The Chant of Savant

Sunday 18 November 2012

Makanisa yanayojengwa kwa pesa ya mafisadi ni safi?


Siku hizi jina la Mungu limeisha thamani. Linatumiwa na kila tapeli fisi na fisadi kujipatia riziki au umaarufu. Hapo juu waziri mkuu aliyeondolewa madarakani na kashfa ya Richmond, Edward Lowassa akishiriki harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa kule Manyara.
Katika tukio hili Lowassa alitoa mpya kwa kusema kuwa Tanzania inaweza kutoa elimu ya sekondari bure. Kauli hii iliwashangaza wengi wanaojua matendo ya Lowassa hasa alivyosaidia kampuni feki kujipatia mabilioni ya shilingi. Pia wanashangaa kwanini Lowassa analiona hili baada ya kuondoka madarakani. Je huu si unafiki na ubabaishaji wa kawaida na kutafuta sifa?

1 comment:

Anonymous said...

we mpagani achana na watu wejenge makanisa wacha chokochoko