The Chant of Savant

Wednesday 31 December 2014

Happy New Year 2015


For some a few hours are left just for the New Year 2015 to kick in. Others are just a few minutes away from New Year. We, once again, wish you all a very spiffy and prosperous New Year 2015.

Bado serikali ya Kikwete si ya Ubia?

Japo rais Jakaya Kikwete huwa haishiwi vituko au mazingaombwe au sanaa kama watani zake wapendavyo kusema, juzi aliwaacha wengi hoi. Alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipoulizwa na Kamati ya Bunge alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL.” Kama fedha kweli ni za IPTL na si mizengwe na upotoshaji, ilikuwaje Kikwete huyu huyu akamfukuza kazi Anna Tibaijuka waziri wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi? Je ilikuwaje Kikwete huyu huyu akakubali kujiuzulu kwa mwanasheria wa serikali wa zamani Jaji Fredrick Werema? Je Kamati ya Bunge iliyofichua kashfa nzima na kugundua kuwa fedha ya umma ni uongo au uvumi kama alivyowahi kusema Tibaijuka wakati akijitetea asijue ataenda na maji? Je inakuwaje Kikwete aone fedha za IPTL asione za umma alizosema CAG kuwa zilikuwa kwenye escrow? Je ameishakatiwa chake?
Je anachosema Kikwete ndiyo msimamo wake na serikali yake au atabadilisha lugha kama alivyokaririwa akisema wakati akimwajibisha Tibaijuka aliposema, “Tumezungumza na Profesa Tibaijuka na tumemuomba atupishe ili tuweze kuteua waziri mwingine kwani viashiri vyote vinaonyesha kuwa alikiuka kanuni na sheria ya maadili ya Umma.” Je haya maadili ya umma anayosema Kikwete ni yapi wakati mgao wa fedha aliyopewa Tibaijuka ni fedha ya IPTL?  Rais anatuma ujumbe gani kati ya anachosema kuhalalisha fedha ya umma kuwa ya IPTL anayodaiwa kuisaidia kuingia nchini akiwa waziri wa Nishati na Madini na kile kinachosemwa na Bunge kuwa fedha ni ya umma?
Kimsingi, kama Kikwete hatakanusha madai yake, ni dhahiri, kuna mgongano baina ya mihimili mitatu ya dola jambo ambalo ni hatari sana. Je Kikwete ameshindwa kutangaza mgogoro huu hadi akaamua kutumia lugha ya mafumbo? Je ni wangapi wanauona huu mgogoro ambao unaweza kulizamisha taifa kama siyo kuliingiza kwenye machafuko pale ukweli utakapojulikana? Je Kikwete amejipa usemaji wa IPTL au ni kutimia madai ya CHADEMA kuwa alikuwa akipokea amri toka kwa James Regamalira juu ya jinsi ya kushughulikia kashfa ya escrow bila kuumiza maslahi yao? Je Kikwete ni mwenye shea kwenye IPTL au IPTL ina shea kwenye serikali yake? Kuna mantiki katika kuhoji. Kwanini serikali ya Kikwete ilikaa kimya sana wakati umma ukihanikiza watuhumiwa wa escrow washughulikiwe? Kama hakuna ubia ilikuwaje Kikwete akadharau hata mapendekezo ya Bunge kwa kuwawaweka kiporo kingpin au wawezeshaji wakuu wa wizi mzima?
Wengi wanahoji mantiki ya rais kuhalalisha wizi wa fedha za umma. Kama fedha ni za IPTL, je ushahidi wote uliotolewa na kamati ya Bunge ni uongo mtupu?  Inahitaji nguvu ya ziada kuwashawishi watanzania kuwa fedha ni ya IPTL. Fedha ni ya Watanzania. Kikwete anasema hakuna hasara. Hasara ipo tena kubwa.
Kwa waliofuatia sakata zima la escrow watakubaliana nasi kuwa watu kama waziri mkuu Mizengo Pinda, Saada Mkuya, Profesa Benno Ndullu na wengine waliotajwa wana ubia kwenye serikali. Maana hawakuwa na sababu ya msingi kubaki maofisini wakifanya madudu yale yale. Hivi mantiki ya kuendelea kulumbana juu ya uhalali wa mmilki wa fedha ya escrow ni yapi wakati tumeishaanza kuwachukulia hatua baadhi ya wadau wa kashfa husika? Je nini mantiki ya kuwaacha watuhumiwa wakuu yaani James Rugemalira na Harbinder Sethi Singh kuendelea kuchezea mahakama zetu kama si kuwa na ubia kwenye serikali husika? Hivi hili nalo linahitaji PhD in Political Science?
 Marehemu baba wa taifa aliwahi kulalamikia CCM kutekwa na mafisadi asijue watateka kila kitu. Baada ya kuiteka CCM wameteka na serikali yake kiasi cha kuwa mtumishi wao aliyewasaliti wananchi. Haiwezekani kila mwaka utokee ufisadi wa kutisha serikali isiushughulikie iwe haijatekwa na kufungiwa kwenye mifuko ya mafisadi wanaowakatia viongozi wetu zawadi za kipuuzi kama vijisenti vya ugolo, suti, saa na upuuzi mwingine. Serikali ya Kikwete haiwezi kujidai kuwa si ya ubia. Uliza, wauza unga majambazi na wahalifu wengine wamefanywa nini na kwanini? Kuna watu wanajulikana. Utajiri wao ima umetokana na kuuza unga au ujambazi na jinai nyingine. Nani anawawagusa zaidi ya kuwa wafadhili wakubwa wa CCM? Mfadhili mmojawapo wa CCM anayetafutwa na vyombo vya kimataifa ni Alex Massawe ambaye kama si vyombo vya kimataifa kuingilia kati angekuwa huru akiendelea na ujambazi kama kawaida.
Kuonyesha IPTL ilivyo mbia wa serikali ya Kikwete, vyombo vya habari vimeripoti matukio ambapo mtuhumiwa anayejifanya kuimilki IPTL inayosemakana kupatikana kinyume cha sheria Harbinder anaonekana akimwaga fedha kwa jeshi la polisi linalopaswa kuchunguza uchafu wake. Je jeshi kama hili linalofadhiliwa na fisadi kama huyu linaweza kumchukulia hatua? Kibaya zaidi, unapoona wakubwa wa polisi wakipokea msaada wa fedha toka kwa fisadi kama huyu usidhani mambo yanaishia hapo. Nao lazima wakati chao binafsi.
Kwa tabia na mazingira tajwa hapo juu, ufisadi na utawala vinafunga ndoa na kutenda na kuishi pamoja kama ilivyo sasa ambapo rais anapata kigugumizi kuwatimua hata mawaziri wachache waliotolewa kafara kunusuru serikali yake. Hata ukiangalia sakata zima lilivyoshughulikiwa kwa papara na Bunge unagundua aina nyingine ya ubia kwenye vyombo vingine vya dola.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 31, 2014.

Kijiwe chalaani mizengwe ya escrew


          Leo Msomi amejilawa kweli kweli. Anaingia akiwa ameweka ndita usoni huku akiwa amevaa magunia. Leo wanakijiwe wote wametinga kwenye magunia, kwa mara nyungine, kama alama ya kuombolezea kaya yetu inayoliwa huku ikiojiona.
          Msomi hata aamkui zaidi ya kumwaga usongo wake. Anakwanyua mic na kuchonga, “Wapendwa, kwanza najua mna majonzi kama yeyote ambaye si fisadi wala nepi yao. Pili, najua mna maswali mengi kuliko majibu kuhusiana na usanii na ujambazi vilivyotokea. Tatu, najua mnalaani jinai yote tena kwa herufi kubwa.  Nne, hebu tujifariji kwa lau kufanya kile ambacho wataalamu wa utatuzi wa migogoro yaani Conflict Resolution Studies professionals huita venting au kumwaga usongo. Je mnakielezeaje kigwena cha tarehe 21 Desemba baina ya Njaa Kaya na wazembe wa  Dar si Salaama?”
          “Yakhe wantibua sasa. Unfurahisha ulipoita ule mkusanyiko kigwena. Ungeongeza: kile kigwena cha kuhalalisha haramu na ujambazi kayani wallahi. Sijui hawa watu wameingiliwa na nini! Wafanywe nini na vipi ndiyo wakengeuke wajue wakati wabadilika?”
          Kabla ya kuendelea Mgosi Machungi anampoka mic na kuronga, “Hakuna kitu kiiniumiza kama kuona wae wote walioiba njuuku yetu kuwekwa eti kipoo utadhani ni ughai. Yaani huyu anadhani kumtoa kafaa poofwesa Ana Kajuamlo Tiba atatuliza mizuka yetu? Lazima tikubaiane jinsi ya kuwashughuiikia hawa wezi.”
          Mijjinga ananyakua mic, “Yule mama aliniudhi kuitisha mkutano wa waandishi wa umbea na kujitapa eti hakuwa na hatia na hivyo asingewajibika kwa kuhofia eti kutoitendea haki dhana nzima wakati alinuka na kuchafuka kulhali. Kusema ukweli nimefarijika kuona alivyotimuliwa kama mbwa koko. Halo halo nenda Ana nenda tu wala usilalamike.”
          “Hapa ndipo Njaa Kaya kawapiga wadanganyika changa la macho. Hukuona watumiwa wazembe wa Dar walivyolipuka kwa shangwe wasijue wanashangalia maafa yao. Shame on them all! Yaani tumekubali kafara ya ngurumbili moja wakati kuna mamia nyuma ya pazia!” Anazoza Mipawa.
          Kapende anapoka mic, “Inashangaza pamoja na unshomile na uporofwesa wake hakuliona lililokuwa likimjia ukiachia mbali kutumiwa na mafisadi kama nepi na zana. Kwanini hakujinyamazia kama kondoo akangoja kuliwa huku akitulia tuli kama alivyotulizwa na Jimmy Rugemalayer ambaye alimchengua hadi akampa vijisenti vya ugolo?”
          Mbwamwitu anadandia mic na kupayuka, “Huyu bi mkubwa kiboko! Anamchengua fisadi hadi anamkatia bilioni na ushei! Sijui alimfanyia vituz mtindo upi tapeli huyu hadi akamzimia hivyo! Hata hivyo namuona mjanja. Maana huo mshiko ni mkubwa kuliko hata marupurupu ambayo angepewa baada ya kumaliza ngwe yake kama waziri.”
          “Nyie hamjui, nyuma ya pazia yanafanyika mambo hadi watu wanakatiana mishiko mizito. Nisichoelewa hadi sasa ni mantiki ya kuweka wezi wakubwa viporo. Je huyu bibie kaponzwa na kiranga chake cha kujifanya anajua falsafa hadi akanonihino bila kuchamba au ameisuka na bingwa wa sanaa ili kuokoa jahazi? Maana hakuna anayeongelea tena zile bilioni 400 wala kushinikiza mibaka husika inyongwe kama siyo kuvuliwa nguo na kufanyiwa kitu mbaya.” Anazoza Mipawa huku akiwasha sigara kali.
          Kanji kapata upenyo. Anakula mic, “Pawa veve kosea sana. Hapana pendekeza vatu fanyia kitu baya venzao. Hii si tawala ya sheria.”
          Kapende anamkwapua mic Kanji na kuchonga, “Peleka tawala yako ya sheria India. Wewe unaona kuhalalisha ujambazi na ushenzi ndiyo utawala wa sheria? Utawala wa sheria ilikuwa ni kuwanyonga hawa gendaeka lau tupumue. Maana wamezidi.”
          “Nani amnyonge nani wakati wote ni nyani wakifanya unyani wao? Nadhani huyu mama nshomile ameponzwa na domo lake kuongea bila kuwasiliana na kichwa. Jitu limepokea mshiko wa wizi tena kwa kutoa huduma chafu halafu linasema eti halioni kosa.” Msomi anaongea kwa hasira.
          Kabla ya kuendelea Mheshimiwa Bwege anachomekea, “Msomi una maana bi mkubwa alimkatia mavitus Jimmy na Jimmy akaamua kumkatia pochi siyo?”
 “Who knows? Lolote lawezekana hasa ikizingatiwa kuwa bi mkubwa ni open check usawa huu? Maana katika tambo zake zote za kutowajibika hakutaja mshiko wote mzito kama huo alipewa kwa kazi gani. Bila shaka ni kazi ya siri isiyopaswa kujulikana.” Msomi anajibu huku akijiweka vizuri kwenye benchi.
          Sofia Lion aka Kaungaemba kashika pabaya! Anamnyang’anya Msomi mic kwa hasira na kuzoza, “Una ushahidi na unachosema au unadhani wote ni kama wewe kuvutiwa na mambo ya nguoni?”
          “Kama unataka ushahidi nenda kawaulize waliokatiana. Kama si hivyo mbona wahusika hawataji walilipana nini na kwanini?” Mzee Maneno anaamua kumjibia Msomi anayebaki kutabasamu.
Kepende anapoka mic mic na kusema, “Nadhani dada Sofi anajiumiza bure. Hivi yeye angeahidiwa njuluku lukuki hivi angebania?”
          Msomi huku akicheka anachomekea, “Muulize Sofi. Nadhani analo jibu.” Baada ya kuona Sofia amekaa kimya Msomi aliendelea, “Mie hakuna waliponiacha hoi hawa mafisadi kama kumtoa kafara porofwesa na kuwaacha wezi wenyewe wakitanua. Nani anahimiza Muongo, Ndururu, Mkuyati, Endelea Chenge hata Njaa Kaya wawajibishwe wakati ndiyo wenye dili zima? Tungeachana na dagaa kama Porofwesa na kuwashughulikia papa hawa kwanza ingeleta maana.”
Kijiwe kikiwa kinanoga si alikuja Ana Kajuamlo Tiba kutuhutubia akitubia. Tulimkamata na kumpeleka kwa Rugemalayer akamtulize na kumkatia tena.
Chanzo: Tanzania Daima Desemba 31, 2014.

Tuesday 30 December 2014

Leo nimemkumba Samira Said wallahi


Huu wimbo ni zawadi ya mwaka kwa viongozi feki wa dini

Tokana na kutamalaki kwa utapeli kwa kutumia jina la Mungu, blog hii imeamua kutoa wimbo huu kama dedication kwa wote wanaoibiwa na matapeli wa kidini kwa kutumia mbinu mbali mbali kuanzia kutenda miujiza, kutabiri, mihadhara,kupanda mbegu, kufukuza majini, kuombea taifa na nyingine nyingi. Ni vizuri watu wakaacha imani za kibubusa ambapo wanageuzwa mashamba ya bibi na matapeli wanaojificha nyuma ya neno la Mungu. Taifa letu linaanza kugeuka la kishirikina kiasi cha kuhitaji magwiji wa fikra na falsafa kuingilia kati. Haya ndiyo matokeo ya viongozi wenye uoni mfupi na watokanao na jamii za kishirikina.

Tuisaidie CCM kulikomboa taifa


          Kwa hali iliyo, ni dhahiri. Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya uongozi wa mwenyekiti wake, rais Jakaya Kikwete, kimeanzisha, bila kujua, safari ya kulikomboa taifa toka kwenye mikono michafu ya utawala mbovu na fisadi. Najua unayesoma makala hii unafanya hivyo kwa mshangao. Unajiuliza: CCM iliyozamisha taifa hili inawezaje kulikomboa tena dhidi ya nani zaidi ya CCM yenyewe.
          Kama tutaangalia utendaji mbovu wa serikali za CCM kuanzia awamu ya pili, tutakubaliana kuwa CCM imejenga mazigira mazuri ya kutupwa nje ya madaraka kwenye uchaguzi ujao. Hili linategemea mwamko wa wapiga kura na jinsi wanavyochambua na kuona madudu yanayoendelea. Pia inategemea uoni wa umma juu ya umuhimu wa kutumia njia ya kidemokrasia kuondoa utawala mbovu ambao hauna cha kujivunia zaidi ya kulinda na kutenda maovu. Rejea kutamalaki kwa wizi wa fedha za umma na uhujumu wa taifa kwa ujumla kupitia ufisadi.
          Kama watanzania hasa wapiga kura wataamua kujikomboa, bila shaka, watapigia kura upinzani ili kuiunga mkono CCM katika kuiondoa madarakani kwa njia ya kuinyima kura a kutoiruhusu kuendelea kuchezea chaguzi zetu kupitia mtindo iliouasisi na kuuzoea wa uchakachauaji. Matokeo ya hivi karibuni ya uchaguzi wa serikali za mitaa ni kiashiria kuwa kama umma ukiamua unaweza tena kwa siku moja tu. Pamoja na ushindi mwembamba wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ikilinganishwa na tulikotoka ambapo CCM ilizoea kushinda asilimia tisini ya viti vyote, si haba, tunasonga mbele. Muhimu, tusiridhike na huu ushindi kidogo bali tuuendeleze kwa kuzidi kuinyang’anya CCM viti vingi hasa kwenye ubunge ili tuwe na Bunge linaloweza kuiwajibisha serikali wakati wowote.
          Kama tulivyosema hapo juu, CCM, tangia awamu ya pili haina cha kujivunia zaidi ya utiriri wa kashfa zenye kuendelea kuwafanya watanzania kuwa maskini pamoja na kujaliwa raslimali lukuki. Je kikwazi ni nini? Je tuendelee kuilamu CCM iliyokwishajichokea na kuonyesha wazi kuhitaji kupumzishwa au ujinga wa wapiga kura kuchagua kitu kile kile wakitegemea matokeo tofauti? Hakika, hapa ndipo ilipo sababu ya kusema kuwa CCM isaidiwe katika kulikomboa taifa, ipigiwe chini kama wasemavyo watoto wa mjini. Inashangaza na kuchukiza kuona chama ambacho kimeiweka nchi kwenye mifuko ya mafisadi na wezi kila aina kuendelea kushinda. Je kwa kuipa kura CCM hatushiriki jinai zote inazotenda? Je hapa nani alaumiwe hasa ikizingatiwa kuwa hakuna serikali inaweza kuwa madarakani bila ridhaa ya serikali?
          Rais Kikwete, kwa makusudi au bahati mbaya, kwa kukosa uwezo au kutojua, ameruhusu serikali yake, kwanza, kuridhi uchafu wa serikali iliyotangulia. Na pili, ameruhusu serikali kuwa mshirika wa maovu wakati ilipaswa kuyapiga vita. Rejea kashfa ya EPA ambapo fedha ya umma iliibwa na kutumika kuwahonga wapiga kura na kuingiza awamu hii. Nani anabishia hili? Rejea kutuhumiwa kwa rais Kikwete na Benjamin Mkapa kuwa nyuma ya EPA na kitendo chake cha kutotaka kuongelea tuhuma hizi.
          Tukio la kuonyesha wazi kuwa CCM imeasisi ukombozi wa taifa ni kashfa ya escrow ambapo shilingi bilioni 400 ziliibwa toka kwenye fedha ya umma. Baada ya kufichuliwa jinai hii, Kikwete wala hakuhangaika kutoa maelezo wala kuchukua hatua hadi wafadhili walipoamua kumtolea uvivu wakatoa shinikizo awawajibishe watuhumiwa ingawa hajafanya hivyo zaidi ya kumtoa kafara waziri wake wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Anna Tibaijuka kwa kosa la kukatiwa shilingi bilioni 1.65 huku wanaotuhumiwa kusomba fedha husika kwenye viroba na maboksi akiendelea kuwaweka kiporo. Hii ni nini kama siyo kuwaonyesha wananchi kuwa ameshindwa na hivyo wamwajibishe na chama chake?
          Bahati mbaya sana, pamoja na Kikwete na serikali na chama chake kutoa taarifa rasmi ya kushindwa, Bunge lilifurukuta likaishia kujiaibisha baada ya kushindwa kushughulikia serikali nzima na badala yake likashupalia maajenti wake. Baada ya kuhitimisha uchunguzi na mjadala hata kwa kumtaka Kikwete awawajibishe hao wachache waliotolewa kafara serikali yake, Kikwete aliendelea kupuuzia kutekeleza maazimio ya Bunge akijaribu kungoja wafadhili watulize hasira zao aendelee na utamaduni ule ule wa kulizamisha taifa. Rejea matamshi yake ya hivi karibuni alipokaririwa akisema, “Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipoulizwa na Kamati ya Bunge alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL.” Bunge limesema fedha hii ni ya umma, Tume ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) imesema fedha ni ya umma na Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa fedha za serikali (CAG) amesema fedha ni ya umma. Kikwete anapata wapi jeuri ya kusema fedha ni ya IPTL ile ile anayotuhumiwa kuiingiza nchini na kuiruhusu iendelee kuliibia taifa kama siyo kuwatukana watanzania matusi ya nguoni? Je watanzania hasa wapiga kura wanataka watukanwe vipi au kuguswa wapi ndipo wastuke, kuchukia na kuifurusha CCM ili kulikomboa taifa? Je hapa bado tunailaumu CCM kwa kutuonyesha uovu na uhovyo wake au kujilaumu kwa kushindwa kuitimua madarakani? Je hili nalo linahitaji wafadhili au kuamua kujikomboa vilivyo?
          Tumezidiwa akili na wenzetu wa Kenya ambao waliitimua KANU madarakani tena kwa sababu ya kashfa moja ya Goldenberg tofauti na sisi ambapo tuna kashfa lukuki? Wengi walitegemea angalau umma uingie mitaani kulazimisha serikali iondoke kama walivyofanya wenzetu wa Burkina Faso hivi karibuni. Hili halikuwa tokana na woga wetu na kudanganywa kuwa hii ni nchi ya amani. Amani gani wakati wachache wanaiba watakavyo huku umma ukiendelea kusikinishwa na jinai hii? Je hapa tuilaumu CCM au tujilaumu?
Chanzo: Dira Desemba 29, 2014.

Saturday 27 December 2014

Go Tibai-juka go

Prof Annae Kajuamlo Tiba-ijuka former minister for Lands, Housing and Human hoo-ha is a very interesting character. She’s offered a whopping 1.6 billion dafus from the guy who called 75 million bucks vijipesa vya tumbaku. Such humongous  hush-hush dosh’s no a joke especially for a bint-Adam from the ever-begging-and-loaning hunk like Bongolalaland. After being cornered (linked with escrew dosh), she dashed out saying: She’s innocent! Trapped and exposed, she’s quoted as jittery saying, “I don’t see any reason for me to step down because up to now the government has not declared that I am guilty.  I will only resign if it is proven that I am guilty.” Wow! Didn't you see any culpability in receiving dirty dosh dear? Why? Does it really need a PhD in law to grasp whether you’re guilty or not madam? She says that the powers that be have nary declared her guilty as if it is the court of law. Again, boozers have already declared you guilty. Thus, you’re supposed to hit the road the day your dirty linens were exposed. Mind you. The dosh in question doesn’t belong to the govt. It belongs to the boozers who wanted you to bow down ASAP.
          To tarnish things a great deal more, Tiba added salt to injury saying, “I will not resign because the state has not declared that I was given dirty money, but I will step down if only the above management will declare that it was some of those dirty money or when I will be charged into the court of law. (Sic).” Phew! Didn't you know that the dosh you received was, and still is, dirty, PILLAGED ONE!!?? What type of PhD do you've to fail to know such simple things?
Saying that you didn't feel any guilty till the powers that be declare so was but hooey!  Saying that the dosh you received was meant for development is hogwash. How many private school owners were given the cut? What type of development is attained by looted dosh and for whom? Again, why was the dosh deposited in your personal account in lieu of school account? The dosh’s yours but it doesn't belong to the school. If it were meant for the school, it’d be wired through school account. Rightly so, you seem to be in a slumber and a state of denial. Pack it in, and vanish to stupor after messing big time. Why don't you tell us why you're given this rancid dosh and what for if you think you’re innocent?  In law, an actual doer or an accessory are all equally guilty, simple. If you think a public office’s your private one you must have goofed a big time dear. Weep not for the milk you spilled yourself thanks to your “greed for development.” Go sister go. Maybe, dosh-disher Rugemalayer’ll employ you. It was the right time for you to pack and go just like Judge Freddie Werema, who, like you, vowed to nary bow down. What happened thereafter? Instead of staying put, he ended up licking his vomit. Time for you to cascade from grace is now.
You might see no crime committed by being wired dosh for doing nothing. Again, nothing’s for free. You must have offered some services to Rugemalayer. I remember. When the scam surfaced you said that Rugemalayer’s your brother. Well. Well. Why are you the only sister that appears in the list of the bigwigs he corrupted? Are bishop Method Kilainy or/and Emmy ole Kambanene his brothers too? Prof, go tell it the birds. There’s something fishy and smelly.
Dear Prof, when you survived another scam after promising to bring down the killer building in Indians’ street and failed, boozers wanted you to hit the road. You applied Ping-Pong and survived. This you goofed. Again, how dare you call Parliamentary report mere rumours?  Isn’t this insulting the parliament, the boozers who entrusted their power in the hands of MPs even President that you forced to fire you unnecessarily?
For the person drummed to even run for the highest office in the land to land in such mud is indeed telling. Sometimes, greed, myopia and selfishness can make schooled Homo sapiens more unschooled ones. How come that escrow seems to have sunk many Profs than others? Is our education wanting or the victims are fake Profs?
Is it true that your “bro” Ruge donated the dosh to your private school? Doesn't owning a private school create conflict of interest mheshimiwa? Is real your aim development as you asserted or just using a school as a ruse to mint dosh? How many shule za kata do you have in your constituency that needs less than such dosh but you didn't even remember to offer a little to?
In sum, I bade you farewell but blame nobody except yourself. If you think you've been offended then you can sue the parliamentary committee or ask your boss to start a fresh investigation that’ll vindicate you. Otherwise, clinging into denial and far-fetched innocence won’t do you good. Again, what were you waiting for Prof?
Source: Guardian Dec., 28, 2014.

Mlevi aomba ateuliwa mwanasheria mkuu


Baada ya jamaa yetu tuliyemtonya kuwa alivyokuwa akifanya sivyo, jaji Freddie We-rema kuachia ngazi kwa aibu na kuzomewa, mlevi anataka kuomba ateuliwe kuziba pengo lake ili aisafishe kaya. Japo huwa mlevi si mpenzi wa vyeo vya kuteuliwa ambavyo mhusika asipoangalia humfanya awe wa kujikomba badala ya kukomboa walevi, ana mpango wa kuomba rungu hili ili awakomeshe wote wanaowahujumu walevi haraka sana iwezekanavyo. Anataka kurejesha heshima ya kaya toka kuwa shamba la chizi kwenda kuwa kaya ya kuogopwa, kuwajibika na kuheshimika.
Nikishaapishwa, nitahakikisha wote waliokwapua njuluku za escrew na nyingine kama vile EPA wananyea debe kwenye magereza yote kayani bila kujali nyadhifa wala mitandao yao. Sitakuwa tayari kuwekwa mfukoni wala kumwangalia nyani usoni. Hivyo, wale wote wanaojijua walifanya monkey biz wajiandae kufia lupango.
Nitahakikisha nafunga yeyote atakayetuma njuluku kwenye akaunti yangu bila kujali ametoa mamilioni au mabilioni.
Nitahakikisha mabenki yanayosaidia wizi na utoroshaji wa njuluku za umma yanafungiwa na kufilisiwa mara moja huku wakubwa zake wakiishia lupango. Nataka nipige kaya msasa na kuanza upya kuanzia chini hadi juu. Jamaa waliozoea kutoroshea njuluku India na Dubai na Uswazi wakae mkao wa kuliwa.
Nitapendekeza kwa dingi watuhumiwa wachunguzwe na watakaopatikana na hatia wanyongwe ili liwe somo kwa wengine waliogeuza kaya shamba la bibi. Pia nitapeleka mswada bungeni kubadili sheria za sasa zinazowalinda majambazi, wauza unga, mafisadi na waharifu wengine wote.
Pia nitapeleka mswada mwingine bungeni kuhakikisha kiongozi yeyote atakayebainika au kuondolewa madarakani kwa vitendo vya kifisadi asilipwe marupurupu yoyote wala stahiki yoyote kwani hakufanikisha kile alichokuwa ameapa kutekeleza. Hivyo, watu kama Were na Eddie Ewassa watakoma kupokea marupurupu. Hivi ni aibu na uzezeta kiasi gani au tuseme ufisadi wa kimfumo kumlipa mtu marupurupu wakati alitenda jinai? Hizi ni akili au matope? Ukiwanyima maulaji na makandokando yake unakuwa umetoa onyo kwa wote wanaofuata kuwa atayakwapua hatapeawa kiinua mgongo baada ya kuibia kaya.
Pia nikiwa mwanasheria mkuu nitahakikisha maadili ya uongozi yanarejeshwa ili kuondoa huu ujambazi wa madili uliochukua nafasi ya maadili. Nitawaomba wahishimiwa warejeshe Azimio la Arusha na kutangaza kifo cha Azimio la kijambazi la Zenj lilipotishwa na wale marehemu mzee Mchonga aliowaita wahuni. Nadhani wote waliofanya hivi wanakumbuka walivyoingiza kaya msambweni kiasi cha kugugunwa na kila matapeli wa ndani na wa kigeni.
Nitahakikisha nawasaka wote waliotoroka kaya kwenda kujificha nje ili wasikamatwe. Nitarejesha wale wanyama waliosafirishwa kwenye Qatari.
Nitapeleka mswada mwingine wa kuwabana wanakaya wote kutangaza mali zao na jinsi walivyozipata. Zoezi hili litafanyika kila mwaka na atakayekaidi kutangaza utajiri hata umaskini wake anafungwa jela miaka kumi.
Kimsingi, nataka nijulikane kama mwanasheria mkuu wa mageuzi ya kisiasa na kiuchumi. Pia nitahakikisha wale wote wanaotumia fedha na ofisi za umma vibaya wanakiona cha mtema kuni. Tangia nitakapotia mguu ofisini, ziara za hovyo hovyo za wazito kwenda ughaibuni zitageuka historia.
Pia nitahakikisha nashirikiana na mamlaka za Uswizi kurejesha njuluku zote zilizofichwa kule. Kwanza, nitamwomba msamaha balozi wa Uswizi bwana Olivier Chave tokana na vitisho alivyofanyiwa na Were. Baada ya hapo ni kukusanya taarifa za wezi wote na kuhakikisha wananyea debe bila kumwangalia nyani usoni.
Nikimalizana na walioficha njuluku ughaibuni, nawageukia wauza bwimbwi. Nitaanzia kwenye mipaka na viwanja vya ndege kwa kuwakamata maafisa wote wanaojulikana kwa kuruhusu madini na mibwimbwi kupita bila kujali koo zao au mitandao yao. Nitahakikisha nafukuza hata watumishi wa wizara ya mambo ya kaya wanaosifika kuuza pasi zetu za kusafiria kama njugu kwa wauza unga na wazamiaji.
Pia nitapeleka mswada bungeni kubadili sheria ya uchaguzi ili kuondokana na uchakachuaji unaozalisha viongozi wabovu. Nitapendekeza katiba iandikwe upya huku madaraka ya dingi nayo yakipigwa panga. Nitaamuru wote walioshiriki kwenye mauaji ya rasimu ya Jaji Jose Waliobora wakamatwe na kuwekwa lupango huku wote waliohudhuria vigwena vya kupitisha katiba mchakachauo ya kifisadi wanarejesha njuluku zao na kufungiwa kugombea cheo chochote kwenye kaya yetu.
Kuhakikisha mjengoni kunafanyika kazi inayotegemewa na walevi, nitapeleka mswada wa kuwatimua mjengoni na kuwanyang’anya uhishimiwa waishiwa wote watakaolala mjengoni au kutuhumiwa kuomba au kupokea rushwa toka kwa mafisadi kuanzia wale wa serikali za mitaa hadi wachukuaji waitwao wawekezaji.
Mwisho, nitahakikisha kampuni jizi la IpTL, Dowanis, na mengine mengi yanafungiwa huku wakubwa zake wakiozea lupango baada ya kufilisiwa.
Pia napanga kutoa pendekezo la kubadili sheria za ajira ambapo watumishi wa umma wanaotuhumiwa kufanya madudu kama wale walioidhinisha kujengwa kwa mghorofa wa uhindini ulionyotoa walevi wanahukumiwa kifo tena cha kupigwa mawe huku mafisadi ambao kwangu wataitwa mibaka watachomwa moto kama vibaka wafanywavyo.
Kitu kingine ni kwamba nitarekebisha mikataba yote ya uwekezaji hasa kwenye madini na nishati. Hapa wale wote waliowahadaa na kuwatisha walevi kuwa mikataba haiwezi kuonwa na bunge wangoje kitanzi siku nitakapoingia ofisini.
By the way, mmeona iron lady wa vijisenti vya ugolo alivyopigwa teke pamoja na kusema kuwa asingeenda popote utadhani ndiye mwenye ulaji. Tunangoja kusikia atakachosema baada ya kupigwa panga huku wengi wakitaka kujua kama atarejesha uchache wetu au kuishia nao. Pia hili la Muongo na wenzake kuwekwa kiporo kama linakera na kuchanganya. Nani anataka watendaji viporo wanaowekwa viporo ili kuwa re-cycled baadaye? Je Tiba baada ya kuonyeshwa mlango atateuliwa kwenye bodi za ulaji au ubalozi. Let’s wait and see. Nawatakieni Heri ya Mwaka Mpya wenye kila fanaka hasa kujisuta na kubadilika na kuacha kuwa waangaliaji wakati kaya ikiibiwa bali wachachezaji mitaani kama jamaa zetu wa Burkina Faso.
Chanzo: Nipashe leo.

Thursday 25 December 2014

Nukuu mbovu za mwaka 2014

“Watanzania tumejaa ubinafsi, kila mtu anafikiria kila anafanya jambo anategemea kupata posho, na niwahakikishieni mimi sina uchu wa ubinafsi wala tamaa za vyeo kwani kama ni cheo nilichoacha UN kilikuwa kikubwa zaidi,” Profesa Anna Kajumlo Tibaijuka. Hii nukuu imechukua nafasi ya kwanza kwa ubovu kwanza, kutokana na hadhi ya aliyeitoa kielimu. Na pili mjumlisho wake. Hivi huyu hakusoma kanuni na miiko ya uwasilishaji taarifa? Je hajui kuwa mjumlisho ni kiashiria kikubwa na cha juu cha ujinga? Inakuwaje profesa mzima anasema eti watanzania wote wana ubinafsi wakati yeye anayesema si mbinafsi ni mtanzania? Unawezaje kusema "kila mtanzania" utadhani umeongea na watanzania wote? Angalau angetoa hata takwimu lau kuficha ujinga na ujuha wake.
“Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipoulizwa na Kamati ya Bunge alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL,” Rais Jakaya Kikwete. Je kama fedha ni za IPTL ni kwanini umekubali kujiuzulu kwa Mwanasheria mkuu wa serikali na kumtimua waziri wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Tibaijuka kwa kukatiwa fedha hiyo hiyo ambayo si ya umma bali IPTL?
Hebu soma nukuu nyingine ya Kikwete ili uamue mwenyewe, “Tumezungumza na Profesa Tibaijuka na tumemuomba atupishe ili tuweze kuteua waziri mwingine kwani viashiri vyote vinaonyesha kuwa alikiuka kanuni na sheria ya maadili ya Umma.” Maadili gani ya umma yamekiukwa kwa kupokea fedha halali sawa na serikali inavyopokea misaada toka Ughaibuni?

Zawadi yangu bora ya Krsimas

 Huwa napokea zawadi nyingi na mbalimbali wakati wa Krsimas. Mwaka huu nimepokea zawadi ambayo imenifurahisha kuliko nyingi nilizowahi kupewa. Nimefurahi kiasi cha kushindwa kujizuia kuiweka hapa ugani. Hebu andamana nami uone zawadi niliyopewa ambayo bila shaka yaweza kukufaa hata wewe. Karibu.

Kwanza Samahani Mhango, sisi tunamfumo wetu wa utawala unaitwa sirikali siyo hiyo unayofikiri wewe serikali. Wewe haufahamu hatua za maendeleo ya sirikali yetu

Pili kimsingi sisi hatulazimishwi na taasisi au serikali yoyote duniani kufanya maamuzi kwa maslahi yetu.

Tatu utafiti tunaofanya sasa tutatumia watalaamu wetu kutoka peponi na kalumanzira ili kuwaletea majibu shetani wetu atakapojalia.

Nne katika kundi ketu la sirikali mtu ambaye siyo Kundi letu tumekwisha muondoa kwa kumfukuza madarakni tena bila shukurani.

Tano Jamaa zetu wa kundi letu tumekubaliana umma nchi za magharibi waikutishika kooni basi tunawashauri kujiuuzulu au kuwasimamisha tunawapatia mafao yao yote na kuwateua vyeo vingine pia, tunatoa shukurani kwa utendaji wao mzuri uliyotukuka kudumisha sirikali yetu.

Nategemea Mhango utakuwa umetuleewa na pia hii ni zawadi yako krismasi na heri ya mwaka mpya. Shetani wetu akubariki kwa mwaka ujayo.

Maana tutawekeza juhudi zetu katika kupata viungo vingi kutoka Zaruzaru kama mahitaji yetu kutoka kamati zetu karumanzira inavyosema ili tushinde uchaguzi katika sirikali yetu.

Wednesday 24 December 2014

Let's celebrate with a drummer boy


Uwendawazimu wetu, ufisadi na wafadhili

 Si uchochezi kusema kuwa watawala wetu wameshindwa, tena vibaya sana. Ni aibu kwa taifa ambalo limesherehekea miaka 53 ya uhuru kushindwa kufanya maamuzi magumu hadi lishinikizwe na wafadhili. Tishio na amri ya hivi karibuni toka kwa serikali ya Marekani kwa Tanzania kuwa haitatoa fedha za Changamoto za Milenia (MCC) kama serikali haitawachukulia hatua watuhumiwa wa kashfa ya uchotaji wa mabilioni ya fedha za umma, escrow ni somo tosha.
          Heri wafadhili wamenena. Hili ni pigo na aibu kwa rais Jakaya Kikwete, serikali na CCM ambao wamekuwa wakiwahadaa watanzania kuwa wako madarakani kwa maslahi yao wakati hali ni tofauti. Huu ni ushahidi kuwa CCM na serikali yake wamewekwa mfukoni na mafisadi. Hali ikiendelea hivi, watawala wetu wataipeleka nchi kubaya. Huu ni ushahidi tosha kuwa utawala wa sasa umechoka, upumzishwe ili wenye uwezo watawale na kusafisha uchafu uliopo. Inakuwaje wananchi wanashindwa kuona haya na kuiwajibisha vilivyo CCM kwa kuishikisha adabu?
          Ni ajabu kwa nchi inayojidai kuwa na utawala wa sheria lakini ikawekwa mifukono mwa matapeli wachache, wasaka tonge na wahalifu wa kawaida. Ziko wapi tambo za kupambana na biashara ya madawa ya kulevya? Nani anawagusa? Je hawa hawana ubia kwenye serikali ya sasa? Je hawa hawajaiweka serikali mfukoni? Asitokee mtu akaniambia kuwa hawajulikani. Mbona rais alishakiri kupewa orodha ya wauza unga asiifanyie kazi kwa sababu ajuazo? Je inakuwaje tunashindwa kupambana na ufisadi ilhali tukijua kuwa ni kikwazo kwa maendeleo ya taifa? Je ni kwa vile mafisadi ni washirika wa nyuma ya pazia ya watawala wetu?
          Najua wengi wanaweza kusema tunaizushia serikali.  Kama watachunguza sababu za serikali kuruhusu ufisadi kuwa sehemu ya maisha ya serikali yetu, wataelewa tunachosema. Hivi kweli nchi inayoamriwa na wafadhili la kufanya ni huru? Je kwa uzembe na upofu wetu tunapaswa kuwalaumu wafadhili kwa kuingilia mambo yetu? Watashindwaje kuingilia iwapo tunafanya mambo ya kitoto na ya hovyo? Imefikia mahali hata bunge linatoa maagizo halafu wakubwa wanayadharau na kuja na mambo yasiyo ingia kichwani kama ilivyotokea juzi wakati Ikulu iliposema kuwa haitawawajibisha watuhumiwa wa wizi wa escrow wala kuchukua hatua hadi ifanye uchunguzi wake. Tambo za ikulu zimeishia wapi baada ya kubanwa? Ndani ya wiki moja ikulu, ikiwa imechanganyikiwa na kujichanganya ilitoa tamko jingine la kijichanganya zaidi ikisema kuwa rais atawashughulikia watuhumiwa ndani ya wiki moja. Hii maana yake ni kwamba ikulu imeminywa na kufanya kile ambacho haikutaka kufanya. Maana ukiangalia timing ya tamko la Marekani na mkengeuko wa Ikulu unagundua kuwa hata kama rais atawawajibisha wahusika si kwa kutaka bali kulazimishwa na wafadhili. Je rais au chama kinachounda serikali vya namna hii bado vinawafaa watanzania? Je ni vibaya kusema kuwa rais amegeuka mhimili wa ufisadi anaopaswa kuuchikia na kupamba nao? Je ni kwanini inakuwa hivi kama rais hanufaiki na jinai hii au kuishiriki?
          Ushahidi wa kimazingira unaonyesha wazi kuwa, kama si papara za bunge, au tuseme kuwekwa sawa na kuingia mkenge, lilipaswa kuiwajibisha serikali yote. Kwa vile inaonyesha escrow ni dili lao. Haiwezekani mawaziri tena waandamizi na maafisa wengi wa serikali waruhusu wizi wa mabilioni hivi kusiwe na mkono wa wakubwa zao. Nani anakanusha kutajwa kwa afisa wa ikulu Prosper Mbena anayedaiwa na kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuwa aliandika barua ya kushinikiza pesa zichotwe? Je hapa tunatafuta ushahidi upi wa kuihusisha ikulu? Ushahidi mwingine ni ukimya wa muda mrefu wa serikali. Hata kitendo cha rais kusuasua hadi alazimishwe na wafadhili kuchukua hatua ni ushahidi tosha ukiachia mbali rais kuhusishwa moja kwa moja na uletaji wa kampuni jizi ya IPTL hapo mwaka 2004.
          Laiti wafadhili wangekwenda mbele zaidi na kuhakikisha hili jinni linalotunyonya damu IPTL linafurushwa na wahusika kufungwa, wangekuwa wametukomboa hata kama wakubwa watalalamika kuwa wanaingiliwa. Kwanini wasiingiliwe iwapo wamejirahisi kiasi cha kuacha mafisadi wajifanyie watakavyo? Kwanini wasiingiliwe iwapo wameonyesha wazi walivyo wa hovyo na fisadi? Nani angeweza kumwamrisha baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere katika lolote? Je ilikuwaje Nyerere akaogopewa na kutopewa amri? Jibu ni rahisi. Alikuwa msafi na mwenye visheni tofauti na hawa walioigeuza ikulu deni la wezi kama alivyowahi kuonya Nyerere huku akiwakataa wengi wa tunaowaona leo madarakani wakiyafuja ili kutimiza utabiri na madai ya nguli huyu (Mungu amlaze pahali pema peponi). Rais anayeamrishwa kufanya alichoapa kufanya amebaki na nini? Je nafsi zo zinawasuta? Je sisi tunawasuta na kuwawajibisha au kuendelea kuwagwaya?
          Tumalizie kwa kuwataka watanzania kutorudia makosa. Kwenye uchaguzi ujao licha ya kuhoji ni kwanini ufisadi uliachiwa kuwa sehemu ya utawala wasiangalie sura wala ukongwe wa chama. Wahakikishe wanajipatia serikali safi, mpya, yenye mapya na si huu wendawazimu wa siku zetu. Maana waingereza husema “insanity is doing the same thing over and over again and expecting different results.” Tuachane na wendawazimu huku tukijitofautisha na mafisadi ili mataifa mengine yasiendelee kutucheka kwa kuruhusu taifa letu kuwa shamba la bibi tena bibi mwenyewe hamnazo. Imetosha, wananchi wanapaswa kuanza kwajibika kwa kuwawajibishwa watawala fisadi na wachovu na wabovu.
Chanzo: Tanzania Daima leo.

Kijiwe chamuaga Werema kwa mipasho!

          Mgosi Machungi anaingia huku akiimba kana kwamba ana mtu wake anayempa vipande vyake.
          Anaamkua bila kujali na kuendelea kuimba, “Nenda Fedick Weeema nenda. Nenda jaji junk. Nenda jaji janga. Nenda tu umenyea kambi. Ushakula vya kutosha nenda kabuikie mbali.”
          Mpemba akionyesha furaha na mstuko wa wazi anaamua kutia timu kana kwamba walikuwa wamepanga wimbo huu na Mgosi. Anakwanyua mic, “Nenda wala usiangalie nyuma. Nenda tu mwanakwenda. Msiba ulotuachia watosha. Nenda ukaajiriwe na PAPu na VIPi kama Pat Rutabanonihino. Nenda ukawatumikie mabwana zako. Nenda tu hakuna anayekuhitaji.”
          Ngoma inzidi kunoga kwani Mgosi anaendelea, “Nenda sasa unanuka.Unanuka ufisadi. Umeoza na kuozeana nenda tu mwanakwenda.     Nenda huna wa kukulilia isipokuwa Kikwekwe.Kikwekwe atakulilia. Atakumiss.Amekusifia kwa kazi "njema" kwake na IpTL.”
          Mbwamiwtu anadandia mic na kuweka kibwagizi akiwaigiza Mgosi na Mpemba, “Hata hivyo, umma hauoni kazi njema zaidi ya machukizo ujambazi na hujuma. Nenda mura ukale bukima na musuli. Nenda kwa haraka nenda Harbinger Sethi Sing atakumiss. Mafisi watakumiss.”
          Mijjinga anaamua kuingia kwa wimbo tena kwa lafudhi ya kisukuma. Anahanikiza, “Jimmy Rugemalayer atakuombolezea.Wadanganyika watakuzomea. Jagishi nkwinga. Jagi ng’wana jaga. Jaga kajagi lulu, pela ng’wana njinga.”
Akiwa anaendelea kurap Kapende analalamika kuhusu yeye kuimba kisukuma.
          Mijjinga anaamua kurejea kwenye mstari na kuhanikiza huku akimtazama Kapenda kuonyesha amemwelewa, “Nendaga mwana kwendaga.Tokomea huko utokomeako hata ukicheza litungu. Nenda usigeuke nyuma tukakuonea huruma. Nenda huko usirejee tena kwenye ofisi zetu. Nenda na balaa lako.”
           Leo ni kuimba kwa kwenda mbele. Naona na Mheshimiwa Bwege ameamua kutia timu huku akiwaonyesha dole akina Sofi Lion aka Kanungaembe na Kanji. “Nenda na kazi zako chafu. Nenda msomi aliyefanya ujinga kuliko hata mbumbumbu. Nenda msomi mbumbumbu. Nenda tu. Tangulia mwana kutangulia. Muongo anangoja kukufuata. Nenda tu usigeuke nyuma ukawa jiwe la chumvi japo u zigo la uoza. Nenda tu mwanakwenda mura. Nenda usinung'unike. Nenda usisingizie. Nenda usilaumu. Nenda huenda bosi wako atakuzawadia. Kwa kazi "njema" ulofanya ya kutetea uoza wake.”
          Tulidhani ulikuwa mwisho wa mashairi ngonjera na nyodo tusijue ndiyo vilikuwa kimeanza. Mara nona mzee Maneno anauganisha akaiimba kwa lafudhi ya kizaramizi, “Huenda atakupa ubalozi kama wengine. Siku akikuteua. Nitararua nguo zangu. Nitavaa magunia. Nitajipaka majivu.Nitaomboleza. Nenda mjalaana nenda. Nenda usigeuke nyuma. Nenda ushatuchafua. Nenda ushatuibia. Nenda wala hatukutaki.Nenda kwatumikie hao waliokuumba.”
          Mipawa naye hataki kuachwa nyuma. Anamua kukamua kwa lugha ya kisukuma kama mwenzake Mijjinga, “Nendaga tuache tusherehekeeage. Tusherehekee anguko lako takatifu.Umetoka kwenye utukufu na kuangukia kwenye ukufu. Nenda usivuruge sherehe zetu. Nenda tuache tujipongeze.”
          Wakati akijiandaa kuendelea kumwaga mipasho mzee Kidevu anaamua kunyang’anya mic na kumwaga mistari, “Kama kibwengo nenda. Nenda na mzigo wako wa moto kichwani.Kama mtalaka nenda. Ndoa imekushinda. Nenda kaolewe na akina Harbinder wako. Nenda na nyodo zako. Nenda usilete fyoko. Nenda mura nenda.”
          Baada ya Msomi Mkata tamaa kuridhika kuwa watu wamemwaga usongo na nyodo zao anaamua kuingilia kati. Anakohoa kidogo na kusema, “Jamani imetosha na naamini ataipata ajue tulivyompenda sana kiasi cha kumsindikiza kwa nyimbo na ngonjera. Hata hivyo, nimegundua kuwa mipasho yenu inafikisha ujumbe. Hakuna sehemu mmnigusa kama kusema huenda jamaa anaweza kuteuliwa ubalozi kama jamaa yangu Kamara aliyeghushi na Komba aliyesafirisha wanyama wote wakaishia kuteuliwa ulaji nje.”
          Sofia aliyekuwa amefura nusu kupasuka anaamua kula mic, “Nanyi sasa mmezidi unazi. Kwani mtukufu akimteua kuna kosa gani iwapo ana mamlaka kikatiba?”
          Kapende anakula mic, “Hivi mnazi ni nani kati ya tunaotetea haki na uwajibikaji nawe unayetetea ukale na ufisadi?”
          Mheshimiwa Bwege anadandia, “Kwanini da Sofi usiombe kazi kwenye ofisi ya uenezi ukatia timu na Nipe Mapepe ambaye huongea utadhani hakujaliwa ubongo bali utumbo? Kama unampenda mura si uende akuwowe? Maana jamaa walivyo kwa kuwowa hovyo hovyo sina mfano.”
          Kanji naye hajivungi, anakula mic, “Sasa dugu yangu Bwege sasa veve bwege kweli kweli. Kwanini taka mura oa Sofi kwenda gombana na bibi yake? Kama naona oa zuri sana basi toa bibi yako kwa mura.”
          Mheshimiwa Bwege kaguswa pabaya. Anajibu mapigo, “Nenda kakuoe wewe kama Harbinger. Unadhani hatujui kuwa huyu ponjoro mwenzako anatumiwa?”
          “Sasa dugu tusi mimi. Mimi hapana iko kama Harbinger. Ile kama tumiwa sauri yake. Mimi hapana tumika. Kama iko mtu nataka tumika basi mimi napenda tumia yeye.”
          Mbwamwitu, huku akimtazama Kanji anasema, “Basi dugu yangu nenda tumia Sofi yako.”
          Msomi anaamua kula mic, “Japo mnaweza kusema msemayo kama masihara, ukweli ni kwamba hawa matapeli tunaoshuhudiwa wanatumiwa mbele nyuma kulia kushoto. Rejea Rugemalayer alivyotembeza mshiko karibu kwa vigogo wote kuanzia wa siasa hadi wa majoho. Huu ni ushahidi kuwa hii biashara si ya mtu mmoja bali wengi hata usiowategemea. Nadhani ndiyo maana wanashikwa kigugumizi kuwajibishana.”
          “Hebu ngoja,”anasema Msomi huku akiangalia upande wa Kamata. Anaendelea, “Hivi lile siyo shangingi la Mura We-rema?”

          Anatugeukia na kusema, “Hebu twende tukamtia adabu nyani dume huyu.” Wote tunatimka kuelekea Nyerere Road kwenda kumfanyia kitu mbaya mura We-rema. Tulimfanya nini? Please don’t ask.
Chanzo: Tanzania Daima leo.