The Chant of Savant

Saturday 24 December 2016

Yaani hata machangu mnaimpoti toka Ugabacholini!

 
            Niliposoma kuwa ndata walidaka vyangudoa toka Nepali na India nilicheka sana. Kwanza nilijiuliza; Hawa jamaa walivyo wabaguzi, vyangu wa kibongo wakienda kule watapata soko kweli? Je inakuwaje tunaruhusu kila uchafu toka ugabacholini kiasi cha kuamua hata kutuletea migonjwa ya ajabu ajabu? Je huu nao ni uwekezaji auuteketezaaji?  Kama siyo hivyo, inakuwaje hawa jamaa wanaleta vyangu toka ugabacholini wakati tunao wa kumwaga hadi wanageuka kero kwenye mitaa yetu?  Hapa kuutakuwa na namna ima kwenye mfumo au kwa wale magabacholi wanaowaleta vyangu hawa. Je sisi tunaweza kuwapelekea vyangu wetu kule wasirudi kwenye majeneza baada ya  wa kule kuwanyotoa roho kwa kuingilia ulaji wao? Je wanakuja kuhudumia waswahili wakati wanawabagua au ni ile caste system ya kumbagua mswahili kiasi cha magabacholi kuamua hata kuleta vyangu wao ili kuepuka kuchanganyikana na waswahili?  Mbona nilipokuwa nasoma kule niliwahi kuona vyangu wengi wakijigonga kwa waswahili kiasi cha kuamsha chuki hadi wajalaana kutoana roho? Hawa jamaa licha ya kuwa wabaguzi wana roho mbaya sina mfano. Pamoja na kuletwa kujenga reli na kung’ang’ania wamekaa miaka yote wakiendeleza ubaguzi dhidi ya wale wanaowategemea kwa kila kitu. Hivi walevi wakiamua kuacha kununua bidhaa zao na kununua kwa walevi wenzao wanaweza kuwa matajiri? Hata hivyo, walevi nao wamelaaniwa. Pamoja na kubaguliwa kwa miaka nenda rudi, bado wengi wanajigonga kwa wabaguzi hawa wa kunuka. Sijui nani aliwaroga hawa wajalaana wanaobaguliwa lakini bado wakajigonga na kuwazimia watesi wao? Huoni walivyoamua kuachia kila kitu hadi majumba ya Asajile Mwaijumba kwa magabacholi wakati wenyewe wakibanwa mbavu kwenye mbavu za mbwa Uswekeni? Tutaendelea kulea ubaguzi huu wa wazi utokanao na udhalili wa hiari hadi lini? Yaani tumeridhika na umachinga wakati wenzetu wanaendelea kukalia kila kitu kiuchumi?
            Pamoja na kwamba ukisema unaonekana mbaguzi kuliko wanaotenda wazi wazi, bila kubadili mfumo na kuwaadabisha hawa jamaa, kuna siku watatia kaya kibiriti na kujiondokea. Kama sisi tunaonekana kinyaa kiasi cha kubaguliwa hivi, kwanini wasilete na nyanya, unga, mchele na hata maji yao kuepuka kutumia vitu vya Kiswahili? Kwanini hata huo uchuuzi wakafanyie kwao kwani kuna aliyewaita au shida zao? Mbona waswahili wanaojipeka kule kusoma wanabaguliwa hadi wengine kuuawa wakati huku miswahili ikiangalia bila kuchukua hatua mujarabu kuhakikisha kuwa tabia hii ya kidhalimu inakomeshwa ima kisheria au vinginevyo? Mnakumbuka yule binti wa kibongo aliyedhalilishwa na kupigwa baada ya Msudani kumgonga gabacholi? Kuonyesha tulivyo wa hovyo, uliza nini kilifanyika? Lisirikali lenyewe lilikaa kimya huku wanene wakiwapongeza magabacholi kuwa wana uwezo wa kupiga kura huku na kule wakati sisi tunazuiliwa uraia wa kaya mbili.
            Kwa vile wenye madaraka wameamua kula pini kuogopa kuwaudhi wateule, mimi kiongozi mkuu wa walevi lazima nisema kuwa ubaguzi wa namna hii utakuja kuwa bomu huko tuendako. Haiwezekani wajalaana watubague hadi wanaleta vyangudoa wao kana kwamba sisi hatuna vyangudoa. Wakati mwingine walevi wanapaswa kujilaumu. Wanabaguliwa nao wanajigonga. Wamenikumbusha mfumo wa kibaguzi ambao tunaanza kuuzoea. Siku moja si nikaupiga na kumtokea mtoto wa kimanga. Kimwana alionekana kunizimia. Lakini wazazi wake walipoipata si wakamkimbizia umangani na kumuozesha kule haraka ili nisimuwowe mie. Ajabu hawa nao wanapenda kuoa vibinti vyetu chuma na kuwakimbizia wao umangani ambako nasikia wanabaguliwa na kuitwa waswahili.  Wabaguzi hawa wako tayari hata kuoa dada zao ilmradi walevi wa Kiswahili wasiwapate. Huwa namkumbuka marehemu Abeid Karumekenge aliyewalazimisha kuchanganyikana kwa kuwowana kiasi cha kuleta usawa na kuheshimiana. Laiti na mzee Nchonga angechukua msimamo wa kuigiwa mfano kama huu tuliponyaka uhuru, nadhani tusingekuwa tunadhalilishana hadi kuleteana vyangudoa toka Ugabacholini ili kuepuka magabacholi kuwatumia vyangu wetu.
            Nasikia kama tumbo linauma. Acha niende kwa mama Kote lau nipate mapupu na kutuliza hii njaa.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.

No comments: