The Chant of Savant

Saturday 8 March 2014

Tutapata Katiba Mpya au Kanuni Mpya?


Kwa hali ilivyo ni kwamba wateule wetu waliko Dodoma wakigombea udohoudoho hawakutuangusha tu bali wametutia aibu. Kila siku wanazusha upuuzi huu na ule bila kujali maslahi ya mamilioni wanaowaangalia. Tumezidiwa na wakenya. Walipotaka katiba mpya waliipata tena kwa haraka na amani tofauti na hawa walaji wetu wanaokwenda pale kugombea mshiko. Je watanzania tufanye nini ili kupata Katiba Mpya inayofanana na matarajio yetu? Je hii nayo si aina nyingine ya ufisadi? Hakika aliyeliroga taifa letu alishakufa zamani!

No comments: