akisema kuwa serikali imepiga marufuku mihadhara ya kidini inayokashfu dini nyingine hadi hali itakapotulia. Mihadhara hii imekuwa ikiendeshwa na kushabikiwa na waislam hasa wa kada ya chini hasa wasio na elimu ukiachia mbali kudhaminiwa na wafanya biashara wengi wenye asili ya kiarabu. Huu ni upuuzi. Kwanini kuipigia mihadhara marufuku hadi hali itakapokuwa shwari wakati wameishakiri kuwa inakashfu dini za wengine? Kinachokera ni kwamba hawa wanaojifanya wahubiri hawana elimu si ya Ukristo wala Uislam bali njaa na kutafuta sifa. Kuna haja ya kufanya mihadhara kuwa kosa la jinai hasa wahusika wanaposhambulia dini nyingine au kutokuwa na elimu juu ya kile wanachohubiri.
        Hii imekuwa staili ya serikali yetu ya nguvu ya soda katika kupambana na matatizo. Leo tunaambiwa hata Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar (SMZ) nayo imepiga marufuku mihadhara ya wana Uamsho. Too late. Mwanzoni chini ya kihoro cha kutaka muungano SMZ iliridhia na hata kushirikiana na Uamsho kuhubiri chuki na dhihaka dhidi ya muungano ikidhani ingeweza kuwatumia kufikia ajenda zake bila kujua kuwa nao walikuwa na ajenda zao fichi. Maalim Seif Shariff Hamad alipigia upatu hili . Kwani hii imekuwa ajenda yake tangu akiwa CCM hata baada ya kufukuzwa CCM na kurejea kwa mlango wa nyuma chini ya kisingizio cha serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU) ambayo hata hivyo inamhusu yeye na si chama chake. Leo wamegundua janja ya kutumiana wanaamka na kuanza kupiga mihadhara marufuku. Yote hii ni matokeo ya kuwa na watawala wasioona mbali.
           Hakuna anayehitaji mihadhara katika maisha. Mbona mihadhara imeanza juzi juzi miaka ya 90? Mbona kabla ya hapo tulikuwa tunaheshimiana na kupendana. Kesho wataibuka wahubiri wa mihadhara wa Kikristo waanze kuonyesha udhaifu wa Uislamu na waislamu wataanza kuja juu na kuchoma makanisa kutokana na kutokuwa na subira. Je namna hii tutafika? Maana kila dini ina udhaifu wake. Ndiyo maana dini zote hupenda kuwaaminisha watu badala ya kuwaelimisha. Hivi kwa mfano mtu leo akija anaongelea maisha ya Khadija mke wa kwanza wa Mtume aliyemwamuru Mtume amuoe si watu mtakatana shingo bure?
            Wengi wa waendesha mihadhara ni watu wasio na kazi ambao kimsingi ni wanyonyaji. Hata Uislam kama utatafsiriwa vizuri unazuia ujinga huu. Sayydina Omar ibn Al- Khatab Khalifa wa pili alipiga marufuku watu kumaliza salat na kuendelea kupiga mdomo wakiswali taraweh badala ya kwenda kufanya kazi.
Ila baada ya Tanzania kuruhusu utapeli wa kutumia majoho ya dini, tumeshuhudia kuibuka utitiri wa mihadhara na madhehebu ya kikristo mengi yakiendeshwa na matapeli wanaotaka utajiri wa haraka.
Je serikali inamdanganya nani zaidi ya kujidanganya na kulea huu uhuni usio na faida kwa watanzania?

Friday 19 October 2012

Vurugu za kidini je ni akili kumfia Mungu asiyekufa na mwenye nguvu?

Kinachoendelea nchini Tanzania ambapo vurugu zimeishatokea kinaelezewa kama vurugu za kidini. Je ni kweli ni chuki za kidini au kukata tamaa kwa watu wetu? Nimejaribu kujihoji na kuhoji mantiki ya mtu ambaye ni kiumbe dhaifu kuliko vyote kuwa tayari kuua hata kuuawa eti kwa ajili ya ima dini au Mwenyezi Mungu. Nashindwa kuelewa kutokana na ukweli kuwa Mungu hafi ila binadamu anakufa. Je hapa wahusika hawasemi ukweli kuwa wanapambana kupata maisha bora kwa wote kwa kutumia mgongo wa dini? Kama tutamfia Mungu asiyekufa yeye Mungu atafanya kazi gani? Kwanini tufie dini zake wakati mwenyewe yupo anaangalia? Je sisi ni vichaa na mataahira au ni wajanja wenye hoja fichi? Wanangu nataka maoni yenu lau tujadili jinsi ya kulielekea hili. Maana tukilinyamazia litalimaliza taifa letu.

Kikwete toa tamko na msimamo wako





Ingawa wengi ambao tumekuwa tukikosoa staili ya utawala wa rais Jakaya Kikwete, tumeonekana wabaya. Ingawa lengo letu ni kumsaidia kufanya anachopaswa kufanya badala ya kugeuka kiguu na njia kila siku angani akizurura ughaibuni, tunaonekana wabaya. Hakuna ubishi kuwa nchi yetu sasa iko msambweni ikitishiwa kusambaratishwa na udini utokanao na ujinga, ukosefu wa ajira, usongo na husda kwa baadhi ya watu wetu tulioshindwa kuwaendeleza. Hapa ndipo unatakiwa uongozi wenye visheni na mipango madhubuti ili kupangua  janga hili la kujitakia. Kumekuwa na malalamiko kuwa serikali inatumia nguvu nyingi kupambana na upinzani badala ya kutimiza wajibu wake. Jeshi la polisi limekuwa jepesi kuwahi kusitisha mikutano ya upinzani. Bila kujua kuwa kuna upande mwingine ambao umekuwa ukiutumia udhaifu huu, sasa serikali inajikuta uso kwa uso na wahafidhina wenye hoja zao fichi. Je ni wakati wa utawala wa Kikwete kuwekwa kwenye mizani au kuumizwa na wale uliowadharau na kuwafumbia macho. Ingawa tunaona machafuko yanayoendelea kama matokeo ya udini, ukweli ni kwamba ni matokeo ya ufisadi, umaskini, ujinga, ufisi, uroho na kasumba.
Watu wetu wengi hawana ajira na hawajui kesho yao itakuwaje. Wamekata tamaa na wanaweza kutumiwa na yeyote awezaye hata kuwaahidi jibu achilia mbali kutoa hilo jibu. Hii ndiyo maana hot spots za vurugu ni kwenye makazi ya watu maskini kama vile Mbagala na siyo Oyester Bay wala Masaki. Walioko kule wana uhakika wa maisha wagombee au kuandamana kwa kitu gani?
Sasa Kikwete amerejea. Tumshinikize atoe mwelekeo wa taifa. Kwa mazoea yake ya kutojali unaweza kuambiwa kuwa kesho ana safari ya kikazi kwenda nje. Amekuwa akituchezea akili hivyo. Kila kukitokea matatizo Kikwete na genge lake wako nje wakitanua huku umma wetu ukiendelea kuteseka. Amekuwa akitumia jeshi la polisi kuzuia rabsha. Sasa ameishiwa hadi anaanza kutumia jeshi ambalo kikatiba kazi yake ni kupambana na maadui wa nje na si wa ndani.
Tumalizie kwa kumuasa Kikwete kuwa kama hatabadili staili yake ya kutawala ataiweka nchi pabaya. Ameacha mambo yajiendee ambapo kila tapeli anaweza kuanzisha dhehebu au kundi la dini kama walivyofanya Uamsho na Ponda Issa Ponda. Tunao wachumia tumbo wengi waliojificha nyuma ya majoho ya dini kutokana na kuujua udhaifu wa Kikwete. Rais Kikwete toa tamko na msimamo kuhusiana na mwelekeo wa taifa letu.
Mungu ibariki Tanzania.