The Chant of Savant

Sunday 26 May 2013

Tuwakumbuke na kuwaombea ambao hawakujaliwa watoto

Huwa nawakumbuka na kuwaombea wale wote ambao hawakubahatika kama mimi katika maisha. Kwani yote maisha na ajuaye ni Mungu. Tulivyo si matokeo ujanja wala  ujinga wetu, si uzuri au ubaya, ubora wala udhaifu bali yote ni mapenzi ya Mungu. Kwa ufupi, huu wimbo Favour wa Methias Mhere unaongelea hayo ingawa kwa ufinyu kwa kuangalia mali na watoto. Uhai, ufu, mafanikio hata maanguko vyote ni matokeo ya maisha ambayo kwetu ni zawadi kama si ajali.
Nawatakieni tafakari njema huku tukiwakumbuka ndugu zetu wa Mtwara waliojaliwa neema inayoanza kugeuka nakama kwao kutokana na kutawaliwa na mafisadi na watu wenye mawazo mgando waroho na wenye roho mbaya.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Nimependa maombi yako. .
Nipo katika haya maombi

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Da Yacinta nimefurahi kusikia kuwa tu kwenye the same page. Yeah. We need to pray for our colleagues who have nary been gifted with children and other amenities they badly need in life.